Sehemu za kutembelea hapa Dar

Sehemu za kutembelea hapa Dar

Kama unaweza jaribu camping siku 1 utaenjoy. Fanya na marafiki cost sharing, haizidi elfu 80 hapo hadi kula, hiking, camping, boat, yaani alot utaenjoy madam.
Hebu anaetaka camping aje PM twende sio lazima awe KE hata mkiwa ME fresh tu

tuwe mtu 4 twendeni hii coming weekend Jumapili, Mad Max hebu nielekeze

mgeni ninaetokea Hapa Mbezi Mwisho,nielekeze napita njia ipi hadi nifike nipe idea idea

halafu ntajazia jazia nyama na Google Map,Last sunday niliboeka kinoma ikabd nifanye tour ya kuzunguka Dar nzima kuhakikisha tu ule mshale wa mafuta unatoka kwenye full unainama kidogo,ndio ikawa mwisho wa tour yangu.

Jumapili ijayo nataka nijaribu tena huko...
 
Pamoja sana. Unaweza kwenda day trip. Itakua chini ya elfu 20 kwa mtu ila mkiwa wengi inakua cheap. Bei zipo hivi:
  • Kiingilio 2500 (kwa mtu),
  • Hela ya guide 20,000 (guide mmoja anahudumia watu 10 so mkienda 10 kila mtu anachangia elfu 2 so better mkiwa crew)
  • Boat elfu 10 (sio lazima)
  • Ukitaka camp tent zipo za 15,000 (maximum watu 4) na zipo kubwa za 40,000 izo ata watu 10.
  • Ukienda na camera kubwa unailipia elfu 5, drone 50,000 ila nadhani hautaenda nazo.
  • Ndani hamna vyakula (ila wameanza kutengeza mahala pa kula) so nunua bites na vinywaji nje.
  • Gari kuingia elfu 5 ila ukipaki nje free.
Washkaji wakarimu sana pale yaani wako peace knm. Utaenjoy sana boss.

Hapa Hiking on top kabisa unakua unaiona Dar kwa chini. Wamejenga ngazi sahivi kupanda rahisi.

View attachment 2391100

Hapa chini camping pembeni mwa bwawa.
View attachment 2391103


PS: Gharama naweza kua nimekosea kidogo sana. Ila zinaenda humo humo.
Bei zao nzuri sana and very fair.
Napenda sana adventure za hivyo
Nimependa option ya kwenda na msosi wako as najifungashia wa kutosha
Kuna kuogelea?

Lavit njoo uone mambo yako
 
Wale wanaoenda ushoroba nakumbusha msisahau kubeba camping mattress ya dharula, pod tent wanazo, unaweza beba camping stove ndogo maana unaweza andaa chakula mwenyewe hukohuko vile simple, anyway pametulia sana nililala mara moja nilitoka akili ikiwa mpya,
 
Zifuatazo ni Beach Safi,maji Safi na privacy kubwa katika visiwa vya Dar

-Sinda -kigamboni,panda boti kutokea barakuda au Kipepeo hotel Nauli
20,000(go return) msipungue wanne.

-Bongoyo- Nauli boti 30000 (go-return)
Misitu na sauti za ndege na fukwe za zisizo na watu wengi (pandia boti Msasani Slipway)

-Mbudya-Nauli 10000 ( go+return)
(Beach zote hizo utalipa 10000 kiingilio)/mwanafunzi 5000)
uzuri wake hizo fukwe hiyo pesa utaona ndogo(Hiki ni kisiwa wanakopenda kutembelea wasanii,Wafanyakazi wa kampuni za kimataifa,wanafunzi wa vyuo)
-ukiwa na hema lako unalala huko 54,000

Funguyasini - Hiki kisiwa ambacho unaweza kusema "mchanga unaelea juu ya maji" Si kwamba unaelea ila ukiipeleka familia yako huku watafurahi na hawatasahau hio trip.-Pandia boti Whitesand hotel utasimulia hutaamini uko Tanzania hii,ni zaidi ya Maldives watoto watacheza na ndege hapo utafurahi mwenyewe,kisiwa kipana sana mchanga tupu maji ya kwenye ugoko,kifua,magoti watoto watacheza bila hofu yeyote

Kumbuka beach dress ili ufurahi zaidi bukta,pensi,T-shirt or beach shirt,vest,sandals ambazo zikiloa maji hazina shida,miwani Kama utapenda kwa sababu ya mchanga mweupe,kofia
 
Mmh uku ndo walishoot MOVIE YA BWAWA LA SHETANI kila la kheri wakuu
Mnh naona unatupia ndoa ki dizian flani hiviiii.... Ila nimekue
Hebu anaetaka camping aje PM twende sio lazima awe KE hata mkiwa ME fresh tu

tuwe mtu 4 twendeni hii coming weekend Jumapili, Mad Max hebu nielekeze

mgeni ninaetokea Hapa Mbezi Mwisho,nielekeze napita njia ipi hadi nifike nipe idea idea

halafu ntajazia jazia nyama na Google Map,Last sunday niliboeka kinoma ikabd nifanye tour ya kuzunguka Dar nzima kuhakikisha tu ule mshale wa mafuta unatoka kwenye full unainama kidogo,ndio ikawa mwisho wa tour yangu.

Jumapili ijayo nataka nijaribu tena huko...
Mnnnh naona unatupia ndoano ki dizian flan hivi ii tusiku shtukie.. Ila nimekuelewa
 
Natumaini wewe unaesoma uzi huu ni mzima wa afya.

Nimekuwa nikikaa hapa Dar kwa muda mrefu kidogo na kumakinika na kazi tu. Hii imekuwa ni 'one way go and return home'. Kwa sasa naona kuna umuhimu wa kutembea sehemu mbalimbali za kutulia na hata kuona jinsi watu wanavyokula maisha hapa Dar.

Kwa hiyo kama kuna anayejua sehemu mbalimbali nzuri iwe ni bichi, klabu, migahawa au mahali mtu anaweza kwenda kutuliza akili kidogo kwa muda na kurudi ambazo zipo hapa Dar. Na hizo sehemu nikienda kutulia hata vinywaji na chakula gharama ya chini iwe 20k.

Kuwe na watu wengi ambao wanakuja sehemu hiyo, muingiliano uwepo kidogo wa watu, hata kukiwa na 'vibe' kidogo sawa kabisa. Eneo na jina la mahali ndicho nachohitaji ili nianze kwenda kupoa siku za wikiendi na siyo kuzubaa tu nyumbani.

Kwa msaada wa google maps yote yanawezekana!
Ahaaa unataka kelele?
Nenda Juliana😂
 
Back
Top Bottom