Salaam kwa Ismail Aden Rage - Tabora Mjini; Jiandae...

Hossam

JF-Expert Member
Feb 10, 2011
3,538
2,155
Mheshimiwa Kiongozi Wetu,

Kwa masikitiko makubwa napenda kukutumia salaam za kukuamsha na kukutaka sasa uwatumikie wakazi wa Tabora Mjini kama ambavyo uliahidi katika kampeni zako mwaka 2010. Sasa hakuna mzaha tena...

Mkoa wa Tabora umekuwa ni mkoa wa mwisho kabisa kimaendeleo japo kwa hakika ulitakiwa uongozwe na watu makini ili uwe kileleleni kabisa kwa kuwa kuna kila opportunity na resources za kufanya hilo, na sio kuongizwa na nyie wenye kupenda michezo zaidi kuliko kuugua kwa tabu za wananchi wenu. Wewe na viongozi wetu waheshimiwa waliopita mnaona kama Tabora sio yenu. Ni sawa nakubaliana na wewe, na hilo wazo lenu, Tabora sio yenu maana hata asili zenu zinaonyesha nyie sio wenyeji wa Tabora, lau hili ndio linawapa uvivu wa kuuendeleza mkoa huo maskini kabisa.

Wewe toka umechaguliwa kuwa mbunge wa Tabora mjini umejikita zaidi kwenye michezo, basi potelea mbali ingekuwa hata michezo huko jimboni kwako, wewe umekazania Simba simba simba hata umesahau majukumu yako kama mbunge, na mimi sasa ni wajibu wangu na ni wajibu wa kila mwenye kufikiri sawasawa kukukumbusha ili usije sema hukuambiwa. Tabora imebakia hata timu ya mkoa ile ya Milambo ya daraja la kwanza sasa haziko vichwani mwenu nyie wapenda kucheza, sasa hivi kwako wewe mheshimiwa kipi ni bora, nyumba yako iteketee huku ukiiacha na kwenda kuokoa ya jirani, ama uokoe yako kwanza na kisha ya jirani yako? Jibu kiukweli bila unafki!

Tuangalie elimu huko Tabora. Suala la elimu wewe kwako sasa ni kitendawili mheshimiwa, ni karibu tu na mjini kabisa huko kata ya Malolo, ama huko Ntalikwa, hebu tupa jicho kwa shule zetu za msingi na zahanati huko kiloleni. Hebu ona huruma kwa akina mama wa Ng'ambo wanavyohaha kugombania maji visimani, hivi wewe huoni usalama wa raia wako ulivyo rehani huko Chemchem, ama ndio sababu nasikia siku hizi unabeba na bastola kujilinda? Ona miundombinu ilivyo hovyo, halafu unaishia kupoteza muda na Simba, sasa nakuomba chagua moja kati ya Simba ama Siasa.

Maana inafikia wakati sasa wapiga kura wako wanakutafuta wakueleze shida zao na hawakupati, wanashida na mbunge wao lakini wanaambulia patupu.

Imefika wakati sasa uondoke, vuguvugu na wimbi la mabadiliko sasa linapiga hodi Tabora mjini na sisi tunao vijana wazuri tena wenyeji wa hukohuko wenye huzuni na hasira na umwinyi wenu wa kupenda ukubwa hali hamfanyi lolote kwa watu wenu. Hawa sasa tunawapika kuanzia sasa hadi mwaka 2015 ili tuone kati ya vijana wa mabadiliko na wazee wa umwinyi ni wepi hasa watakaoleta mabadiliko na maendeleo hapo Tabora mjini. Hili ni lazima liwe jambo ambalo wewe kama mteuliwa na sauti ya wananchi unatakiwa sasa kuanza kufikiri kama uache wewe mwenyewe kwa hiari yako ama uache baada ya kupoteza mapesa mengi muda na aibu tupu.


