Samuel Sitta awapa somo Kagame (Rwanda), Museveni (Uganda)

Samuel Sitta awapa somo Kagame (Rwanda), Museveni (Uganda)

Na wewe unakuwa kama mtoto ambaye hajasoma wapi sitta kamtaja jk na kagame? Yeye kasema wanasiasa wawili wewe unajuaje kuwa ni jk na kagame kama siyo umbea,kwa nini isiwe slaa na jk au kagame na slaa au kenyatha na jk au vinginevyo acha kuwekea maneno watu mdomoni.


We nae kibwengo umetokea kichaka gani? Make haujui hata unachokichangia,Think be4 you talk
 
Rais aseme hatuna ugomvi na Rwanda halafu Cabinet minister tena wa wizara ya EAC anakubali kuna ugomvi kati ya wanasiasa hawa wawili yaani Kikwete na Kagame !
Hi Ben,
Nasikia wewe ni Next Target ya kuondolewa upinzani kwa 70 m baada ya 50m @ iliyowaondoa kina Shoza.is that true
 
Serikali yetu haichezi ki-timu, inapaswa icfanye mambo zao kiumoja zaidi na si kutuletea maneno mbofumbofu, kuna haja gani ya kujaza mafoleni kisa kuwepo kwa magari ya kutoa makontena bandarini na kwa nini asishirikiane na Mzee wa Sembe wakaboresha reli na kuhakikisha makontena ya rwanda burundi na uganda yanapelekwa kwa treni mpaka bukoba kisha ndo yamaliziwe kwa magari ambapo itakuwa imepunguza hizo mavikwazo na marushwa yao ya waziwazi.

wajipange hawa majamaa na siyo longolongo....!
 
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema ugomvi wa wanasiasa katika jumuia hiyo hauwezi kuathiri shughuli za kibiashara na uchumi wa Tanzania kwa kuwa wafanyabiashara wanaangalia faida zaidi katika shughuli zao.

Sitta alitoa kauli hiyo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua athari za kiuchumi zitakazopatikana baada ya kuwapo kwa taarifa ya wafanyabiashara wa Rwanda kutaka kupitisha mizigo yao katika bandari ya Mombasa badala ya ile ya Dar es Salaam.

Alisema kuwa taarifa ya wafanyabiashara wa Rwanda kuazimia kutumia bandari ya Mombasa si za ukweli na kwamba wanaofanya hivyo ni wale waliokosa zabuni mbalimbali ambazo pia hakuzitaja ni zabuni ya nini.

"Mimi ninachojua suala la hapa ni uchumi. Huu ugomvi wa wanasiasa wawili hauwezi kuwakimbiza wafanyabiashara na ukiangalia wanaopitisha mizigo ni wafanyabiashara na si serikali zinazolumbana," alisema.

Aliongeza kuwa migongano baina ya nchi na nchi haiepukiki hususan zilizo jirani na kuita hali hiyo ya mpito huku akisisitiza kuwa maelewano baina ya Tanzania na Rwanda yatarejea muda si mrefu.

Waziri Sitta alisema umbali kati ya Mombasa na Kigali ni kilometa 2300 na kutoka Dar es Salaam hadi Kigali ni kilometa 1400, suala alilodai wafanyabiashara wataangalia umbali katika kutafuta faida ya kazi wanazozifanya.

Alieleza kuwa mkakati mwingine wa kuwafanya wafanyabishara wazidi kuitumia bandari ya Dar es Salaam ni kupunguza vizuizi vya njiani kutoka 15 vya sasa hadi vitatu.

Alisema kuwa na vizingiti vingi barabarani ni tatizo huku akiwashangaa askari wanaosimamisha magari yenye lakiri ambazo hawawezi kuzifungua na kueleza hali hiyo ni kero kwa madereva na wafanyabiashara.

Juzi, msemaji wa Chama cha mizigo nchini (Tatoa) Elias Lukumay, aliiambia kamati ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi za Rwanda na Uganda zimekubaliana kutumia bandari ya Mombasa kutokana na urasimu unaodaiwa kuwepo katika bandari ya Dar es Salaam.

