kuusoma..... unaona sisi sio kama nyinyi. Wewe mwenyeo umesema imani hutumii akili, kwaio wewe umezaliwa katika ukatoliki, ulichokifanya ni kuisoma biblia ya kikatoliki tu. Hukuusoma ukiristo na ukaishuhulisha akili yako. Wala hukuhoji kitu katika ukristo na ndio maana ukawa unawashawishi watu wasitumie akili.
Sisi huwa tunapelekwa madrassa kufundishwa huo uislam. Na unapokuwa na masuali unauliza na unapokuwa na hoja unahoji, na panapokuwa na majibu unajibiwa kwa kufahamishwa.
Kupitia kusoma huko na kuujua uislam na kutumia akili yangu nimewaza kujiridhisha kwamba kamwe Mungu hawezi kuwa binaadamu wala hakuna kiumbe chenye uwezo wa kumtesa/kumsulubu mungu.
Nimezaliwa katika uislam, lakini uislam ukiwa na amdhehebu nyingi, vile vile nilizaliwa kwenye dhehebu fulani, huku nikiwa kwenye dhehebu hilo sina nnachikifuata zaidi ya jinsi ya kusali tu, nilishawahi kusali kutumia njia ya dhehebu fulani na fulani, lakini nilikuja kujiridhisha jinsi ya kusali katika dhehebu ambalo nimezaliwa nalo. Vile vile kutoka kwenye dhehebu hilo hilo nilozaliwa, kuna mambo sikubaliani nayo bali nakubaliana na mambo yalioko kwenye dhehebu jengine. Kwaio pamoja na kwamba nimezaliwa kwenye dhehebu fulani, lakini bado nafuata baadhi ya mafunzo kutoka dhehebu jengine ambayo akili imeridhika nayo.
Kupitia kwa kutumia akili, katika uislam tuna vitabu vya hadithi ambavyo vimepokelewa na watu na watunzi tofauti, vikiwa na hadithi kwa malaki, lakini kwa vile uislam unamtaka mtu atumie akili, basi utakuja kuona kuwa maimamu wamekaa na wamechambua hadithi ilokuwa sahih na isiokuwa sahih, katika njia izo za kutambua usahih wa hadith, huwa inapimwa hadithi na Quran, ikiwa hadithi imekwenda kinyume na Quran basi hadithi hio inachukuliwa kuwa sio sahih na imetungwa (ni sifa ya binaadamu kutunga kitu), njia nyingine inatizamwa sanad, yaani waliopokea hio hadith, ndani yake akipatikana mpokezi mmoja tu mwenye mushkeli hadithi hio inahesabiwa kuwa ni dhaifu, na sio ya kuaminika.
Tofauti na dini uifatayo, ambayo watu wanakaa kitako na kuchagua sura ipi iekwe kwenye biblia ipi iondolewe, ulitakiwa ujiulize, dini hio ya Mungu au ya watu ambao wanaamua nini kiandikwe? Lakini masikini kwa vule huwez kutumia akili wala hutakiwi kuhoji, ndio umejikuta kuifuata.