Saudi Arabia kuwanyonga wanaharakati 3 baada ya Ramadhan

Saudi Arabia kuwanyonga wanaharakati 3 baada ya Ramadhan

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,132
Reaction score
24,438
Saudia kuwanyonga wanazuoni 3 mashuhuri baada ya Ramadhani


Utawala wa Aal-Saud umepanga kuwanyonga wanazuoni watatu mashuhuri nchini Saudi Arabia baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, ikiwa ni katika muendelezo wa ukatili na ukandamizaji dhidi ya wasomi na wapinzani unaoongozwa na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa utawala huo, Mohammed bin Salman.

Tovuti ya habari ya Middle East Eye yenye makao makuu yake mjini London imeripoti kuwa, watawala wa Riyadh wamepanga kuwanyonga wanazuoni hao mashuhuri ambao ni Sheikh Salman al-Ouda, Sheikh Awad al-Qarni na Ali al-Omari kwa tuhuma bandia za ugaidi.

Sheikh Ouda ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Kiislamu, ambayo Riyadh imeiweka katika orodha yake ya mashirika ya kigaidi. Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanamfahamu mwanazuoni huyo kama mwanamageuzi.

Sheikh al-Qarni pia ni mwanachuoni mashuhuri nchini Saudia, mwanaakademia na mwandishi mtajika, huku al-Omari akifahamika zaidi kuwa mtangazaji mashuhuri wa Kiislamu.

Mwezi uliopita, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudia ilitangaza kuwa imewaua watu 37 raia wa nchi hiyo ambapo 32 kati yao ni Waislamu wa Kishia kwa tuhuma za kile kilichotajwa na wizara hiyo kuwa ni ugaidi.

Kanali ya televisheni ya al-Jazeera ya Qatar imenukuu duru za habari ndani ya utawala wa Aal-Saud zikisema kuwa, kitendo hicho cha Riyadh kuwanyonga kwa umati Waislamu wa madhehebu ya Shia kilikusudia kupima kiwango cha lalama za jamii ya kimataifa.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International mwaka jana, utawala wa Aal Saudi uliwaua watu 149 kwa tuhuma hizo hizo za ugaidi.

4bsh3ad8ce0cf11fbs5_800C450.jpg
 
Uitishwe mgomo watu wasiende kuhiji huko.
 
Si ndiyo utawala qa kidhalim utafurahi.

Kinachotakiwa Waislam waende hijja kwa wingi sana wakalianzishe huko kuutoa utawala wa Saud kwa maandamano tu.

Haitawezekana kuandamana shekhati virungu vitawahusu Sana.Hili jambo ni internal affair.Utawala wa kifalme unabebwa na Amerikiya Kwa gharama yoyote.Kiwango chetu Cha kuhusika ni kupaza sauti kwenye media zote kadri iwezekanavyo.
 
Si ndiyo utawala qa kidhalim utafurahi.
Kinachotakiwa Waislam waende hijja kwa wingi sana wakalianzishe huko kuutoa utawala wa Saud kwa maandamano tu.
Wewe bibi ndio sheria za Mussa hizo acha kubwata kaa utulie.

Unaishi nchi ya amani ambayo haina sheria za kizwazwa ungekuwa Oman au Saudia wangeishakunyonga zamani sana, huna nidhamu na wanaume unatuzoea kama dada zako, una_interact nasi hovyo WEWE WATCH YOUR MDOMO bahati mbaya You're just Keyboard hero tu huna lolote😏😏
 
Wewe bibi ndio sheria za Mussa hizo acha kubwata kaa utulie.

Unaishi nchi ya amani ambayo haina sheria za kizwazwa ungekuwa Oman au Saudia wangeishakunyonga zamani sana, huna nidhamu na wanaume unatuzoea kama dada zako, una_interact nasi hovyo WEWE WATCH YOUR MDOMO bahati mbaya You're just Keyboard hero tu huna lolote😏😏
Heee! Mwenzetu vipi? Ndo nyie nyie wanyongaji au? Mbona unaongea ovyo namna hiyo?
 
