Serikali hii ikitoka madarakani,vyama vya wafanyakazi vitakuja kufungua kesi kudai nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma ambayo sasa haitolewi

Serikali ya awamu ya tano,kama ilivyo kwa serikali zote za CCM zilizotangulia,imeendeleza tabia ya kutolipa watu haki zake huku awamu hii ya tano ikija na maajabu ya kutotoa nyongeza ya mishahara ya kila mwaka kwa watumishi wa umma nyongeza ambayo ipo kisheria na ambayo haitolewi kwa mapenzi ya Raisi au serikali anayoiongoza bali hutolewa kwa mujibu wa sheria.

Kwakuwa nyongeza hii iko kisheria,basi ni swala la muda tu kabla ya watumishi kupitia vyama vyao vya wafanyakazi(visivyoongozwa na makada), kuja kufungua kesi mahakamani na kudai nyongeza hiyo ambayo itakuwa ni kwa mabilioni kwani katika miaka yote minne ya utawala huu, nyongeza hii imetolewa mara moja na kama sikose ni katika mwaka wa fedha uliiopita(2018/2019) ila miaka mingine yote ukiwemo mwaka huu wa wa fedha wa 2019/2020 hakuna kilichoongezwa hivyo ni wazi deni litakuwa kubwa tu.

Kama nyongeza hiyo ilitolewa kwa miaka yote niliyoitaja ukiwemo na mwaka huu wa fedha wa 2019/2020,basi niko tayari kukoselewa.

Tundu Lissu alikuwa sahihi sana kusema tuwe na sheria inayoruhusu kukamata mali za serikali kwani hii ndio njia pekee ya kulazimisha hizi serikali zilipe madeni yake.

Wao(wanasiasa) wanajilipa vizuri tena kwa wakati ila kulipa haki za watu wengine wanaona tabu(ubinafsi)!!
Awamu ya 5 inabidi ije kushitakiwa hapo baadae kwa kutoongeza Mshahara kwa wafanyakazi wake,watakuja kudai fidia na sirikali kuja kulipa.
 
Mkiongezwa mishahara hizi kesi zilizoachwa na nyerere tutatoa wapi pesa ya fidia? Tusipojenga vitega uchumi hiyo mishahara itatoka wapi? Jpm sio mganga wa jadi kuwa anapiga ramli pesa inapatikana,
 
Mkiongezwa mishahara hizi kesi zilizoachwa na nyerere tutatoa wapi pesa ya fidia? Tusipojenga vitega uchumi hiyo mishahara itatoka wapi? Jpm sio mganga wa jadi kuwa anapiga ramli pesa inapatikana,
Hilo ni takwa la kisheria
Sheria haijaelekeza nyongeza itoke wapi, ila inasema kila mwaka wafanyakazi wanatakiwa waongezwe.
Kwanza serikali sio mjasiriamali mdogomdogo kwamba eti atapata hasara
 
wakiona maisha magum si waache kazi kuna vijana kibao hawana kazi wapo street tu
 
Balimar, wakati ukidai nyongeza kumbuka kuna mama yuko leba hana vifaa vyakujifungulia, kuna ambulensi haina mafuta, kuna mtoto hana dawati, kuna mkulima hana pembejeo, kwanza kudai nyongeza ni umasikini, ulishasikia mtumishi wa japan au marekani akidai nyongeza?
 
