Duc in altum
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 2,076
- 4,645
Nero ni alikuwa mfalme wa Roma aliyechukiwa zaidi katika historia ya Roma mpaka kupelekea kujiua.
Nero ni nani!?
Nero alizaliwa dec 15, AD 37, katika makuzi yake akiwa mvulana alipenda sana muziki na sanaa sana sana.
Alikuwa mtoto wa Agrippina Nero alimpenda sana mama yake Nero alikuwa mfalme akiwa na miaka 16 tu.
Agripinna ni nan!?
Agripina alikuwa mtoto wa moja ya mashujaa wa Rome aitwaye Germanicus.
Agrippina alikuwa mrembo, mwenye akili nyingi na mchora michoro(master plan). Agrippina kwa kuwa alikuwa mtoto wa mashujaa wa roma alikulia ikulu pamoja na nduguze. Agrippina amekua akizungukwa na watu wenye ushawishi kama wazee wa mahakama alijipatia uwezo wa ushawishi(art of manipulation). Wanaume walimpenda na kutaka kumuoa lakini yeye alikuwa na mahusiano na kaka yake wa damu Caligula kitu kilichopelekea scandal kubwa ndani ya ikulu. Mjomba wake mfalme wa roma Tiberius akaamua kumuozesha kwa Gnaeus, mtu tajiri ila mwenye mambo mengi na hakuwa na mda na Agrippina sana. Hapo ndipo Nero alipozaliwa.
Baada ya mfalme Tiberius kufaliki mwaka 37AD.., kaka yake Agrippina Caligula akawa mfalme. Mfalme Caligula hakuwa na mipaka kwenye mapenzi alilala na yeyote wanaume, wanawake, hata mtu wa familia yake kama Agrippina ilivyokuwa. Alisema kuwa mfalme alikuwa halazimiki kufuata sheria yeyote. Baadae akaamua kumuoa dada yake wa damu Julia. Licha ya kumuoa Julia mfalme Caligula bado alimtaka na dada yake Agrippina, baada ya kuona Agrippina ameshapata mtu mwingine na hana mda nae kwa wivu akaamua amfukuze Roma na kumnyang'anya mtoto wake Nero aliyekuwa na miaka miwili tu na kumpeleka kwa shangazi yake kuishi kule.
Baada ya mwaka mmoja baba yake na Nero akawa amefariki.
Mwaka 49 A.D. mfalme Caligula akawa ameuwawa, mjomba wake claudius akawa mfalme, Cladius akawa amemuita mpwa wake Agrippina arudi Roma aje aungane na mtoto wake Nero. Agrippina baada ya kurudi akaanzisha kampeni ya kumugombanisha mfalme Cladius na mke Messalina, akamtafutia tuhuma zisizo eleweka mpaka mfalme akamchukia na kupelekea kuuwawa. Agrippina kuona amefanikiwa hilo akaanza kupanga mipango mfakme amuoe yeye kitu kilicho fanikiwa sasa akanza kumshawishi mfalme amchukue Nero kama mtoto wake(am-adopt) na awerithi wa ufalme na amuache mtoto wake wa damu Britanicus.
Agrippina mwenye shauku ya kisiasa alitumia ushawishi wake wa kimapenzi bongo tungesema libwata kumshawishi mfalme mpaka mtoto wake awe mrithi wa ufalme, alikuwa hana huruma na mtu alimuua yeyote aliyesimama kwenye njia ili afanikishe jambo lake. Na kweli alifanikiwa Nero akawa mfalme akiwa na miaka 16 tu, Agrippina akawa anajiona yeye na mfalme Nero mtoto wake kama wote ni wafalme na sarafu ikatengenezwa mwanzoni wa utawala wa Nero ikiwa na picha ya Nero na mama yake.
Agrippina alitaka Nero amsikilize kwa kila kitu na atawale kwa maelekezo yake, Nero alipoanza kuzoea madaraka na kukua akaanza kutaka uhuru, mama yake akaanza kuchukia akaanza kuchora michoro ya kumtoa kwenye kitu huyo mtoto wake kwa kumuua.
