Tetesi: Sakata la Zanzibar lawagawa CCM, watendaji serikalini

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Taarifa hizi zilipatikana kipindi cha kama mwezi mmoja hivi na juhudi za kutaka kuthibitishwa zinaendelea. Tetesi zinadokeza kuwa Kutokana na hali ya nchi ilivyo maamuzi magumu yanahitajika na tayari yamewagawa wana CCM na baadhi ya watendaji wa serikali zote mbili za SMZ na SMT.

Suala la Zanzibar, (uchaguzi wa 2015) na kufutwa kwake na Jecha kumeacha sintofahamu baina ya wahisani na serikali ya JMT na kutaka suala hili lipatiwe ufumbuzi. Jumuiya ya Kimataifa na wadau wa maendeleo hasa Ulaya na Marekani wametowa masharti mazito kuhusu suala la Zanzibar kupatiwa ufumbuzi kiasi cha kuathiri mwenendo wa bajeti kwa JMT. Taarifa zinadokeza kuwa kuna changamoito kubwa sana ya utengenezaji wa bajeti kwa mwaka 2017/2018 ikiwa Tanzania haitakubali masharti yaliyowekwa na jumuiya za Kimataifa kuhusu suala la Zanzibar.

Hali hiyo inartipotiwa kuwagawa wana CCM na watendaji wengine wa serikali zote mbili wengine wakitaka masharti yatekelezwe ili kuinusuri nchi na hatua kali zinazoweza kuchukuliwa na wengine wakipinga.

Imeripotiwa kuwa kuna viongozi waandamizi wa SMZ wakiongozwa na kiongozi mkubwa wanapinga hatua yoyote ya kukubali mabadiliko Zanzibar kama miongoni mwa masharti ya wahisani na jitihada za chini chini za kujenga misimamo kwa wanachama zinaendelea kufanywa na kundi hili kwa upande wa Zanzibar.

Kundi linalounga mkono kutii masharti inaelezwa kuwa linaegemea zaidi katika maslahi ya Taifa na kuangalia zaidi mkwamo unaoweza kulikumba Taifa na kupoteza haiba a yake kimataifa. Tayari kunaripotiwa uwezekano wa kugawika wana CCM wa Tanzania Bara ambao inaripotiwa kuguswa zaidi na athari inazozipata Tanzania ambayo kwa mara ya kwanza imeonja uchungu wa moja kwa moja wa kunnyimwa baadhi ya misaada na nchi wahisani kwa suala la Zanzibar na wale wa Zanzibar hasa Wahafidhina ambao hawataki kusikia neno lolote la mabadilko.

Tunaomba wenye taarifa za uhakika waziweke hapa kwa maslahi ya Taifa.


Kwa hisani ya msamaria mwema.


Kishada.
 
CCM ni chama kisicho na mtazamo na kimekosa Dira tume ya kurekebisha Katiba ilipokuja na Hoja ya serikali tatu wao wakaipinga kwa kuangalia maslahi ya wanadamu na ninadhani wengine walisahau kuwa binadamu leo upo kesho haupo ila katiba itadumu vizazi hata vizazi, suala la uchaguzi wa zanzibar wamelichukulia poapoa kwa kudhani wanakomoa wapinzani leo maji shingoni mnasema sintofahamu,sintofahamu gani kwani hawakujua madhira ya matendo yao.

Tatizo lao FAFAFAFAFA ndio wanapewa nafasi ya kusikilizwa wajuzi na wenye hekima wanafichwa mifukoni utadhani Condom.wazanzibar waombe tu talaka yao.wafanye mambo yao wenyewe.
 
Kama mlijitungia hotuba wenyewe mkasema Ni hotuba ya Mh. Raisi Shein Na bado hakuna lolote la maana mlilo achieve, naona hata haya uliyoandika hapa Ni ujinga wa kiwango cha lami!!
Kubalini tu kwamba Safari hii mmechemka, subirini 2020
 
CCM ni chama kisicho na mtazamo na kimekosa Dira tume ya kurekebisha Katiba ilipokuja na Hoja ya serikali tatu wao wakaipinga kwa kuangalia maslahi ya wanadamu na ninadhani wengine walisahau kuwa binadamu leo upo kesho haupo ila katiba itadumu vizazi hata vizazi, suala la uchaguzi wa zanzibar wamelichukulia poapoa kwa kudhani wanakomoa wapinzani leo maji shingoni mnasema sintofahamu,sintofahamu gani kwani hawakujua madhira ya matendo yao.

Tatizo lao FAFAFAFAFA ndio wanapewa nafasi ya kusikilizwa wajuzi na wenye hekima wanafichwa mifukoni utadhani Condom.wazanzibar waombe tu talaka yao.wafanye mambo yao wenyewe.

Makondokando ya Uchaguzi wa 2015 kule Zanzibar ni mengi. Athari za wazi zilitikisa utekelezaji wa Bajeti ya 2016/2017 ingawa viongozi hawataki kukiri.

Busara inahitajika na kwa hili la Zanzibar basi ni hakika linaendelea kutikisa Muungano wetu.