Ni sawa kwamba Tabora mjini haijawahi kupata wagombea vijana makini zaidi ya Mr Zambia kwa kipindi chote, lakini sana haijapata mgombea mwenye ushawishi kwa vijana kwa kipindi hicho na mwisho wagombea hao wamekuwa hawana uwezo kifedha na hivyo kazi ya kuyafikia maeneo yote ya jimbo inakuwa ngumu. Sasa tunaanza rasmi mwaka ujao, tutaeleza uozo wako kwa wapiga kura wako na tutaandaa vijana wetu kwa mabadiliko na maendeleo yao kupitia jukwaa la siasa. Tutawaonyesha wana Tabora matumaini yaliyopotea na tutaimba wimbo wa mabadiliko hadi wewe na vibaraka wako muusikie na mfungashe vilivyokuwa vyenu.


Haingii akilini kabisa wakazi wa Cheyo kukosa kituo cha polisi kwa kipindi chote, hakuna mtu anayekuelewa kama soko la pale National, kule Tambukareli, na Rufita, na hata Ipuli, yanavyosuasua na sasa ushuru wa manispaa unalegalega bila mpangilio na wewe upo na unatazama haya bila kusema lolote. Haileti picha njema kuona wafanya biashara wadogowadogo wamachinga ukishindwa kuwatafutia eneo maalum, wewe kazi simba tu simba tu, hivi nikuulize hili, hao Simba ndio walikutuma uwe mbunge wa Tabora mjini mheshimiwa?

Huko Kwihara, pale Kipalapala, pale si ndio yule Mzungu, Dr Livingstone aliacha Tembe lake ambalo ni eneo zuri sana la utalii mkoani Tabora? Pale ndio nyumba ya Chief Abdallah Fundikira aliacha nyumba yake, na pana jiwe kubwa, jabali, mahali ambapo wachawi walikuwa wanauawa? Wewe huoni kama hiyo ni sawa na utalii? Basi wewe labda sema vipaumbele vyako ni vipi hasa mheshimiwa! Maana hatukuelewi kabisa.


Hebu ona wananchi wa Mbungani wanavyohaha na magonjwa ya kuhara kwa sababu mitaro ni hadi milangoni kwao, wewe uko na hamsini zako tu, ama hawakuambii? Hata polisi sasa wanaishi kwenye vibanda vya chuma kama wakimbizi wewe kwako heko tu, labda kwa sababu wanawashikaga wakati wa kampeni.

Tabora mjini sasa ni lazima iwe zaidi ya Wilaya ya Nzega, ni lazima sasa ufike wakati, wanatabora waone kweli mbunge wao na nchi yao inawatendea haki na wote kwa pamoja wanafaidi matunda ya uhuru wao. Kama hayo huyawezi, basi sie akina PANGU PAKAVU TIA MCHUZI, tuko nyuma yako unyayo baada ya mwingine kuhakikisha unaondoka haraka kwenye umwinyi na kuacha ya Tabora kwa wana Tabora.

Hizi na ziwe salaam zako za Krismas na Mwaka Mpya.

Ni Mimi Pangu Pakavu,
Nakusalimia.
 
Muamshe kaka, hawa bila kuamshwa wanalewa na usingizi. muamshe

Angalia asije toka na bastola huyo,huyu kama askari wa al-sha- okoslok kipermekunjugere.

Ni mwenyekiti wa chama cha cimba na katibu wa kile chama cha watu kule wapi vile!! nimesahau sorry.tetee
 
hahaha kaka huyo kamanda wa al....u utamuweza? mwenzio anatembea na bunduki
 
Ni vema umeujuza ulimwengu hayo yanayotokea huko tabora. lakini kama unaweza, siku moja nenda kwenye mkutano wake wa hadhara umweleze moja kwa moja
 
Kwa taarifa hilo jimbo ni term moja tu kwa siku hizi. Kama akishinda next term atakuwa wa kwanza.
Bora umemstua umwinyi na koo ndio tatizo pia viking'olewa tabora itasonga. Kufa kwa railway ndio kumeua tabora kabisa
 
Nyie simmeamua kuichagu CCM na kupenda kupewa kanga,kofia,chupi za CCM na sh,2000,2000,sasa hayo ndiyo matatizo yake,mtaendelea kuwa maskini wa maisha na hatari zaidi nyie na maskini wa fikra! Endeleani na upumbavu wenu wa kuichagua CCM.
 