Nero alipo tulia kwenye kiti akaanza kumuweka mbali mama yake kwenye mambo ya utawala, akaanza kukataa ushauri wake, mama yake alitaka Nero atawale kwa mkono wa chuma(dictator) tukumbuke roma japo inamfalme lakini ilikuwa na senate(ni kama bunge linalopitisha kila kitu na wafalme waliliheshimu), alitaka mtu yeyote anaye mpa changamoto amuue. Nero alikaa ushauri huo kutoka kwa mama yake.
Agrippina alitaka mwanae awe mtiifu kwake na Nero alipoanza kukataa ushauri wa mama yake, mama yake alianza kupoteza uoenda nae na kumchukia taratibu akaanza kupanga mipango ya kumuondoa madarakani na kumuua. Agrippina alianza kumtisha Nero kwa wazi kabisa kuwa atamuua na kumuweka madarakani Britaniccus yule mrithi halali wa ufalme. Usiku mmoja kwenye chakula cha usiku, Britannicus alianguka ghafla chini na kufa masaa machache baadae. Nero alisema aliugua ghafla na kufa lakinj mama yake Agrippina alisema Britannicus amepewa sumu na Nero. Mda haukupina Nero alituma wauaji wakamuue mama yake Agrippina akiwa nyumbani kwake.
Wakazi wa Roma waliposikia habari hizo walishtuka japo walikuwa wanasema Agrippina alikuwa na ushawishi mbaya(negative influence) ndani ya ufalme huo. Kwa sauti za chini wakawa wanasema mfalme ndiye aliyemuua Agrippina.
Walisema kama Nero anaweza kumuua mama yake mzazi hakuna kitu anashindwa kufanya.
Miaka ya mwanzo ya utawala wa Nero ilijawa na kila aina ya anasa kumbuka aliingia akiwa na miaka 16 tu, alitumia pesa na akiba ya mali katika kufanya vitu vya burudani kama michezo, matamasha, sanaa na kila aina ya burudani iliyo fahamika Roma ya wakati huo. Kitu hicho kililichukiza sana bunge la senate kwa sababu senate ilitakiwa ipitishe kila matumizi na iidhinishe kama yana tija kitu ambacho Nero hakufany na Nero hakujali kabisa uwepo wa senate japo walipinga matumizi hayo Nero hakuwa na mda nao. Nero alipendwa sana miaka ya mwanzoni kwa sababu ya matamasha na michezo aliyo waandalia watu.
Miaka mitano ya utawala wake ilikuwa miaka ya utulivu, amani na furaha ndani ya Roma jamii ilimpenda sana sana kipindi hichi Nero alifanya vyote lakini hakuwa na udictator wa kuua watu wala kuzuia watu wasiseme. Washauri wake wakuu Seneca na Afranius walikuwa wakimshauri asifuate njia za watawala wa zamani za kuua watu katika utawala wake Nero alifuata ushauri wao na kiuhalisia Nero hakuwa akijari mambo ya siasa na utawala yeye alijali mambo yake ya sanaa.
Ni kama Seneca na Afrinius Nero aliwaachia waamue wanavyoona yeye alikuwa anafocus na mambo yake ya michezo na sanaa aliyo ipenda kuliko chochote.
Nero alikuwa akiandika mashairi, alisoma visa vya ugriki na kuchukua madarasa ya kuimba. Hii ni miaka ya mwanzo bado hata hajamuua Agrippina wala mtu yeyote. Agrippina akawa anamsihi aachane na sanaa ajikite kwenye utawala.
Nero alianza kuwa anaigiza mbele ya watu, anaimba aliwakonga nyoyo watu wananchi hasa watabaka la chini. Japo tabaka la juu liliona kama anapotokawatu wa hali za kawaida walifurahishwa na michezo hiyo ya Nero.
Siku zimeenda watu wakaanza kuchoshwa na michezo hiyo ya Nero waanza kupunguza kugudhuria matamasha yake na kutokimshangilia akiwa anaimba au kuigiza kwenye hayo matamasha yake. Nero akaanza kukosolewa kwenye utawala wake, Watumishi wa mfalme Nero kuona Nero amaenza kupoteza ushawishi wake wakaanza kulipa kisiri watu wakamuone mfalme akiwa anaimba na kufanya sanaa zake ili mfalme Nero ashangiliwe, Nero kuona anashangiliwa zaidi Nero alibakia kwenye stage hata kwa masaa zaidi ya aliyo panga akijua anashangiliwa kweli kweli na akazidi kufanya sanaa zake mara kawa mara kwa masaa mengi kufurahisha waliolipwa kumshangilia.
