VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Katika kile kinachoonekana kama kufanikisha mipango ya kuyaidhinisha kwa lazima Matokeo ‘mapya' ya Kidato cha Nne,Serikali imedhamiria kutumia ipasavyo nafasi ya kutokuwepo kwa Prof .Rwekaza Mukandala kuyapitisha.
Prof.Mukandala ,ambaye ni Mwenyekiti wa NECTA na Makamu Mkuu wa UDSM, hayuko nchini kwasasa.Taarifa rasmi zinaoonesha kuwa Prof.Mukandala yuko nchini Marekani kuhudhuria Mahafali ya mtoto wake ambaye anahitimu katika chuo kimojawapo nchini humo.
Huku yeye akitarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa juma lijalo,Serikali imeapa kuyapitisha na kuyaidhinisha matokeo hayo bila ya uwepo wa Mwenyekiti wa NECTA. Yuko kigogo mmoja wa NECTA ambaye amepangwa kukaimu Uenyekiti wa NECTA kwa ajili ya kupitisha matokeo hayo mapya tu.
Prof.Mukandala,akiungwa mkono na Katibu Mtendaji waNECTA,Dr.Joyce Ndalichako,tangu mwanzo wa mchakato wanapinga kusahihishwa au hata kupangwa upya kwa Matokeo ya Kidato IV-2012 kwa kile wanachosema kuwa Serikali ilishiriki kuyaidhinisha ya mara ya kwanza na hivyo haiwezi kuyabadili.
Katika siku za hivi karibuni,kumekuwa na mvutano mkali kati ya Maafisa Waandamizi wa NECTA na wale wa Serikali juu ya upangwaji upya wa matokeo hayo. Serikali inasisitiza kuwa matokeo hayo lazima yabadilishwe ili kukidhi haja ya Taifa kupata ‘elimu bora'.
Mengi yatajitokeza na mtayajua waungwana wote wa Tanzania!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
Prof.Mukandala ,ambaye ni Mwenyekiti wa NECTA na Makamu Mkuu wa UDSM, hayuko nchini kwasasa.Taarifa rasmi zinaoonesha kuwa Prof.Mukandala yuko nchini Marekani kuhudhuria Mahafali ya mtoto wake ambaye anahitimu katika chuo kimojawapo nchini humo.
Huku yeye akitarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa juma lijalo,Serikali imeapa kuyapitisha na kuyaidhinisha matokeo hayo bila ya uwepo wa Mwenyekiti wa NECTA. Yuko kigogo mmoja wa NECTA ambaye amepangwa kukaimu Uenyekiti wa NECTA kwa ajili ya kupitisha matokeo hayo mapya tu.
Prof.Mukandala,akiungwa mkono na Katibu Mtendaji waNECTA,Dr.Joyce Ndalichako,tangu mwanzo wa mchakato wanapinga kusahihishwa au hata kupangwa upya kwa Matokeo ya Kidato IV-2012 kwa kile wanachosema kuwa Serikali ilishiriki kuyaidhinisha ya mara ya kwanza na hivyo haiwezi kuyabadili.
Katika siku za hivi karibuni,kumekuwa na mvutano mkali kati ya Maafisa Waandamizi wa NECTA na wale wa Serikali juu ya upangwaji upya wa matokeo hayo. Serikali inasisitiza kuwa matokeo hayo lazima yabadilishwe ili kukidhi haja ya Taifa kupata ‘elimu bora'.
Mengi yatajitokeza na mtayajua waungwana wote wa Tanzania!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.