Sayansi yashindwa kwanini Afrika haijaathirika na Corona, sawa na nchi nyengine

Tz boy 4tino

JF-Expert Member
Sep 14, 2014
1,598
1,816
Wataalamu wa magonjwa ya kuambikiza Duniani kwa umoja wao wakiri kutofahamu kwa nini nchi za Kiafrika hazijaathirika kwa kiwango sawa na nchi nyengine Duniani.

Wataalamu hao wamesema , “ Hali ya ugonjwa wa Corona katika nchi za Afrika hata wao zinawashangaza”. Wengi wamekiri kuwa wakati ugonjwa unaanza kusambaa Duniani walitegemea hali itakuwa mbaya zaidi katika bara la Afrika kutokana na msongamano wa watu, umasikini na uwezo wa mdogo wa serikali za kiafrika kupambana na magonjwa. Lakini hali imekuwa tofauti na walivyotegemea kwani Afrika ndiyo bara lililoathiriwa kidogo zaidi na ugonjwa huo.

Wanasayansi hao pia wamekiri kushangazwa zaidi kwani kuna baadhi ya nchi zilizomo nje ya Afrika kama Brazil na India pia zina masikini wengi na msongomano wa watu katika makazi tofauti na Afrika hizo nchi zimeathirika sana. Jambo ambalo linalozidi kuwachanganya, kwa nini Waafrika peke yao ndiyo wanaonekana kupona katika janga hil??.

Tafiti hii imefanywa na wanasayansi wa Marekani wakishirikiana na wale wa Afrika Kusini, Uingereza na India . Na kuripotiwa na New York Post ya Marekani.
 
We are real human of this world originale we have MELANIN na tumewazidi kwa ubara watu weupe kwa vitu 9 vya kiasili
Usisahau bado kuna Acquired Immunodeficiency Syndrome, ebola zinatuchapa sana tu.

Kwa corona labda ni sababu za kijiografia.
 
Mbona hata mafua ya kawaida tu hywa hayawasumbui Waafrika kama wazungu?

Waafrika huenda wana vinasaba vinavyowapa kinga ya kiasili dhidi ya Covid-19.

Huenda miili yetu ina hormones nyingi zilizokuwa mwilini kwa ajili ya kukutana na vijidudu vingi, na hormones hizo zinatulinda kama chanjo.

Pia, nchi kama Tanzania, life expectancy yetu, 65 years, ndipo high risk age ya Covid-19 inapoanzia.

Kwa hiyo tunaweza kujisifu watu wetu hawafi kwa Corona, kumbe hawafi kwa sababu kwa kiasi kikubwa walishafariki kabla Corona haijawasili.
 
Kwa hiyo Mungu ana upendeleo?
Ushawahi kusikia mwafrika kalazwa kwa mafua? Wenzetu mafua , mtu hulazwa hospitali pia ndugu na jamaa huenda hospitali kumtembelea . Yawezekana ni kweli tumependelewa au mazingira na vyakula tunavyokula pia vinachangia baadhi ya magonjwa kutowaathiri wa Afrika.
 
Hao wazungu Wanafanya mambo ya ovyo hiyo ndio zawadi yao. Shikamoo Mungu wewe ni mkuu
Unaamini kati ya waafrika na wazungu wanaofanya mabaya zaidi ni wazungu? Siku ukisafiri nje ya Bongo ndiyo utajua kumbe hakuna watenda mabaya kama wabongo! Kama ni makanisa au misikiti ni kweli Ulaya watu wengi hawaendi lakini kutenda mambo mazuri hatuwezi kuwashinda. Huku kwetu makanisa na misikiti kila kona lakini maovu ndiyo yametamalaki. Mchngaji au Sheikh akivua kanzu anaingia kwenye kazi ya kuzini na kujirikodi clip ya porn, kama kina Gwajima.
 
Kwa hiyo Mungu ana upendeleo?
kumbuka wazungu walitusema kwamaneno ya mazarau baada ya mlipuko wa korona..wakijiamini wao ni wao..sasa Mungu kaamua kuadhihirishia yakwamba Yeye ndio anaamua apige wpa na aache wap.Tabia ya Mungu huwa umtetea Mnyonge..ila kama unanguvu usijikweze jishushe atakutea na kukusaidia ila ukijiona wewe ni unaweza ataakuacha utumie akili zako.
 
Unaamini kati ya waafrika na wazungu wanaofanya mabaya zaidi ni wazungu? Siku ukisafiri nje ya Bongo ndiyo utajua kumbe hakuna watenda mabaya kama wabongo! Kama ni makanisa au misikiti ni kweli Ulaya watu wengi hawaendi lakini kutenda mambo mazuri hatuwezi kuwashinda. Huku kwetu makanisa na misikiti kila kona lakini maovu ndiyo yametamalaki. Mchngaji au Sheikh akivua kanzu anaingia kwenye kazi ya kuzini na kujirikodi clip ya porn, kama kina Gwajima.
Aiseeee!!!! Kweli? Ila wazungu ndio juu
 
Mbona hata mafua ya kawaida tu hywa hayawasumbui Waafrika kama wazungu?

Waafrika huenda wana vinasaba vinavyowapa kinga ya kiasili dhidi ya Covid-19.

Huenda miili yetu ina hormones nyingi zilizokuwa mwilini kwa ajili ya kukutana na vijidudu vingi, na hormones hizo zinatulinda kama chanjo.

Pia, nchi kama Tanzania, life expectancy yetu, 65 years, ndipo high risk age ya Covid-19 inapoanzia.

Kwa hiyo tunaweza kujisifu watu wetu hawafi kwa Corona, kumbe hawafi kwa sababu kwa kiasi kikubwa walishafariki kabla Corona haijawasili.
Vipi ma-black waliojazana Marekani hawajaathirika?
 
Back
Top Bottom