Sera ya Chadema ya "Utawala wa Majimbo"

Mtoa mada, naweza ipata wapi hiyo sera ili niisome kwanza niielewe ndio nije nitoe mchango.

Hata kama ni nzuri kiasi gani lazima wananchi tuelimishwe, isije kuwa another sera maslah.

Mikoa mimngine haina hata ulanga sijui itakuwaje.

Kila mkoa nchi hii una rasilimali za kutosha kwa namna yake.
Hebu taja mkoa m1 tu ambao ni maskini wa rasilimali?
 


Pax,

..majimbo huwa na mamlaka fulani ktk mambo ya kodi, elimu,sheria etc etc.

..USA kuna majimbo yanayoruhusu hukumu ya kifo na kuna majimbo yanakataa hukumu hiyo.

..yalikuwepo majimbo USA ambayo yalikuwa yamehalalisha segregation na ndoa za weusi na weupe zilikuwa zimepigwa marufuku, ingawa federal government ilikuwa inaelekeza vingine.

..pia sasa hivi kuna majimbo yamekwenda mahakamani kupinga utaratibu wa Health Care aliopendekeza Obama.

..katika masuala ya kodi, USA yapo majimbo ambayo hayana sales tax na mengine yana sales tax.

..kwa mtizamo wangu bado demokrasia yetu haijakomaa kiasi cha kuweza kuhimili utawala wa majimbo.

..ninachoogopa mimi ni gharama kubwa zinazotokana na mfumo huo, pamoja na kutunishiana misuli kunakoweza kutokea baina ya majimbo, au baina ya majimbo vs serikali kuu.

JokaKuu, sio lazima tufuate Model ya USA, kuna nchi nyingi zinafuata mfumo huo na hakuna mwingiliano wa ki-maslahi kati ya Taifa na Majimbo. Mfano mzuri ni Ujerumani-maswala unayozungumzia ya kodi nk ni mambo ya ki-Taifa na yanamhusu kila raia bila kujali anaishi Jimbo Gani!!
Ndo maana naomba sana jamani viongozi wa Chadema mtuwekee bayana hili jambo hadharani ili tuweze kutembea pamoja!!!!!!
 
vyovyote vile itakavyokuwa, tunachotaka hata kama hakutakuwa na majimbo, basi wakuu wa mkoa wachaguliwe kwa kura, kama vile walivyo ma seneta au magavana wa majimbo. ambacho hatutaki hapa, ni uteuzi wa rais wa chama tawala kwa wakuu wa mkoa na wilaya. wakichaguliwa at least itakuwa bora kuliko. hiki cha mkuu wa wilaya ndo naomba Mungu kiondoke kabisa kwasababu hakina umuhimu zaidi ya kutumika chama badala ya nchi. mkuu wa mkoa akichaguliwa kwa kura, na kupewa mamlaka ya kusimamia vizuri mkoa wake, basi ata kuwa kwenye nafasi nzuri kuuendelea ule mkoa na atakuwa accountable sana kwa mkoa wake. tofauti na hapo anakuwa acountable kwa rais tu, akifanya mchezo anapigwa chini na rais kama hatakuwa ameendeleza interest za chama na rais.
 
Back
Top Bottom