sio kweli,yule mzee katika wazalendo wachache wa nchi hii,basi yeye na dr slaa ni namba moja na mbili,watupinzani wake huwa wanamchafua tu kwa kutumia siasa za maji taka!
Ni kweli ndani ya CCM wengi si wasafi, lakini na sisi wananchi tuwe makini kuweza kuelewa na kuunga mkono hoja safi kwa ajili ya nchi yetu hata kama zimetoka kwa watu tunaowakea alama za masuali.Hakuna msafi ndani sisiem wote wameoza hawa wanaojaribu kuropoka kwa unafiki ni kwa sababu ya maslahi yao binafsi nasi ya maslahi ya nchi.
SS my HERO with a vision; mtajua sababu baadae!!Jana nilisikitika sana kumsikia kwenye redio Mh. Samuel Sitta akipinga wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika kilimo cha zao la janthropa. Zao hili linatumika kutengeza diesel ya mimea. Kuna wawekezaji wameonesha nia ya kuwekeza kwenye kilimo kikubwa cha zao hili na SS alikuwa anatoa maoni yake.
SS anadai kuwa uwekezaji huo, unaohitaji mashamba makubwa sana (e.g. heka 20,000) utakuwa ni uwizi wa ardhi ya waTZ. Anadai kwamba badala ya haya mashamba, tuwekeze kwenye uzalishaji wa umeme wa jua.
- Hivi SS anajua kuwa teknolojia iliyopo hairuhusu uzalishaji wa umeme mwingi kutokana na jua? Mradi mkubwa kuliko yote ya umeme jua DUNIANI unazalisha MW 40 tu. Uwezo huu ni sawa na; nusu ya Mtera, au pungufu ya nusu ya IPTL, au moja ya tano ya Ubungo, au asilimia moja (1%) ya Steigler kama ikijengwa)
- Hivi SS anashindwa kujiongeza na kuona kuwa mradi mkubwa kama shamba la heka 20,000 litazalisha ajira za maana za kutosha sehemu ambapo sasa hivi hakuna ajiri? Miradi hii italeta ajira za moja kwa moja kwa wataoajiriwa na haya mashamba (wataalama wa kilimo, watawala, madereva, wahasibu, watu wa tehama etc). Vile vile italeta ajira zisizo za moja kwa moja (wauza maduka, wahuduma wa nyumbani, mafundi gereji, mafundi ujenzi, walimu, polisi etc)
- Hivi SS, ambaye anasafiri na ndege kila siku, anaweza kusema kweli Tanzania tunatumia ardhi yetu vizuri? Ukiruka na ndege kuelekea S. Africa, utaona kuwa ukishatoka tu juu ya anga ya DSM, Tanzania yote ni pori. Hii ni tofauti na unapokuwa juu ya S. Africa unakuta kila sentimita imetumiwa na mashamba makubwa.
- Huo mradi wa umeme jua, kuna mwekezaji gani wa maana ameonesha nia ya kuwekeza? Ni mwekezaji gani atae leta pesa yake ya maana kuja kuzalisha umeme huu mdogo ili awauzie shirika muflisi kama Tanesco? Tanesco imeshindwa kufanya biashara na IPTL, Songas wanalalamika, halafu ujilete na wewe upoteze hela yako never. Labda Tanesco ibinafsishwe.
- Mwisho, mradi wa janthropa utaongeza mauzo ya nje ya Tanzania. Hii itapunguza nakisi ya mizani ya balance of trade na kufanya shilingi yetu angalau isiwe inaporomoka tu kila siku.
Hapana, mnafiki namba moja yuko kwenye lile jumba jeupe karibu na feri, sio sixSS ni mnafiki namba mmoja Tanzania
hapana, mnafiki namba moja yuko kwenye lile jumba jeupe karibu na feri, sio six
Mzee sitta ana busara sana! Sio kama mkenua meno vasco da gama!
kuna mtu aliwahi kusema graduate wa miaka ya 70 hawezi kuwa thinktank kwenye karne ya 21 kwa sasa mh. Sitta ana reason kama std seven leaver.
Vasco da Gama!!! Ndio matatizo ya kukurupuka bila kusoma thread vizuri!