Salaam kwa Mh Kikwete

Salaam kwa Mh Kikwete

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
Joined
May 14, 2010
Posts
2,182
Reaction score
309
Mheshimiwa Rais, mimi ni mpiga kura wako ambaye nimekuwa sifurahishwi na maneno yanayoanza kuzoeleka sasa kama misamiati sahihi ya kuwapa matumaini yasiyokuwepo ama kwa sababu hamna utashi wa kisiasa ama hamna uwezo (ninyi kama wanasiasa) kuyatekeleza na badala yake inakuwa kana vile siye ni midoli yenu ya kujiburudisha nayo.

Naongelea maneno ambayo wewe na wanasiasa wenzako mnapenda kuyatumia kama haya hapa:
  1. Tutawapatia wanafunzi wote wa Tanzania Komputa
  2. Tutajenga barabara za kupita juu kwenye mji wa Dar es Salaam
  3. Tutaboresha masilahi ya wafanyakazi
  4. Tutapeleka maji ya ziwa Viktoria hadi Tabora
  5. Tutaunganisha kila makao makuu ya mkoa kwa njia ya rami
n.k., n.k. tatizo langu kubwa ni kwamba kama hizi tuta- zingekuwa tume- au tuna- tungekuwa hatuko kwenye hili janga la umasikini wa kutisha, nashauri ama msitupe matumaini makubwa kuliko uwezo wa serikali yako kwani kufanya hivyo ni kutokutuheshimu sisi wapiga kura wenu kwa kutudaganya vitu ambavyo ama hamfanyi ama hamna uwezo navyo
 
Na tunafundisha kwa kutumia mkongo wa taifa. Bila TV, Bila Kompyuta, Sisi ccm wakali bwana.:focus:
 
JK bora asafiri ughaibuni akatafute kocha wa kufundisha viduku kama alivyotafuta wa timu ya taifa ili atupunguzie hizi tuta-
 
TUTAFANYA MABADILIKO MAKUBWA NDANI YA CHAMA! Kweli matuta yamekuwa mengi!
 
Mheshimiwa Rais, mimi ni mpiga kura wako ambaye nimekuwa sifurahishwi na maneno yanayoanza kuzoeleka sasa kama misamiati sahihi ya kuwapa matumaini yasiyokuwepo ama kwa sababu hamna utashi wa kisiasa ama hamna uwezo (ninyi kama wanasiasa) kuyatekeleza na badala yake inakuwa kana vile siye ni midoli yenu ya kujiburudisha nayo.

Naongelea maneno ambayo wewe na wanasiasa wenzako mnapenda kuyatumia kama haya hapa:
  1. Tutawapatia wanafunzi wote wa Tanzania Komputa
  2. Tutajenga barabara za kupita juu kwenye mji wa Dar es Salaam
  3. Tutaboresha masilahi ya wafanyakazi
  4. Tutapeleka maji ya ziwa Viktoria hadi Tabora
  5. Tutaunganisha kila makao makuu ya mkoa kwa njia ya rami
n.k., n.k. tatizo langu kubwa ni kwamba kama hizi tuta- zingekuwa tume- au tuna- tungekuwa hatuko kwenye hili janga la umasikini wa kutisha, nashauri ama msitupe matumaini makubwa kuliko uwezo wa serikali yako kwani kufanya hivyo ni kutokutuheshimu sisi wapiga kura wenu kwa kutudaganya vitu ambavyo ama hamfanyi ama hamna uwezo navyo

Tatizo siyo Mheshimiwa Rais bali watendaji wake kwani Raisi akisema kitu HILO NI AGIZO linalopaswa kufanyiwa kazi. Nimesikia vile vile amesema shule zitaunganishwa kwenye Mkonga wa taifa ili utumike kufundishia; sasa sijui hizo computer zitawashwa kwa Solar au huu umeme wa Tanesco ambao hauna uhakika!!!
 
