Sera ya Chadema ya "Utawala wa Majimbo"

Subirini muone; kwa uzuri wa sera hii, soon kupitia mgongo wa Katiba Mpya na propaganda nyingine MAGAMBA watai-download, kui-customize then watadai ni yao.

Kinachoudhi sio ku-implement hizo sera za wizi alimradi ni kwa faida ya wananchi na taifa kwa ujumla bali tatizo ni hizo dhihaka, dharau, na kejeli zao dhidi ya waasisi wa wazo husika.

Nashauri CHADEMA waiwekee hatimiliki (copyright) fasta ikibidi CCM wai-copy baada ya ku-acknowledge maana magamba wameishiwa ubunifu kabisa sasa hivi.
 
..naipinga sera ya majimbo.

..itaongeza gharama za utawala nchini.

..italeta migogoro[kutunishiana misuli] isiyo ya lazima kati ya serikali kuu na serikali za majimbo.

..itarudisha nyuma juhudi zetu na mafanikio tuliyoyapata ktk kujenga utaifa wa Tanzania.

..tatizo letu siyo mfumo wa utawala, bali viongozi na watawala wanaotuongoza.

..watetezi wa hoja hii wamejikita ktk malalamiko dhidi ya mgawanyo mbaya wa rasilimali za maeneo mbalimbali. tatizo hilo litatuliwe kwa kuleta formula nzuri zaidi ya mgawanyo na matumizi ya rasilimali zetu, na siyo kutuletea sera za majimbo.
 
kindafu

Asante kwa topic yako, binafsi niliwahi kuanzisha thread ya aina hii yenye heading 'CHADEMA haijajiandaa kuunda serikali' ikaondolewa. Lakini nilitegemea kujadili hasa juu ya sera ya majimbo ambayo CDM inatarajia kuitumia kuunda serikali endapo itafanikiwa kuingia madarakani. Tatizo lililopo kwa CDM hata kama hii sera ni nzuri au la haijulikani wala viongozi hawaiuzi majukwaani, ni bahati nzuri juzi nimemsikia m/kiti wa CDM akiizungumzia bungeni. Lakini hiyo haitoshi wananchi wanapaswa kuelimishwa na kuanza kuizoea jinsi inavyofanya kazi. Thread yenyewe niliyoanzisha ni hii hapa...

CHADEMA haijajiandaa kuunda serikali

Baada ya serikali ya CCM kupoteza imani kwa wananchi Chadema kimeonekana kuwa kimbilio la mwisho kwa wanyonge na wasio wanyonge. Kwa sababu hiyo lazima CDM kitapata wanachama wapya wengi, lakini pamoja na hayo sioni kama CDM kimejiandaa au kinajiandaa kwa ujio huo.

Najua CCM kwa vile wana serikali ina vitengo vingi na uwezo mkubwa hata wa kuwaahidi wanachama wake u-DC nk kitu ambacho CDM hawana. Lakini tunajua CDM ina taasisi yenye muundo wa serikali (serikali ya majimbo), ina vitengo vyake na idara zake kuanzia wilayani, majimboni, mikoani, hadi taifa, kwa hiyo kwa vyovyote vile haiwezi kushidwa kuwa accomodate wageni hasa wanaokuja tayari na CV zao mkononi kama kina Millya.

Lakini cha kujiuliza, CDM kama taasisi, viongozi wa wilaya wako wapi, viongozi wa mikoa ni akina nani, je, sera ya majimbo inaongozwa kwa organs na structure zipi mbona hazijulikani? Chama kama taasisi hakiwezi kukamilika kama hivi vyombo viko dormant vikisubiri ujio wa mtu mmoja (Slaa) kufanya mkutano wa hadhara na kuondoka. Hivi leo nikienda Masasi kwa mfano nimuulize m/kiti wa tawi anaweza kumjua kiongozi wake wa jimbo ni nani? Kama hamjui je CDM wanatekelezaje kwa vitendo sera yao ya serikali za majimbo, au iko vitabuni tu?

