Saudi state-owned media warns Russia will exploit vacuum if US imposes sanctions

Ukweli mtupu
 
Hawaelewi kitu hao matutusa wala usibishane na watu ambao hawafuatiliii makala za vitabu na documentary zenye uchambuzi yakinifu wamarekani wenyewe wanaelewa nguvu ya biashara mafuta na influence kubwa iliyonayo katika thamani ya pesa yao halafu we mmatumbi toka sijui wapi eti unabisha .......wtf !
 
mkuu naona munkari umepanda.
hahahahaha
Trump ameshawambia akiondoa majeshi hapo patageuka kama mogadishu au syria.
' Ufalme hauwezi kudumu wiki bila kupinduka bila US army presence hapo Saudia'.
mikwara ya kizungu huwa inanifurahisha sana
Marekani alichemka baada ya kukubali kukalishwa na urusi na kushindwa kumuondoa Asad. Sasa hivi kila aliekuwa anategemea silaha na ulinzi toka marekani,anamuona mrusi ni mbadala. Marekani akileta tu maringo,wanageukia Russia.
Marekani aondoe jeshi lake Russia ashushe S400 kama marekani hawajafa kwa kihoro
 
Hahaha..''assad na wairan wake wakaoga mabomu''..I like that. Basically nachokiona kwa hawo jamaa wawili (US+Russia) wanatekeleza makubaliano ya Nuke pact pamoja na treaty mbalimbali on security. ndo maana inakuwa ngumu kushambuliana. On economic point of view, Russia inamuhitaji US alegeze vikwazo ili waendelee kiuchumi. Russia anaumizwa na vikwazo vya uchumi vya Marekani na hana la kufanya. kwa Upande wa Nchi kama UAE hakuna madhara kwani Waarab wana hela ila hawana akili Plus technology. Naturally, Mwarab haaminiki na ndo maana wanakuwa expendable. Kwa upande mwingine, US anaweza kuzamisha uchumi wa UEA in a just brink of eye! Kama mwarab angetumia busara, angeomba haya mambo wayamalize in a diplomatic way kuliko kuwa vocal kama wanavyofanya.
 
Huelewi hata tatizo kubwa likalomkabili mmarekani ni wafanya biashara wakubwa ( manufacturing and high tech industries ) wamehamishia biashara zao offshores countries ? au huelewi hata hilo , makampuni mengi tu yalishaanza kumkibia mmarekani na kuinvest Europe na China , Trump mwenyewe anatoa povu sababu ya hilo halafu wewe unaleta story za blablaa tu hapa
 
nimekusoma mkuu. hao nadhani ni kama wanandoa wawili walioamua kugombana mbele ya hadhara kwa sababu ambazo hata hazikuwa na mashiko. sisi wapambe tunaona kama wanaachana, ila jioni unaona wanatoana Out kwa vicheko vingi.
Hizo kelele ni kujaribu kuwatuliza na kuwafurahisha wapiga kura wa Marekani hasa media zao na asasi za kiraia za kutetea haki za binadamu.
 
Aiseee inaweza kweli lolote kuhusu economics ila najua vingi mno kuhusu history ya US ninaelewa kafikaje hapo na hatokaa atoke kwanini.
umesoma historia na empire zingine duniani,kama kweli umesoma hiyo usa mpaka mwaka 1950 ilikua inamiliki uchumi wa dunia kwa kiasi gani na kwa sasa inamiliki kiasi gani?hebu angalia hiyo trend halafu umeniambie us empire inaelekea

mkuu hakuna empire duniani iliyokaa milele amini,usiamini inaweza ikawa sio leo wala wala miaka 50 ijayo,ila ipo siku usa itaanguka na wengine wata rise

historia inaonyesha watu hawakutegemea kama british empire itaanguka wala hata wakina roman empire,kasome historia vizuri,na kwa jinsi sasa hivi usa inavyotapatapa inaonyesha kabisa wanaelekea mwisho

muda wote limekua taifa la kulalamika na kuwawekea vikwazo wenzako na amini mkuu kuna siku zitafika vikwazo vitakua ni useless mfano kwa sasa watu wa eu wameanza kutengeneza mfumo wa fedha wa kwao ikiwa kama mdadala wa swift ili waweze kufanya banking transactions bila kuwepo na mkono wa usa,huu ni mfano wa jinsi vikwazo vinavyoanza kukwepwa na baadae vitakua useless kabisa
 
