Sensa 2012: Yanayojiri

Kwa uzoefu wangu humu ndani, kwenye hicho kipengele cha mwisho Mkandara angekujibu: Msiwalazimishe waislam wafanye kama wakristu(kusign MoU). Huku ni kuhalalisha dhambi ileile wanayofanya wakristu. Kinachotakiwa ni serikali kujitoa kwenye makubaliano na vyombo vya dini, ijenge shule nyingi, hospitali na kutoa huduma nyingine za jamii vizuri.
Maskini yeye hajui ni serikali ndiyo inayolinyemelea Kanisa linapotoa huduma za jamii ambapo serikali haifiki.
Juzijuzi imefunguliwa hospitali ya kanisa katoliki nadhani ni arusha kama sikosei. Kilichosababisha kujengwa kwa hiyo hospitali ni baada ya askofu kuona wanakijiji wanateseka sana especially wakina mama wajawazito kwa kukosa huduma ya hospitali. Pinda alikuwepo na akaahidi serikali itatoa gari la wagonjwa. Mkandara and co watakuambia huo Mfumo Kristo.Waislam wanadhulumiwa. Wenyewe hawataki kuchangia kuanzisha miradi ya maana kama hii , wanachoweza ni kuchangia radio za uchochezi na mabango ya kugomea sensa kama tulivyoona alivyofanya msomi mkubwa Ibrahim Lipumba. Wanataka serikali ifanye kila kitu. Serikali haiwezi. Kanisa linaanzisha miradi. Serikali inanyemelea. Watu wanasema Mfumo Krisu. Waislam tunadhulumiwa. Tuweke kipengele cha dini ili ionekane tuko wengi tugawane madaraka sawa na wakristu nk
Mkuu sooth, hilo swali la mwisho linaweza likakufanya ukeshe na Mkandara hapa.
 
Maswali mengine sio lazma akuulize na kuna makarani wa dodoso fupi na refu!
 
Sijui ni option pia, na ipo kwenye dodoso. Au wewe ulitakaje, wakufuate ulipoenda?

Kubwa zima halioni aibu kusema linakaa kwa kakaake. Akili za kula bure bwana
Mkuu,hiyo ni nyumba ya familia ambayo nimeijenga mimi.Huenda kule weekend tu.Karibu kwangu Mikocheni B Mkuu...
 
Nimepatwa na mshangao!

Hii Sensa ya mwaka huu kweli tutapata takwimu sahihi? Hebu naomba mnaoshiriki Ku-sensisha watu mnisaidie! Hivi mlielekezwa kwamba msipokuta watu wazima hata watoto wanaweza ku-sensiwa? Nyumbani kwangu binti yangu wa miaka 7 amejibu maswali ya Sensa - Big up my daughter - una akili kama mpaka watu wa sensa wanaridhika na majibu yako?!!.

Sasa najiuliza kama na huko vijijini ndo hali itakuwa hii tutapata takwimu sahihi kweli? Angalau mtoto wa mjini unaweza kusema ana ujasiri wa kujieleza sasa huko vijijini wataweza? Nahitimisha kwa kusema "SENSA HII NI BURE KABISA" ninazidiwa na sensa zinazofanywa kwa Wakimbizi. Bora tusiwe na zoezi hili linalokula pesa yetu na kutupa takwimu za hovyo!
 
Ndugu Job K, Utafiti wa kuwa Mtoto/watoto wa kijijini hana/hawana ujasiri wa kujieleza kuliko wa mjini wewe umeufanyia wapi?
 
Kama ni katika mojwapo ya nchi za wenzetu walioelimika na kustaarabika, muda huu utaratibu wa kuwawajibisha wote waliohusika kulifanya zoezi la sensa kuwa la ovyo na la kipuuzi kama liliyvo ungekuwa umeshika kasi.

