Imefika saa 8:30 usiku mhudumu wa hoteli amekuja kuginga mlango wa chumba changu, akaniambia nitoke nje kuna watu wa sensa wananihitaji, nikawaambia kwa muda huu siwezi kutoka waje asubuhi, nikakomea mlango nikarudi kulala, inawezekana hawakuridhika na majibu yangu mhudumu akarudi tena kugonga mlango tena mara hii kwa nguvu kweli sikuweza kufungua, nikaona hali iko hivyo kwa vyumba vya jirani wanagongewa hawafungui, si mmoja wa waliogoma lakini kwa style na muda wenyewe nililazimika kutotoa ushirikiano, niliwaambia warudi asubuhi mpaka muda huu nimeamka sijaona dalili kama kweli wanaweza kurudi kuja kutuhesabu tena, wewe ni zipi changamoto zimekupata kwa zoezi hili la sensa lililoanza saa 6:01 usiku?