Serial killer in Dar!

Kama kuna mtu ambae atakua hajaelewa anaeza pata mtu kumsaidia kufafanua.binafsi siwezi kutafsiri kwa kiswahili!
Thanks for your concerns anyways!
TAARIFA MUHIMU:
Kuna muuaji ameibuka jijini Dar kwa sasa, leo ameuwa mtu mmoja maeneo ya Kinondoni. Amempiga risasi ya kifua Mtu mmoja ndani ya gari alilokuwa anaendeshawa kwenye Barabara ya Kinondoni, katikati ya Mkwajuni na Magomeni.

Tukio kama hilo lilitokea Juzi kwenye Barabara ya Bagamoyo, Muuwaji huyo ni mwembamba na huendesha Pikipiki.
Ni vyema mkawa makini mnapokuwa mnaendesha Magari, maana chanzo chake kikuu huwa ni kusababisha Ajali na punde unapoanzisha mabishano nae huamua kutoa Bastola na kumpiga risasi Dereva.

Tafadhali, tusaidiane kusambaza ujumbe huu kwa wote tunaowajali na kuwapenda.......!


 
Nilisikia juzi usiku kwnye kipindi cha matukio cha Wapo fm, mtangazaji alisema huyo jamaa ni Singasinga na anaendesha pikipiki. Anasema alisababisha ajali lakini dereva wa gari alifanikiwa kumkwepa ili asiumie na gari likagonga ukuta wa barabarara likapata pancha. dereva akarudi pale ambapo jamaa wa pikipiki amelala barabarani ili wanegotiate namna ya kumsaidia fidia ya tairi. Jamaa akawa mkali akatoa bastola akampiga risasi kifuani yule dereva, watu waliokuwepo wakaanza kukimbia na yeye akawasha pikipiki yake akatimua hakuna hata aliefanikiwa kuandika namba za pikipiki.
 
hafiki mbali wapi bandugu....? watu police wapo kimya na kuzuia maandamano na kuimarisha ulinzi kwa kesi ya Ponda na Lwakatare huku wengine wanakufa...

sasa hivi daladala zitakua zinagonga kila jamaa mwenye pikipiki anayeonekana hatari kwao na watamlamba tu, tanzania hatujafikia kuwa na efficient serial killers

akifikisha wanne basi huyo sio mtanzania
 
Mkuu mie hii nchi nshaifahamu vizuri sana hasa awamu hii ya JK, wakija I'll dance wit em, michezo ya kitoto sana hii, what matters is who takes the bullet first, either way the game ends there...!! wha ha ha ha

I salute you and love your honest. Hii serikali ya JK ni wababaishaji sana, yaani wao wanaona bora wafanye maovu ila wasifuatiliwe na wananchi wakati sie ndiyo mabosi wenyewe. JK kila kukicha yeye na kucheka kwani anajuwa anatusanifu na anajuwa fika kwamba whatever he says tutamuamini ila ukienda kinyume kwa kutaka kuchambua upuuzi wa maneno yake ndo unakutana na vibaka wake. Wanakuja kukutakia habari kisha wanakumwagia tindi kali ama kupigwa na kuumizwa then anajifanya kuja hospitali kukupa pole huku akikugombeza kuwa usirudie tena kunikashifu ila nitakupeleka Afrika kusini ukapate matibabu ya uhakika.
 
sasa hivi daladala zitakua zinagonga kila jamaa mwenye pikipiki anayeonekana hatari kwao na watamlamba tu, tanzania hatujafikia kuwa na efficient serial killers

akifikisha wanne basi huyo sio mtanzania
Ni kweli na lazima atakuwa bedui tu au jeshi la mtu mmoja wa kiukweli. Nilishangaa leo maeneo ya kariakoo. Yaani jamaa (muhindi/mwarabu) anaendesha pikipiki kavaa jaketi la kuzuia upepo wakati akiendesha pikipiki, yaani lile daladala la Buguruni baadhi ya watu walianza kushuka wengine kukimbilia nyuma ya daladala kumuhofia jamaa wakati yeye hana hili wala lile yuko tu na safari zake za mjini. Alipokuja polisi kuuliza akaambiwa jamaa anafanana na mtu anayezungumzwa redioni. Yaani wabongo kwa ujingaaaa, samahani for the few ambao hawako hivi. naona kina Joti na Ze Comedy yao wametufanya kutostaharabika, tumekuwa wajinga wa kutupwa. Utashangaa mtu ana anguka na pikipiki watu watamkibilia kumuona na kumshangaa huku wakiacha kazi zao na msaada hawatoi, sasa why are they there at first?
 
