PostGE2025 Samia alikuwa na uwezo wa kujenga kukubalika baada tu ya kuwa rais na angeweza kuwashinda upinzani lakini uwezo mdogo umempeleka pabaya

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
3,560
Reaction score
7,914
Samia alipata nafasi ya kuonesha maono yake na watanzania na dunia ili muamini na kushangilia, lakini kutokana na kile ninachokiita "uwezo mdogo" alishindwa kujenga misingi ya kukubalika.

Samia angeweza kuwashinda wakina lissu, kwanini lissu akubalike lakini samia asikubalike, hapana samia alikuwa na nafasi nzuri ya kuonesha na kufanya awe kinara wa siasa na anaye kubalika.
 
Mkumbuke yule ni mwanamke, na tunaelewa mambo yaoo

Kilichomponza ni wahuni
 
Hana uwo uwezo na hakuwa na huo uwezo. Aliwekwa pale na Kikwete kumpa taarifa za ikulu. Hadi atakapopindua serikali.
 
Nilishawahi kuandika humu Samia na ccm wangeamua kudeal na shida za wananchi wangekubalika tu badala yake wao wakawa wezi, wabadhilifu, mafisadi na majangili Huku huduma Kwa jamii zikidorora na haki za watu zikikanyagwa.

kuwa win Watanganyika ni kitu rahisi sana deal nao pia kuwa mwenzao basi.
 
Waliku
walikuwa na uwezo wa kushinda basi tu wamejichanganya mno kuanza KU deal na Chadema badala ya kudeal na shida za wananchi..
 
URais wa kurithi ungemtosha sijui ni wahuni gani walimdanganya agombee awamu yake, ameaibika vibaya!!!.
Rais wa kwanza Tz kupata kura ml 32 ambazo hazijulikani zimetoka wapi, plus kwenda kuapishiwa maporini!!.
 
Samia alianza vizuri ila aliponegewa na keki ya taifa tu ndipo alipoharibu.

Samia alikuwa na uwezo wa kuacha legacy ya kuwa kinara wa amani kama tu angemaliza kama vile alivyoanza, kwa maridhiano na angeamua kukomea 2025.

Leo hii nchi nzima ingejaa mapambio juu yake.
 
Nahisi alibadili washauri akaamini sana waliomsifia ili wale keki ya taifa kupitia yeye na sio wenye uwezo wa kumshauri kwa maslahi mapana nchi na ya legacy yake. Wajanja wakamuweka busy maskini kupambana na legacy ya mtangulizi pamoja na pressure ya kuwa mwanamke kwenye hiyo nafasi. Ninaamini makosa yake akitulia atajua wako waliomshauri kutumia nguvu kwasababu watu wanamdharau kwasababu ni mwanamke,kumbe ukweli ni tofauti. Yeye kama binadamu anayeongoza binadamu,hakuna namna asingekosolewa kwa maamuzi yake na ya wale aliowateua na walio serikalini.
Inanipa tabu kwamba anazidi kukosea na haoni umuhimu wa kusikiliza watu wenye mawazo tofauti na yeye na watu wake wa karibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…