Serikali ichunguze makampuni ya gas

Serikali ichunguze makampuni ya gas

Last emperor

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2015
Posts
10,346
Reaction score
9,881
Mimi ni mmoja wa watumiaji wa mwanzo kabisa wa gas za majumbani za mitungi mara tu ilivyoanza kusambazwa...Ila katika siku za karibuni Kumekuwa kuna uhuni unafanyika kwa haya makampuni ya gas zinazotumika majumbani.

Maana mtungi uleule wa kampuni lileile uliokuwa ukitumia kwa matumizi yaleyale ya nyumbani, kwa mfano ule mdogo ambao ulikuwa ukidumu let say kwa mwezi mzima, sasa hivi unaisha haraka tu ndani ya wiki mbili.

Kama ni ule wa size ya kati ulikuwa ukidumu kwa miezi mitatu, sasaivi unaisha ndani ya mwezi mmoja tu! Hii inashangaza,inakuwa kana kwamba kuna uhuni unafanyika wanaweka gas nyepesi inayoisha haraka, ili gas iishe haraka na waweze kufanya biashara zaidi..

Naomba mamlaka za serikali zinazosimamia mambo ya gas lichunguze hili suala hili,maana sisi wananchi ndo tunaumia!
 
Hiyo sio kazi ya serikali bali wewe mwenyewe unapaswa kureport malalamiko yako Ewura.
 
Mimi ni mmoja wa watumiaji wa mwanzo kabisa wa gas za majumbani za mitungi mara tu ilivyoanza kusambazwa...Ila katika siku za karibuni Kumekuwa kuna uhuni unafanyika kwa haya makampuni ya gas zinazotumika majumbani. Maana mtungi uleule wa kampuni lileile uliokuwa ukitumia kwa matumizi yaleyale ya nyumbani, kwa mfano ule mdogo ambao ulikuwa ukidumu let say kwa mwezi mzima, sasa hivi unaisha haraka tu ndani ya wiki mbili.Kama ni ule wa size ya kati ulikuwa ukidumu kwa miezi mitatu, sasaivi unaisha ndani ya mwezi mmoja tu! Hii inashangaza,inakuwa kana kwamba kuna uhuni unafanyikawanaweka gas nyepesi inayoisha harak, ili gas iishe haraka na waweze kufanya biashara zaidi..Naomba mamlaka za serikali zinazosimamia mambo ya gas lichunguze hili suala hili,maana sisi wananchi ndo tunaumia!
Ukienda kununua wambie wakupimie kg uone. Mimi nilianza na Oryx wakati naishi ulikuwa unakaa miezi nani ule mtungi wa 30.5kg, lakini nilipoanza kuishi na watu wengine yani tukawa watu watatu na mtoto mmoja, ukawa unakaa wiki 5 yani mwezi na wiki moja, ila nilienda badilisha nikakuta oryx hakuna kuna O-gas jamaa akanipa hiyo hiyo O-gas toka kipindi hicho ilikuwa mwez wa tano mwaka huu natumia O-gas, uzuri O-gas inauzwa 45000 huku ninakoishi wakati ryx ni 50000, na matumizi ni yale yale na inakaa wiki 5 pia.

Toka nilipojua kuwa mitungi wanajazia sehemu moja hakuna nayechimba na kujaza peke yake, sijali kampuni mimi najali kipimo tu cha mtungi maana gasiiliyomo ni ile ile.
 
Mimi ni mmoja wa watumiaji wa mwanzo kabisa wa gas za majumbani za mitungi mara tu ilivyoanza kusambazwa...Ila katika siku za karibuni Kumekuwa kuna uhuni unafanyika kwa haya makampuni ya gas zinazotumika majumbani. Maana mtungi uleule wa kampuni lileile uliokuwa ukitumia kwa matumizi yaleyale ya nyumbani, kwa mfano ule mdogo ambao ulikuwa ukidumu let say kwa mwezi mzima, sasa hivi unaisha haraka tu ndani ya wiki mbili.Kama ni ule wa size ya kati ulikuwa ukidumu kwa miezi mitatu, sasaivi unaisha ndani ya mwezi mmoja tu! Hii inashangaza,inakuwa kana kwamba kuna uhuni unafanyikawanaweka gas nyepesi inayoisha harak, ili gas iishe haraka na waweze kufanya biashara zaidi..Naomba mamlaka za serikali zinazosimamia mambo ya gas lichunguze hili suala hili,maana sisi wananchi ndo tunaumia!
hahahahahahahaaaaaa,
umenichekesha unavyosema wanaweka ile gesi nyepesi inayo isha haraka.

Gesi ya kwenye mitungi mnayotumia kupikia majumbani ni ile LPG(Propane +Butane). Gesi hiyo inapimwa kwa uzito (kg) hicho ndio kipimo rahisi kwasababu gesi haionekani hivyo ukiishindilia kwenye mtungi uliowekwa kwenye mzani utaona uzito unaongezeka. Basi kama imeisha haraka ujue wanawaibia, hawapimi uzito sahihi.
Inabidi mpeleke malalamiko EWURA, ili wakachunguze kwenye hayo makampuni.
 
hahahahahahahaaaaaa,
umenichekesha unavyosema wanaweka ile gesi nyepesi inayo isha haraka.