Licha ya mashabiki wa kulipwa nao walianza kuchoka, wakawa hawamalizi mda kidogo wanaondoka, kitu kilichofanya milango ya uwanja iwe inafungwa ili watu wasitoroke kabla mfalme hajamaliza sanaa zake.
Washauri wake wakuu kwenye mambo ya utawala Seneca na Afrinius wakaamza kuchoka sasa kuona vituko vya mfalme. Mfalme, akiwa anavizia watu njiani na wasaidizi wake ili wake usiku awalazimishe kuangalia maigizo yake. Mtu mmoja aliyetaka kumlazimisha amuangalia alimpiga ngumi ya jicho na kumiacha na jicho jekundu bila kujua yule ni mfalme na kesho yake ndio kujua alipiga mfalme akaamua kujinyonga.
Washauri wa Nero sasa wakaamua wamtafutie mke Nero akakubali wakawa wamemuozesha binti aitwaye Acte wakiwa wanaamini anaweza kutulia akioa.
Baada ya miaka michache ule utawala wa Nero wa amani ukawa umekoma akaagiza mama yake Agripinna auwae na mke wake Acte auwawe.
Afrinius mshauri wake hakuka mda akawa amekufa na akamua kumteua Tigellinus mtu wa rushwa na asiye na maadili. Mshauri wake huyy mpya akamshauri arudishe ile michezo ya watu kuuliwa hadharani( walio angalia movie za gladiator wanaelewa) Nero akairudisha na akaanza kutoa amri kwa mtu yeyote ndani ya serikali yake ajiue akimhisi tu kwa kitu chochote.
Seneca kuona hivyo akaanza kuomba astaafu kwa usalama wake akisema umri wake umemtupa mkono na hali yake ya kiafya inazorota Nero akakubali akampa nafasi yake Rufus aliye kuwa senator.
Bila Seneca na Africanius Nero akawa dikteta kamili akazidi kuua watu hovyo bila hata makosa ya kueleweka akanza kuchota pesa kujijengea ikulu yake yenye vyumba 300. Aliacha kazi zake za kifalme ili awa muigizaji na muimbaji kwenye majukwaa ya michezo Nero alikuwa delusinal kiasi kwamba aliamini hata wapinzani wake vitani anaweza kuwashinda vita kwa kuimba tu.
Kuanguka kwa utawala wake, baada ya kutumia pesa na akiba zote kwenye michezo Nero hakuweza kurudisha ushawishi wake kwenye jamii, Roma ilikumbwa na balaa la njaa na ukame kutokana kutumia akiba yote. Watu wakaanza kumpinga wazi wazi, Nero hakujali akaamua aende matembezini ugriki na akaicha Roma kwa moja mshuauri wake Helius.
Nero akafika ugriki akanza kufanya matamasha yake ya kuigiza, kuimba na kushindana na waimbaji wa ugriki kwenye matamasha yao, pamoja na kukimbia kwa farasi. Kwenye hayo mashindano mara zote aliibuka kidedea. Utawala wale kama mfalme ulikuwa kama njia ya kukuza hadhi yake kijamii na umaarufu na sio kutatua changamoto za wananchi wake.
Nero kuigiza na kuimba kwake ilikuwa kila kitu na hakujali kingine. Watu wa Roma kuona mfalme wao ameendoka na kuwaacha kicha ya ukame na njaa yeye ameenda kuigiza na kuimba nchi nyingine waliona amewasaliti na kuwatenga. Waliona kama anawakejeli na dharau ya hali ya juu kwenda kuigiza na kuimba nchi nyingine.
Ukosefu wa chakula na kutokuwepo kwa mfalme kuliwachukiza sana wananchi majimbo ya Roma kama uhispania na Africa(egpt) yakaanza yakaanza kukataa kuutambua utawala wa Nero.
Kutona na hali hiyo Helius aliyekuwa amemuachua madaraka kamuomba mfalme arudi Roma na mwaka 68 A.D Nero akarudi.
Kutokana na Nero kuwatenga watu wake mda mrefu Senate(bunge) na Praetorian(Jeshi la ulinzi wa mfalme) wakaacha kumtambua kama mfalme na kumuondoa madarakani, Nero akatangazwa kama adui wa Roma. Kuona hivyi Nero aliamua kujichoma kisu kwenye koo na kufa.