Alisema nchi hizo zimekubaliana kuanza kutumia bandari ya Mombasa kuanzia Septemba mwaka huu.

Uamuzi huo wa Rwanda na Uganda unatafsiriwa kuwa unatokana na msigano wa kisiasa ulioibuka hivi karibuni baina ya Rais Jakaya Kikwete na Paul Kagame wa Rwanda baada ya ushauri wake wa kumtaka Kagame akutane na waasi kwa ajili ya kujadili amani ya taifa lao

Kuna mapungufu matatu kwenye kauli ya Sitta... Kwanza amekubali kuna ugomvi kati ya kikwete na kagame wao personall na sio nchi ya tanzania na rwanda jambo ambalo ni tofauti na kauli ya bosi wake anayeseama hakuna mgogoro na rwanda na yeye alichoongea ilikuwa ni ushauri tuu.... sasa huo ugomvi anaueleza yeye ni upii?!!! kama mwanadiplomasia hakupaswa kuongelea mgogoro wa marais wawili kama kitu ambacho ni personal weakness za kikwete na kagame... hii kwa upande mwingine ni dharau kubwaa..
Pili serikali ina maamuzi makubwa ya kuwafanya wafanyabiashara wapi wanunue au wauze bidhaa na kauli yake kwamba, ''"Mimi ninachojua suala la hapa ni uchumi. Huu ugomvi wa wanasiasa wawili hauwezi kuwakimbiza wafanyabiashara na ukiangalia wanaopitisha mizigo ni wafanyabiashara na si serikali zinazolumbana," ni utata na inaonyesha hii nafasi haiwezi hata kidogo.. Hivi anawaambiaje wakulima wa mahindi sumbawanga? ni kwanini serikali inawazuia wasipeleke mahindi zambia na drc ambapo watapata faida kubwa na kuinua maisha yao??? kwanini serikali ilizuia uvushaji wa sukari kwenda Kenya hali ya kuwa wafanyabiashara wangefaidika na kuinuka kiuchumii??!! Sasa basi kama serikali ya tanzania iliweza kuzuia bidhaa zisitoke kuelekea kenya zambia au drc rwanda inashindwa nini kulazimisha bidhaa zake zote zisipitie tanzania?!!
Tatu, anakiri kuwa vizuizi ni vingi na polisi wanaongeza ucheleweshwaji na usumbufu wa usafirishaji wa mizigo kwa kusimamisha gari ambazo hawana hata uwezo wa kuzikagua... Swali je hili mbona limeongelewa muda mrefuuu, mlikuwa masubiri nini kuondosha hiii keroo??!! Mpaka rwanda na uganda watishie kujitoa ndio mfanyie kati urasimu ulikuwa unaiitia hasara nchii?!! Lori za mizigo zilikuwa zinapoteza wastani wa masaa matano kwenye foleni za mizani na ukaguzi usio wa lazima wa trafiki wengi walio katika check point za barabaranii, muda huu ni mabilioni ya fedha kwa mwakaa.. Je serikali ina mpango gani wa kutumia technologia katika kuthibitia mwendo wa magari badala ya kuweka trafiki check point tano hadi sita katika barabara moja ndani ya mkoaa?!!
 
Bwana acha wahame kama wanataka sisi hatuwezi kuwalazimisha! Kama wanaona hailipi kusafirishia kupitia bandari ya Salama na waache na wala wasitutishe! Ila jambo la msingi ni kuondoa vikwazo yaani vizuizi barabarani ili kuwavutia wafanyabiashara wengi zaidi kuitumia bandari ya salama!
Burundi hawana tatizo kwani kikao walikaa Marais watatu ni kweli mombasa ni mbali sana lakini Mombasa hawana usumbufu bandarini kama Dsm na pengine gharama za usumbufu ni kubwa kuliko umbali toka mombasa hadi Uganda na Rwanda ikumbukwe pia wakati mwingine mizigo ya Rwanda hupita Sirari Tarime hadi kagera na kuingia Rwanda je?wakiamua kuhama Dsm kwenda mombasa hawatapitia Tanzania?
 
