Samsung wanatuibia kwenye hizi A

Nina bajeti ya 800-850k naombeni mnielekeze nikanunue simu ya specs zipi. Ila mimi ni mpenzi wa Samsung. A72 zipo au A71? Na ni bei gani?
 
Hizi A series ni mid range ndio maana haziko kwenye top quality
Sema tafuta hela hakuna finger print inakaa nyuma ya simu
 
Sasa nitafute ipi mkuu? Ninayo A70 ila imezimika tu ghafla leo na tatizo sijui ni nini na nimekaa nayo miaka miwili tu

Watu kibao wanalia na A series hata iweje usinunue Samsung A maana ni tatizo unaweza kaa nayo mwaka halafu ikazima ghafla

Navyokwambia hapa kuna A imelala ndan ya begi ilizima hivyo hivyo
 
Oya nmeibiwa A20S vp naweza angaikia nkaipata
 
Watu kibao wanalia na A series hata iweje usinunue Samsung A maana ni tatizo unaweza kaa nayo mwaka halafu ikazima ghafla

Navyokwambia hapa kuna A imelala ndan ya begi ilizima hivyo hivyo
Kama huna ya ya kununua S series si bora ununue infinix

Mnanunua midubwana kisa brand name halafu mnaishia kulia
 
Mkuu Chief-Mkwawa samahani kidogo naomba kujua zaidi kuhusu simu aina ya Blackview Max1 na pia simu gani nyingine ambayo ni projector phone yenye bei ya kawaida
 
Mkuu Chief-Mkwawa samahani kidogo naomba kujua zaidi kuhusu simu aina ya Blackview Max1 na pia simu gani nyingine ambayo ni projector phone yenye bei ya kawaida
hii simu ni lowend sana mkuu, thamani yake around laki 2.

simu mpya mpya labda moto z force ya 2016 ina addon ya projector

ila kwa bei ya hizi simu why usinunue projector smart? kama Anker nebula capsule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…