Gudlucky
Member
- Feb 9, 2011
- 22
- 1
Ndugu Mh. Samwel Sitta, napenda kutumia nafasi hii kukupa taswira halisi ya kile nionacho mimi katika swala zima la siasa.
Katika tafakari yangu kwa muda sasa juu ya maisha yako kisiasa, huku nikifuatilia matukio mbalimbali yanayokupata, hatimaye nimekuja kutambua/kugundua kuwa, mwisho wako ni tofauti na mwanzo wako. Nimegundua kuwa, ijapokuwa ulianza siasa kupitia CCM, Utamaliza siasa hiyo kupitia CHADEMA. Kwa nini?: CCM ni chama kisichozingatia haki ya wananchi na Taifa lao {Tanzania} na badala yake huangalia maslai yao wenyewe. Hivyo basi kutokana na Wewe Kupenda Haki itendeke kwa watu wote, na kusimama kikamilifu, kwa ujasiri na uaminifu uloambatana na ushupavu thabiti kutetea haki na maslai ya watanzania kinyume na mafisadi hawa, umekuwa mwiba ktk chama hiki CCM hata kufikia kukupa vitisho vya kukuvua uanachama, kukuvua nafasi za uongozi (mfana ulezi wa vijana Tabora-UVCCM), Kukuondoa ktk kiti cha usipika na mengine mengi. Hii inaonyesha kuwa wewe si sehemu ya mafisadi kwa maana ufanani nao kabisaaa.
Ufuatao ni msemo wangu ambao hupenda kuutumia kwamba, Panya na Paka hawawezi kukaa pamoja na kula chakula sahani moja kwa sababu mtazamo wa paka ni kumla panya. Hivi ndivyo ilivyo kwako wewe na wazalendo waaminifu wanavyoonekana kwa CCM, ipo siku moja watakula kama walivyowala wengine ambao hatunao duniani tena.
Chadema ni Chama cha watu wote, kinatetea haki za watu na taifa lao. Nguvu ya chadema iko kwa umma ili kuitetea umma hiyo ktk mchakato mzima wa kupata haki yao. Chama hiki kina mtazamo ule ule ulionao wewe; Ndugu Mh. Sitta, peke yako huwezi kusalimika ndani ya mafisadi hao wengi ktk kutetea watanzania. Hatima yako ipo chadema, sasa ni wakati wako kung'atuka CCM kuja CDM kuwapigania watanzania. Na huu ndio ukweli halisi. 2015 ni mwaka wa kurudisha haki ya watanzania iliyopotea kwa miaka mingi sasa kupitia CDM na wewe ni mmoja wapo kati ya hao. Come to people... power, you are meant to destiny here.
W E L C O M E
Katika tafakari yangu kwa muda sasa juu ya maisha yako kisiasa, huku nikifuatilia matukio mbalimbali yanayokupata, hatimaye nimekuja kutambua/kugundua kuwa, mwisho wako ni tofauti na mwanzo wako. Nimegundua kuwa, ijapokuwa ulianza siasa kupitia CCM, Utamaliza siasa hiyo kupitia CHADEMA. Kwa nini?: CCM ni chama kisichozingatia haki ya wananchi na Taifa lao {Tanzania} na badala yake huangalia maslai yao wenyewe. Hivyo basi kutokana na Wewe Kupenda Haki itendeke kwa watu wote, na kusimama kikamilifu, kwa ujasiri na uaminifu uloambatana na ushupavu thabiti kutetea haki na maslai ya watanzania kinyume na mafisadi hawa, umekuwa mwiba ktk chama hiki CCM hata kufikia kukupa vitisho vya kukuvua uanachama, kukuvua nafasi za uongozi (mfana ulezi wa vijana Tabora-UVCCM), Kukuondoa ktk kiti cha usipika na mengine mengi. Hii inaonyesha kuwa wewe si sehemu ya mafisadi kwa maana ufanani nao kabisaaa.
Ufuatao ni msemo wangu ambao hupenda kuutumia kwamba, Panya na Paka hawawezi kukaa pamoja na kula chakula sahani moja kwa sababu mtazamo wa paka ni kumla panya. Hivi ndivyo ilivyo kwako wewe na wazalendo waaminifu wanavyoonekana kwa CCM, ipo siku moja watakula kama walivyowala wengine ambao hatunao duniani tena.
Chadema ni Chama cha watu wote, kinatetea haki za watu na taifa lao. Nguvu ya chadema iko kwa umma ili kuitetea umma hiyo ktk mchakato mzima wa kupata haki yao. Chama hiki kina mtazamo ule ule ulionao wewe; Ndugu Mh. Sitta, peke yako huwezi kusalimika ndani ya mafisadi hao wengi ktk kutetea watanzania. Hatima yako ipo chadema, sasa ni wakati wako kung'atuka CCM kuja CDM kuwapigania watanzania. Na huu ndio ukweli halisi. 2015 ni mwaka wa kurudisha haki ya watanzania iliyopotea kwa miaka mingi sasa kupitia CDM na wewe ni mmoja wapo kati ya hao. Come to people... power, you are meant to destiny here.
W E L C O M E