tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,956
- 25,345
Siku moja tu baada ya BoT kuzindua sarafu mpya ya sh 500 kwa mbwembwe za hali ya juu, imebainika kwamba sarafu hiyo ni kanyaboya! Ni dhahiri kwamba hapa serikali imeingia choo cha kike kwa makusudi yanayofanywa na mafisadi wachache baada ya kujitoa akili na kujitia upofu. Kwanini?
Sehemu kubwa ya sarafu hiyo imetengenezwa kwa madini ya chuma (iron), na tabaka (layer) dogo sana la madini ya nikeli (nickel). Kama mjuavyo, madini ya chuma hupata kutu kwa urahisi sana. Na kwa kuwa tabaka la nikeli ni dogo mno, pindi sarafu hiyo ikipata mkwaruzo kidogo chuma kitakuwa exposed na kupata kutu, hivyo kuharibu sarafu mzima. Kwa maana hiyo sarafu ya sh 500 ikiguswa na unyevu kidogo tu imekula kwako! Wataalamu wa BoT waliochagua kutumia madini ya chuma kutengeneza sarafu hii ama walitumia akili za bandia au walijitoa akili kwanza ndipo wakafanya maamuzi hayo. Walipaswa kumuomba hata mtoto wa shule ya msingi awape ushauri. Ni bora wangetumia madini ya fedha au bati kwa kuwa madini haya hayapambani (unreactive).
:yield:
Sehemu kubwa ya sarafu hiyo imetengenezwa kwa madini ya chuma (iron), na tabaka (layer) dogo sana la madini ya nikeli (nickel). Kama mjuavyo, madini ya chuma hupata kutu kwa urahisi sana. Na kwa kuwa tabaka la nikeli ni dogo mno, pindi sarafu hiyo ikipata mkwaruzo kidogo chuma kitakuwa exposed na kupata kutu, hivyo kuharibu sarafu mzima. Kwa maana hiyo sarafu ya sh 500 ikiguswa na unyevu kidogo tu imekula kwako! Wataalamu wa BoT waliochagua kutumia madini ya chuma kutengeneza sarafu hii ama walitumia akili za bandia au walijitoa akili kwanza ndipo wakafanya maamuzi hayo. Walipaswa kumuomba hata mtoto wa shule ya msingi awape ushauri. Ni bora wangetumia madini ya fedha au bati kwa kuwa madini haya hayapambani (unreactive).
:yield: