SAUT main campus, mambo haya yanakera acheni!

Mimi ni first year hapa saut,nimesajiliwa kwa laki tatu tu na hawakunisumbua labda inategemea na huyo mtu alikutana na nani.Kuhusu hostel sikai za ndani na hawajanisumbua wala nini na rafiki zangu wanne wapo wamepanga kitaa.Chuo nimekiona kizuri mnoo sijaona izo longolongo unazosemea.
 
Hoja yako nini ? Subiri utaona tu MTU mwenyewe upo orientation week kelele kibao haaa
 
Hoja yako nini ? Subiri utaona tu MTU mwenyewe upo orientation week kelele kibao haaa
Acha kunitisha kizembe wewe.Wewe ndo umeandika hoja hapo... Yani unaprove ulivo limbukeni.
 
Hii dunia bhana,UDSM kupata room ni dream ya kila mwanafunzi,UDOM naona kila mwanafunzi ni lazima apate room, SAUT wadau wanalazimishwa kukaa hostel na ninasikia kuna chuo hawana hata room moja kwa ajili ya mwanafunzi
Udsm main campus rooms karibia zote mbovu ila watu wanahaha kuzipata...ila tukumbuke ule usemi penye miti mingi
 
Mi nimekuja tu hapa kumcheki 'man' mvua mwenye avatar hii..

 
Yatima asiye na baba na mama hataki Hostel ya chuo ya Tsh 300,000/=, kwa mwaka. Anataka za nje za Tsh 500,000/= hadi Tsh 1,000,000/=. Wakati huo kaenda chuo na Tsh 200,000/=. Niseme tu SAUT rekebisheni hili. Nadhani mmenielewa (in JPM voice)
 
Mtoa mada nadhani ni vyema ungetembelea vyuo vingne tena vyenye majina makubwa na uone changamoto zake utamshukuru Mungu kwa kukupeleka SAUT.

Nlikua juzi tu hapo,kwa upande wa gharama za maisha ziko chini.Hostel hata unazodai ni mbaya huwezi ukazifananisha na vibox vile vya Muhimbili ambavyo wanafunzi wanabebana au wanauziana mamillioni ya pesa kwa mwaka.

Nlipata wasaa pia wa kutembelea hostel flan za nje hapo za laki 6, kiukweli nlitamani hata nizibebe nikaziweke upanga na bei ipande hata hadi 1.4 mil na wanafunzi wa muhimbili wangeshukuru sana...

Nachotaka kusema SAUT bado changamoto zenu za kimakazi sio mbaya kuanzia za chuo mpk za nje.Tembea uone na hutotamani tena kuomba chuo chenu kifungwe
 
Kwa maelezo yako tu sizani hata kama shule umeenda wewe..

Chuo gani ambacho wanafunzi anasajiliwa bila kulipa kiasi chochote?? Hata kama unalipiwa 100% kuna amount lazima ulipie.

Afu swala la hostel sheria na mamlaka ya chuo ndo hudetermine kama wanaweza kubeba wanafunzi wote walio nao kwa kipindi hcho kwenye hostel zao why mwanafunzi akae nje??
Huko nje ndo wanajifunza matebdo ya hovyo wanakabwa wanaibiwa afu tuje kulaumu chuo kutowalinda wanafunzi wake..
Embu taja ni chuo gani bora chenye hostels ambazo zinajitosheleza na wanafunzi wanaruhusiwa kukaa nje???

Wewe kweli akili hauna unadhan anae toa vigezo vya chuo kikuu ni Bibi yako yani unafananisha chuo na sekondari?? Embu kahakiki vyeti vyako kwanza namashaka kama kweli ulimaliza hata hapo Pugu manake sijaona wanafunzi wa pugu wenye uwezo mdogo wa kujenga hoja kama wewe.

Huyo mwanafunzi kama ulikua na uwezo wa kumsaidia ungemsaidia asiombe sauti aombe UDOM na vyuo unavyo vijua wanavyo pokea wanafunzi bila kulipa chochote ,
 
Umenena vyema hawa division five wanaongea ujinga tu hapa enzi zetu za father kitima daaah kwanza hapo chuo hlo jam la kuwahi viti vya mbao ilikua tabu tupu
 
Kwa kuwa bado nakusanya kianzio,nashukuru kwa taarifa niko mbioni kwenda kujionea mwenyewe.naamini kuwa popote kambi,kama kuna kubanwa basi sina jinsi nitajitahidi kuwaelewa nipate nilicho fuata.
 
