Same: Wakulima wa Tangawizi wakosa soko baada ya Kiwanda kusitisha uzalishaji kwa miaka 3

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280
Wakulima wa tangawizi katika wilaya Same mkoani kilimanjaro wamesema hawana soko la uhakika la zao hilo baada kiwanda cha kuchakata tangawizi cha Mamba kushindwa kufanya kazi kwa zaidi ya miaka mitatu.

Wakulima hao wamesema kiwanda hicho ambacho walikitegemea kwa ajili ya kuuza tangawizi kwa sasa kimegeuka kero kutokana na wakulima kulazimika kuuza tangawizi kwa walanguzi kwa bei ndogo ya kati ya shilingi 700 hadi 1000 kwa kilo badala ya shilingi 2000.

Wamesema wanatumia gharama kubwa lakini wamekuwa wakipata hasara huku wengi wao wakikata tamaa kutokana na gharama za pembejeo zikiwa kubwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Goha Bw. Evance Mbalazi amesema tangu kujengwa kwa kiwanda hicho wananchi hawajawahi kuuza tangawizi badala yake wakulima walikopesha tangawizi ambayo ilitupwa baada ya kuoza kwa madai kuwa mitambo iliyofungwa katika kiwanda hicho imeshindwa kuchakata tangawizi.
 
Si walimsifikiaga ma anna kilango kwa kujenga hicho kiwanda na kitakuwa mkombozi? Ni kama kujenga majengo ya mahospitali na zahanati kwa wingi na hamna madawa, vifaa, manesi na Madaktari halafu na kung'akang'aka maendeleo.


Best friend of Jesus!
Mimi nilijua tu,kuwa ni usanii,Mitambo imeundwa na SIDO ,wakati wanajaribu operations changamoto zilikuwa chungumzima.Pale watu wamepiga hela kwisha
 
Mitano tena! Ahadi kibao ! Tumecheleweshwa na upinzani !

30 Sept 2017

Tanzania Ya Viwanda​

Mfuko wa Pensheni LAPF kwa kushirikiana na chama cha ushirika cha wakulima wa Tangawizi wanatarajia kufufua kiwanda cha Tangaziwi cha mkoani Kilimanjaro, imetenga shilingi bilioni moja !
 
Back
Top Bottom