Gesi ya kwenye mitungi mnayotumia kupikia majumbani ni ile LPG(Propane +Butane). Gesi hiyo inapimwa kwa uzito (kg) hicho ndio kipimo rahisi kwasababu gesi haionekani hivyo ukiishindilia kwenye mtungi uliowekwa kwenye mzani utaona uzito unaongezeka. Basi kama imeisha haraka ujue wanawaibia, hawapimi uzito sahihi.
Inabidi mpeleke malalamiko EWURA, ili wakachunguze kwenye hayo makampuni.
Na inabidi akumbuke kuwa gas wanajazia sehemu moja wenye kampuni wanamiliki mitungi tu hakuna gas nyepesi wala nzito
 
Na inabidi akumbuke kuwa gas wanajazia sehemu moja wenye kampuni wanamiliki mitungi tu hakuna gas nyepesi wala nzito
Makampuni yanajaza gesi yenyewe mkuu. Oryx gas wanajaza wenyewe sio kazi ngumu hats, Lake Gas pia wanajaza wenyewe mkuu.
 
Makampuni yanajaza gesi yenyewe mkuu. Oryx gas wanajaza wenyewe sio kazi ngumu hats, Lake Gas pia wanajaza wenyewe mkuu.
Labda kama hili limeanza miaka ya karbuni ila miaka ya nyuma wote walikuwa wanaenda kujazia sehemu moja maana gas ilikuwa inakuwa imported
 
sasa mlaji asipoenda Ewura kupeleka malalamiko akiwa na ushaidi wa bidhaa husika atakua anapoteza muda wake bure.
ni kweli kwa namna flani, ila chukua mamlaka kama TFDA utaanzaje kupeleka malalamiko labda paracetamol unayokunywa labda haina ubora? kwanza utaanzia wapi kufahamu uborab wa dawa husika huda ujuzi wala vitendea kazi? kwahio Ewura na wao km mamlaka husika hilo ni jukumu lao la msingi kama vile wanavyofuatilia kwe mafuta, ingawa nakubali pia kupeleka malalamiko itasaidia sana utendaji wao
 
Mi nadhani kuna namna hapa.Maana kuna kipindi nilisikia mahali watu walikuwa wanauwezo wa kupiga nyoka kutoka kwenye gas iliyojaa wanachukua kidogo kidogo wanajazia kwenye mitungi mitupu.hivyo uhuni kama huo upo
 
Mimi ni mmoja wa watumiaji wa mwanzo kabisa wa gas za majumbani za mitungi mara tu ilivyoanza kusambazwa...Ila katika siku za karibuni Kumekuwa kuna uhuni unafanyika kwa haya makampuni ya gas zinazotumika majumbani.

Maana mtungi uleule wa kampuni lileile uliokuwa ukitumia kwa matumizi yaleyale ya nyumbani, kwa mfano ule mdogo ambao ulikuwa ukidumu let say kwa mwezi mzima, sasa hivi unaisha haraka tu ndani ya wiki mbili.

Kama ni ule wa size ya kati ulikuwa ukidumu kwa miezi mitatu, sasaivi unaisha ndani ya mwezi mmoja tu! Hii inashangaza,inakuwa kana kwamba kuna uhuni unafanyika wanaweka gas nyepesi inayoisha haraka, ili gas iishe haraka na waweze kufanya biashara zaidi..

Naomba mamlaka za serikali zinazosimamia mambo ya gas lichunguze hili suala hili,maana sisi wananchi ndo tunaumia!

Je siku hizi zinatoboa sufuria zako ambazo sio kwa ajili matumizi ya gesi.

Gesi inapunguzwa makali ili kupunguza mahafa maana hata ikivuja kulipuka sio rahisi kama zamani
 
Watu elimu ya gesi hawana ndio maana kila siku wanalalamika,unaponunua gesi hakikisha unapima tena kwenye mzani wa digital.Kwanini mzani wa digital ?kwasababu hauibiwi hata point 1,ununuaji wa gesi upo wa mtungi mdogo 6kg, mtungi wa kati 15kg na mkubwa 38kg.Kwahiyo unaponunua mtungi mdogo mathalani wa 6kg ,unachukua uzito wa gesi ambao ni kilo 6+uzito wa cylinder normally unakuwa kilo7 au 8 kwahiyo unachukua 6+8 =14kg,a wanandika kwenye cylinder Tare weight ujuwe ni uzito wa empty cylinder hapo una add uzito wa ges I unayo nunua.
Wasalam
 
Watu elimu ya gesi hawana ndio maana kila siku wanalalamika,unaponunua gesi hakikisha unapima tena kwenye mzani wa digital.Kwanini mzani wa digital ?kwasababu hauibiwi hata point 1,ununuaji wa gesi upo wa mtungi mdogo 6kg, mtungi wa kati 15kg na mkubwa 38kg.Kwahiyo unaponunua mtungi mdogo mathalani wa 6kg ,unachukua uzito wa gesi ambao ni kilo 6+uzito wa cylinder normally unakuwa kilo7 au 8 kwahiyo unachukua 6+8 =14kg,a wanandika kwenye cylinder Tare weight ujuwe ni uzito wa empty cylinder hapo una add uzito wa ges I unayo nunua.
Wasalam
Watanzania wengi hawana utamaduni wa kuwa na mzani nyumbani

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom