Zimmermann
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 4,045
- 3,603
Kwa uzoefu wangu humu ndani, kwenye hicho kipengele cha mwisho Mkandara angekujibu: Msiwalazimishe waislam wafanye kama wakristu(kusign MoU). Huku ni kuhalalisha dhambi ileile wanayofanya wakristu. Kinachotakiwa ni serikali kujitoa kwenye makubaliano na vyombo vya dini, ijenge shule nyingi, hospitali na kutoa huduma nyingine za jamii vizuri.Kaka, toka nimejiunga na JF, nimekufahamu kama mtu ambaye yuko objective, sijawahi kushawishika kuhoji msimamo wako ktk masuala mbali mbali, wala sitaanza leo.
Nimesoma post zako ktk hii thread, sikushawishika kuhoji kwasababu nilielewa mantiki yako hata kama siamini unachokisema kwa 100%. Maoni yangu niliyaelekeza kwa Ritz kutokana na msimamo wake.
Nikirudi ktk hoja zako; nani mwenye jukumu la kutoa takwimu? Kwa mujibu wa JK, NBS pekee ndio wenye mamlaka ya kutoa takwimu. Serikali ina uwezo wa kumuzuia mtu au taasisi yoyote kutoa takwimu ikiwemo mimi na wewe hapa kwenye mtandao?Kuna ugumu kidogo..
Hakuna mahali ktk post yangu niliposema kipengele cha dini kisiwekwe. Wacha kiwekwe tu, pamoja na vipengele vingine kama kabila, sexual orientation, n.k. Nisichopenda ni kuona hii ndo inafanywa kuwa "ishu" ya liwalo na liwe! Ushauri: Rais ni msikivu, viongozi wa kiislamu wakaongee naye. Ukimpa rais ultimatum unamfanya awe defensive. Hao wanaopata ruzuku ktk afya na elimu nao waligomea sensa? Hizi harakati na "fujo" ndizo zinafanya uislam uwe na image mbaya.
Viongozi wa kislamu wamefikia wapi ktk kudai mkataba na serikali toka Rais atamke akiwa dodoma kwamba hawajaomba wakati "wenzao" waliomba?
Maskini yeye hajui ni serikali ndiyo inayolinyemelea Kanisa linapotoa huduma za jamii ambapo serikali haifiki.
Juzijuzi imefunguliwa hospitali ya kanisa katoliki nadhani ni arusha kama sikosei. Kilichosababisha kujengwa kwa hiyo hospitali ni baada ya askofu kuona wanakijiji wanateseka sana especially wakina mama wajawazito kwa kukosa huduma ya hospitali. Pinda alikuwepo na akaahidi serikali itatoa gari la wagonjwa. Mkandara and co watakuambia huo Mfumo Kristo.Waislam wanadhulumiwa. Wenyewe hawataki kuchangia kuanzisha miradi ya maana kama hii , wanachoweza ni kuchangia radio za uchochezi na mabango ya kugomea sensa kama tulivyoona alivyofanya msomi mkubwa Ibrahim Lipumba. Wanataka serikali ifanye kila kitu. Serikali haiwezi. Kanisa linaanzisha miradi. Serikali inanyemelea. Watu wanasema Mfumo Krisu. Waislam tunadhulumiwa. Tuweke kipengele cha dini ili ionekane tuko wengi tugawane madaraka sawa na wakristu nk
Mkuu sooth, hilo swali la mwisho linaweza likakufanya ukeshe na Mkandara hapa.