Wahafidhina wanajificha nyuma ya Muungano kulinda maslahi yao ya kupora na kuvuruga chaguzi zote za Zanzibar. Bahati mbaya sasa inayoadhibiwa ni Tanzania nzima na si Zanzibar.

CCM kama chama tawala tafakarini hii hali kwa maslahi ya Taifa.
 
Kama mlijitungia hotuba wenyewe mkasema Ni hotuba ya Mh. Raisi Shein Na bado hakuna lolote la maana mlilo achieve, naona hata haya uliyoandika hapa Ni ujinga wa kiwango cha lami!!
Kubalini tu kwamba Safari hii mmechemka, subirini 2020

Wewe soma kama tetesi halafu tuachie wenyewe.
 
Taarifa hizi zilipatikana kipindi cha kama mwezi mmoja hivi na juhudi za kutaka kuthibitishwa zinaendelea. Tetesi zinadokeza kuwa Kutokana na hali ya nchi ilivyo maamuzi magumu yanahitajika na tayari yamewagawa wana CCM na baadhi ya watendaji wa serikali zote mbili za SMZ na SMT.

Suala la Zanzibar, (uchaguzi wa 2015) na kufutwa kwake na Jecha kumeacha sintofahamu baina ya wahisani na serikali ya JMT na kutaka suala hili lipatiwe ufumbuzi. Jumuiya ya Kimataifa na wadau wa maendeleo hasa Ulaya na Marekani wametowa masharti mazito kuhusu suala la Zanzibar kupatiwa ufumbuzi kiasi cha kuathiri mwenendo wa bajeti kwa JMT. Taarifa zinadokeza kuwa kuna changamoito kubwa sana ya utengenezaji wa bajeti kwa mwaka 2017/2018 ikiwa Tanzania haitakubali masharti yaliyowekwa na jumuiya za Kimataifa kuhusu suala la Zanzibar.

Hali hiyo inartipotiwa kuwagawa wana CCM na watendaji wengine wa serikali zote mbili wengine wakitaka masharti yatekelezwe ili kuinusuri nchi na hatua kali zinazoweza kuchukuliwa na wengine wakipinga.

Imeripotiwa kuwa kuna viongozi waandamizi wa SMZ wakiongozwa na kiongozi mkubwa wanapinga hatua yoyote ya kukubali mabadiliko Zanzibar kama miongoni mwa masharti ya wahisani na jitihada za chini chini za kujenga misimamo kwa wanachama zinaendelea kufanywa na kundi hili kwa upande wa Zanzibar.

Kundi linalounga mkono kutii masharti inaelezwa kuwa linaegemea zaidi katika maslahi ya Taifa na kuangalia zaidi mkwamo unaoweza kulikumba Taifa na kupoteza haiba a yake kimataifa. Tayari kunaripotiwa uwezekano wa kugawika wana CCM wa Tanzania Bara ambao inaripotiwa kuguswa zaidi na athari inazozipata Tanzania ambayo kwa mara ya kwanza imeonja uchungu wa moja kwa moja wa kunnyimwa baadhi ya misaada na nchi wahisani kwa suala la Zanzibar na wale wa Zanzibar hasa Wahafidhina ambao hawataki kusikia neno lolote la mabadilko.

Tunaomba wenye taarifa za uhakika waziweke hapa kwa maslahi ya Taifa.


Kwa hisani ya msamaria mwema.


Kishada.
Well said,nchi imekwama kifedha ni aibu tupu,wahisani wamegoma kuchangia bajeti ,halafu eti watumishi wanataka kuongezwa hela hela hakuna amino nawabieni
 
Well said,nchi imekwama kifedha ni aibu tupu,wahisani wamegoma kuchangia bajeti ,halafu eti watumishi wanataka kuongezwa hela hela hakuna amino nawabieni
Wabunge nao kimyaaaa majimboni! Kuna mbunge wetu mmoja kahamia shambani kulima; Hapa Kazi Tu,mambo mengine hayasomeki.
 
Badala ya kudeal na tatizo wao wanamuongezea dau polofesa uchwara kuivuruga cuf! Mwafwaaaa
 
Kama mlijitungia hotuba wenyewe mkasema Ni hotuba ya Mh. Raisi Shein Na bado hakuna lolote la maana mlilo achieve, naona hata haya uliyoandika hapa Ni ujinga wa kiwango cha lami!!
Kubalini tu kwamba Safari hii mmechemka, subirini 2020
Tanesco hawana itikadi
 
Kwani hilo deni la TANESCO wanalipa serikali ya Zanzibar au watumiaji wa umeme ndio wanaolipa? Kwa kipindi chote ambacho walikuwa hawalipi, je wananchi wanapelekewa bill ama la! Kama wananchi wanauziwa umeme kwa kila unit wanayotumia ni kwa nini serikali ya mapinduzi isilipe hizo hela kwa TANESCO? Yani watu kama vile wanadhani serikali ya zanzibar ndio inayoilipa TANESCO kutoka kwenye makusanyo yao mengine
 
Tanzania bara tunapata maumivu makali ya maisha kwa sababu ya Tanzania visiwani, waache CUF iongoze CCM imekata pummzi
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom