SAKATA la UWANJA wa NYAMAGANA: Ubomoaji Wake na Migongano ya Taasisi Husika

na Sitta Tumma , Mwanza



SAKATA la kuvunjwa kwa uwanja wa michezo wa Nyamagana uliopo katikati ya Jiji la Mwanza, limeanza kuchukua sura mpya, kutokana na Chama cha Mapinduzi (CCM), mkoani hapa kulifikisha kwa uongozi wa taifa ili utoe tamko rasmi.
Uamuzi huo umekuja baada ya CCM Mkoa kuonekana kuingia kwenye mgogoro mzito na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, baada ya chama hicho kupinga kitendo cha halmashauri hiyo, kuubomoa uwanja huo kwa ajili ya kupisha uwekezaji wa hoteli ya kitalii.

Taarifa ya CCM Mkoa kwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho taifa kwa upande wa Bara, Pius Msekwa, imeeleza kusikitishwa na kitendo cha uongozi wa jiji kuvunja uwanja huo, na kwamba hatua hiyo inakinzana na Ilani ya uchaguzi ya chama hicho ya kukuza na kuboresha michezo hapa nchini.

Mbali na taarifa hiyo kulaani ubomoaji wa uwanja huo, pia imeeleza kuwa uamuzi uliofikiwa na uongozi huo wa jiji, unapaswa kusitishwa mara moja ili kwenda sambamba na utekelezaji wa ilani hiyo ya uchaguzi.

Mwezi mmoja uliopita, uongozi wa Jiji la Mwanza chini ya Mkurugenzi wake, Wilson Kabwe ulianza ubomoaji wa uwanja huo, pasipo kueleza dhamira halisi ya kuuvunja, licha ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Pombe Magufuli kutoa amri ya kutovunjwa.

Habari za ndani zinaeleza kuwa, sababu ya kuvunjwa Nyamagana, inatokana na mmoja wa wafanyabiashara wakubwa jijini hapa, kupewa nafasi hiyo na jiji kwa ajili ya kujenga hoteli.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa kwa Msekwa na Mwenyekiti wa CCM Nyamagana, Athuman Zebedayo, uongozi wa jiji umekaidi amri ya kusitisha zoezi hilo la ubomoaji.

"Makamu mwenyekiti, kuna mgogoro umeanza kufukuta kati ya chama na jiji, na sababu ya yote hayo ni Uwanja wa Nyamagana ambao jiji linaubomoa bila sababu za msingi, na chama hakitaki kubomolewa kwa uwanja huo," alielezwa Msekwa.

Mwenyekiti huyo aliyekuwa akizungumza huku akionyesha dhahiri kukerwa na kitendo hicho, aliyaeleza hayo juzi kwenye Baraza la Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), jijini hapa lililokutana kwa ajili ya ugeni wa Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM taifa.

Akifafanua zaidi kuhusu suala hilo, huku akishangiliwa na wajumbe, Zebedayo alisema, kuvunjwa kwa uwanja huo ni sawa na kuvunjwa kwa sera na ilani ya CCM na kwamba uwanja huo ndiyo tegemeo kwa vijana kufanyia mazoezi.

Aliitumia nafasi hiyo, pia kumuomba Msekwa pamoja na Mwenyekiti wa Taifa CCM, Rais Jakaya Kikwete kutumia mamlaka yake ya kichama kutoa amri ya kutovunjwa kwa uwanja huo mkongwe.

"Kwa mfano, uchaguzi umekaribia na vijana tumeanza kuwabughudhi, tofauti na tulivyowaahidi katika kampeni za uchaguzi mkuu, hivi tutaponea wapi? Kwa nini jiji likiuke ilani na sera za chama tawala?" alihoji Zebedayo.

Hata hivyo, habari zilizopatikana jijini hapa na kuthibitishwa na kiongozi mmoja wa ngazi ya juu mkoani hapa, zimeeleza kuwa mmoja wa wana CCM mkoani hapa, ndiye anayetaka kujenga hoteli katika viwanja hivyo na kwamba kamwe chama hakitaridhia kubadilishwa matumizi ya uwanja huo.
WAkuu heshima mbele,Je kuna mtu anafahamu ni mfanyabiashara gani anataka kuchukua eneo hilo?,Je wana bodi mnasemaje kuhusu hili la kubomolewa?.sijafika Mkoa wa Mwanza muda kujua kama kweli uwanja huo umebomolewaa.
 
Kuna fununu kuwa mjenzi huyo ni MOIL yule ambaye petrol station yake ilibomolewa kwa amri ya Magufuli.Jina ni Mansoor na kiongozi wa CCM mkoa.
 
Kwani huu uwanja ni mali ya city au ccm? nadhani mwenye mali anahaki juu ya maamuzi ya mali yake ilimradi havunji sheria, kwani mipango miji hawajahusishwa? nadhani hii issue inamhusu zaidi Mizengo Pinda na Magufuli sio Msekwa. Kama kuna hoja yamsingi Laurence Masha Mbunge wa Nyamagana anauwezo wakuishughulikia.

