Seif al Islam ni mtoto wa kiongozi wa Libya aliyepinduliwa. Kijana huyu alikamatwa na wapiganaji wa koo na kukabidhiwa kwa majeshi ya serikali ya mpito ya Libya. Tangu akamatwe kijana huyu takribani mwaka mmoja sasa hajafikishwa mahakamani wala kufunguliwa mashitaka. Anateswa sana gerezani kwa mfano wamemkata vidole vyake 3 vya mkono, anashikiliwa sehemu ya pekee bila hata kuonana na ndugu zake wala mwanasheria wake, anaumwa na wala hana nafasi ya kuonana na daktari na mateso mengi ambayo si yakibinadamu.
Hivi hawa watetezi wa haki za binadamu mpo wapi? The Hague ipo kwa ajili ya nani? Inasikitisha sana. Seif ni mtuhumiwa tu bado hajatiwa hatiani na mahakama yoyote hivyo anastahili kuheshimiwa utu wake.
Hivi hawa watetezi wa haki za binadamu mpo wapi? The Hague ipo kwa ajili ya nani? Inasikitisha sana. Seif ni mtuhumiwa tu bado hajatiwa hatiani na mahakama yoyote hivyo anastahili kuheshimiwa utu wake.