Salma Kikwete versus Regina Lowassa

MIGNON

JF-Expert Member
Nov 23, 2009
4,083
5,066
Wawili hawa ni wake wa marafiki wawili ambao ni Jakaya Kikwete na Eduard Lowasa.

Salma aliingia katika kampeni na kumsaidia mno mumewe kwa kutembea nchi nzima huku akiomba kura kwa kutumia neno "Mume wangu" ingawa wakati huo kuna watu walikuwa wakimshambulia Jakaya kwa baadhi ya tabia zake lakini Salma hakuvunjika moyo na akapata alichopigania, first lady kwa miaka kumi.

Regina alijitokeza wakati mumewe alipohamia CDM na akafanya kazi kubwa ya kumnadi mumewe pamoja na matusi mazito mpaka ya nguoni, hakuvunjika moyo ingawa hakufanikiwa kuwa first lady.

Baada ya uchaguzi CDM katika kuenzi jitihada za Regina walidhamiria kumpatia Ubunge wa viti maalum lakini alikataa

Salma baada ya miaka kumi ya u first lady na kuwa katika pension ya u rais amekubali uteuzi wa ubunge.

Tujadili bila matusi wala kashfa,karibuni waungwana.
 
Regina ni mama mwenye hekima na anaridhika na kile alichopewa na Mungu pasipo shusha hadhi yake.

Huyu mwingine hata hajui first lady maana yake nini. Mume akiwa Rais, kwa maana nyingine mke ni Rais mdogo. Mke wa Rais akitaka kwenda mtembelea ndugu yake, lazima ulinzi uimarishwe pale anapokwenda. Ndiyo maana Salma alikuwa akipokewa na RPCs huko mikoani kipindi anapoenda.

Mtu muelewa na anayetosheka, hauwezi toka kwenye position ukaenda kwenye bunge na kukaa upande wa ccm ambako unajoin kundi la kuzomea hoja za upinzani ukisema "hiloooooo"

Moja ya sababu za Hillary Clinton kushindwa kwenye uchaguzi ni jambo ili la u first lady. Kwamba hayo aliyosema atafanya kama akipewa urais, mbona hakufanya akiwa first lady?. Kwa USA, state secretary ni karibia sawa na vice President, je alishindwa nini fanya hayo mambo akiwa secretary to the state.

Wamarekani walisema mbona huyu hatosheki? Wakasema hata mke wa Obama anaposema mama Clinton atafanya moja mbili, je kwanini yeye mrs Obama hakufanya hayo kipindi akiwa first lady?

Juzi Salma anamshukuru Magufuli kupeleka maji Lindi, je alishindwaje yeye kumwambia mumewe tupeleke maji ukweni kwako?

Salma Kikwete hatambui maana ya first lady. Kwenda kwenye ubunge ni demotion.
 
Naona siku hizi nyuzi za WAATHIRIKA WA UKOSEFU WA VIROBA(UKOVI) zinachekesha sana.....Tambueni Nafasi za watu wawili tofauti Mama REGINA akustahili kabsa kukubali ile nafasi maana yeye pale hajatoa jasho kukifikisha hicho chama mahali kilipo...Kwa hiyo kukataa ile nafasi ilikuwa ni jambo jema tu pia tutambue kabsa HUYU MAMA HAKUFURAHISHWA KABSA KUWA MWANACHADEMA hapa UKOVI najua mtalipinga hili ila kwa tunaojua ndio tunasema sasa.....
Na pia bila kupepesa macho huyo mama hakustahili kabsa kupewa hiyo nafasi ya UBUNGE na hili lazima tu lilikuwa ni AMUZI binafsi la mwenyekiti la kumpooza mzee baada ya kula kipigo kitakatifu toka kwa MAGU.......
Tukija kwa upande wa MAMA SALMA kwa vyovyote vile ata kama hakupenda ule UTEUZI wake lazima tu HAKUBALI....maana angekataa ile ingeleta picha mbaya sana baina ya JK na MAGUFULI.....na pia tambueni huyu MAMA NI MSHIRIKI MKUBWA SANA KWENYE USHINDI WA MAGUFULI and she was one of the best FIRST LADY ndani ya nchi hii...well presentable mama ana jua kuongea na ni mtu ambaye amekuwa akijumuika na jamii ipasavyo....
Afu kingne kama tu mama SALMA angekataa huu uteuzi na NADHANI VIONGOZI WA UKOVI mngepata pakutokea mtaani na la kuongea mpaka 2020......na ingekuwa ni furaha kweli CDM na hili lingekuwa pia ni ngazi kwenu kupata sapoti ya kile mnachokisema kila siku ya KUWA MAGUFULI hapendwi na wana ccm.....KUMBE UPUUZI MTUPU
NA kingne kwanini hamsemi kuhusu yeye kipindi kile alikuwa ni FIRST LADY lakini still anaenda gombania UNEC kwao??????

NYIE UPINZANI wa kipindi CHA MAGUFULI ukweli mmechanganyikiwa ipasavyo...