Wakati anakufa alisema"what an artist dies in me".
Nero ni nani!?
Nero alizaliwa dec 15, AD 37, katika makuzi yake akiwa mvulana alipenda sana muziki na sanaa sana sana.
Alikuwa mtoto wa Agrippina Nero alimpenda sana mama yake Nero alikuwa mfalme akiwa na miaka 16 tu.
Agripinna ni nan!?
Agripina alikuwa mtoto wa moja ya mashujaa wa Rome aitwaye Germanicus.
Agrippina alikuwa mrembo, mwenye akili nyingi na mchora michoro(master plan). Agrippina kwa kuwa alikuwa mtoto wa mashujaa wa roma alikulia ikulu pamoja na nduguze. Agrippina amekua akizungukwa na watu wenye ushawishi kama wazee wa mahakama alijipatia uwezo wa ushawishi(art of manipulation). Wanaume walimpenda na kutaka kumuoa lakini yeye alikuwa na mahusiano na kaka yake wa damu Caligula kitu kilichopelekea scandal kubwa ndani ya ikulu. Mjomba wake mfalme wa roma Tiberius akaamua kumuozesha kwa Gnaeus, mtu tajiri ila mwenye mambo mengi na hakuwa na mda na Agrippina sana. Hapo ndipo Nero alipozaliwa.
Baada ya mfalme Tiberius kufaliki mwaka 37AD.., kaka yake Agrippina Caligula akawa mfalme. Mfalme Caligula hakuwa na mipaka kwenye mapenzi alilala na yeyote wanaume, wanawake, hata mtu wa familia yake kama Agrippina ilivyokuwa. Alisema kuwa mfalme alikuwa halazimiki kufuata sheria yeyote. Baadae akaamua kumuoa dada yake wa damu Julia. Licha ya kumuoa Julia mfalme Caligula bado alimtaka na dada yake Agrippina, baada ya kuona Agrippina ameshapata mtu mwingine na hana mda nae kwa wivu akaamua amfukuze Roma na kumnyang'anya mtoto wake Nero aliyekuwa na miaka miwili tu na kumpeleka kwa shangazi yake kuishi kule.
Baada ya mwaka mmoja baba yake na Nero akawa amefariki.
Mwaka 49 A.D. mfalme Caligula akawa ameuwawa, mjomba wake claudius akawa mfalme, Cladius akawa amemuita mpwa wake Agrippina arudi Roma aje aungane na mtoto wake Nero. Agrippina baada ya kurudi akaanzisha kampeni ya kumugombanisha mfalme Cladius na mke Messalina, akamtafutia tuhuma zisizo eleweka mpaka mfalme akamchukia na kupelekea kuuwawa. Agrippina kuona amefanikiwa hilo akaanza kupanga mipango mfakme amuoe yeye kitu kilicho fanikiwa sasa akanza kumshawishi mfalme amchukue Nero kama mtoto wake(am-adopt) na awerithi wa ufalme na amuache mtoto wake wa damu Britanicus.
Agrippina mwenye shauku ya kisiasa alitumia ushawishi wake wa kimapenzi bongo tungesema libwata kumshawishi mfalme mpaka mtoto wake awe mrithi wa ufalme, alikuwa hana huruma na mtu alimuua yeyote aliyesimama kwenye njia ili afanikishe jambo lake. Na kweli alifanikiwa Nero akawa mfalme akiwa na miaka 16 tu, Agrippina akawa anajiona yeye na mfalme Nero mtoto wake kama wote ni wafalme na sarafu ikatengenezwa mwanzoni wa utawala wa Nero ikiwa na picha ya Nero na mama yake.
Agrippina alitaka Nero amsikilize kwa kila kitu na atawale kwa maelekezo yake, Nero alipoanza kuzoea madaraka na kukua akaanza kutaka uhuru, mama yake akaanza kuchukia akaanza kuchora michoro ya kumtoa kwenye kitu huyo mtoto wake kwa kumuua.
Nero alipo tulia kwenye kiti akaanza kumuweka mbali mama yake kwenye mambo ya utawala, akaanza kukataa ushauri wake, mama yake alitaka Nero atawale kwa mkono wa chuma(dictator) tukumbuke roma japo inamfalme lakini ilikuwa na senate(ni kama bunge linalopitisha kila kitu na wafalme waliliheshimu), alitaka mtu yeyote anaye mpa changamoto amuue. Nero alikaa ushauri huo kutoka kwa mama yake.