What I'm trying to advocate here is that, CDM kipanue wigo wa utawala wake isijibane sana makao makuu, i-practice kwa vitendo sera yake ya majimbo wananchi waanze kuizoea. Hawa wanachama wapya wanaokuja waungane na viongozi wenyeji (of course baada ya kuwa-screened) wagawane hayo majimbo, wajitanabahishe huko kiasi kwamba tukisema jimbo la kanda ya Ziwa kwa mfano tujue nani atakuwa answerable kusimamia uhai wa chama kwa kuanzisha matawi, kuingiza wanachama, kuanzisha miradi n.k. Nafikiri huo ndio mfano mzuri kwa chama kinachojiandaa kushika dola.

Chama hakiongozwi kwa kutegemea head office (ikulu), head office inachotakiwa ni kutoa directives, highest decision-making na support lakini day-to-day activities zinafanywa na na organs zilizo chini yake, lakini kwa CDM the opposite is true, chama ni Mbowe, Slaa, Zitto basi, wanaonekana kana kwamba wao ndio wanaopokea directives na wao ndio wanafanya day-to-day activities.

Chama kinaonekana kama kimepwaya kipo makao makuu na kwa wananchi lakini hapa katikati hakuna kiungo kabisa, wanachama wanaelea elea tu hakuna wa kuwa handle kiasi kwamba siku yeyote wanaweza ku-deflect. Kama bado unapanda majukwaani kuomba watu wajiunge wakati hujajiandaa kuwa accomodate ni uzembe na upungufu wa strategies. Inauma sana chama kama kinapata nguvukazi na kushindwa kuitumia.

CDM wasiishie tu kumfanyia tafrija kubwa Millya na wengine watakaojiunga, wajiandande ni vipi wanatumia hizo nguvu mpya zinazoingia kuimarisha chama na kuandaa makada wake tayari kwa kuongoza serikali. Lakini kama chama kitaendelea kutegemea head office tutarudi kule kule kwa Pinda kutokuwa na uwezo wa maamuzi hadi amsubiri rais arudi toka ziarani.

Luteni.
 
Chadema ina uhakika mkubwa wa kushika Dola katika uchaguzi ujao kama utakuwa kweli huru na wa haki. Naunga mkono Sera yao ya „Utawala wa Majimbo“, na ningependekeza kwamba waiweke hadharani tangu mapema ili iweze kufanyiwa „Pannel beating“ kwenye „Vijiwe“, „Media“, „Mitandao“ na „Forums“ mbali mbali. Wakati mwafaka ukifika wataunda tu kamati maalum kuchambua maoni yatakayokuwa yametolewa na wadau na kutoa kitu kilicho bora - kinachokubalika na kinachowezekana! Ningetamani kwa sasa waainishe bayana yafuatayo:
i. Ni jinsi gani wataigawa Tanzania ki-Majimbo i.e. Majimbo mangapi na mipaka yake ki-Jiografia.
ii. Mfumo wa Utawala utakavyokuwa – ngazi ya Taifa na ngazi ya Jimbo.
iii. Mfumo wa uchaguzi utakaotumika kuwapata viongozi ya Kitaifa na wa Majimbo.
iv. Mipaka ya Utawala/Maamuzi – Kitaifa na katika Majimbo.
v. Mfumo wa Utawala wa Fedha – Kitaifa na katika Majimbo.
vi. Nk, nk, nk,….. – waweza kuongeza vipengele kadiri ya upeo wako!

My Take:
i. Hili litapunguza muda na gharama za „Uelimishaji Umma“ wakati utakapofika.
ii. Itawezesha wanachama wengi zaidi kuifahamu vema sera ya Chama chao na kuweza kuinadi katika ngazi na nafasi zao.
iii. Itawezesha wanachama wanaotamani kuwania nafasi mbali mbali za Uongozi kuanza kujipanga mapema kwa nafasi za Kitaifa na katika Majimbo.
iv. Nk, nk, nk……… Waweza kuongeza!

Naikubali mno hii sera ya Majimbo, kwani italeta chachu ya uwajibikaji na kuharakisha maendeleo
 
Mkuu hii sera ni bomba sana, nchi nyingi duniani zinaitumia. Jimbo linatoa kiongozi mmoja wa juu tumwite Senetor ambaye anakuwa amechaguliwa na wananchi wa jimbo husika, huyu zaidi ya kuwa ni kiongozi mkuu wa jimbo pia ni muwakilishi wa jimbo kwenye bunge la nchi, kama ilivyo sasa, sema jimbo linakuwa kubwa zaidi mfano unganisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Arusha na Manyara kuwa jimbo tuliite Serengeti. Hii ina maanisha kutakuwa hakuna wakuu wa mikoa wala wa wilaya, ila wakurungezi wa manispaa na madiwani ambao wote wanachaguliwa.

