pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 249
- 489
Itakuwa ni kama risk allowance maana wale wenzetu wameruhusiwa kula kwa urefu wa kamba na pia ita discourage wahitimu kujazana Internet cafe ku apply ajira za utumishi ambazo hazikidhi soko..Sasa kukatwa kodi ndogo itakua ni suluhu ya kitu gani hapa mkuu?
Mmmmmh??? OkItakuwa ni kama risk allowance maana wale wenzetu wameruhusiwa kula kwa urefu wa kamba na pia ita discourage wahitimu kujazana Internet cafe ku apply ajira za utumishi ambazo hazikidhi soko..
Pangani shehe karibu dagaa wa uwonoUna hoja nzuri ulitaka kuiweka ila vichambo vimezidi.. Kwenu Tanga au pwani?
Huyu ni wa Musoma kabisa.Una hoja nzuri ulitaka kuiweka ila vichambo vimezidi.. Kwenu Tanga au pwani?
Lakini sekta binafsi si ndiyo mnalipwa pesa ndefu.Wasaaalam wana jukwaa, leo katika pita pita zangu za mjini nilienda ofisi moja ya muhimu sana, nikakuta watumishi wako muda wa mapumziko, nilifanikiwa kuchangamana nao na kujadili mawili matatu, nilimsikia mmoja akisema kwamba amemaliza kusoma na hataki tena (training) ya aina yoyote kwa maana mpaka sasa bado hajapanda daraja, na akasema kwamba anataka ahamie sekta binafsi wenzake wakaanza kumpinga kwa maneno makali kuwa kule sekata binafsi hakuna usalama wa ajira (job security), wakaendelea kusema kuwa kule ukiiba kidogo tu unafukuzwa nikajiuliza maswali mengi sana mpaka nikajua kuwa siye tuliopo sekta binafsi tume risk kwani ajira zetu zipo mikononi mwa waajiri hivyo kama hauna misuli ya kusimamia sheria ya mahusiano kazini basi ajira yako inaweza kuisha kizembe tofauti na wale wenzetu wanaovaa jeans na vitenge na walioruhusiwa kula urefu wa kamba zao yaani watumishi wa umma...baada ya kufikiria nikaona nije na wazo kuwa kiasi cha kodi tunachokatwa sekta binafsi kiwe na nafuu kidogo ukilinganisha na hawa ndugu zetu wenye ajira za kudumu ambao wameambiwa kuwa wale kidogo wasile mpaka wakavimbewa wanaovaa kama wasabato na majibu ya hovyo maana wanajua utaratibu wa kuwaondosha kazini ni mgumu ama hauwezekani...naomba kuwasilisha
Hakuna mkoa unaoitwa musoma labda kama unamaanisha mara ...jitahidi usitutoe kwenye madaHuyu ni wa Musoma kabisa.
Ukifika Dar kuna chuo kinaitwa CBE kinatazamana na zilipokuwa ofisi za wizara ya kazi ambapo pembeni kuna afisi ya usuluhishi "Centre for mediation and abitration" (CMA) nenda pale utasikia kesi zote ni za sekta binafsi watu wanalalamikia unfair termination...sasa kwa nini watu hawa wawe na kodi sawia na wale walioruhusiwa kula kwa urefu wa kamba?Lakini sekta binafsi si ndiyo mnalipwa pesa ndefu.
Kweli kabisa ila na wewe ukaendelea kuchangia mada ya mtu aliyechanganyikiwa na pombe ...yaani chizi kaiba nguo zako wakati unaogelea na wewe ukamfukuza sasa sijui chizi ni nani hapo..Mtoa mada unaonekana kama vile pombe imekuchanganya.
Achana na kauli ya raisi pengine kila mmoja ana tafsiri binafsi. Lakini ukweli ni kwamba sekta ya umma maslahi ni kiduchu Sana. Na ukijaribu kuishi kwa muktadha wa raisi ukosefu wa ajira una kuhusu.Ukifika Dar kuna chuo kinaitwa CBE kinatazamana na zilipokuwa ofisi za wizara ya kazi ambapo pembeni kuna afisi ya usuluhishi "Centre for mediation and abitration" (CMA) nenda pale utasikia kesi zote ni za sekta binafsi watu wanalalamikia unfair termination...sasa kwa nini watu hawa wawe na kodi sawia na wale walioruhusiwa kula kwa urefu wa kamba?