Saumu aomba ulinzi wa CCM!

Saumu aomba ulinzi wa CCM!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Hatimaye kada wa CCM aliyetimkia huko baada ya kuwa CHADEMA Makao Makuu, Saumu Malungu ameomba ulinzi CCM. Hii inafuatia kutajwa kwake na Mkurugenzi wa Sheria wa CHADEMA,Wakili Msomi Tundu Lissu kuwa ndiye anayeratibu mipango ya kupika ushahidi na kuandaa ushahidi dhidi ya Winfred Lwakatare.

Ni leo tu ambapo Saumu aliripotiwa na gazeti la Tanzania Daima kuwa alinaswa akiwasiliana na kiongozi mwandamizi wa CCM ambaye ni mratibu wa mpango wa Lwakatare kichama. Saumu anatumiwa kwakuwa alikuwa Idara ya Usalama ya CHADEMA na kwakuwa anajua kila linaloendelea CHADEMA Makao Makuu.

Mnamo majira ya saa kumi na mbili na nusu jioni hii, Saumu alifika hapa Ofisi Ndogo za CCM Lumumba ili kuwasilisha ombi lake la kuomba ulinzi na haraka akakabidhiwa kwetu kama Kitengo cha Ulinzi cha CCM. ‘Niko hatarini. Inadaiwa kuwa nimeshtukiwa. Kuna ‘wenzangu’ wamenisaliti ndani ya CHADEMA. Wamevujisha siri za mipango yetu’ alisema Saumu akionekana kuwa na shaka kuu.

‘Nilindwe. Mwigulu Nchemba kwasasa hanipi msaada wa kutosha. Nilianzia UVCCM pale ambapo wamenielekeza nije hapa. Tafadhali nilindwe ilinimalizie kazi yangu’ aliongeza Saumu Mulungu.

Baadhi ya vigogo hapa Lumumba wameonesha hofu kuu katika kuharibiu taswira ya chama juu ya suala hili. Wameapa kuwatenga wote wanaohusika na mpango huu haramu,kama kweli upo. Kuna sintofahamu kubwa hapa Lumumba.

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
 
Mwigulu yuko loliondo huko akimtetea Mwarabu mwekezaji
 
Hahahaha porojo sa chakubanga na wajukuu zake. Hakuna kitu kama hicho. Chadema inakufa haya ni matanga
 
Napenda kuamini kuna ukweli hapa., kwakuwa kuna mzaha mwingi JF hivi karibuni., inaondoa maana ya Forum hii.
 
VUTA-NKUVUTE nakuamini sana huwezi kupost ujinga. Wape ushauri huyo jamaa achane na huo usaliti utamgharimu sana. Mwigulu ni kama mhindi kwenye box, haaminiki kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Hivi leo ndio tarehe mosi Aprili au??
Maana threads za leo sizielewi elewi na zinaingia kwa kasi kama abiria wanavyopigania daladala za mbagala Taifa...baada ya mechi ya Azam....
 
Mbona walisema CHADEMA hakuna WAISLAMU? Ah NDIO MAANA anaomba ULINZI wa CCM? au ULAJI wa CCM? How NICE
 
Watanzania yetu macho wito wangu kwa rais Kikwete hivi kweli umeacha chama alichoasisi Baba wa Taifa sorry mzee nyerere kikimalizwa na akina Mwigulu Nchema shauri utakabidhi nchi kwa CHADEMA.
 
Wito wangu kwa vijana, achani kuwaabudu wanasiasa. Fight kivyako, sasa hivi demokrasia tanzania inakuwa, huna haja ya kujikomba kwa chama fulani ili malengo yako ya kisiasa yatimie. Jambo la mhimu, wateteeni wananchi wanaoonea, wao ndo wananguvu ya kuwaweka madarakani.
 
Kama kasingiziwa nategemea muda mfupi ntasikia kafungua charge mahakamani dhidi ya gazeti la Tanzania Daima kwa kumwandikia uwongo.Sasa ni mbele kwa mbele. Uwongo uwongo na ujinga hatutaki. Na asipojitokeza kupeleka kesi mahakamani tayari ajilinde sana maana dhambi hii aifanyayo,. Saumu anaonekana ni mpagani hajui kama yuko Mungu wa kweli.
 
Kila kitu kitawekwa wazi!! Saumu anaomba ulinzi amalizie kazi yake..... Na ikiisha atakuwa tiyari kutupwa jalalani.... Na laki nne zitakuwa zimekwisha.... Kitakachokuwa kimebaki ni kutuvulia pichu!! Pathetic!!
 
Hawa jamaa wana hali mbaya sana.
Wananchi wamechoka na ccm, wakumbuke ya kuwa wao wanaishi miongoni mwa wananchi waliochoshwa na mfumo mzima.
Wataomba ulinzi leo, kesho je watakimbilia wapi?
Nguvu ya umma inakuja, watake wasitake!
Kitaeleweka tu!

Kitunguu saumu pole sana...
 
Inasikitisha kuona mtu kama saumu tuliyemuona kwenye TV akikabidhiwa kadi ya CCM akiwa katika harakati za kutengeneza ushahidi mabomu mawili tu ya mawakili chali atachanganyikiwa mpaka atasahau kila kitu rejea MACCM,Arusha,Singida,Ilemele,Maswa ,Igunga MACCM hayana akili hawawezi mbinu
 
Asante kwa taarifa mkuu mwache aendelee kutapata kama kuku aliyekoswa na kisu.ikiwezekana kikosi cha mizinga wampe ulinzi
 
Duh!!!! Kweli Mungu si Athumani!!!!




Hatimaye kada wa CCM aliyetimkia huko baada ya kuwa CHADEMA Makao Makuu,Saumu Malungu ameomba ulinzi CCM. Hii inafuatia kutajwa kwake na Mkurugenzi wa Sheria wa CHADEMA,Wakili Msomi Tundu Lissu kuwa ndiye anayeratibumipango ya kupika ushahidi na kuandaa ushahidi dhidi ya Winfred Lwakatare.

Ni leo tu ambapo Saumu aliripotiwa na gazeti la Tanzania Daima kuwa alinaswa akiwasiliana na kiongozi mwandamizi wa CCM ambaye ni mratibu wa mpango wa Lwakatare kichama. Saumu anatumiwa kwakuwa alikuwa Idaraya Usalama ya CHADEMA na kwakuwa anajua kila linaloendelea CHADEMA Makao Makuu.

Mnamo majira ya saa kumi na mbili na nusu jioni hii,Saumu alifika hapa Ofisi Ndogo za CCM Lumumba ili kuwasilisha ombi lake la kuomba ulinzi na haraka akakabidhiwa kwetu kama Kitengo cha Ulinzi cha CCM. ‘Nikoha taraini. Inadaiwa kuwa nimeshtukiwa. Kuna ‘wenzangu' wamenisaliti ndani ya CHADEMA. Wamevujisha siri za mipango yetu' alisema Saumu akionekana kuwa na shaka kuu.

‘Nilindwe. Mwigulu Nchemba kwasasa hanipi msaada wa kutosha.Nilianzia UVCCM pale ambapo wamenielekeza nije hapa. Tafadhali nilindwe ilinimalizie kazi yangu' aliongeza Saumu Mulungu.

Baadhi ya vigogo hapa Lumumba wameonesha hofu kuu katika kuharibiu taswira ya chama juu ya suala hili. Wameapa kuwatenga wote wanaohusika na mpango huu haramu,kama kweli upo. Kuna sintofahamu kubwa hapa Lumumba.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.



 
Back
Top Bottom