Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Kuna uwezekano mkubwa muda si mrefu ujao tutatangaziwa rasmi upatikanaji wa mafuta ya kiasi cha kutosha tu kuweza kufanya biashara ya kimataifa. Labda kuanzia kwenye Ziwa Tanganyika na hadi maeneo ya ndani zaidi ya Tanzania na hata kwenye pwani yetu. Kwa vile tumeshajua matatizo mengi ambayo tumeyaona kwenye madini ni vizuri kujua sera yetu ya mafuta ikoje? Na kwa vile tumeshaona mambo ya Angola, Chad na hata Guinea linapokuja suala la mafuta je Tanzania tumejiandaa vipi kusimamia sekta hiyo nyeti sana?
Je vyama vyetu vikubwa vya kisiasa vinazo sera za mafuta au wote tunasubiri mafuta yapatikane ndio tuanze mjadala wa sera?
Je vyama vyetu vikubwa vya kisiasa vinazo sera za mafuta au wote tunasubiri mafuta yapatikane ndio tuanze mjadala wa sera?