Habari wana jukwaa!
Ina julikana yakuwa siku ya Juma mosi ya kesho kutwa tarehe 17/11/2018 Wanafunzi wa kidato cha nne wanafanya mahafali ya kuhitimu. Uongozi wa LORETO GIRLS MWANZA umeakuja na maamuzi ya kusikitisha ya kutaka kila mgeni afikaye siku hiyo ya mahafali shuleni hapo kuwa na kiingilio cha Tsh. 10,000/=
Binafsi naweza sema ni maamuzi ya ajabu hasa yasioshirikisha walengwa ambao ni wazazi, kuna familia zina watu 20 mpaka 10 hufika kuungana na ndugu yao katika siku hii muhimu, maana yake hii familia itapaswa kuacha Tsh. 200,000/= getini kama kiingilio.
Shule hii inageuza kumbukumbu za Wanafunzi wao kuwa mradi wa kujipatia mamilioni bila sababu sababu za msingi.
Haya yana umiza na yanawanyima wanafamilia haki yao ya msingi ya kujumuika na ndugu yao(zao).
Pia yanawanyima wanafunzi wao haki yao ya kujumuika na familia zao katika kumbukizi hi.
Inafahamika ya kuwa siku zote mzazi au mlezi aendapo loreto kusalimia mwanae au kuonana na uongozi hapakui na mambo ya ajabu kama haya, iweje uongozi ulete mambo haya katika siku muhmu sana ya kumbukizi kwa wanafunzi wao na wanafamilia wa wanafunzi wao.
Ombi langu kwa serikali, hii taasisi ichunguzwe tabia za aina hii si tu zinawaathiri wanafunz kisaikolojia kwa kuwanyima fursa ya kuonana na ndugu zao wote kwa furaha na upendo katika siku hii bali pia zina wapa masononeko ya mioyo na msongo wa mawazo jamii ya mwanafunzi na mwanafunzi kwa ujumla.
Wazazi na walezi wito kwenu pia tupazeni sauti kwa tabia za aina hii zinazo wanyima haki wanetu na ndugu zetu kujumuika nasi katika mazngira waliyoyazoea kwa miaka minne.
Naomba kuwasilisha.