Una maelezo mazuri ila kuna sehemu mbili umevuruga. Hostels UDOM zinajitosheleza lkn hukatazwi kukaa nje..
Pili UDOM hawasajili mwanafunzi kama hajalipa kitu. Sijui kama umenielewa.
 
Hilo swala la first year kulipa nusu ya Ada kabla ya registration lipo vyuo vingi, yaan unalipa gharama zote zinazotakiwa pamoja na nusu ya tuition fee, hivyo mleta mada usione km SAUT wanawaonea. Pugu umenikumbusha mbali sn, unaenda ''beto" unaacha nguo zote nje.
 
Umeeleza vyema mkuu
 
Unajua SAUT ni watu wa MUNGU wameshaota kuwa mdogo wako ni hoe hae hivyo kumlazimisha kukaa hostel wanataka kumsaidia maana maisha ya hostel binafsi ni gharama sana.
So mshukuru MUNGU kwa upendo wake na uache kulalamika.
Kuhusu hayo mengine kaka hakuna haki bila wajibu.
Hata sie kina Msichoke tumesoma SAUT japo kwa kuunga hadi tumemaliza bila kulalama kwenye mitandao ya kijamii
 
Huu ujinga wako usikurupuke kuuanika humu siku nyingine. Hujui mfumo wa elimu ulivyo mgumu tz. We umeenda kukagua miundo mbinu au kusoma??. Mbona kwenu unalala kwenye kijumba cha tembe haujalalamika. Kijana usitafute sifa za kijinga kilichokupeleka pale ni kitabu usitafute umaarufu kwa nguvu. Kila chuo na kanuni zake we ukishindwa teleza kimya kimya kaombe tena tcu wakupeleke harvad university chuo chenye hadhi yako.
 
Wakala wao wewe
I am product of SAUT siwezi vumilia mtu aongee uongo kuhusu saut ikiwa miye ni zao la saut naye ujua ukweli wa saut kwa vitendo si kusimuliwa

Raha, shida za saut kitaaluma nazijuia, raha, shida za saut nje ya saut yani ukiwa unafanya maisha yako nje ya chuo ila wewe ni mwanafunzi wa chuo hapo nazijuia

Kwa kukupa faida ya maneno tu hakuna mwanafunzi aliyesoma saut miaka mitatu akamaliza akaja mtaani alafu ukamkuta kazubaa zubaa tu, au kapata ajira alafu ukamkuta anaishi maisha ambayo si rafiki

Hiyo ni kutokana na changamoto alizokutana nazo chuo chuo cha saut kinamjenga mtu kitaluma na kimaisha kwa ujumla, hivi unafikilia maisha ya kulipa kodi milioni mchezo, maisha ya mtu kujipikia ghetto kwani ukila kwa mama lishe garama kubwa nk

Kwaiyo hivi ni baadhi ya vitu vinavyomuandaa Kijana hata akija katika soko la ajira anakuwa si muoga wa maisha tofauti na yule aliteushi kwenye mabanda ya njia umeme, maji bure msosi sahani buku
 
SAUT mwanza main campus kipo vizuri. Nime mleta mwanangu. Lami mpaka chuoni kutoka barabara kuu.
Nimeenda administration block nimepokewa vizuri na wahudumu nikapelekwa kwa mkuu wa utawala. Kauli njema. Ushauri mzuri
Hostel za chuo 300,000/ ziko vzr. Akanishauri kwa kijana wa first year ni BUSARA akae ndani.
Tuka survey out campus, daaaah! Rooms nzuri sana 800,000/per year self, security nzuri, solar system ipo, maji reserve tanks zipo.
Jikoni kila mwanafunzi ana kikabati chake akitaka kupika misosi.
Canteen zipo. Tena nilikula canteen inaitwa Burger. Nikapiga burger na soda.
Mnyonge Mnyongeni haki yake mpeni.
Fees ni 1,260,000/per year. SAUT oyeeee.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…