Wewe bibi ndio sheria za Mussa hizo acha kubwata kaa utulie.

Unaishi nchi ya amani ambayo haina sheria za kizwazwa ungekuwa Oman au Saudia wangeishakunyonga zamani sana, huna nidhamu na wanaume unatuzoea kama dada zako, una_interact nasi hovyo WEWE WATCH YOUR MDOMO bahati mbaya You're just Keyboard hero tu huna lolote😏😏

Jazba za nini mzee? Wanaume wa kweli hatubwatuki tuu.. Tunatulia na kutafakari
 
Saudia kuwanyonga wanazuoni 3 mashuhuri baada ya Ramadhani


Utawala wa Aal-Saud umepanga kuwanyonga wanazuoni watatu mashuhuri nchini Saudi Arabia baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, ikiwa ni katika muendelezo wa ukatili na ukandamizaji dhidi ya wasomi na wapinzani unaoongozwa na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa utawala huo, Mohammed bin Salman.

Tovuti ya habari ya Middle East Eye yenye makao makuu yake mjini London imeripoti kuwa, watawala wa Riyadh wamepanga kuwanyonga wanazuoni hao mashuhuri ambao ni Sheikh Salman al-Ouda, Sheikh Awad al-Qarni na Ali al-Omari kwa tuhuma bandia za ugaidi.

Sheikh Ouda ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Kiislamu, ambayo Riyadh imeiweka katika orodha yake ya mashirika ya kigaidi. Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanamfahamu mwanazuoni huyo kama mwanamageuzi.

Sheikh al-Qarni pia ni mwanachuoni mashuhuri nchini Saudia, mwanaakademia na mwandishi mtajika, huku al-Omari akifahamika zaidi kuwa mtangazaji mashuhuri wa Kiislamu.

Mwezi uliopita, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudia ilitangaza kuwa imewaua watu 37 raia wa nchi hiyo ambapo 32 kati yao ni Waislamu wa Kishia kwa tuhuma za kile kilichotajwa na wizara hiyo kuwa ni ugaidi.

Kanali ya televisheni ya al-Jazeera ya Qatar imenukuu duru za habari ndani ya utawala wa Aal-Saud zikisema kuwa, kitendo hicho cha Riyadh kuwanyonga kwa umati Waislamu wa madhehebu ya Shia kilikusudia kupima kiwango cha lalama za jamii ya kimataifa.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International mwaka jana, utawala wa Aal Saudi uliwaua watu 149 kwa tuhuma hizo hizo za ugaidi.

View attachment 1104453
Haya mashiriki uliyotaja mfano Middle East Eye na Amnesty ingekuwa yamemsema IRAN USINGEUNGANA NAYO.
Ubaya na uzuri wa kitu utegemea msimamo wa kila mmoja
 
Si ndiyo utawala qa kidhalim utafurahi.

Kinachotakiwa Waislam waende hijja kwa wingi sana wakalianzishe huko kuutoa utawala wa Saud kwa maandamano tu.


utawala qa kidhalim = X
utawala wa kidhalim =

Sihitaji hata kukuuliza kama huko shuleni ulienda kufundishwa ujinga kwa sababu ni dhahir hujaenda shule, huwezi kuweka q mahali pa w
 
Jazba za nini mzee? Wanaume wa kweli hatubwatuki tuu.. Tunatulia na kutafakari
Sijabwata wala kubwatuka nadhani hujanielewa ndio maana unanikosea heshima, huyu Ajuza mimi namfahamu toka 2012 hivyo najua ana misimamo gani na anaamini nini nilichokiandika kina mantiki kubwa sana ila kwa kuwa una mlengo fulani huwezi kuelewa.
 
Saudia kuwanyonga wanazuoni 3 mashuhuri baada ya Ramadhani


Utawala wa Aal-Saud umepanga kuwanyonga wanazuoni watatu mashuhuri nchini Saudi Arabia baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, ikiwa ni katika muendelezo wa ukatili na ukandamizaji dhidi ya wasomi na wapinzani unaoongozwa na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa utawala huo, Mohammed bin Salman.

