Samwel Sita anaota mchana, aikataa Tanganyika kwakuikumbatia Zanzibar

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
[h=1][/h]Written by zamko // 11/07/2011 // Habari // 9 Comments

Asalam-alaikhum ndugu wazanzibari wa ndani na nje ya Nchi yetu tukufu ya Zanzibar. ama sina mengi yakusema ila kumshukuru (AS) kwakutupa Uhai, Uzima, Afya, Umoja na Amani katika Nchi yetu. Hii leo tumesikia kauli ya baadhi ya Wabunge kule DODOMA jinsi wanavonguruma juu ya Uharamu wa muungano na kutokuwepo kwa Uwiano wa magawanyo na mapato ya Muungano.

Kama tulivoona habari ya Samuel Sitaa kwamba kuanzishwa kwa Serikali TATU ni bora tusiwe na MUUNGANO kabisa: Naam wazanzibari hayo ndiyo wanayoyataka kama Serikali TATU haitowezekana.

Hizi zote ni cheche za moto wanazotishiwa wazanzxibari ili wasiendelee kudai haki zao. Mfano:
Sitta kasema (ati) kuwepo kwa Tanganyika nikuanzisha ushindani na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Ushindani huu tunaoutaka sisi sio wakupigana makombora bali niwakushindana Kibiashara . Na zipo nchi nyingi tu zenye muungano wa Seriakli Tatu bila ya Matatizo.

Mfano:
UK na Scandanavian zina muungano ambao Mdenish, Mnorway, Msweeden, wanahaki yakuishi katika nchi hizi na wanatumia pasport zao za nchi wanazotoka kama itahitajika. Lakini ikija wakati wa Ulipaji Tax (kodi) Mdenish kama anafanyakazi Sweeden analipa ile kodi ya Sweeden katika GDP na katika GNP anaipatia nchi yake ya Danmark kwani Serikali ya Denmark ina recordi ya Wadenish wangapi wanaoishi katika nchi hizi za scandanevian. Na nchi nyengine kama Norway na Sweeden zinafanya hivo2. Mashindano walionayo (Offcaourse ) ni yakibiaashara na kila nchi inatakiwa afanye vizuri kunyanyua uchumi wake wa ndani.

Muungano wao upo na unaingilia mambo machachge tu kama shirika la Ndege la Scandanevian ni la Muungano na wafanyakazi wanatoka sehemu zote Tatu na faida inagawanywa sawasawa kwani hakuna weye mdogo kipopulation na kinchi utapata kidogo katika faida ya Muungano . au mie mdgo nataka kubebwa na weye na badala yake silipi kodi. Laa.

Danmark ni Ncvhi ndogo katika Scandenevia kieneo na kipopulation lakini inalipa kodi sawa kama nchi nyengine za scandanevian na inapata faida sawa. kila mtu anamuheshimu mwenzake na kila nchi ina pesa yake. japokua ni Koroner hiyo hiyo lakini koroner ya Danmark ni kubwa kuliko ya Norway na Sweedan. Na Norway nitajiri kuliko hizi nchi mbili kwasababu kuna mafuta.

Kwa hivo Nawaomba ndugu WABUNGE wetu na Wazanzibari wote watakao soma Makala hii. musiogope maneno ya SUITA wala Saba, kamba iwe hii hii na tudai Serikali Tatu au kuvunjwa kwa muungano.

Sitta alisema Tukiwa na Serikali TATU itakayopata hasara ni Zanzibar kwasababu itatakiwa ichangie Serikali ya Muungano ambayo ( amekusudia itakua ni ndogo) Huu Ndugu wazalendo ni Ujinga wa Mzee huyu aliesoma lakini hakufahamu. Kwanini zanzibar ipate hasara wakati Fauida na hasara zitakazopatikana kwenye Muungano zitakwenda 50% kwa zanzibar badala ya 0.4% na 50% kwa Tanganyika badala ya 99.6%…? huu sio ujinga tunaoukataa.

Ikiwa Mambo ya Muungano yatapunguzwa na kila Serikali itakua na uchumi wake huru na kujitangaza kwake kiuchumi kwanini wazanzibari tusiofika watu millioni tatu tushindwe Kuwa Matajiri wakati resources tunazkio na Manmpower tunayo+


Wazalendo hizi ni sababu zisizomashjiko na inaonyesha Watanganyika CCM wanafuata kanuni za Dictator nyerere kwakutaka kuimeza zanzibar . hii sio nyengine ila CHOYO CHAO HAWATAKI KUIONA ZANZIBAR INAKUA TAJIRI NAINANYANYUKA KIUCHUMI.

Wembe ni huu huu tusirudi nyuma wakati umefika wakurekebisha Muungano huu kwa Serikali TATU au Kuvunjika. kama sitta hataki Mahakama ya Dunia hawatokataa wakati wazanzibari tunaushahidi wote na Vielelezo vyotye vyakukataa Kukandamizwa na Kutawaliwa kimabavu.
 
Back
Top Bottom