Rais aseme hatuna ugomvi na Rwanda halafu Cabinet minister tena wa wizara ya EAC anakubali kuna ugomvi kati ya wanasiasa hawa wawili yaani Kikwete na Kagame !

Sitta yuko sahihi; beleshi analiita beleshi wala sio kijiko kikubwa kama boss wake anavyotaka tuamini! ukifuatilia kwa makini kauli na body language ya maafisa waandamizi wa serikali ya Rwanda utakubaliana na Sitta kwamba "tunagombana" lakini hatujafikia mahali pa kipigana; lakini zingatia kwamba mwanzo wa ngoma ni lele!!
Lakini nasita kukubaliana na Sitta kwamba ugonvi wa wanasiasa wawili wa ngazi ya Urais hauwezi kusababisha athari za kiuchumi kwa Tanzania, hata kidogo;
kauli za Charles Njonjo, mwanasheria mkuu wa Kenya 70's kwamba "Tanzania is a man eat nothing society" na sisi tukijibu "ubepari ni unyama" zilipelekea kuvunjika kwa jumuia ya afrika mashjariki with all its attendant consequences; case ya vita vya Uganda likewise, the rest is history!!
 
Samuel Sitta mtu makini sana na mpenda haki ndio mana ccm wakamtoa kwenye kiti cha spika wa bunge
 
Burundi hawana tatizo kwani kikao walikaa Marais watatu ni kweli mombasa ni mbali sana lakini Mombasa hawana usumbufu bandarini kama Dsm na pengine gharama za usumbufu ni kubwa kuliko umbali toka mombasa hadi Uganda na Rwanda ikumbukwe pia wakati mwingine mizigo ya Rwanda hupita Sirari Tarime hadi kagera na kuingia Rwanda je?wakiamua kuhama Dsm kwenda mombasa hawatapitia Tanzania?

inatengenezwa reli kutoka mombsa hadi uganda then mkeka kampala-mbarara-Kagitumba-Kigali sirari tena?
 
ugomvi wa wanasiasa wawili....? atleast tumeelewa kinachoendelea....TZ na RWND zilikuwepo kabla yao..na ztakuwepo baada yao. nivyema tuhakikishe hatupotezi mapato yetu kiuchumi kisa wanasiasa wenye nia zao tofauti na malengo ya wananchi wanaowaongoza...
 
mmh.....sitta alifaa abaki tu kwenye u-spika huku kapotea kabisa....serikali ina say kubwa kwa wafanyabiashara wake kuhusu wapi watrade na wapi wasi-trade....mfano hai kuna mfanyabiashara wa mchele alikuwa akinunua maeneo ya shinyanga na mwanza kipindi cha nyuma....guesss what mara ya mwisho kupigiwa simu alisema hatoweza kuendelea na hiyo business kwa sasa kwa sababu ya hali ya kisiasa kati ya tZ na RW,"hali ikikaa vizuri tutaendelea" (Kayumba)...alafu umbali si issue sana kama ukiritimba na rushwa za hapa zinapelekea gharama kuongezeka hata zaidi ya gharama za umbali wa km 1000....jua gharama za umbali zinajulikana kabla predetermined ila rushwa na ukiritimba mwingine haupo predetermined .....they will definitely choose the best option....nakubali ushauri alotoa....zile nyingine zilikuwa longo longo tu.....

Meandika mengi bt pumba tupu,pole sana ndugu hukufundishwa vzur shule ulioipitia.
 
Uchumi wa Tanzania utatikisika, huo ndio ukweli. Jambo la maana ni kuangalia tatizo lipo wapi ambalo wote tunalijua. Bandari yetu imejaa wezi na ushuru wetu umevuka mipaka, Vigogo wameua usafiri wa reli, wanatoza bei za juu kusafirisha mizigo na 18 wheelers zao
 
Na wewe unakuwa kama mtoto ambaye hajasoma wapi sitta kamtaja jk na kagame? Yeye kasema wanasiasa wawili wewe unajuaje kuwa ni jk na kagame kama siyo umbea,kwa nini isiwe slaa na jk au kagame na slaa au kenyatha na jk au vinginevyo acha kuwekea maneno watu mdomoni.

huhtaji kuwa na dgree kuelewa ujumbe wa sita...wote tunafahamu uhusiano wetu na rwanda kwa sasa sii sahii...na chanzo cha mgogoro chafahamika....sasa pengne utueleze jinsi slaa alivyosababisha hali hyo..otherwise wote ktk chama mpo sawa tu miwani za mbao. hamtazami kwa macho wanayotazamia wananchi mnao waongoza, mmelewa madaraka.
 