Tovuti ya habari ya Middle East Eye yenye makao makuu yake mjini London imeripoti kuwa, watawala wa Riyadh wamepanga kuwanyonga wanazuoni hao mashuhuri ambao ni Sheikh Salman al-Ouda, Sheikh Awad al-Qarni na Ali al-Omari kwa tuhuma bandia za ugaidi.

Sheikh Ouda ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Kiislamu, ambayo Riyadh imeiweka katika orodha yake ya mashirika ya kigaidi. Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanamfahamu mwanazuoni huyo kama mwanamageuzi.

Sheikh al-Qarni pia ni mwanachuoni mashuhuri nchini Saudia, mwanaakademia na mwandishi mtajika, huku al-Omari akifahamika zaidi kuwa mtangazaji mashuhuri wa Kiislamu.

Mwezi uliopita, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudia ilitangaza kuwa imewaua watu 37 raia wa nchi hiyo ambapo 32 kati yao ni Waislamu wa Kishia kwa tuhuma za kile kilichotajwa na wizara hiyo kuwa ni ugaidi.

Kanali ya televisheni ya al-Jazeera ya Qatar imenukuu duru za habari ndani ya utawala wa Aal-Saud zikisema kuwa, kitendo hicho cha Riyadh kuwanyonga kwa umati Waislamu wa madhehebu ya Shia kilikusudia kupima kiwango cha lalama za jamii ya kimataifa.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International mwaka jana, utawala wa Aal Saudi uliwaua watu 149 kwa tuhuma hizo hizo za ugaidi.

View attachment 1104453
Hata Ramadan yao ni bandia
 
Si ndiyo utawala qa kidhalim utafurahi.

Kinachotakiwa Waislam waende hijja kwa wingi sana wakalianzishe huko kuutoa utawala wa Saud kwa maandamano tu.
Sijui kama kwenye baadhi ya mambo huwa mnatumia japo 0.01% ya akili ya vichwa vyenu kufikiri kwa usahihi,yaani wewe na rangi yako hiyo nyeusi mwarabu anayekuona nyani ukaandamane kwenye ardhi yake?

Kila siku dada zako sijui wadogo zako wanavurumishwa kutoka maghorofani kwa kuzidisha tu kiungo chumvi kwenye chakula wewe leo ukapaze sauti kwenye ardhi yao eti “tunataka utawala huu dhalimu utoke” wakuache!!!

Thubutuu.
 
Sijui kama kwenye baadhi ya mambo huwa mnatumia japo 0.01% ya akili ya vichwa vyenu kufikiri kwa usahihi,yaani wewe na rangi yako nyeusi mwarabu anayekuona nyani ukaandamane kwenye ardhi yake?

Kila siku dada zako sijui wadogo zako wanavurumishwa kutoka maghorofani kwa kuzidisha tu kiungo chumvi kwenye chakula wewe leo ukapaze sauti kwenye ardhi yao eti “tunataka utawala huu dhalimu utoke” wakuache!!!

Thubutuu.
Punguzeni jazba wazee, Dada watu kafunga jama
 
Sijui kama kwenye baadhi ya mambo huwa mnatumia japo 0.01% ya akili ya vichwa vyenu kufikiri kwa usahihi,yaani wewe na rangi yako nyeusi mwarabu anayekuona nyani ukaandamane kwenye ardhi yake?

Kila siku dada zako sijui wadogo zako wanavurumishwa kutoka maghorofani kwa kuzidisha tu kiungo chumvi kwenye chakula wewe leo ukapaze sauti kwenye ardhi yao eti “tunataka utawala huu dhalimu utoke” wakuache!!!

Thubutuu.
Wewe unaeituma akili yako vizuri mpaka leo hajafamu kuwa Uarabu si rangi.

Watanzania Leo tunajivunia ustaarabu unafahamu maana ya neno ustaarabu.

Kawabadili rangi Waarabu million 40 wa Sudan. Ukimaliza nenda Saudi Arabia ambao zaidi ya 50% ni weusi.

Mmejazwa ujinga wa kusomea huko mashuleni msituambukize na sisi huo ubaguzi wa kijinga.
 
Back
Top Bottom