Agrippina alitaka mwanae awe mtiifu kwake na Nero alipoanza kukataa ushauri wa mama yake, mama yake alianza kupoteza uoenda nae na kumchukia taratibu akaanza kupanga mipango ya kumuondoa madarakani na kumuua. Agrippina alianza kumtisha Nero kwa wazi kabisa kuwa atamuua na kumuweka madarakani Britaniccus yule mrithi halali wa ufalme. Usiku mmoja kwenye chakula cha usiku, Britannicus alianguka ghafla chini na kufa masaa machache baadae. Nero alisema aliugua ghafla na kufa lakinj mama yake Agrippina alisema Britannicus amepewa sumu na Nero. Mda haukupina Nero alituma wauaji wakamuue mama yake Agrippina akiwa nyumbani kwake.
Wakazi wa Roma waliposikia habari hizo walishtuka japo walikuwa wanasema Agrippina alikuwa na ushawishi mbaya(negative influence) ndani ya ufalme huo. Kwa sauti za chini wakawa wanasema mfalme ndiye aliyemuua Agrippina.
Walisema kama Nero anaweza kumuua mama yake mzazi hakuna kitu anashindwa kufanya.
Miaka ya mwanzo ya utawala wa Nero ilijawa na kila aina ya anasa kumbuka aliingia akiwa na miaka 16 tu, alitumia pesa na akiba ya mali katika kufanya vitu vya burudani kama michezo, matamasha, sanaa na kila aina ya burudani iliyo fahamika Roma ya wakati huo. Kitu hicho kililichukiza sana bunge la senate kwa sababu senate ilitakiwa ipitishe kila matumizi na iidhinishe kama yana tija kitu ambacho Nero hakufany na Nero hakujali kabisa uwepo wa senate japo walipinga matumizi hayo Nero hakuwa na mda nao. Nero alipendwa sana miaka ya mwanzoni kwa sababu ya matamasha na michezo aliyo waandalia watu.
Miaka mitano ya utawala wake ilikuwa miaka ya utulivu, amani na furaha ndani ya Roma jamii ilimpenda sana sana kipindi hichi Nero alifanya vyote lakini hakuwa na udictator wa kuua watu wala kuzuia watu wasiseme. Washauri wake wakuu Seneca na Afranius walikuwa wakimshauri asifuate njia za watawala wa zamani za kuua watu katika utawala wake Nero alifuata ushauri wao na kiuhalisia Nero hakuwa akijari mambo ya siasa na utawala yeye alijali mambo yake ya sanaa.
Ni kama Seneca na Afrinius Nero aliwaachia waamue wanavyoona yeye alikuwa anafocus na mambo yake ya michezo na sanaa aliyo ipenda kuliko chochote.
Nero alikuwa akiandika mashairi, alisoma visa vya ugriki na kuchukua madarasa ya kuimba. Hii ni miaka ya mwanzo bado hata hajamuua Agrippina wala mtu yeyote. Agrippina akawa anamsihi aachane na sanaa ajikite kwenye utawala.
Nero alianza kuwa anaigiza mbele ya watu, anaimba aliwakonga nyoyo watu wananchi hasa watabaka la chini. Japo tabaka la juu liliona kama anapotokawatu wa hali za kawaida walifurahishwa na michezo hiyo ya Nero.
Siku zimeenda watu wakaanza kuchoshwa na michezo hiyo ya Nero waanza kupunguza kugudhuria matamasha yake na kutokimshangilia akiwa anaimba au kuigiza kwenye hayo matamasha yake. Nero akaanza kukosolewa kwenye utawala wake, Watumishi wa mfalme Nero kuona Nero amaenza kupoteza ushawishi wake wakaanza kulipa kisiri watu wakamuone mfalme akiwa anaimba na kufanya sanaa zake ili mfalme Nero ashangiliwe, Nero kuona anashangiliwa zaidi Nero alibakia kwenye stage hata kwa masaa zaidi ya aliyo panga akijua anashangiliwa kweli kweli na akazidi kufanya sanaa zake mara kawa mara kwa masaa mengi kufurahisha waliolipwa kumshangilia.