MAGUFULI HUYOOOO yeye anajizidi chanja mbuga tu
 
Wote wanamoyo wa kuwatumikia watanzania,ila kwa namna tofauti.tusipende kulinganisha kila tunachokiona
 
Naona siku hizi nyuzi za WAATHIRIKA WA UKOSEFU WA VIROBA(UKOVI) zinachekesha sana.....Tambueni Nafasi za watu wawili tofauti Mama REGINA akustahili kabsa kukubali ile nafasi maana yeye pale hajatoa jasho kukifikisha hicho chama mahali kilipo...Kwa hiyo kukataa ile nafasi ilikuwa ni jambo jema tu pia tutambue kabsa HUYU MAMA HAKUFURAHISHWA KABSA KUWA MWANACHADEMA hapa UKOVI najua mtalipinga hili ila kwa tunaojua ndio tunasema sasa.....
Na pia bila kupepesa macho huyo mama hakustahili kabsa kupewa hiyo nafasi ya UBUNGE na hili lazima tu lilikuwa ni AMUZI binafsi la mwenyekiti la kumpooza mzee baada ya kula kipigo kitakatifu toka kwa MAGU.......
Tukija kwa upande wa MAMA SALMA kwa vyovyote vile ata kama hakupenda ule UTEUZI wake lazima tu HAKUBALI....maana angekataa ile ingeleta picha mbaya sana baina ya JK na MAGUFULI.....na pia tambueni huyu MAMA NI MSHIRIKI MKUBWA SANA KWENYE USHINDI WA MAGUFULI and she was one of the best FIRST LADY ndani ya nchi hii...well presentable mama ana jua kuongea na ni mtu ambaye amekuwa akijumuika na jamii ipasavyo....
Afu kingne kama tu mama SALMA angekataa huu uteuzi na NADHANI VIONGOZI WA UKOVI mngepata pakutokea mtaani na la kuongea mpaka 2020......na ingekuwa ni furaha kweli CDM na hili lingekuwa pia ni ngazi kwenu kupata sapoti ya kile mnachokisema kila siku ya KUWA MAGUFULI hapendwi na wana ccm.....KUMBE UPUUZI MTUPU
NA kingne kwanini hamsemi kuhusu yeye kipindi kile alikuwa ni FIRST LADY lakini still anaenda gombania UNEC kwao??????

NYIE UPINZANI wa kipindi CHA MAGUFULI ukweli mmechanganyikiwa ipasavyo...

MAGUFULI HUYOOOO yeye anajizidi chanja mbuga tu
Umeingiza viroba,umeingiza upinzani na umeandika yote uloyoweza lakini umeshindwa kujua kwa nini uzi huu upo hapo.
 
Mama Salma hata angekataa uteuzi maneno yasingekosa!
Kwani lazima atangazwe ndipo akatae?Wakati wa kushauriwa kuwa atateuliwa si anaweza kukataa tu kama Makongoro Nyerere alivyokataa ubunge kwa Mkapa?
 
Regina ana akili na busara nyingi na ndo maana aliona vyema nafasi hiyo watumikie wengine lakini huyo mwingine mtajua wenyewe
Regina sio mwanasiasa ni mfanyabiashara..salma kikwete ni mwanasiasa..ni haki kufanya siasa vyovyote
 
Regina ni mama mwenye hekima na anaridhika na kile alichopewa na Mungu pasipo shusha hadhi yake.

Huyu mwingine hata hajui first lady maana yake nini. Mume akiwa Rais, kwa maana nyingine mke ni Rais mdogo. Mke wa Rais akitaka kwenda mtembelea ndugu yake, lazima ulinzi uimarishwe pale anapokwenda. Ndiyo maana Salma alikuwa akipokewa na RPCs huko mikoani kipindi anapoenda.

Mtu muelewa na anayetosheka, hauwezi toka kwenye position ukaenda kwenye bunge na kukaa upande wa ccm ambako unajoin kundi la kuzomea hoja za upinzani ukisema "hiloooooo"

Moja ya sababu za Hillary Clinton kushindwa kwenye uchaguzi ni jambo ili la u first lady. Kwamba hayo aliyosema atafanya kama akipewa urais, mbona hakufanya akiwa first lady?. Kwa USA, state secretary ni karibia sawa na vice President, je alishindwa nini fanya hayo mambo akiwa secretary to the state.

Wamarekani walisema mbona huyu hatosheki? Wakasema hata mke wa Obama anaposema mama Clinton atafanya moja mbili, je kwanini yeye mrs Obama hakufanya hayo kipindi akiwa first lady?

Juzi Salma anamshukuru Magufuli kupeleka maji Lindi, je alishindwaje yeye kumwambia mumewe tupeleke maji ukweni kwako?

Salma Kikwete hatambui maana ya first lady. Kwenda kwenye ubunge ni demotion.
Umejenga hoja nzuri sana na pia umedhihirisha NGUVU YA HOJA yako.

Kimsingi kwa Salma kukubali nafasi hii kwa haraka haraka sio jambo baya lakini kwa jicho la tatu na kwa kufikirisha akili sana ni kama kejeli kwake.
 
Back
Top Bottom