TUTAFANYA MABADILIKO MAKUBWA NDANI YA CHAMA! Kweli matuta yamekuwa mengi!

Unajua Henge sometimes huwa una mambo ya ajabu sana. Sasa hata hili nalo unawachapa nalo? Kweli we kiboko. Unamchapa Ng'ombe na mkia wake!

Jamaa wamesahau mpaka wanajidanganya wenyewe......kweli kazi ipo!
 
interesting; all future tenses...with no specified time for said promises......haya ccm.....danganya tootoo jinga
 
Tatizo siyo Mheshimiwa Rais bali watendaji wake kwani Raisi akisema kitu HILO NI AGIZO linalopaswa kufanyiwa kazi. Nimesikia vile vile amesema shule zitaunganishwa kwenye Mkonga wa taifa ili utumike kufundishia; sasa sijui hizo computer zitawashwa kwa Solar au huu umeme wa Tanesco ambao hauna uhakika!!!
hapa nisamehe kabisaaaaaaaa
Tatizo namba moja la nchi hii kwa sasa ni JAKAYA KHALFAN MRISHO KIKWETE bila chenga.
 
Tatizo siyo Mheshimiwa Rais bali watendaji wake kwani Raisi akisema kitu HILO NI AGIZO linalopaswa kufanyiwa kazi. Nimesikia vile vile amesema shule zitaunganishwa kwenye Mkonga wa taifa ili utumike kufundishia; sasa sijui hizo computer zitawashwa kwa Solar au huu umeme wa Tanesco ambao hauna uhakika!!!

Vincent, twende taratibu kwanza. Tatizo sio Raisi? Ni watendaji wake?

Raisi ni nani?

Watendaji ni nani?

Kama agizo lake halijafanyiwa kazi anatoa agizo lingine au anafanyaje?

Tujadili.
 
Tatizo siyo Mheshimiwa Rais bali watendaji wake kwani Raisi akisema kitu HILO NI AGIZO linalopaswa kufanyiwa kazi. Nimesikia vile vile amesema shule zitaunganishwa kwenye Mkonga wa taifa ili utumike kufundishia; sasa sijui hizo computer zitawashwa kwa Solar au huu umeme wa Tanesco ambao hauna uhakika!!!

Mkuu naomba kutofautiana na wewe, kama hayo maagizo hayatekelezwi na mtoa maagizo hawawajibishi nani wa kulaumiwa? Urais siyo lelemama
 
Vincent, twende taratibu kwanza. Tatizo sio Raisi? Ni watendaji wake?

Raisi ni nani?

Watendaji ni nani?

Kama agizo lake halijafanyiwa kazi anatoa agizo lingine au anafanyaje?

Tujadili.


There you are Msando....

Udhaifu wa kiongozi huthibitishwa na watendaji walioko chini yake...

Ni sawa na kuwa na paka asiekimbiza panya, panya watacheza na kufanya kila kituko ndani ya nyumba,

Wa kulaumiwa na mwenye nyumba ni paka kwa kule kuacha uhuru....

Tatizo la JK ni Laissaze Affaire
na hawezi kufuatilia utendaji wa walio chini yake

Ninachoelewa, kiongozi akitoa tamko watendaji wanatetemeka na kupigana vikumbo kutekeleza, huyo ndie kiongozi imara,

Lakini kiongozi anaetoa tamko then watendaji wanamngoja wampe mgongo wamng'ong'e na kutupilia agizo lake lazima ana upungufu tena ulio wazi mpaka kwa watendaji wake kuwa HANA UBAVU WA KUWACHUKULIA HATUA YOYOTE
 
Haya maTUTA ya serikali ya CCM ndiyo maana tunakwama hatuendelei. Sisi wanatuahidi maTUTA wao wanazichota kwa kwenda mbele.
 
Vincent, twende taratibu kwanza. Tatizo sio Raisi? Ni watendaji wake?