Licha ya mashabiki wa kulipwa nao walianza kuchoka, wakawa hawamalizi mda kidogo wanaondoka, kitu kilichofanya milango ya uwanja iwe inafungwa ili watu wasitoroke kabla mfalme hajamaliza sanaa zake.
Washauri wake wakuu kwenye mambo ya utawala Seneca na Afrinius wakaamza kuchoka sasa kuona vituko vya mfalme. Mfalme, akiwa anavizia watu njiani na wasaidizi wake ili wake usiku awalazimishe kuangalia maigizo yake. Mtu mmoja aliyetaka kumlazimisha amuangalia alimpiga ngumi ya jicho na kumiacha na jicho jekundu bila kujua yule ni mfalme na kesho yake ndio kujua alipiga mfalme akaamua kujinyonga.
Washauri wa Nero sasa wakaamua wamtafutie mke Nero akakubali wakawa wamemuozesha binti aitwaye Acte wakiwa wanaamini anaweza kutulia akioa.
Baada ya miaka michache ule utawala wa Nero wa amani ukawa umekoma akaagiza mama yake Agripinna auwae na mke wake Acte auwawe.
Afrinius mshauri wake hakuka mda akawa amekufa na akamua kumteua Tigellinus mtu wa rushwa na asiye na maadili. Mshauri wake huyy mpya akamshauri arudishe ile michezo ya watu kuuliwa hadharani( walio angalia movie za gladiator wanaelewa) Nero akairudisha na akaanza kutoa amri kwa mtu yeyote ndani ya serikali yake ajiue akimhisi tu kwa kitu chochote.
Seneca kuona hivyo akaanza kuomba astaafu kwa usalama wake akisema umri wake umemtupa mkono na hali yake ya kiafya inazorota Nero akakubali akampa nafasi yake Rufus aliye kuwa senator.
Bila Seneca na Africanius Nero akawa dikteta kamili akazidi kuua watu hovyo bila hata makosa ya kueleweka akanza kuchota pesa kujijengea ikulu yake yenye vyumba 300. Aliacha kazi zake za kifalme ili awa muigizaji na muimbaji kwenye majukwaa ya michezo Nero alikuwa delusinal kiasi kwamba aliamini hata wapinzani wake vitani anaweza kuwashinda vita kwa kuimba tu.
Kuanguka kwa utawala wake, baada ya kutumia pesa na akiba zote kwenye michezo Nero hakuweza kurudisha ushawishi wake kwenye jamii, Roma ilikumbwa na balaa la njaa na ukame kutokana kutumia akiba yote. Watu wakaanza kumpinga wazi wazi, Nero hakujali akaamua aende matembezini ugriki na akaicha Roma kwa moja mshuauri wake Helius.
Nero akafika ugriki akanza kufanya matamasha yake ya kuigiza, kuimba na kushindana na waimbaji wa ugriki kwenye matamasha yao, pamoja na kukimbia kwa farasi. Kwenye hayo mashindano mara zote aliibuka kidedea. Utawala wale kama mfalme ulikuwa kama njia ya kukuza hadhi yake kijamii na umaarufu na sio kutatua changamoto za wananchi wake.
Nero kuigiza na kuimba kwake ilikuwa kila kitu na hakujali kingine. Watu wa Roma kuona mfalme wao ameendoka na kuwaacha kicha ya ukame na njaa yeye ameenda kuigiza na kuimba nchi nyingine waliona amewasaliti na kuwatenga. Waliona kama anawakejeli na dharau ya hali ya juu kwenda kuigiza na kuimba nchi nyingine.
Ukosefu wa chakula na kutokuwepo kwa mfalme kuliwachukiza sana wananchi majimbo ya Roma kama uhispania na Africa(egpt) yakaanza yakaanza kukataa kuutambua utawala wa Nero.
Kutona na hali hiyo Helius aliyekuwa amemuachua madaraka kamuomba mfalme arudi Roma na mwaka 68 A.D Nero akarudi.
Kutokana na Nero kuwatenga watu wake mda mrefu Senate(bunge) na Praetorian(Jeshi la ulinzi wa mfalme) wakaacha kumtambua kama mfalme na kumuondoa madarakani, Nero akatangazwa kama adui wa Roma. Kuona hivyi Nero aliamua kujichoma kisu kwenye koo na kufa.
Wakati anakufa alisema"what an artist dies in me".