Reuben Challe
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 2,761
- 5,050
- Thread starter
- #41
- Flagship ni zile simu ambazo kampuni ya simu inakuwa imewekeza teknolojia yake yote kwa asilimia kubwa na kuwa miongoni mwa simu bora zaidi kwenye mwaka husika. Lakini sio kila kampuni ya simu hutengeneza flagship, HMD Global hawatengenezi flagship kwa simu zao za Nokia. Karibia kila kitu kwenye flaghip ni highend. Kwa mfano Samsung Galaxy S22 Ultra, iPhone 14 Pro Max, Google Pixel 7 Pro, Xiaomi 12S Ultra, Xiaomi 13 Pro na Vivo X90 Pro Plus ni baadhi ya flagship za 2022. Simu hizi zinatumia chipset za juu zaidi kwenye smartphones za 2022 mfano Qualcomm Snapdragon 8 Gen 2, Bionic A16 chipset, Google Tensor G2, etc. Pia ni simu zenye uwezo na ubora wa hali ya juu zaidi kwenye kamera, kioo, software, features, charging speed, speakers, water resistance, gaming perfomance na kila kitu. Ni nzuri ila bei nazo zimechangamka Pia flagship huwa na muonekano premium ili kuzitofautisha na simu za bei rahisi. Flagship nyingi za 2022 zinapatikana kwa bei ya shilingi milioni 2 hadi 4 na kuendelea.Naomba mwenye uelewa hapa anifafanulie Nini maana ya flagship, midrange na official brand me haya nayasikia tu Kwan Nini hasa kwenye bidhaa za simu?
Je Zina utofaut gan?
- Midrange smartphones ni zile simu zenye uwezo wa kati. Yaani hazipo juu hazipo chini ni standard. Zinatumia chipset ambazo ni weaker kuliko chipset za flagship ila ni stronger kuliko chipset za low-end smartphones. Mfano midrange nyingi za Xiaomi ni baadhi ya Redmi na POCO, na kwa Samsung midrange ni baadhi ya A-series. Mfano wa midrange phones za 2022 ni Xiaomi Redmi Note 12 Pro, Samsung Galaxy A73 5G, Samsung Galaxy A53 5G. Xiaomi Redmi Note 12 Pro Plus, Infinix Note 12 Pro, Oppo Reno 7, TECNO Camon 19Pro, Xiaomi Civi 2, Xiaomi POCO F3 Pro, pamoja na simu nyingine nyingi. Chipset za midrange phones ni kama MediaTek Dimensity 700, Qualcomm Snapdragon 778G, MediaTek Helio G99 na kadhalika. Kwa midrange za 2022 be inaweza kuanzia laki 5 hadi milioni 1 na nusu.
- Low-end smartphone/ entry level smartphones ndio simu za chini hizi za laki tatu tatu laki nne, hizi zimejaa bila shaka unazijua bhana