Raisi ni nani?

Watendaji ni nani?

Kama agizo lake halijafanyiwa kazi anatoa agizo lingine au anafanyaje?

Tujadili.
Jamani mnanifunja mbavu, hilo agizo analotoa mh. Rais, analitoa akiwa jukwaani ili afurahishe wananchi na wafuasi wake. Je hao watendaji wake amewapa maagizo kimaandishi? Mnadhani watendaji wa serikali wanafanyia kazi hotuba za majukwaani? Rejea maagizo aliyotoa waziri wa afya kuhusu suala la babu Loliondo, mkuu wa mkoa alijibu hafanyii kazi maagizo kupitia Tv.
 
Acheni kuwa mlengo usio na mwelekeo tusubiri miaka 4 ndio tufanye tathmini hayakutimia tufanye uamuzi hizi propaganda za ushabiki hazina tija
 
Acheni kuwa mlengo usio na mwelekeo tusubiri miaka 4 ndio tufanye tathmini hayakutimia tufanye uamuzi hizi propaganda za ushabiki hazina tija
ebo kakaa miaka mitano pale, alikuwa anjifunza?
 
hapa nisamehe kabisaaaaaaaa
Tatizo namba moja la nchi hii kwa sasa ni JAKAYA KHALFAN MRISHO KIKWETE bila chenga.

Vincent, twende taratibu kwanza. Tatizo sio Raisi? Ni watendaji wake?

Raisi ni nani?

Watendaji ni nani?

Kama agizo lake halijafanyiwa kazi anatoa agizo lingine au anafanyaje?

Tujadili.

Mkuu naomba kutofautiana na wewe, kama hayo maagizo hayatekelezwi na mtoa maagizo hawawajibishi nani wa kulaumiwa? Urais siyo lelemama


There you are Msando....

Udhaifu wa kiongozi huthibitishwa na watendaji walioko chini yake...

Ni sawa na kuwa na paka asiekimbiza panya, panya watacheza na kufanya kila kituko ndani ya nyumba,

Wa kulaumiwa na mwenye nyumba ni paka kwa kule kuacha uhuru....

Tatizo la JK ni Laissaze Affaire
na hawezi kufuatilia utendaji wa walio chini yake

Ninachoelewa, kiongozi akitoa tamko watendaji wanatetemeka na kupigana vikumbo kutekeleza, huyo ndie kiongozi imara,

Lakini kiongozi anaetoa tamko then watendaji wanamngoja wampe mgongo wamng'ong'e na kutupilia agizo lake lazima ana upungufu tena ulio wazi mpaka kwa watendaji wake kuwa HANA UBAVU WA KUWACHUKULIA HATUA YOYOTE

Nimenyanyua mikono
 
Tatizo siyo Mheshimiwa Rais bali watendaji wake kwani Raisi akisema kitu HILO NI AGIZO linalopaswa kufanyiwa kazi. Nimesikia vile vile amesema shule zitaunganishwa kwenye Mkonga wa taifa ili utumike kufundishia; sasa sijui hizo computer zitawashwa kwa Solar au huu umeme wa Tanesco ambao hauna uhakika!!!

Sasa ndiyo ujiulize anatoaje agizo kama hilo wakati anajua hali ya umeme ilivyo na DOWANS pia anaijua...Tafakari!!
 
Acheni kuwa mlengo usio na mwelekeo tusubiri miaka 4 ndio tufanye tathmini hayakutimia tufanye uamuzi hizi propaganda za ushabiki hazina tija

Kaka uko nchi gani??tunasubiri miaka minne ipi tena??kuna miaka mitano ya kwanza imeshapita imepita tayari na vingi viliahidiwa au wewe hukumbuki??vipi tena??
 
........Tatizo sio watendaje wake.Raisi kalegea kama bwabwa kwa nini wasimzarau.
 
Back
Top Bottom