Muwekezaji Tanga Cement ataja umeme kama chanzo cha kuchemka biashara, bodi yapitisha hisa zake zote ziuzwe kwa mmiliki wa Twiga Cement

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,446
7,817
Mwanahisa mkubwa zaidi anayemiliki 70% ya hisa kwenye kiwanda cha Tanga Cement ameamua kuuza hisa zake zote kwa kampuni ya Scancem inayomiliki kiwanda cha Twiga Cement, Wazo Dar es Salaam.

Wawekezaji hao wa Afrisam wamesema kikwazo kikubwa wanachokutana nacho ni kiasi na ubora wa umeme unaopatikana nchini vinavyoathiri uwezo wao wa uzalishaji. Wamesema kutatua tatizo la umeme ni gharama kubwa sana kwa muwekezaji na inahitaji uwekezaji mkubwa kuweza kutatua kutokana na gharama kubwa za kuagiza na kuingiza nchini majenereta makubwa.

Wamesema pia hatua hiyo inapelekea kuongezeka kwa kiasi kikubwa gharama za uzalishaji ambayo mwisho inakuwa na athari hasi kwa mtumiaji wa mwisho.

Mwenyekiti wa bodi ya Tanga Cement, Patrick Rutabanzibwa amesema Afrisam amekubali kuachia hisa zake na kuziuza kwa Scancem na waliitisha mikutano miwili na wameridhia.

Miaka 8 iliyopita, Tanga Cement ilichukua mkopo mkubwa kujenga tanuri lake la pili kuongeza uzalishaji lakini ikakumbana na changamoto kubwa walipofika sokoni ya viwanda vipya vilivyoibuka nchini huku Tanga pekee kwasasa kukiwa na viwanda vinne vya Tanga cement, Huaxin, Kilimanjaro na Sungura.

Soko la cement likapata ushindani mkubwa na bei zikashuka hivyo Tanga Cement wakashindwa kupandisha bei, mwaka jana Tanga cement walirokedi hasara. Tanga Cement haijatoa gawio kwa wanahisa wake takriban miaka mitano sasa.

Octoba 2021 Scancem walifikia makubaliano ya kununua aslimia 68 ya hisa za Tanga cement kwa thamani ya bilioni 137 huku sababu kubwa wakati huo ikiwa madeni yaliyokuwa yanakikabili kiwanda hicho yaliyofikia bilioni 230 na kupelekea uwezekano wa kufilisika.

Pamoja na ombi hilo kupitishwa na tume ya ushindani lilikumbana na kizingiti kutoka bodi ya ushindani baada ya Chalinze Cement na TCAS kuweka mapingamizi mwaka 2022.

Bodi ya ushindani ilisema muungano wa Twiga na Tanga Cement utaleta utawala sokoni hivyo kupelekea uwezekano wa kupanga bei.

Scancem ameahidi kuweka mtaji kununua mitambo na kukarabati mashine na viwanda hivyo viwili kufanya kazi kama kitu kimoja.

Simba Cement.png
 
Kuhusu umeme kwakeli hapo nafikiri bei ndio kikwazo maana nilifanya mradi wa kuwateremshia line yao peke yao toka Hale kuja hapo kiwandani TANGA CEMENT. Hizi biashara za kushirikiana na Serekali bahna huwa zina mazingaombwe mengi sana kwakweli.
 
Umeme kidogo au bei kubwa au anasemaje? Kama ni kidogo angevumilia hasara Kwa miezi 6 umeme utatengamaa

Miezi sita hasara haivumiliki, unafilisi mtaji na unaweza kutoka barabarani.

Bei ya umeme ni kubwa, umeme wenyewe pia sio reliable, mitambo mikubwa ya uzalishaji inahitaji umeme stable ambao hauna variation za mara kwa mara, umeme wa Tanzania sio stable, up and down ni nyingi kiasi kwamba operation kwenye mitambo zinakuwa sio smooth na ni hatari kwa mitambo yenyewe, ndio wengine kama migodi wanaopt kutumia tu magenerator kwenye sensitive machinery na plants.
 
miezi sita hasara haivumiliki, unafilisi mtaji na unaweza kutoka barabarani.

Bei ya umeme ni kubwa, umeme wenyewe pia sio reliable, mitambo mikubwa yauzalishaji inahitaji umeme stable ambao hauna variation za mara kwa mara, umeme wa Tanzania sio stable, up and down ni nyingi kiasi kwamba operation kwenye mitambo zinakuwa sio smooth na ni hatari kwa mitambo yenyewe, ndio wengine kama migodi wanaopt kutumia tu magenerator kwenye sensitive machinery na plants.
Ingekuwa ni hasara inayoongezeka sawa lakini hasara ya kupungua inavumilika.
 
Ingekuwa ni hasara inayoongezeka sawa lakini hasara ya kupungua inavumilika.

Umeongelea kuvumilia hasara kwa miezi sita.

Hiyo ni mass production kaka, ukientartain loss unatoka barabarani haraka ndio maana umakini unahitajika kila mahala.

Tushushe bei ya umeme, tufanye complete overhaul ya mitambo na lines zetu za umeme ziwe reliable, tujitahidi kuwa na standaby plants za umeme kuensure constant supply ya umeme hapo utakuwa na watumiaji wengi wa umeme wakubwa, utavutia uwekezaji wa umeme, matumizi ya umeme majumbani yatakuwa makubwa, mwisho Tanesco itaongeza revenue za kutosha.
 
Karne ya 21, tuna mito na maporomoko ya kutosha, uranium pale Namtumbo, gas kusini, Makaa ya mawe pale Songea, upepo wakutosha pale Singida, Yaani Mwenyezi Mungu ametubariki kila kitu halafu tunapiga kelele za umeme miaka nenda rudi..
 
Umeongelea kuvumilia hasara kwa miezi sita.

Hiyo ni mass production kaka, ukientartain loss unatoka barabarani haraka ndio maana umakini unahitajika kila mahala.

Tushushe bei ya umeme, tufanye complete overhaul ya mitambo na lines zetu za umeme ziwe reliable, tujitahidi kuwa na standaby plants za umeme kuensure constant supply ya umeme hapo utakuwa na watumiaji wengi wa umeme wakubwa, utavutia uwekezaji wa umeme, matumizi ya umeme majumbani yatakuwa makubwa, mwisho Tanesco itaongeza revenue za kutosha.
Hahahahahah mtu anazungumzia hasara ya kiwanda kama kuchaniwa mkeka wa jero kila siku. 🤣
 
Kwani shida ya umeme Tanzania imeanza leo? Lini Tanzania iliwahi kuwa na umeme wa uhakika kwa 100%

Kama shida ni umeme mbona wenzao wa viwanda vya cement vya Huaxin, Sungura, Kilimanjaro na Tanga wanapiga kazi

Huyo Simba Cement katupa kitaulo kachemka ushindani sokoni, kusema shida ni umeme ni ule msemo mfa maji haachi kutapatapa
 
Back
Top Bottom