Katika pita pita zangu kwenye ofisi za umma nimejifunza Haya!
- Ukipeleka maoni yako au kero yako kwa unaeamini ni boss (In charge) wa ofisi ndiyo kwanza unaiongezea ugumu huduma unayotafta
- Ukiandika maoni yako na kuyaposti kwenye kisanduku cha maoni (suggestion box), Unaemlalamikia ndiye mwenye funguo wa hicho kibox
- Ukilalamika kwa boss kwamba mfanyakazi (A) kakuomba rushwa! Wataonesha kukusikiliza kwa makini kama wameguswa, lakini ukitega mgongo wanang'ong'a nakuambizana "yule mteja bwege kweli yaani anataka mambo kirahisi rahisi" Achana nae!