Vifaa hakuna, wasensishaji wanaomba rushwa kusensisha, baadhi ya waislam wamegoma kusensiwa, kutokuwa na standard coordination from top-bottom nk nk

How could they turn the sensitive thing like sensus becoming a public mockery and a plain comedy show! Someone should be held full accountable and NOW!
 
kwanza kuna maswali mengine nadhani huwa wanajitungia wenyewe hapo hapo. halafu sometimes wanaboa, eti kama mimi aliniuliza elimu yangu nikamwambia chuo kikuu, badae akaniuliza naongea lugha ngapi nikamwambia mbili na ya kwetu ya tatu. akaniuliza hizo mbili ni kiingereza na kiswahili? nikamjibu ndiyo, akaniambia ni kweli au unanidanganya? nikamwambia nakudanganya sijui kiingereza (manake niliboreka) sasa sijui alijaza nini. Haya Mr. hakuwepo, akamuona mtoto mmoja mwingine alikuwa kalala, eti baba yake ni mtanzania, nikamwambia ndio, mbona huyo mtoto kama shombe? na wakati mtoto ni mweusi (mimi ni mweupe sana) bora angekuwa amefuata hata huo weupe wangu, nikamwambia kalete DNA test na mtafute babake uwapime! In short mambo ya kuboa yalikuwa mengi. nitakesha nikiyaandika.
 
Ningemjua huyo mtoto wako ningempongeza maana kaonyesha ujasiri na ukomavu wa kiakili kuliko watu wazima ambao waliambiwa wahesabiwe wakagoma. Watoto kama hao ndo wanastahili kuwa vichwa vya familia hata kama Baba zao wapo home.
 
Hayo ya lugha mbona wengine hatukuulizwa? Mtaalam wa sensa atusaidie kwa hili...
 

sensa hii ni bure kabisa!!
 
Hayo ya lugha mbona wengine hatukuulizwa? Mtaalam wa sensa atusaidie kwa hili...

Unajua ndo maana ndugu zangu wa Iringa walisema sensa isije ikahatarisha ndoa zao!!!!! hapo kwa mtoa maada najua aliyeuliza alikuwa na lake jambo ndo maana alikuwa analeta viswali vya kizushi akijua atamvuta bibie... upumbavu mtupu
 
Ndugu Job K, Utafiti wa kuwa Mtoto/watoto wa kijijini hana/hawana ujasiri wa kujieleza kuliko wa mjini wewe umeufanyia wapi?

Ndugu kuna watu wazima tena siyo watoto maeneo ya vijijini bado wapo katika hali ya woga nakutoelewa kinachoendelea.

Akifika mgeni watu wanamshangaa au kumkimbia kwa hofu, sembuse watoto ukamuulize maswali akujibu THUBUTUUUUUUUUUUUU!!!!!!!

Tunaomba wahusika na kuhesabu watu (SENSA) watumie busara na siyo ili kutimiza wajibu wa kuzunguka mitaani) Hapa mnaweza kutupa wasiwasi hata kuweza kujaza takwimu zauongo katika makaratasi ya sensa. Na mwisho wa siku kwenda kukinga mshiko!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Bottom Line, usipohesabiwa hutapiga kura 2015-JMakamba
 
Mkuu wangu paragraph yako ya kwanza inajieleza vizuri sana na jibu lake linapatikaa paragraph ya pili.. Unaposema shule ya St Sebastin ni ya Wakristu ina maana tayari serikali imewapa kibali hawa wenye shule hiyo (kwakristu) kujihusisha ktk shughuli za maendeleo. Ni kutokuwa na takwimu hizi ndio maana muafaka wa Muo Uliundwa, ni kutokana na takwimu hizi ndio maana mnawakatalia waislaam kujiunga na OIC ama hata kuwarudishia shule zao kama mlivyorudishiwa wakristu na hata kuwa sehemu ya serikali ktk kuendesha shughuli za Elimu na Afya. Wewe nambie imekuwaje leo serikali imeingia muafaka na dini ya Kikristu kuendesha Elimu na Afya ikiwa huamini ktk utengano wa kiimani?.. Je hizi sio shughuli za maendeleo ambazo mnaiweza sensa hii...

Na unapozungumzia umiliki usio kuwa wetu hapo ndipo swala la umuhimu wa matabaka haya linapoingia. Kutokana na mfumo kristu ndio maana kila mahala mnatumia neno sisi hatuoni sababu! ya kwamba nyie ni watu tofauti na sisi na kwa dini yenu.Hili neno SISI, kama sio tabaka nyie ni kina nani? ina maana Wakristu wanakataa hoja ya Waislaam! hivyo tayari mnaonyesha jinsi mnavyotawala nchi hii kiasi kwamba mmefikia kufanya maamuzi juu ya Waislaam na kujipa mashule ambayo yalikuwa milki ya serikali.

