johnmashilatu
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 718
- 703
CCM ni walewale jana, juzi na hata kesho.Huku kibaha umeme umekata anzia saa saba usiku hadi dakika hii.
Tena inasemekana mama anakuja huku leo.
Tubebe bango la maji au umeme au bidhaa kupanda.
Hii nchi huko juu ni kama wameamua kutukomoa
Magu though uliniumiza ila nimekumisi.
Kwahiyo unahisi Kalemani alikuwa Waziri kutoka chama gani na Makamba anatoka wapi?Ndugu waziri nakuletea salaam zangu kutoka nakatunga wilaya ya Ngara, ambazo kwa hakika zimebeba mtazamo wa wilaya yote.
Ndugu waziri, wanaomkumbuka Kalemani hadharani na moyoni sio kwamba wachuki na wewe, bali wanaangalia utendaji wako ukilinganisha na kalemani.
Hapa Rusumo kuna mradi wa ujenzi wa umeme kutokana na maporomoko ya maji kutoka nchi tatu, Tanzania, Burundi na Rwanda.
Kalemani alikuwa akifanya ziara za mara kwa mara, kukagua maendeleo ya mradi huu wa kuzalisha megawati 90. Ndugu waziri, tangu umechukua nafasi hiyo hujafika kukagua na hatuna taarifa utakamilika lini, ibgawa kwa kalemani tuliambiwa utakamilka April hii.
Ndugu waziri, hapa Ngara umeme ni anasa! Hauwaki siku mbili bila taarifa na ukipatikana huwezi kutumia mashine ya kunyoa nywele. Umeme mdogo.
Ndugu waziri, matokeo yake huduma za msingi hakuna nawe upo ofisini, mbaya zaidi hatuelezwi tatizo ni nini na litaisha lini, ingawa za chini chini tunaambiwa kuna nguzo imeanguka wilsyani biharamulo.
Ndugu waziri, sababu hii inayoungwa mkono na tanesco wilaya haiingii akilini. Nguzo ianguke tatizo lidumu zaidi ya miezi miwili?
Ndugu waziri juzi umeme ulikatwa saa 10 jioni , hakuna taarifa. Msemajj wa Tanesco mkoa hapokei simu, namba ya meneja ni sawa na nyara za serikali, nikamtafuta Naibu waziri kwa namba..., hapokei, nikatuma sms hakuna majibu hata sasa!
Ndugu waziri, nimesema huduma zimekosa sitanii, mashine za kusukuma maji hazifanyi kazi, pale hospitali ya rulenge ambayo ndio pekee wilaya hii yenye huduma za x-ray, huduma haziwezi kufanyika na hali ilikuwa mbaya zaidi siku nne nyuma pale mafuta yalipofichwa.
Ndugu waziri, nisikuchoshe kwa ujumbe mrefu lakini toka ofisini, njoo huku kwetu kama alivyofanya mtangulizi wako, kuiga kitu kizuri sio ujinga.
Wasalaam.
walioko juu wanatutazama sisi wengine kama wanaoweza kutufanyia chochote na hatuwezi kubadili hali iliyopo. Swali ni je, Hatuwezi kubadili hii hali?Huku kibaha umeme umekata anzia saa saba usiku hadi dakika hii.
Tena inasemekana mama anakuja huku leo.
Tubebe bango la maji au umeme au bidhaa kupanda.
Hii nchi huko juu ni kama wameamua kutukomoa
Magu though uliniumiza ila nimekumisi.
🤣Makamba anaonekana anapenda sana issue zinazohusu Viingereza kutumika. Mi vikao ambayo hata manufaa yake hayaonekani. Anasahau kabisa majukumu yake ya Umeme wa uhakika kwa Wananchi
Mkuu, Jeneretor hizo zilipelekwa bila shaka nyumbani kwao makamu, huku kwa sababu hatuna mjomba tumeachwa hivyo hivyo.kwa nini Tanesco hawawashi hayo magenerator ya hapo nakatunga kwenu au yalishakufa
Huko kwenu mafuta yalifichwa na nani mkuu wakati sheli zinamilikiwa na mtu mmoja(meddy)
by the way msalimie tajiri Asa mwenye ligodown la cement hapo Nakatunga
halafu yule mbunge wenu kijana wa tajiri wa kahawa katerere si nasikia ni msomi sana anashindwaje kutatua tatizo la nguzo moja kuanguka au ndio anataka 2025 mumreplace na aliekuwepo(kashaza) ama jambaz mstaafu Sama
kwahiyo generators zilirudishwa kakonkoMkuu, Jeneretor hizo zilipelekwa bila shaka nyumbani kwao makamu, huku kwa sababu hatuna mjomba tumeachwa hivyo hivyo.
Hawa jamaa Mungu anawaona, wakatulaghai tukaachana na "Solar" zetu sasa wanakuja kutupiga upya na Majenereta.Acheni kulalamika, nunueni majenereta muweke mafuta, tupo kwenye maboresho yasiyokuwa na kikomo🐒
View attachment 2181224
Inaelezwa zilipelekwa Kigomakwahiyo generators zilirudishwa kakonko
Tanesco walisema wamehitimisha maboresho tarehe 10/02/2022 kama ilivyotangazwa na Waziri Makamba, lakini tarehe 27/03 tukaambiwa kwamba umeme utaendelea kupatikana kwa shida mpaka matengenezo na maboresho mbali mbali yatakapoisha, Sema jamaa alikuwa anatafuta shida ya umeme kwa ulazima, alianza maji kupungua, mara kufanya maboresho...kuna kitu anakaitafutaHawa jamaa Mungu anawaona, wakatulaghai tukaachana na "Solar" zetu sasa wanakuja kutupiga upya na Majenereta.
Maushungi ameniweka pale junction ya Mbezi masaa 2½ kisa anapita kumbe ilikuwa safari ya Kibaha.Huku kibaha umeme umekata anzia saa saba usiku hadi dakika hii.
Tena inasemekana mama anakuja huku leo.
Tubebe bango la maji au umeme au bidhaa kupanda.
Hii nchi huko juu ni kama wameamua kutukomoa
Magu though uliniumiza ila nimekumisi.
Hapo kwenye "shell" mtu mmoja ana miliki biashara ya mafuta na taarifa za sasa hivi mafuta hasa Petrol hakuna, maeneo kama Mugoma Leo hii asubuhi wachuuzi yanayuzwa lita moja Tsh 3,500.kwa nini Tanesco hawawashi hayo magenerator ya hapo nakatunga kwenu au yalishakufa
Huko kwenu mafuta yalifichwa na nani mkuu wakati sheli zinamilikiwa na mtu mmoja(meddy)
by the way msalimie tajiri Asa mwenye ligodown la cement hapo Nakatunga
halafu yule mbunge wenu kijana wa tajiri wa kahawa katerere si nasikia ni msomi sana anashindwaje kutatua tatizo la nguzo moja kuanguka au ndio anataka 2025 mumreplace na aliekuwepo(kashaza) ama jambaz mstaafu Sama
vipi Burundi bei sh ngapi mkuu halafu nauli ya kutoka ngara mjini mpaka Rulenge ni ngapi sasa hiviHapo kwenye "shell" mtu mmoja ana miliki biashara ya mafuta na taarifa za sasa hivi mafuta hasa Petrol hakuna, maeneo kama Mugoma Leo hii asubuhi wachuuzi yanayuzwa lita moja Tsh 3,500.