Nimetoka kusoma ukurasa wa fb wa millard ayo amesema amepata habar kuwa kuna dereva ameuawa kwa risasi/bunduki na wanedesha pikipiki maeneo ya TEGETA
 
Serial killers ata kwenye nchi za dunia ya kwanza na serikali imara wapo sasa aje kuhusisha na kikwete.JF ni nyumba ya great thinkers,think hard sio mtu anakurupuka kwa kuongozwa na hisia na mapenzi ya chama chake
 
Mzimu wa Dito, sipiti Bagamoyo road tena.
 
Ni Tanzania pekee tu ndio unaweza ukaona mgeni akitumia silaha na kumpiga risasi Mtanzania tena kwa kukusudia na bado anaendelea kufanya hivyo bila hata woga.
Serikali iwekeze ktk CCTV ilikuweza kupambana na watu wahuni kama hawa.
 
Kuna thread inayomtaja singasinga kufanya mauaji kama hayo.
 
wakuu mkumbuke kama wiki tu iliyopita dereva wa dala dala alippigwa risasi na kijana huyu pia pia mwishoni mwa wiki iliyopita pia kuja jamaa alipigwa risasi bagamoyo road kwa staili hiyo hiyo sasa jana pia ikawa hivi

[h=5]Kuna muwaji ameibuka jijini Dar kwa sasa, leo ameuwa mtu mmoja maeneo ya Kinondoni. Amempiga risasi ya kifua Mtu mmoja ndani ya gari alilokuwa anaendeshawa kwenye Barabara ya Kinondoni, katikati ya Mkwajuni na Magomeni.
Tukio kama hilo lilitokea Juzi kwenye Barabara ya Bagamoyo, Muuwaji huyo ni mwembamba na huendesha Pikipiki.
Ni vyema mkawa makini mnapokuwa mnaendesha Magari, maana chanzo chake kikuu huwa ni kusababisha Ajali na punde unapoanzisha mabishano nae huamua kutoa Bastola na kumpiga risasi Dereva.
Tafadhali, tusaidiane kusambaza ujumbe huu kwa wote tunaowajali na kuwapenda......
[/h]




KIFUPI TANZANIA HATUNA POLISI WAMEKALIA SIASA TU HUKU WANANCHI TUNATESEKA TU
 
KIFUPI TANZANIA HATUNA POLISI WAMEKALIA SIASA TU HUKU WANANCHI TUNATESEKA TU
du, sasa kujilinda wenyewe si itakuwa kazi zaidi!? japo snipers walisumbua kipindi fulani US lakini nadhani wenzetu walikuwa na nia ya dhati na hapa huwezi jua ni nani anawatuma kama si hao hao wanaopaswa kutulinda. Tuna shida kweli
 
Tanzania sijui tunaelekea wapi jamani. Matukio kila kukicha ina maana polisi hawana taarifa?
 
Ni kitu cha hatari kwa wenye usafiri tuepushe malumbano na hawa jamaa wa pikipiki ndo kitu kilichobaki
 
Tuamini kwamba wote waliouawa walifanya ubishi wa kupisha? ..nchi imeshajichimbia kaburi hii na wenye dhamana wamelala
 
Jana nimeona mtu mmoja akanikumbusha story hii, thank God nilikuwa nimeisikia kwenye power breakfast.

Huyu alikuwa kwenye bajaj nyekundu, amesimama mlangoni kwa bajaj so yuko kama nje tu
Kashika panga kuubwa, bajaj inaendeshwa rough, na haisimami
Ukikataa kuipa upenyo huyo aliyesimama anakunyooshea panga

Nilibaki na maswali kw kweli, ilikuwa mbaya kwa macho ile scene.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…