Mkuu, nimesoma vitabu hivyo ulivyo cite hapo juu except hicho cha mwisho. Nakubaliana na wewe to some point ila kumbuka hizo ni analysis tu kutoka kwa wadau based on their point of view and perspectives. Ila Naamini haitokuwa kirahisi hivyo kushusha nguvu ya dola (USD). Kuna figisu zinaendelea chini kwa chini kati ya IMF & World Bank kuhusu nchi za Kiafrika zinazokopa china. Katika Geopolitics, mchina hana impact but US does. Kwa mtazamo wangu, SAUDIA akiachana na US ndo mwisho wake. Kumbuka uchumi wa SAUDIA unatokana na mafuta na what if US akivuruga bei ya mafuta? Nini itakuwa hatima ya Saudia? Records zinaonyesha kuwa uchumi wa Saudia ni sawa na wa state moja tu kwa US. Kama Marekani akisema liwalo na liwe, Saudia itakuwa another Syria. Nafikiri kwenye Mgogoro huo ulipo, Saudia atumie diplomasia kutatua tatizo kuliko vitisho. Kwa mfano, US akipandikiza ISIS pale SAUDIA...unafikiri ufalme utakuwepo? Nihitimishe kwa kusema, Diplomacy ni bora kuliko vitisho na Saudia anamhitaji USA kuliko US anavyomhitaji Mwarab (Saudia)
 
UAE imeingiaje hapa,mbona ni vitu viwili tofauti kabisa na saudi arabia?
 
Ndo maana nimetangulia kudokeza inawezekana si miaka hii lakini muda si mrefu down the road , hii 21th century Roman empire will fall , petro dollar ina impact kubwa katika uchumi wa marekani zaidi ya unavyodhani mkuu hebu imagine hiyo opec wakiweka ngumu kuuza mafuta kwa dollar , usichukulie poa mkuu Wamarekani wao wanajua jinsi makampuni yao makubwa ya exxon nk yanavyo affect uchumi wao , mkuu juhudi za mmarekani kutia kambi zake huko uarabuni ni kulinda hii petrodollar tu na si vinginevyo ,America doesn't give a *** about humanity or stuffs like those it's all about oil
 
Fact! hoja nzito hii na imejitosheleza nadhani kwenye UAE ulimaanisha Saud Arabia kama sijakosea
 
Saudi hawezi kumpiga mkwara USA hata siku moja. Marekani akitoa msaada wake wa kijeshi saudi mfalme anapinduliwa mara moja.


Fuatilia kwann Mumer(Ghadafi) aliuawa ndio utaelewa kuwa USA ni mtu mbaya lile vuguvugu la mapinduzi nchi za kiarabu alikuwa anatafutwa Ghadafi tu sababu ya mipango yake ya kutengeneza sarafu ya dhahabu kwa ndio iwe inatumika kwny ununuzi wa mafuta
 
Pole hao wengine wanafanya Assembly tu na hakuna bidhaa ya kielectronic inayonunulika US inayotekea Russia na china kwanza kodi yake ni kubwa pili hakuna mahitaji yake hizo zote zinazofanywa Assembly yake china na hongkong wanauza assia na Africa. kwa sababu exportation ya kutokea US mpaka bidhaa ifike africa kwa marine way gharama yake itakua kubwa kumbuka ni nchi chache africa cargo planes zinafika kwingine tunategemea meli china ni karibu na biashara zote kubwa kutoka china kuja Africa kuna mkono wa US people
 
daaahh kuna watu waongo humu sijawahi kuona " Kwahiyo ile sarafu maarufu ya rupee Ili kuwa inatoka USA !!!?
Wapi nimeandika kuhusu rupee ya india hapo, kuna chochote kiko related na rupee nimekiandika? au ndio unaamka sasa hivi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…