Sitta sitta sitta, stop your bootlicking unaramba mpaka ma------ ya jk? Kweli hakuna kitu kibaya kama kukosa confidence huu ushuzi unamwambia nani? Wewe umepewa na nani authority ya kuwasemea wafanyabiashara wakati you know nothing kuhusu biashara isipokua kuiba public funds, waache tpsf na hao mawakala waongee ndio wanavaa hicho kiatu na kujua kinaumia wapi, you jus shut up! Msituone tumenyamaza watanzania sio wajinga kama wewe unatia kinyaa kabisa
 
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema ugomvi wa wanasiasa katika jumuia hiyo hauwezi kuathiri shughuli za kibiashara na uchumi wa Tanzania kwa kuwa wafanyabiashara wanaangalia faida zaidi katika shughuli zao.

Sitta alitoa kauli hiyo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua athari za kiuchumi zitakazopatikana baada ya kuwapo kwa taarifa ya wafanyabiashara wa Rwanda kutaka kupitisha mizigo yao katika bandari ya Mombasa badala ya ile ya Dar es Salaam.

Alisema kuwa taarifa ya wafanyabiashara wa Rwanda kuazimia kutumia bandari ya Mombasa si za ukweli na kwamba wanaofanya hivyo ni wale waliokosa zabuni mbalimbali ambazo pia hakuzitaja ni zabuni ya nini.

"Mimi ninachojua suala la hapa ni uchumi. Huu ugomvi wa wanasiasa wawili hauwezi kuwakimbiza wafanyabiashara na ukiangalia wanaopitisha mizigo ni wafanyabiashara na si serikali zinazolumbana," alisema.

Aliongeza kuwa migongano baina ya nchi na nchi haiepukiki hususan zilizo jirani na kuita hali hiyo ya mpito huku akisisitiza kuwa maelewano baina ya Tanzania na Rwanda yatarejea muda si mrefu.

Waziri Sitta alisema umbali kati ya Mombasa na Kigali ni kilometa 2300 na kutoka Dar es Salaam hadi Kigali ni kilometa 1400, suala alilodai wafanyabiashara wataangalia umbali katika kutafuta faida ya kazi wanazozifanya.

Alieleza kuwa mkakati mwingine wa kuwafanya wafanyabishara wazidi kuitumia bandari ya Dar es Salaam ni kupunguza vizuizi vya njiani kutoka 15 vya sasa hadi vitatu.

Alisema kuwa na vizingiti vingi barabarani ni tatizo huku akiwashangaa askari wanaosimamisha magari yenye lakiri ambazo hawawezi kuzifungua na kueleza hali hiyo ni kero kwa madereva na wafanyabiashara.

Juzi, msemaji wa Chama cha mizigo nchini (Tatoa) Elias Lukumay, aliiambia kamati ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi za Rwanda na Uganda zimekubaliana kutumia bandari ya Mombasa kutokana na urasimu unaodaiwa kuwepo katika bandari ya Dar es Sa
laam.

Alisema nchi hizo zimekubaliana kuanza kutumia bandari ya Mombasa kuanzia Septemba mwaka huu.

Uamuzi huo wa Rwanda na Uganda unatafsiriwa kuwa unatokana na msigano wa kisiasa ulioibuka hivi karibuni baina ya Rais Jakaya Kikwete na Paul Kagame wa Rwanda baada ya ushauri wake wa kumtaka Kagame akutane na waasi kwa ajili ya kujadili amani ya taifa lao

Waandishi wetu kweli mnachengua, sasa hapa ni somo gani ametoa Mh Sitta kwa viongozi hao wa Uganda na Rwanda? Je mna hakika kweli kwamba Uganda na Rwanda walikaa wakakubaliana kutotumia bandati ya Dar?
 