Mapato: Majimbo yanatoa asilimia fulani ya pato lake central government ambayo ina jukumu sasa la kusawazisha kwa kuyapa fungu la hela zaidi majimbo yasiyo na uzalishaji mkubwa. Raisi anabaki kuwa amiri jeshi mkuu wa majeshi na majukumu mengine yote. Kunakuwa na baraza la mawaziri lakini dogo sana. Mfano lazima kuwe na waziri wa ulinzi maana majimbo hayawezi kuwa na jeshi lake. Waziri mkuu ndio kama Hilary Clinton vile. Unaweza kuwa na mawaziri wengine lakini wanakuwa hawana kazi sana za kiutendaji maana majimbo yanajiendesha yenyewe na uchumi wa nchi katika mda mfupi unakuwa unapaa

Chama chenye dola ndicho kinaamua sera kuu za nchi na policy za kufuata. Mfano serikali kuu ikisema afya ni bure na bunge likaridhia then kila jimbo halina budi kufuata. Kiufupi inaamuliwa sera zipi ziwe centralized na zipi majimbo yanaweza kujiamulia.

Sera hii inaondoa bureaucracy sana inayotokana na viongozi wa kuteuliwa na mlolongo mkubwa wa mambo usio na tija. Formula zikishawekwa tayari kila jimbo linakuwa na ofisi kubwa na ndogo za TRA na hapa ufanisi unakuwa mkubwa sana maana ofisi hizi zinakuwa na mamlaka
Pax

Very well said and point taken.
 
Last edited by a moderator:
..naipinga sera ya majimbo.

..itaongeza gharama za utawala nchini.

..italeta migogoro[kutunishiana misuli] isiyo ya lazima kati ya serikali kuu na serikali za majimbo.

..itarudisha nyuma juhudi zetu na mafanikio tuliyoyapata ktk kujenga utaifa wa Tanzania.

..tatizo letu siyo mfumo wa utawala, bali viongozi na watawala wanaotuongoza.

..watetezi wa hoja hii wamejikita ktk malalamiko dhidi ya mgawanyo mbaya wa rasilimali za maeneo mbalimbali. tatizo hilo litatuliwe kwa kuleta formula nzuri zaidi ya mgawanyo na matumizi ya rasilimali zetu, na siyo kutuletea sera za majimbo.


Mkuu JokaKuu,
Ungaliiweka hiyo "Sera" mezani ndo ukaanza kuichambua na kuikosoa ningefurahi sana, ila pengine unakosoa bila hata kujua undani wake! Ombi langu kwa viongozi wa Chadema mnaotembelea hili Jamvi - tafadhali tuwezesheni kutembea pamoja!
 
Chadema ina uhakika mkubwa wa kushika Dola katika uchaguzi ujao kama utakuwa kweli huru na wa haki. Naunga mkono Sera yao ya „Utawala wa Majimbo“, na ningependekeza kwamba waiweke hadharani tangu mapema ili iweze kufanyiwa „Pannel beating“ kwenye „Vijiwe“, „Media“, „Mitandao“ na „Forums“ mbali mbali. Wakati mwafaka ukifika wataunda tu kamati maalum kuchambua maoni yatakayokuwa yametolewa na wadau na kutoa kitu kilicho bora - kinachokubalika na kinachowezekana! Ningetamani kwa sasa waainishe bayana yafuatayo:
i. Ni jinsi gani wataigawa Tanzania ki-Majimbo i.e. Majimbo mangapi na mipaka yake ki-Jiografia.
ii. Mfumo wa Utawala utakavyokuwa – ngazi ya Taifa na ngazi ya Jimbo.
iii. Mfumo wa uchaguzi utakaotumika kuwapata viongozi ya Kitaifa na wa Majimbo.
iv. Mipaka ya Utawala/Maamuzi – Kitaifa na katika Majimbo.
v. Mfumo wa Utawala wa Fedha – Kitaifa na katika Majimbo.
vi. Nk, nk, nk,….. – waweza kuongeza vipengele kadiri ya upeo wako!

