Samuel Sitta huwa anafikiriaje?

Samuel Sitta huwa anafikiriaje?

sio kweli,yule mzee katika wazalendo wachache wa nchi hii,basi yeye na dr slaa ni namba moja na mbili,watupinzani wake huwa wanamchafua tu kwa kutumia siasa za maji taka!

Hakuna msafi ndani sisiem wote wameoza hawa wanaojaribu kuropoka kwa unafiki ni kwa sababu ya maslahi yao binafsi nasi ya maslahi ya nchi.
 
matumizi makubwa ya ardhi kwa kiwango hicho pengine ingekua vizuri likajadiliwa bungeni ili suala hili liangaliwe kwa mapana na marefui hasa kuhusu faida na athari zitakazotokana na upandaji wa zao hili jipya.nazungumzia opportunity cost kati ya kupanda zao la chakula au jatropa.
 
Hakuna msafi ndani sisiem wote wameoza hawa wanaojaribu kuropoka kwa unafiki ni kwa sababu ya maslahi yao binafsi nasi ya maslahi ya nchi.
Ni kweli ndani ya CCM wengi si wasafi, lakini na sisi wananchi tuwe makini kuweza kuelewa na kuunga mkono hoja safi kwa ajili ya nchi yetu hata kama zimetoka kwa watu tunaowakea alama za masuali.

Kuna uwezekano sifa za uchafu wa viongozi wetu hata sisi wananchi tunazo na pengine tukipata nafasi ya kushika uongozi ndio uchafu wetu mkubwa utakapodhihirika ....

Mimi naona Mzee Sitta ana hoja ya kuungwa mkono na kila raia mzalendo kwa manufaa ya nchi yetu. Nafahamu kuna raia wengine wamezamia tu na hawawezi kuwa na mtizamo wa Mzee Sitta
 
Jana nilisikitika sana kumsikia kwenye redio Mh. Samuel Sitta akipinga wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika kilimo cha zao la janthropa. Zao hili linatumika kutengeza diesel ya mimea. Kuna wawekezaji wameonesha nia ya kuwekeza kwenye kilimo kikubwa cha zao hili na SS alikuwa anatoa maoni yake.


SS anadai kuwa uwekezaji huo, unaohitaji mashamba makubwa sana (e.g. heka 20,000) utakuwa ni uwizi wa ardhi ya waTZ. Anadai kwamba badala ya haya mashamba, tuwekeze kwenye uzalishaji wa umeme wa jua.
  • Hivi SS anajua kuwa teknolojia iliyopo hairuhusu uzalishaji wa umeme mwingi kutokana na jua? Mradi mkubwa kuliko yote ya umeme jua DUNIANI unazalisha MW 40 tu. Uwezo huu ni sawa na; nusu ya Mtera, au pungufu ya nusu ya IPTL, au moja ya tano ya Ubungo, au asilimia moja (1%) ya Steigler kama ikijengwa)
  • Hivi SS anashindwa kujiongeza na kuona kuwa mradi mkubwa kama shamba la heka 20,000 litazalisha ajira za maana za kutosha sehemu ambapo sasa hivi hakuna ajiri? Miradi hii italeta ajira za moja kwa moja kwa wataoajiriwa na haya mashamba (wataalama wa kilimo, watawala, madereva, wahasibu, watu wa tehama etc). Vile vile italeta ajira zisizo za moja kwa moja (wauza maduka, wahuduma wa nyumbani, mafundi gereji, mafundi ujenzi, walimu, polisi etc)
  • Hivi SS, ambaye anasafiri na ndege kila siku, anaweza kusema kweli Tanzania tunatumia ardhi yetu vizuri? Ukiruka na ndege kuelekea S. Africa, utaona kuwa ukishatoka tu juu ya anga ya DSM, Tanzania yote ni pori. Hii ni tofauti na unapokuwa juu ya S. Africa – unakuta kila sentimita imetumiwa na mashamba makubwa.
  • Huo mradi wa umeme jua, kuna mwekezaji gani wa maana ameonesha nia ya kuwekeza? Ni mwekezaji gani atae leta pesa yake ya maana kuja kuzalisha umeme huu mdogo ili awauzie shirika muflisi kama Tanesco? Tanesco imeshindwa kufanya biashara na IPTL, Songas wanalalamika, halafu ujilete na wewe upoteze hela yako – never. Labda Tanesco ibinafsishwe.
  • Mwisho, mradi wa janthropa utaongeza mauzo ya nje ya Tanzania. Hii itapunguza nakisi ya mizani ya balance of trade na kufanya shilingi yetu angalau isiwe inaporomoka tu kila siku.
SS my HERO with a vision; mtajua sababu baadae!!
 