Tuseme unatangaza nia au! tuelewashane vizuri Kiongozi! by the way hayo ndio majitu(mazimwi) ya CCM. yanaangalia "kibubu" kipo levo gani . Uchaguzi kwao ni kuhonga tu ndo maana hayajali
 
lakini hii pia inaonyesha kuna haja ya kuwa na sheria ambayo itawapa nguvu wapiga kura kuwawajibisha wabunge wao pale wanapoona kuwa hawatendi vile wanavyopaswa kuitenda katika kutekeleza majukumu yao
 
Na nyie kwa nini mlichagua kuongozwa na gaidi la kisomali?Nyie watani zangu mnachekesha sana mara muongozwe na muajemi mara msomali kwa nini lakini?
 
Jitambueni, jitoeni mikononi mwa wapenda madaraka kuliko kupenda kuwatumikia wananchi
 
mheshimiwa kiongozi wetu,

kwa masikitiko makubwa napenda kukutumia salaam za kukuamsha na kukutaka sasa uwatumikie wakazi wa tabora mjini kama ambavyo uliahidi katika kampeni zako mwaka 2010. Sasa hakuna mzaha tena...

Mkoa wa tabora umekuwa ni mkoa wa mwisho kabisa kimaendeleo japo kwa hakika ulitakiwa uongozwe na watu makini ili uwe kileleleni kabisa kwa kuwa kuna kila opportunity na resources za kufanya hilo, na sio kuongizwa na nyie wenye kupenda michezo zaidi kuliko kuugua kwa tabu za wananchi wenu. Wewe na viongozi wetu waheshimiwa waliopita mnaona kama tabora sio yenu. Ni sawa nakubaliana na wewe, na hilo wazo lenu, tabora sio yenu maana hata asili zenu zinaonyesha nyie sio wenyeji wa tabora, lau hili ndio linawapa uvivu wa kuuendeleza mkoa huo maskini kabisa.

Wewe toka umechaguliwa kuwa mbunge wa tabora mjini umejikita zaidi kwenye michezo, basi potelea mbali ingekuwa hata michezo huko jimboni kwako, wewe umekazania simba simba simba hata umesahau majukumu yako kama mbunge, na mimi sasa ni wajibu wangu na ni wajibu wa kila mwenye kufikiri sawasawa kukukumbusha ili usije sema hukuambiwa. Tabora imebakia hata timu ya mkoa ile ya milambo ya daraja la kwanza sasa haziko vichwani mwenu nyie wapenda kucheza, sasa hivi kwako wewe mheshimiwa kipi ni bora, nyumba yako iteketee huku ukiiacha na kwenda kuokoa ya jirani, ama uokoe yako kwanza na kisha ya jirani yako? Jibu kiukweli bila unafki!

Tuangalie elimu huko tabora. Suala la elimu wewe kwako sasa ni kitendawili mheshimiwa, ni karibu tu na mjini kabisa huko kata ya malolo, ama huko ntalikwa, hebu tupa jicho kwa shule zetu za msingi na zahanati huko kiloleni. Hebu ona huruma kwa akina mama wa ng'ambo wanavyohaha kugombania maji visimani, hivi wewe huoni usalama wa raia wako ulivyo rehani huko chemchem, ama ndio sababu nasikia siku hizi unabeba na bastola kujilinda? Ona miundombinu ilivyo hovyo, halafu unaishia kupoteza muda na simba, sasa nakuomba chagua moja kati ya simba ama siasa.

Maana inafikia wakati sasa wapiga kura wako wanakutafuta wakueleze shida zao na hawakupati, wanashida na mbunge wao lakini wanaambulia patupu.

