ifweero
JF-Expert Member
- Jun 12, 2013
- 7,957
- 1,341
Mwigamba aende ccm pasipo na ubaguzi akapambane na ukoo wa mwinyi,nyerere,kawawa,karume,nnauye,makamba,malecela,kikwete
Kama ameuweza kuuvua nguo Ukoo wa MTEI na MBOWE CCM ataweza tu.
Mwigamba aende ccm pasipo na ubaguzi akapambane na ukoo wa mwinyi,nyerere,kawawa,karume,nnauye,makamba,malecela,kikwete
Hivi alichokizema yeye... WA CCM anaweza kusema dhidi ya VIONGOZI wakuu wa CCM? Kwanini ni kwa CHADEMA tu ndio VIONGOZI wakuu ni Wabaguzi? hawa ea CCM pia... Umejaribu kugombea U-NEC ndani ya CCM? kama haujulikwani na ukatoa hotuba nzuri watakubagua kwasababu wewe sio kwenye KUNDI LAO - A CULT WITHIN
Sasa where is the beef???
MBOWE na SLAA wakiwashinda , tutawatoa sisi tusiyo wanachama kwa sababu tunataka chama kiwe cha watu na siyo taasisi ya mtu.chadema mpango wa Mungu namna alivyo kamatwa msaliti Arusha inajizihilusha kuwa chadema ni mipango ya Mungu..
Sasa si aende huko ambako hakuna ubaguzi au ukanda au hakuna kupigwa au hakuna wasaliti anachosubiri na kulalamika ni nini.
Na swali jingine kwani chama ni CDM tuu kuna vyama vingi kuna CCM kuna NCCR kuna TLP aende huko hakuna ubaguzi wala maneno mengi mbona anang'ang'ania tuu hapa na kutoa matamko mengi na wanamshabikia na kumuanzishia thread ni wale wale waliotuma kufanya kazi yake
Mgogoro wa CHADEMA ni wa wanachadema, wengine ni watazamaji tu na wala msitafute mchawi kwingine. MBOWE na SLAA wakubali tu wameshindwa kutokana na uchu wa madaraka na Ubinafsi na hivyo wakae pembeni wengine wakivushe chama kutoka hapo kinapotaka kuzamia.
Hii wiki ni wiki ya neema Lumumba...s
Lengo ni kukinusuru CHADEMA na si vinginevyo, Akiondoka CHADEMA bado kinaendelea kuendeshwa kama Kampuni, Ni lazima akomae huko huko ili wa-ufyate.
MBOWE na SLAA wakiwashinda , tutawatoa sisi tusiyo wanachama kwa sababu tunataka chama kiwe cha watu na siyo taasisi ya mtu.
Hao watazamaji mbona wamekuwa wao ni wapambe wakubwa wa kutoa na kuandika mabandiko humu
Watazamaji wamekuwa marefa na waamuzi wa pambano badala ya kuwaachia refa na waamuzi wake wamalize mchezo wao
Wasingekuwa wasemaji wakubwa kwani humu tungeona kila saa mabandiko ya Samsom Mwigamba au ya akina Slaaa na Mbowe na Zitto si wageyamalizia huko huko
Kuna vikao vyao na wana nafasi zao kusuluhisha mambo yao ila kila muda mada ni hizo hizo as if hatuna matatizo yetu yanayotukabili
yaani ccm mtuchagulie mwenyekiti na katibu hilo halitatokea..
Hakuna cha kunusuru chama hapa
Huwezi ukatoka nje ya utaratibu na then utegemee refa wa mchezo akuachie tuu kwa vile ukitolewa nje mchezo utaharibika
Na kupambana na refa unajua adhabu yake ni kutolewa kwa kadi nyekundu tuu na unatolewa nje ya uwanja kabisa
Sasa huko nje ya uwanja katafakari na ujione ni wapi ulikosea na kisha urudiufuate sheria za mchezo na sio kujiamulia tuu kucheza rough zako ambazo kisheria hazipo
Iwapo una malalamiko kuna waamuzi mpaka wa akiba na una meneja wako na kocha wako nenda kalalamike huko na nahodha wa mpira pia yupo lalamika kwake ya nini kulalamika kwa watazamaji ambao hawatakusaidia lolote
Vita ya PANZI, furaha ya KUNGURU. sisi watazamaji ni kama kunguru tu, panzi ni CHADEMA kwa CHADEMA na siyo vinginevyo.
kwa mtu yeyote atakayejitokeza na kusema kwamba uongozi wa chadema haufai sisi wanachadema hatuwezi kumuelewa, yaani ni sawa sawa na mtu kujifanya ni baselona alafu anasema mesi asipangwe eti anaaribu mpira
MBOWE na SLAA wenyewe na wafuasi wao wakuu humu JF kama Ben Saanane, molemo na wiegine wameshakubali matokeo mmebaki ambao hamjui lolote kuhusu abc za CHADEMA.
Sawa hao panzi wapo waleni wakamateni muwale mtuachie mambo mengine yaongelewe maana unaweza kushuhudia mpambano wa panzi siku nzima na wewe kunguru una njaa haina maana mkamate panzi mhusika umle na uache kupiga piga kelele za njaa
Umeshaona CDM ina ukabila au ukanda au sijui ni chama cha familia nenda kwenye chama ambacho hakina hayo na uache kukaa na kutoa matamko kila kukicha na waandishi watasema na ambayo hukusema kisa kwa kuwa unajua kutumia chombo cha habari
Kulalamika ni dalili ya kuwa una makosa na unalalamika uonewe huruma na ukishaona kuwa mambo hayaendi hapa jiondoe mapema
We umekaa kwenye gema na unaliona linaanguka badala ya kuondoka unaishia kumlalamikia fulani ndio alichimba mtaro hapo gema litaenda na wewe na utaishia huko
bado kidogo utaanza kujiuliza maswali na kujijibu