Saud Arabia ameamua kuingia vita na Iran

Saud Arabia ameamua kuingia vita na Iran

Adiosamigo

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2013
Posts
10,841
Reaction score
14,485

View: https://youtu.be/aVbfiVTauiM?si=abCE4bBfVPTI561e

Ujumbe ndio huo swali hapa Atafanya kitu gani akingia vita hahaha ikiwa USA na Israel wamemshindwa Iran iwe Saud Arabia.
Walicho kipika USA na Israel ni hicho akingia Saud Arabia na nchi za Gulf states zitaingia halafu USA na Israel wanakimbia wanabaki Warabu kupokea dozi kutoka kwa Iran. Hizo ni plan walizipika USA na Israel siku nyingi.
 
Wamepigwa panapo uma zaidi?
 
Swali je, ufalme upo tayari usalama wao kuwa rehani kisa kuingia vita na Iran ?

Saudia[ viongozi na wananchi wote] ipo tayari kuipokea hali kama ya Iran,Israel,Palestine,Lebanon wanazo kutananazo sasa maana kwenye vita huko na Iran Saudia hawatopewa tende bali mabomu hiki ndicho kinachoendelea katika miji ya Iran,Israel,Lebanon

Kama wapo fit kwa kila hali wazame mzigoni tuone nani anauwezo wa kuvumilia shida na ana uwezo wa kupambana kwa muda mrefu kati yao.
 
Swali je, ufalme upo tayari usalama wao kuwa rehani kisa kuingia vita na Iran ?

Saudia[ viongozi na wananchi wote] ipo tayari kuipokea hali kama ya Iran,Israel,Palestine,Lebanon wanazo kutananazo sasa maana kwenye vita huko na Iran Saudia hawatopewa tende bali mabomu hiki ndicho kinachoendelea katika miji ya Iran,Israel,Lebanon

Kama wapo fit kwa kila hali wazame mzigoni tuone nani anauwezo wa kuvumilia shida na ana uwezo wa kupambana kwa muda mrefu kati yao.
Iran kwa sasa ipo tepetepe, inachofanya sasa hivi ni kurusha makombora hovyo hovyo bila ya malengo yoyote ya kivita, haina hata central command,wameruhusu kila askari mahali alipo afanye chochote anachoweza.
 
Iran kwa sasa ipo tepetepe, inachofanya sasa hivi ni kurusha makombora hovyo hovyo bila ya malengo yoyote ya kivita, haina hata central command,wameruhusu kila askari mahali alipo afanye chochote anachoweza.
Malengo ya Iran katika vita ni yapi ?
 
Hata kama ni wewe, utapigwaje kifala kisa ni rafiki yako? Itabidi ujititimue tu kujibu mapigo. Iran akipigwa mande na hao majirani zake hatoboi.
 
Hata kama ni wewe, utapigwaje kifala kisa ni rafiki yako? Itabidi ujititimue tu kujibu mapigo. Iran akipigwa mande na hao majirani zake hatoboi.
Kama wapo fit kwa kila hali wazame mzigoni.

Muhimu kwenye vita mwenye uwezo wa kuvumilia shida kwa muda mrefu na mwenye uwezo wa kupambana kwa muda mrefu mara nyingi ana advantage ukikosa hivi vitu lazima vita uione ngumu na kushika ndala na kukimbia.

Kama wao Saudia wamejipima na kujiona wapo fit wazame mzigoni ili nao miji yao ipendeze kama Tehran inavyopendeza sasa,Tel Aviv inavyo pendeza sasa kwenye vita hakuna kupeana tende wakae wakijua hilo
 
Madalali wa hijja washaanza kuona kazi yao imeingiwa mdudu
nilihoji hapa kama mwaka huu kutakuwa na hija kutokana na minyukano ya israel/marekani na iran. Hali ya usalama mashariki ya kati ni tete, madalali wa hija itabidi warudishe hela za mahujaji, hakuna kusema kiendacho kwa mganga hakirudi. Saudia wakiingia mzigoni ni totally mwaka huu hakutakuwa na hija
 
nilihoji hapa kama mwaka huu kutakuwa na hija kutokana na minyukano ya israel/marekani na iran. Hali ya usalama mashariki ya kati ni tete, madalali wa hija itabidi warudishe hela za mahujaji, hakuna kusema kiendacho kwa mganga hakirudi. Saudia wakiingia mzigoni ni totally mwaka huu hakutakuwa na hija
Sema hata wao Saudia watabidi wa play smart maana wanajua kiasi gani Hijja inawaingizia mapato.

So hapo ni calculations of the risk.
 
Lengo lao ni nini hasa kama gulf states zitaingia vitani? Ni vita ya kikanda au ya dunia? Zitafaidika na nini kama washirika wao watachakazwa?
 
Iran kwa sasa ipo tepetepe, inachofanya sasa hivi ni kurusha makombora hovyo hovyo bila ya malengo yoyote ya kivita, haina hata central command,wameruhusu kila askari mahali alipo afanye chochote anachoweza.
Anapiga hovyo huku ana hit target una Akili wewe !?
 

View: https://youtu.be/aVbfiVTauiM?si=abCE4bBfVPTI561e

Ujumbe ndio huo swali hapa Atafanya kitu gani akingia vita hahaha ikiwa USA na Israel wamemshindwa Iran iwe Saud Arabia.
Walicho kipika USA na Israel ni hicho akingia Saud Arabia na nchi za Gulf states zitaingia halafu USA na Israel wanakimbia wanabaki Warabu kupokea dozi kutoka kwa Iran. Hizo ni plan walizipika USA na Israel siku nyingi.

Saudi Arabia jinsi ilivyo uchi kiulinzi itaweza kweli kuingia mzigoni na Iran hata kwa week 1 tu!!

Kwanza ninachoona Houth wakiona Saudia imeingia na wenyewe watakuwa wa kwanza kuyachakaza makazi ya mfalme kabla Iran yenyewe haijaamua kujibu.
 
Back
Top Bottom