Imefika wakati sasa uondoke, vuguvugu na wimbi la mabadiliko sasa linapiga hodi tabora mjini na sisi tunao vijana wazuri tena wenyeji wa hukohuko wenye huzuni na hasira na umwinyi wenu wa kupenda ukubwa hali hamfanyi lolote kwa watu wenu. Hawa sasa tunawapika kuanzia sasa hadi mwaka 2015 ili tuone kati ya vijana wa mabadiliko na wazee wa umwinyi ni wepi hasa watakaoleta mabadiliko na maendeleo hapo tabora mjini. Hili ni lazima liwe jambo ambalo wewe kama mteuliwa na sauti ya wananchi unatakiwa sasa kuanza kufikiri kama uache wewe mwenyewe kwa hiari yako ama uache baada ya kupoteza mapesa mengi muda na aibu tupu.


Ni sawa kwamba tabora mjini haijawahi kupata wagombea vijana makini zaidi ya mr zambia kwa kipindi chote, lakini sana haijapata mgombea mwenye ushawishi kwa vijana kwa kipindi hicho na mwisho wagombea hao wamekuwa hawana uwezo kifedha na hivyo kazi ya kuyafikia maeneo yote ya jimbo inakuwa ngumu. Sasa tunaanza rasmi mwaka ujao, tutaeleza uozo wako kwa wapiga kura wako na tutaandaa vijana wetu kwa mabadiliko na maendeleo yao kupitia jukwaa la siasa. Tutawaonyesha wana tabora matumaini yaliyopotea na tutaimba wimbo wa mabadiliko hadi wewe na vibaraka wako muusikie na mfungashe vilivyokuwa vyenu.


Haingii akilini kabisa wakazi wa cheyo kukosa kituo cha polisi kwa kipindi chote, hakuna mtu anayekuelewa kama soko la pale national, kule tambukareli, na rufita, na hata ipuli, yanavyosuasua na sasa ushuru wa manispaa unalegalega bila mpangilio na wewe upo na unatazama haya bila kusema lolote. Haileti picha njema kuona wafanya biashara wadogowadogo wamachinga ukishindwa kuwatafutia eneo maalum, wewe kazi simba tu simba tu, hivi nikuulize hili, hao simba ndio walikutuma uwe mbunge wa tabora mjini mheshimiwa?

Huko kwihara, pale kipalapala, pale si ndio yule mzungu, dr livingstone aliacha tembe lake ambalo ni eneo zuri sana la utalii mkoani tabora? Pale ndio nyumba ya chief abdallah fundikira aliacha nyumba yake, na pana jiwe kubwa, jabali, mahali ambapo wachawi walikuwa wanauawa? Wewe huoni kama hiyo ni sawa na utalii? Basi wewe labda sema vipaumbele vyako ni vipi hasa mheshimiwa! Maana hatukuelewi kabisa.


Hebu ona wananchi wa mbungani wanavyohaha na magonjwa ya kuhara kwa sababu mitaro ni hadi milangoni kwao, wewe uko na hamsini zako tu, ama hawakuambii? Hata polisi sasa wanaishi kwenye vibanda vya chuma kama wakimbizi wewe kwako heko tu, labda kwa sababu wanawashikaga wakati wa kampeni.

Tabora mjini sasa ni lazima iwe zaidi ya wilaya ya nzega, ni lazima sasa ufike wakati, wanatabora waone kweli mbunge wao na nchi yao inawatendea haki na wote kwa pamoja wanafaidi matunda ya uhuru wao. Kama hayo huyawezi, basi sie akina pangu pakavu tia mchuzi, tuko nyuma yako unyayo baada ya mwingine kuhakikisha unaondoka haraka kwenye umwinyi na kuacha ya tabora kwa wana tabora.

Hizi na ziwe salaam zako za krismas na mwaka mpya.

Ni mimi pangu pakavu,
nakusalimia.

pangu pakavu, ah ha ha haaaaaaaaa, sio hossam???haya bwana nadhani kasikia, yupo pale kkoo round about!
 
Muda si mrefu Rufita Street itakuwa hivi

islamist-fighters-Somali.JPG
 
Mimi nina ushahidi aden rage alikuwa ni mmoja wa wanamgambo wa al shabaab na alitoroka kwenye bandari ya lamu kismayu akakimbilia tz akiwa amedandia lori
 
Back
Top Bottom