Sanaa ya upambaji chupa

Sanaa ya upambaji chupa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,928
Reaction score
828,569
Kuna mfanyabiashara mkubwa sana wa chupa tupu Tanganyika ni mwana JF mwenzetu... Na ofisi zake kubwa kubwa zipo Dar.. Wilaya ya Ubungo na Temeke.. Nadhani na mikoani pia ana matawi

Ni mfanyabiashara mkubwa kwakuwa anasafirisha mpaka nje ya nchi hasa Zambia, Rwanda na Kenya
Ni mahiri kwenye hii biashara na ana maghala makubwa.. Ni mahiro kuanzia kwenye kukusanya, kuhifadhi kuzipanda kulingana na rangi aina na ukubwa..

Anatoa Ajira za moja kwa moja kwa watu wasiopungua 100

Yeye kutoa Fuso Tandam mbili au tatu za chupa kwenda nchi za nje sio tatizo kwakwe! Kwa ruhusa take nita mtaja hapa akikubali.. Ili pia atupe hamasa na connection

Sasa ukiachana na hilo la mwenzetu.. Wenzetu wengine walioumbwa kufikiri zaidi hasa kwenye kutatua changamoto za ajira na kipato.. Wakaja na ubunifu wa sanaa ya chupa tupu na kuwa pambo la kuvutia

Mapambo haya ni tofauti na kupamba zile zile chupa zenye vimiminika mbalimbali kwenye matukio ya sherehe mbalimbali.. Hii ni sanaa ya kugeuza chupa tupu kuwa pambo la kuvutia

Sitaweka mtirriko wa namna ya kutengeneza bali nitaweka "ready made products"
Picha zitakuwa nyingi sana na zitakuwa mchanganyiko wa zenye malighafi ndani na tupu..
Ma graduate wetu msimalize sole kutafuta ajira kuna mishe zina kipato kizuri tu mitaani na mtaji si mkubwa.. Kikubwa ni utayari
32f110b3-c299-4c78-924f-298678fbdbaf.jpeg
 
Back
Top Bottom