ukiona mwanasiasa anawaza kwa sauti mfano wa mawazo ya wananchi, mshukuru. Hao wazungu wakitaka fuel waende iceland kuna barafu nyingi sana kule. Wanaweza kutumia akili zao kubadili barafu kuwa nishati. Watuachie mashamba yetu
 
Helo!Sita kaongea ukweli tunashuhudia madini na uwekezaji mwingine hauna tija kwa taifa,hivyo hata hilo zao halitakuwa na faida zaidi ya uporaji wa ardhi kwa wanyonge kama unavyoendelea sehemu mbalimbali Tz
 
Kuna kundi la watu wamejiunga JF kwaajili ya Sitta ?.
 
Mzee 6 kaona mbali ila tatizo la wapumbavu wachache wanatumia uzalendo wake kwa taifa lake kusema eti anataka urais.Mzee 6 mpaka sasa hajatia nia ila mafisadi ndo wameshatangaza nia ya kugombea urais.Msipende kuwapotosha wananchi kwa kuwa sema vibaya wapigania haki wao.VIVA MZEE WETU SITA,Tunakuhitaji sana.
 
Ile haki ya kula chakula kwa shilingi elfu 2 kwa siku, si dhana ya kufanyia mzaha. Tanzania, inapaswa kumuheshimu mkulima kwa jasho analovuja na kutuwezesha kununua vyakula kwa bei che. Tukianza kilimo cha mazao ya biashara bila kukumbuka mazao ya kula, gharama za chakula zitapanda sana, haswa kwa watu waishio majini na haki ya kula tutaipoteza.

Nchi ambayo, haina viwanda vya kutosha hata ya kutengeneza vya kula vya makopo, kujaribu kujikita katika uzalisha wa mazo yasio ya biashara, ni dalili za njaa kwa taifa letu.Wakulima hawatalima tena kuwalisha watu wa mijini. Watalima chao kinachowatosha na kuzalisha kingine kwa biashara. Watoto wao watakuwa manamba kwenye ardhi yao - kuhakikisha wanapata kipato.

Unayoyasema sita, yaweza yasionekane sasa kwa kuwa akili zetu zimejikita kibiashara zaidi na kuchoshwa na umaskini wetu! Lakini faida ya mafuta ya mimea kwa tanzania ni ipi?
 
SITA ni jembe la watanzania,wanaobisha wamevuta bangi ! jipange vizuri mzee SITA hakika mafisadi watakoma kukufahamu.
 
andaa mazingira bila kutangaza nia,toa elimu kwa wananchi wajitambue ili wasije pewa vijisenti wakaangamiza nchi yetu
 
Mimi namuunga mkono sitta hauwezi kushindana na waarabu kuzalisha wese huku wenzako wanachimba tu, huku unacha kilimo cha mazo ya chakula kwa kujihusisha na kilimo cha ja....
 
kuna mtu aliwahi kusema graduate wa miaka ya 70 hawezi kuwa thinktank kwenye karne ya 21 kwa sasa mh. Sitta ana reason kama std seven leaver.
 
kuna mtu aliwahi kusema graduate wa miaka ya 70 hawezi kuwa thinktank kwenye karne ya 21 kwa sasa mh. Sitta ana reason kama std seven leaver.

Hayo ni mawazo yako mkuu!
Wewe kama Graduate wa miaka ya karibuni, tukukumbuke kwa lipi kama 'a great thinker ?
 
Hivi mna habari kuwa SUPER DOLL ndio anasimamia kiwanda cha sukari cha MTIWBA?(Kwa niava ya MKAPA)
Na kwa sasa kuna mashamba ameacha kuyalima na inasemekana anayaa andaa kwa ajili ya KUCHIMBA MADINI?
 
Vasco da Gama!!! Ndio matatizo ya kukurupuka bila kusoma thread vizuri!

hii ishu ni SWAP (Sector Wide Approach). Inagusa nchi in every angle. Sitta ni EA Minister, lkn swala hii limemuuma ndo mana anazungumza.
Ukweli ni kwamba Mkenua meno au mzee wa katavi ndo walitakiwa kuwa wakali na kulizungumzia kwa upana. Lkn si umeona walivyo kimya? As if nothing happens.
Aendelee kukenua meno tu! Think kwa kutumia ubongo sio hayo masaburi!
 
Ardhi ya Tanzania imejaa mali na Watanzania wengi hatujui eneo lipi lina nini lakini wazungu wanajua so wanakuja na proposal zao za kisanii then wakipata they do different.
 
Back
Top Bottom