My Take:
i. Hili litapunguza muda na gharama za „Uelimishaji Umma“ wakati utakapofika.
ii. Itawezesha wanachama wengi zaidi kuifahamu vema sera ya Chama chao na kuweza kuinadi katika ngazi na nafasi zao.
iii. Itawezesha wanachama wanaotamani kuwania nafasi mbali mbali za Uongozi kuanza kujipanga mapema kwa nafasi za Kitaifa na katika Majimbo.
iv. Nk, nk, nk……… Waweza kuongeza!

Kindafu, my take ya nini tena? Ila kama usemavyo nadhani hii ni sawa na ile ambayo ilikuwa enzi hizo (ambayo tulisikia ilikuwepo) ya madaraka mikoani
 
Pax said:
Chama chenye dola ndicho kinaamua sera kuu za nchi na policy za kufuata. Mfano serikali kuu ikisema afya ni bure na bunge likaridhia then kila jimbo halina budi kufuata. Kiufupi inaamuliwa sera zipi ziwe centralized na zipi majimbo yanaweza kujiamulia.
Pax said:
Sera hii inaondoa bureaucracy sana inayotokana na viongozi wa kuteuliwa na mlolongo mkubwa wa mambo usio na tija. Formula zikishawekwa tayari kila jimbo linakuwa na ofisi kubwa na ndogo za TRA na hapa ufanisi unakuwa mkubwa sana maana ofisi hizi zinakuwa na mamlaka


Pax,

..majimbo huwa na mamlaka fulani ktk mambo ya kodi, elimu,sheria etc etc.

..USA kuna majimbo yanayoruhusu hukumu ya kifo na kuna majimbo yanakataa hukumu hiyo.

..yalikuwepo majimbo USA ambayo yalikuwa yamehalalisha segregation na ndoa za weusi na weupe zilikuwa zimepigwa marufuku, ingawa federal government ilikuwa inaelekeza vingine.

..pia sasa hivi kuna majimbo yamekwenda mahakamani kupinga utaratibu wa Health Care aliopendekeza Obama.

..katika masuala ya kodi, USA yapo majimbo ambayo hayana sales tax na mengine yana sales tax.

..kwa mtizamo wangu bado demokrasia yetu haijakomaa kiasi cha kuweza kuhimili utawala wa majimbo.

..ninachoogopa mimi ni gharama kubwa zinazotokana na mfumo huo, pamoja na kutunishiana misuli kunakoweza kutokea baina ya majimbo, au baina ya majimbo vs serikali kuu.
 
..naipinga sera ya majimbo.

..itaongeza gharama za utawala nchini.

..italeta migogoro[kutunishiana misuli] isiyo ya lazima kati ya serikali kuu na serikali za majimbo.

..itarudisha nyuma juhudi zetu na mafanikio tuliyoyapata ktk kujenga utaifa wa Tanzania.

..tatizo letu siyo mfumo wa utawala, bali viongozi na watawala wanaotuongoza.

..watetezi wa hoja hii wamejikita ktk malalamiko dhidi ya mgawanyo mbaya wa rasilimali za maeneo mbalimbali. tatizo hilo litatuliwe kwa kuleta formula nzuri zaidi ya mgawanyo na matumizi ya rasilimali zetu, na siyo kutuletea sera za majimbo.
at least you dont know what you are saying or you are saying the opposite! kila ulichokisema ukweli ni kinyume chake kabisa! yaani mkuu sera ya majimbo hakunaga!
 


Pax,

..majimbo huwa na mamlaka fulani ktk mambo ya kodi, elimu,sheria etc etc.

..USA kuna majimbo yanayoruhusu hukumu ya kifo na kuna majimbo yanakataa hukumu hiyo.

..yalikuwepo majimbo USA ambayo yalikuwa yamehalalisha segregation na ndoa za weusi na weupe zilikuwa zimepigwa marufuku, ingawa federal government ilikuwa inaelekeza vingine.

..pia sasa hivi kuna majimbo yamekwenda mahakamani kupinga utaratibu wa Health Care aliopendekeza Obama.

..katika masuala ya kodi, USA yapo majimbo ambayo hayana sales tax na mengine yana sales tax.

..kwa mtizamo wangu bado demokrasia yetu haijakomaa kiasi cha kuweza kuhimili utawala wa majimbo.

