Mkulu behu niweke wazi kweli hilo maana kuhusu APSON kila mtu anajua alivyo haribu kwa kuweka TISS kuwa kama chaka la ma incopetents lakini hili la R.O sijakuelewa hebu niweke wazi mkulu
Nilidhani hili lilitegemewa na wengi ndio litakuwa toleo la tatu la ripoti ya meremeta, thanks god im still living to witness this prophecy.
sasa hivi mkurugenzi wa TISS ni RO sasa kama hawezi kusafisha madudu ya CAM basi ndio tuna tatizo. Maana sheria ya TISS inampa mkurugenzi nguvu za kutosha tu. Ama sivyo?
kwa kweli unajua mtu mkabila ni mkabila tu; sasa mtu ukifanya ufisadi kwa misingi ya ukabila unategemea watu wa kabila lako kukutetea au kuwa upande wako; sasa unajikuta unashangazwa inakuwaje mtu wa nyumbani hakuungi mkono? Vivyo masuala ya udini. Tumefika mahali tunataka kuangalia fisadi kwa kuangalia ni mtu wa dini yetu au la (zile seti). Sasa mafisadi na wenyewe wameshakuwa wataalamu wa hili.
Wa kwanza kuingizwa mkenge ni mume wa Anne Kilango, anajifanya anapinga ufisadi kumbe anapalilia. Sisi sio wajinga tena. Tanzania hakuna udini wala ukabila.
Navyojua mimi Mzee John Samwel Malechela alikua na share pale Mwadui Diamond Mining wakati akiwa waziri mkuu, sijui anajitoaje kwenye ufisadi.
Baada ya salamu nina ujumbe kwenu: Stand down. Makuwadi na vikaragosi vyenu viambieni virudi nyuma. Miti mingine haikwewi na milima mingine inatosha kuiangalia kwa mbali tu. Mlifanyalo lifanyeni haraka kwani kiza kimeingia.
NB: Salam kwa RO... if you act now you (kwa kumhamisha kuwadi wao) you might change my mind (probably others too) but if you don't nitaamini umesanction the stealth move.
Otherwise; 2010 ni mwisho wao. So like that stupid commercial here in the US "do you want it to hurt now or later".. ?
Vitoto vya Nzi navyo havilali!
Stand down. Makuwadi na vikaragosi vyenu viambieni virudi nyuma. Miti mingine haikwewi na milima mingine inatosha kuiangalia kwa mbali tu. Mlifanyalo lifanyeni haraka kwani kiza kimeingia.
Kwani wanataka kutoa roho ya mtu? Mungu akulinde. Halafu nilikuwa na wasiwasi juu ya kufahamika kwako, zile namba za simu ulizotoa kuchangia ripoti ya Meremeta, si zinaweza kukufanya ukafahamika mzee na hao vikaragosi wakapata kazi ya kufanya?
Na huu ndo uongo mkubwa ambao baadhi yetu tumeuingiza rohoni na kuulinda kama mboni ya jicho.Ni makosa makubwa kufikiri kuwa tunaweza kufanya jambo lolote hata kama ni ovu kiasi gani, pasipo kupata madhara yoyote.Kama hizi kelele zinazopigwa hazitawabadili nia, naam, kuna nguvu nyingine zitakazoweza kufanya hivyo. Mbona Sani Abacha naye himaya yake ilifika ukingoni?Kufahamika mbona nafahamika vizuri tu; kinachonisumbua ni hili kundi ambalo linaamini kabisa kuwa nchi hii ni ya kwao kabisa na sisi wengine ni wapangaji na tunahitaji kuomba kibali kwao ili tuwe.