Hao waliomwita Mufti Kafir (asiyeabudu Mungu) ni swala la kuwauliza wao ni vigezo ni gani wametumia kuwaita makafir. Lakini naweza tu kusema ya kwamba unapomkwaza binadamu mwingine ukamnyma Uhuru wake, ukaondoa usawa baina yao kwa kushindwa kuwapa haki yao huu ni Ukafir maana humwogopi Mungu. Kwa hiyo JK na hao kina Mufti wanaweza kabisa kuondoka ktk Uislaam wanapotumia nyadhifa zao kuwakwaza wananchi. Labda nikwambie hata jinsi JK na CCM inavyowakwaza wananchi hata Kuandamana huu ni Ukafir. Elewa hakuna society ama kundi la watu wanaoitwa Waislaam maana hii ni dini sio kabila bali ni imani na wanaofuata ibada zake tu ndio huitwa Waislaam sio kutiwa maji. Kitendo cha kuua watu wanaoandamana kinakuondoa ktk Uislaam haijalishi wewe unasali mara ngapi msikitini. Uislaam unafundisha kutoa haki sawa kwa binadamu wote, na usimtendee mwenzako vile usivyopenda wewe utendewe.

Ni kosa kumwita binadamu mwenzako Kafir kwa sababu anayejua thamani ya ibada zetu ni Mwenyezi Mungu pekee, hawa watu wanafanya makosa sawa na wale wanaojiita walokole kwani ni Mungu pekee anayejua nani kaokoka.. binadamu hawezi kujipa daraja la kuokoka ama Usaint isipokuwa Mwenyezi Mungu ndiye anajua nani saint, hivyo wasamehe hawa watu kutokana na hasira zao kunyimwa haki.. Hii sensa pekee imenionyesha nchi yetu ina wenyewe. Na wenyewe ndio kina nyie mnaotupanga ktk mafungu mnavyopenda nyie mkiepa ukweli pale mnapoona utabainika.
Na kuhusu kuwatambua watu kwa dini zao ni sawa kabisa na mkulima kwani atabeba jembe begani anapojiandikisha?..Au mwanamke atavua nguo ili uhakikishe kama mwanamke..maswali mengine bana.
 
Hatimaye mimi pamoja na wana kaya yangu tumehesabiwa jioni hii. Mapungufu niliyoyaona katika zoezi zima (makarani kutokuwa na dodoso-wameniambia ni kaya ya 20 wanaandika data zetu katika daftari la kawaida katika siku ya leo; watahamishia katika dodoso wakiletewa kesho au kesho kutwa; kutokuwepo viongozi wa mitaa kuongoza makarani na uchelewaji wa kuanza kazi kwa makarani) vyote vinaashiria kupata taarifa zisizokuwa sahihi mwisho wa zoezi zima la sensa.

Wahusika mnaosoma maoni yetu JF ONENI MAPUNGUFU HAYA NA MAREKEBISHO MAPEMA ILI ZOEZI ZIMA LA SENSA LISIJEKUWA SENSELESS!!!
 

Afadhali Mkuu Mizambwa umenisaidia!

Eti nilikuwa nimeulizwa utafiti nimeufanyia wapi? Tumb..ff Kabisa! Watu tunafanya kazi vijiji mkienda wageni watu wanapanda juu ya miembe na huku nyuma wamewaambia watoto wakiuliza semeni hatupo. Kisa? Wameogopa maswali ya Kiswahili.

Sasa mtoto wa miaka saba atajibu nini? Mara ngapi tumewauliza watoto wa vijijini umezaliwa tarehe ngapi? Hawezi lakini ukimwuuliza mtoto wa mjini anakujibu? Ila hii ya Sensa mpaka sasa hivi sijaamini? Kuna swali lile la kujua lugha gani za kusoma, kuandika na kuzungumza sasa hapo mama watoto kwa vile hakuwapo amejaziwa nini? Hawa jamaa busara ni ZERO kabisa!!
 

kazi ya kuhesabu watu ni ngumu sana lkn inatakiwa mtu ahojiwe mwenyewe hasa kwa wanawake wenye umri kuanzia miaka 12 au zaid lkn makarani wanachoka sana kuja kurudia rudia mana wana kaya wanakua ni wasumbufu hawakai majumbani mwao.

Sasa makarani wanachokifanya ni kumuhoji atakae kuepo tu hata kama ni jirani yako akikubali kukujibiwa maswali yako wao wanamuhoji na kuelekea mbele. Inabidi muvumilie au inabidi musiondoke majumbani mwenu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…