Sitta amefunguka vizuri actually amejaribu kubalance story,well said mzee wa standard and speed.
 
Katika hili tusibiri mawaziri kadhaa wengine kutoa matamko.

Ameanza:

1.WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta:"...taarifa ya wafanyabiashara wa Rwanda kuazimia kutumia bandari ya Mombasa si za ukweli...".

2. Atakuja Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe (maana unapotaja bandari ni eneo linalomuhusu), atasema: "...Wafanyabiashara wa Rwanda bado wanaitumia bandari ya Dar es Salaam...".

3. Atakuja Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Benard Membe (maana hili la kidiplomasia linamuhusu), atasema:"...Kama alivosema Rais wetu,hatuna ugomvi na Rwanda."

4. Atakuja Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi (linamuhusu pia hili la Rwanda), atasema:"...Agizo la Rais tumelitimiza kwa asilimia miamoja.Wahamiaji haramu wote kutoka Rwanda waliokuwa wakiishi Karagwe, tumewarudisha kwao..."

5....orodha inaendelea (Waziri wa Ulinzi..." Jeshi liko imara...?

Maoni yangu
:
Wasemaji wakiwa wengi juu ya suala ambalo Rais amelitolea ufafanuzi ni rahisi kuupotosha umma. Wapishi wengi matokeo yake huunguza chakula.

Katika hili mheshimiwa Sitta yeye angesubiri vikao vyao atapokutana na mawaziri wenzie wa EAC ahoji kwanini marais 3:KKKs wamekuwa wakikutana peke yao bila kuwahusisha nchi wanajumuiya wengine kama Tanzania na Burundi?

Hayo mengine amejibu zaidi ya uwezo wake kimamlaka.
 
Rais aseme hatuna ugomvi na Rwanda halafu Cabinet minister tena wa wizara ya EAC anakubali kuna ugomvi kati ya wanasiasa hawa wawili yaani Kikwete na Kagame !
Mkuu wakati mwingine ni vigumu sana kumuelewa Mh.SITA, yeye ni mwana sheria kitaaluma mtu ungetegemea angetumia walao lugha ya kidiplomasia kidogo, sina shaka alijua fika Mh.JK alitoa kauli hile akiwa na wadhifa gani na alikuwa anawakilisha nchi/kitengo gani cha AU; sasa hili la Mh. Sitta kutoa impression as if ni ugomvi baina ya watu wawili wanaosigana, ana maana gani? Binafsi kauli ya Mh.Sitta inanipa wakati mgumu sana kuielewa!! Kama kauli hiyo ingetolewa na Waziri wa Rwanda ningelewa ni propaganda lakini inapotolewa na Waziri aliye teuliwa na JK kwenye Cabinet yake basi mtu mwenye akili timamu unajua kauli hiyo haikutolewa kwa bahati mbaya, kuna tatizo - somewhere. Nasema hivi, kama Mh.Sitta hana spirit ya collective leadership basi ningemshauri ajiuzuru wadhifa wa Uwaziri ili ajiweke huru kusema apendalo.
 
Hapa inaonekana,hata sita mwenyewe yupo,upande wa kagame.mbona kipindi hiki haja fwatuka,namaneno yake kama anapo washambulia wabunge,waviti maalum,napia kama waziri wadhamana haja wauliza wenzake mawaziri,hivyo vikao vyao vya nchi tatu badala ya nchi tano maana yake nini?east afrika ya sasa niunafiki.



Mkuu umetoka kujichamba nini? Sitta kasema haya kwa sababu alikuwa anajibu hoja ama maswali aliyokuwa anaulizwa na waandishi wa habari. Sasa unataka Sitta atoke huko anakotoka then aanze kuongea tu, si mtasema anaropoka? Mkuu ulikuwa hauna haraka kihivyo, siku nyingine malizia kwanza kujichamba kabla ya kuja hapa kudandia hoja usizozijuwa.
 
Back
Top Bottom