..ninachoogopa mimi ni gharama kubwa zinazotokana na mfumo huo, pamoja na kutunishiana misuli kunakoweza kutokea baina ya majimbo, au baina ya majimbo vs serikali kuu.
kwa taarifa yako mfumo wa majimbo ni rahisi sana kuliko wa sasa ila kuliona hilo inategemea na orientation yako maana rahisi is subjective.aidha mfumo wa majimbo utasaidia sana kukuza demokrasia.aidha kutunishana misuli kutasaidia sana kuwa na serikali makini na imara na pia itaongeza uzalendo wa kuipenda na kuilinda nchi yetu kutoka maadui wa nje
 
kwa taarifa yako mfumo wa majimbo ni rahisi sana kuliko wa sasa ila kuliona hilo inategemea na orientation yako maana rahisi is subjective.aidha mfumo wa majimbo utasaidia sana kukuza demokrasia.aidha kutunishana misuli kutasaidia sana kuwa na serikali makini na imara na pia itaongeza uzalendo wa kuipenda na kuilinda nchi yetu kutoka maadui wa nje

Admiral Elect,

..watu watayapenda majimbo na siyo taifa.

..kutunishiana misuli kutasababisha maendeleo kukwama, na siyo demokrasia.

..wenye majimbo na wakafanikiwa ni wale ambao hawana makabila na hawasumbuliwi na mambo kama udini wa hapa kwetu.
 
Admiral Elect,

..watu watayapenda majimbo na siyo taifa.

..kutunishiana misuli kutasababisha maendeleo kukwama, na siyo demokrasia.

..wenye majimbo na wakafanikiwa ni wale ambao hawana makabila na hawasumbuliwi na mambo kama udini wa hapa kwetu.
ndiyo watayapenda sana majimbo na halafu wataipenda zaidi nchi yao maana upendo ni mbegu ikishaota huzaa matunda mengi zaidi. NB charity begins at home!
misuguano huleta maendeleo na kukuza demokrasia maana wtu wataipractise at their own local areas. NB ukiona vinaelea ujue vimeundwa
hakuna nchi duniani isiyo na makabila! nchi hii hii haina udini ila kuna wajinga wachache wanaowafitini watanzania kwa manufaa yao ya kisiasa .NB divide and rule!
 
ndiyo watayapenda sana majimbo na halafu wataipenda zaidi nchi yao maana upendo ni mbegu ikishaota huzaa matunda mengi zaidi. NB charity begins at home!
misuguano huleta maendeleo na kukuza demokrasia maana wtu wataipractise at their own local areas. NB ukiona vinaelea ujue vimeundwa
hakuna nchi duniani isiyo na makabila! nchi hii hii haina udini ila kuna wajinga wachache wanaowafitini watanzania kwa manufaa yao ya kisiasa .NB divide and rule!

Admiral Elect,

..model unayoizungumzia wewe ni ya wapi??

..mimi naangalia USA na kinachoendelea kwao nadhani kikiletwa Tanzania tutasambaratika muda si mrefu.

..USA mwizi akiiba gari New Jersey halafu polisi wakianza kumfukuza, akiweza kuingia New York polisi hao inabidi wamuache na badala yake wawasiliane na polisi wa New York ili mwizi huyo aweze kukamatwa.

..pia kuna majimbo ya USA mfano California wameruhusu ndoa za ushoga, na wanataka kuvuta bangi, majimbo mengine ya USA yamekataa.

..I feel like the system ur proposing is too complicated and we will just be bogged down in trying to make the system work rather than kushughulikia matatizo ya wananchi.

NB:

..
 
Admiral Elect,

..model unayoizungumzia wewe ni ya wapi??

..mimi naangalia USA na kinachoendelea kwao nadhani kikiletwa Tanzania tutasambaratika muda si mrefu.

..USA mwizi akiiba gari New Jersey halafu polisi wakianza kumfukuza, akiweza kuingia New York polisi hao inabidi wamuache na badala yake wawasiliane na polisi wa New York ili mwizi huyo aweze kukamatwa.

..pia kuna majimbo ya USA mfano California wameruhusu ndoa za ushoga, na wanataka kuvuta bangi, majimbo mengine ya USA yamekataa.

..I feel like the system ur proposing is too complicated and we will just be bogged down in trying to make the system work rather than kushughulikia matatizo ya wananchi.




si lazima tuige USA ghana na china kuna mfumo wa majimbo pia! swala la kuruhu kitu ambacho jamii fulani inakiona ni sawa ndo demokrasia na uhuru.because what is goog to you might not be the case to me! kama italazimu kubomoa ili kujenga nyumba imara zaidi mimi sina shaka wala nongwa, remember the grain of wheat?
 