Kesi zitakuwa nyingi sana msione watu wamepoa sababu wanajua hawawezi pata haki yao sasa, kuna waliobomolewa Nyumba zao, bambikiwa kesi za uhujumu uchumi, kubomolewa Kwa bilicana,Shamba, waliotaifishiwa Mashamba Mali zao,kesi zitakuwa nyingi sana wakati huo uchumi utakuwa huko shimoni kabisa deni La taifa likifikia tilioni zaidi ya 90 yaani mufilisi kabisa,waliokatishwa mikataba yao nao wakikaba koo,miradi yote ikiwa hata nusu haijakamilika hata ikikamilika hakuna cha kurudisha mapema faida sababu ya uchumi kufa mzunguko wa pesa Hakuna. Tuendako si Salama sana na Kesi za kuishtaki serikali iliyopita zikiwa nyingi sana ndani na nje,sababu ya maamuzi ya kukurupuka yasiyofata sheria toka Kwa watendaji.
Kuna ukweli mchungu ambao upo kwenye suala hili.
Sambamba na hili, hata wale wafanyakazi wa Serikali waliofukuzwa kazi kwa kitu walichokiita VYETI FEKI, baadhi yao nao watarudi na kuja kuishitaki Serikali kwa sababu walifukuzwa bila ya kufuata Sheria, kanuni, miongozo, na taratibu za Utumishi wa Umma. Wote walifukuzwa tu KIHOLELA baada ya kutolewa kwa tamko LA Kisiasa kutoka kwa Mkuu wa Kaya.
Hata kama kweli Walikuwa na makosa ya Kughushi Vyeti vya Taaluma zao, lakini bado Sheria zinataka kuzingatiwa kwa Matakwa ya Sheria kabla ya kumfukuza kazi mwajiriwa yeyote yule. Yalifanyika makosa makubwa katika mchakato wa kuwafukuza kazi Watumishi wale, wengi hawakupewa nafasi ya kujitetea na wala hawakukabidhiwa Hati za Mashitaka juu ya Makosa waliyotuhumiwa nayo kama Sheria zinavyotaka.
Kuna walimu kama kumi hivi nawafahamu ambao wamekumbwa na janga hili, walipoenda kuomba ushauri kwa wakili fulani(sitaki kumtaja jina), akawashauri wakusanye vielelezo vyao vyote wawe navyo mkononi, na kisha wasubiri kwanza mpaka huyu bwana Mkubwa amalize awamu yake ndipo waende "Kuanzisha Vita" Mahakamani dhidi ya Serikali.
 
Balimar, wakati ukidai nyongeza kumbuka kuna mama yuko leba hana vifaa vyakujifungulia, kuna ambulensi haina mafuta, kuna mtoto hana dawati, kuna mkulima hana pembejeo, kwanza kudai nyongeza ni umasikini, ulishasikia mtumishi wa japan au marekani akidai nyongeza?
Ni kweli kabisa unayosema na ndio maana tutatumia mabilioni ya shilingi kuwaita watendaji wa kata Magogoni ili tu chama chetu kiendelee ku-survive.
 
Kesi zitakuwa nyingi sana msione watu wamepoa sababu wanajua hawawezi pata haki yao sasa, kuna waliobomolewa Nyumba zao, bambikiwa kesi za uhujumu uchumi, kubomolewa Kwa bilicana,Shamba, waliotaifishiwa Mashamba Mali zao,kesi zitakuwa nyingi sana wakati huo uchumi utakuwa huko shimoni kabisa deni La taifa likifikia tilioni zaidi ya 90 yaani mufilisi kabisa,waliokatishwa mikataba yao nao wakikaba koo,miradi yote ikiwa hata nusu haijakamilika hata ikikamilika hakuna cha kurudisha mapema faida sababu ya uchumi kufa mzunguko wa pesa Hakuna. Tuendako si Salama sana na Kesi za kuishtaki serikali iliyopita zikiwa nyingi sana ndani na nje,sababu ya maamuzi ya kukurupuka yasiyofata sheria toka Kwa watendaji.
Nyerere hakuwahi kutamani makabila makubwa kuitawala Tanzania, ni ubishi wetu tu, lakini pia kuna makabila hayajawahi kumiliki akili
 
Nyerere hakuwahi kutamani makabila makubwa kuitawala Tanzania, ni ubishi wetu tu, lakini pia kuna makabila hayajawahi kumiliki akili

True hata mkoloni aliyatumia kwenye kazi za nguvu sio za kutumia akili wengi walipelekwa tanga kulima mkonge na wengine makuli bandarini.Kazi za kutumia akili huwa wanachemka sana VIATU vinapwaya.
 
Nyongeza ya mishahara inatumika kama ruzuku Kuendesha ndege kuficha aibu ya hasara, thus CAG aruhusiwi kukagua.Ubinafsi wa watawala wa kiafrica ufikiria maslai yao tu
 
Back
Top Bottom