Kweli?
Waislamu wanakatazwa kula mbuzi wa Vatican (kitimoto). Sisi Wagalatia huku tunakatazwa kula nini? Labda Wasabato wanaoshikilia baadhi ya visheria uchwara vya Musa mf. kutokula samaki wasio na magamba, wanyama wasiocheua, wasio na kwato/miguu iliyopasuliwa, nyamafu, kitimoto n.k.
Kihistoria Wachina walishapata njaa kadhaa wakapukutika kweli kweli. Hata majuzi tu hapa wakati wa mapinduzi ya Mao waliteketea sijui milioni mia ngapi sababu ya njaa. Inasemekana walijifunza kula karibu kila kitu katika hekaheka hizi.