Admiral Elect said:
si lazima tuige USA ghana na china kuna mfumo wa majimbo pia! swala la kuruhu kitu ambacho jamii fulani inakiona ni sawa ndo demokrasia na uhuru.because what is goog to you might not be the case to me! kama italazimu kubomoa ili kujenga nyumba imara zaidi mimi sina shaka wala nongwa, remember the grain of wheat?

Admiral,

..unaweza kutueleza Ghana na China mfumo wao wa majimbo unafanya vipi kazi??

..naomba utupe mifano ktk masuala kama kodi, mahakama na sheria, vyombo vya ulinzi kama Polisi etc etc.

..Nigeria wanayo majimbo lakini sidhani kama mambo yao ni mazuri sana.
 
Sera ya majimbo inafaa kwa mataifa makubwa yenye ardhi kubwa na population kubwa, mathalani nchi kama ya china yenye eneo mara kumi ya eneo la nchi yetu wamegawa majimbo ambayo baadhi ya majimbo ni makubwa kuliko nchi yetu, sasa kwa nchi kama ya tanzania ambayo ukubwa wake ni sawa na majimbo katika nchi za wenzetu sioni sababu ya kuigawa zaidi. Mimi naamini tanzania hii hii ikiwa chini ya serikali kuu inaweza kufanya vizuri iwapo sababu za kutofanya vizuri zitafanyiwa kazi.

kWA NCHI AMBAYO BADO INAFANYA JUHUDI KUPAMBANA NA UDINI NA UKABILA Kuigawa nchi katika majimbo ni kukaribisha sumu za " udini" kwenye maeneo yenye watu wengi wa dini moja, ni kukaribisha ukabila kwenye watu wengi wa kabila fulani.

Majimbo yatafaa tu iwapo east africa itakuwa nchi moja otherwise, tanzania kwa eneo lake hili na idadi ya watu wake bado inatawalika vyema na maendeleo kupatikana bila kuwepo kwa serikali za majimbo iwapo kanuni za maendeleo zinazingatiwa.
 


Admiral,

..unaweza kutueleza Ghana na China mfumo wao wa majimbo unafanya vipi kazi??

..naomba utupe mifano ktk masuala kama kodi, mahakama na sheria, vyombo vya ulinzi kama Polisi etc etc.

..Nigeria wanayo majimbo lakini sidhani kama mambo yao ni mazuri sana.
Mkuu nilidhani ya china na ghana ni homework yako? kwa nigeria ni mfumo wa majimbo ambao umesaidia angalau kufika hapo ilipo sasa vinginevyo ingeshagawanyika vipande 3
 
Sera ya majimbo inafaa kwa mataifa makubwa yenye ardhi kubwa na population kubwa, mathalani nchi kama ya china yenye eneo mara kumi ya eneo la nchi yetu wamegawa majimbo ambayo baadhi ya majimbo ni makubwa kuliko nchi yetu, sasa kwa nchi kama ya tanzania ambayo ukubwa wake ni sawa na majimbo katika nchi za wenzetu sioni sababu ya kuigawa zaidi. Mimi naamini tanzania hii hii ikiwa chini ya serikali kuu inaweza kufanya vizuri iwapo sababu za kutofanya vizuri zitafanyiwa kazi.

kWA NCHI AMBAYO BADO INAFANYA JUHUDI KUPAMBANA NA UDINI NA UKABILA Kuigawa nchi katika majimbo ni kukaribisha sumu za " udini" kwenye maeneo yenye watu wengi wa dini moja, ni kukaribisha ukabila kwenye watu wengi wa kabila fulani.

Majimbo yatafaa tu iwapo east africa itakuwa nchi moja otherwise, tanzania kwa eneo lake hili na idadi ya watu wake bado inatawalika vyema na maendeleo kupatikana bila kuwepo kwa serikali za majimbo iwapo kanuni za maendeleo zinazingatiwa.
admiral elect can not respond to this msg! it is below army standards!
 
Somo linahitaji tuition na juhudi ya kutosha ktk kwa mwl.mda hautoshi ila tusichelewe sn.ni hayo 2.
 
Back
Top Bottom