Tunahitaji kujenga mwanza safi, uwanja huu unastahili kuhamishiwa Buswelu na kujengwa kisasa zaidi, hapo pajengwe hotel yenye hadhi ya nyota tano.

Ghati la kamanga ferry lihamishiwe kigongo ferry, kuondoa bugudha hapo mahakama kuu na kupunguza uchafuzi wa mazingira unaofanywa na maroli kutoka mikoani.

Ushauri wangu pia idara za ardhi na mipango miji pale city kivunjwe, wilaya ya Nyamagana na Ilemela zijitegemee ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi. Sasa hivi viwanja vya magufuri vimeisha na hakuna kinachoendelea.
 
Usanii mtupu! Hakuna cha hoteli ya kimataifa isipokuwa ni shopping mall ya kitanzania itayoambatanishwa na glorified guest house.
 
Nyie ccm wanafiki wakubwa, uwanja wenu wa kirumba mmeshindwa hata kurepair vyoo! Wilson Kabwe; ccm waondoe kwanza ukumbi wa uvccm pale kirumba uliojengwa eneo la kuchezea watoto, pia lile danguro la villa park pale ccm kirumba, ndio tuwasikilize.

Shanif kama umepata vibali vyote wewe shusha kitu, wakibomoa watakulipa tena; wanahela za kuchezea. Hebu tizana jengo la nssf linavyopendeza! nihawahawa ccm waling'ang'ania kuweka josho la mbwa pale.

Magufuli na Mizengo Pinda hebu tizama ofisi ya DC wa Ilemela ilivyokaa patamu, ingefaa ofisi za serikali ziwe nje ya mji, maeneo ya kati wapewe wawekezaji kama shoprite watujengee malls kama za J'berg. Hivi nyie ccm hamjui tumeshaingia EPA! naona mnazubaa tu.
 
Hii yote ni kina Gachuma, Mzee Lameck (LAKAIRO) na Sarungi ndio wanohusika.

Na ujue kwamba Gachuma na Lameck walikuwa wafuasi wa Sumaye baada ya kushindwa walipiga U turn na kutoa fedha nyingi kwa kampeni ya mkuu wa kaya ili kujisafisha na sasa wamennunua uwanja huo
 
Mh,
Kweli hapa CCM wanakuwa hypocrites, uwanja huo wa Nyamagana umechoka, kama ni wa kwao hawajautunza kabisaa. Uwanja una official entrance moja au mbili. Halafu un-official entrances kibao. Halafu CCM Kirumba ndo hivyo

Ila sasa tukija kwa wawekezaji wetu, huwa wanapata viwanja vizuri halafu wanashusha lijengo libovu libofu. Hoteli inayopendeza Mwanza ni Tilapia tu. Zingine wanakuwa wanalipua tu. Kama kweli wanashusha kitu hapo, basi waweke kitu cha maana.

Navyoona kama ni kwa biashara, uwanja utoke tu. Kama ni sentimental value, historia, bla bla....basi ubaki. Mshindi ni pesa.
 
Ni lazima hiyo shopping mall ijengwe katikati ya jiji...halafu how will the city breath mnataka iwe kama Dar kila mahali kumejengwa...
Wachukue Mbuga huko Kisesa wajenge!
 
Ni lazima hiyo shopping mall ijengwe katikati ya jiji...halafu how will the city breath mnataka iwe kama Dar kila mahali kumejengwa...
Wachukue Mbuga huko Kisesa wajenge!

Alishasema muungwana mmoja paachwe iwe bustani! Huyu naona alikuwa na busara. Miji yote ya maana ina sehemu ya kupumulia. Mnadhani watu wa New York ni wajinga kuacha Cental Park? Ingekuwa bongo tungejaza mighorofa na baya zaidi mighorofa isiyo na mbele wala nyuma. Hawa wawekezaji uchwara hawatutakii mema.
 
Gachuma & co wameshapitwa na wakati, kachemsha kuwakodisha wasauz hotel, Mzee Lamerk shule ndogo na wapambe wajaluo, wanatuletea siasa za kishamba. Moil ni mfanyabiashara makini mwenye mipango madhubuti, hao wakurya sio tatizo kwake.

Mama Leo ushauri wako mzuri sana, ingefaa tuhamishe hizo ofisi za mahakama na ofisi ya mkuu wa mkoa zikajengwe Buswelu karibu na ofisi mpya ya DC wa Ilemela. Uwanja huu ukajengwe Igoma yanapofanyika maonyesho ya nanenane. Shule ya sekondari Pamba ikajengwe kisesa. Sehemu hizo zijengwe shopping malls na hotel za nyota tano, nasikia shoprite wanatafuta eneo mwanza. Ofisi za majitaka zitahamia nyegezi sio muda mrefu, hivyo msongamano utapungua sana. Kuhusu maeneo ya kihistoria ni moja tu nalo ni mti uliotumiwa na wajerumani kunyonga watu.

Tatizo lilipo ni huyo afisa ardhi Kitilya ni ndondocha fulani, viwanja vya Magufuli vimeisha wala hana habari ya kupima vingine, kazubaa tu. Magufuli nae kakomaa na makazi kasahau kunahitajika viwanja kwa ajili ya viwanda, biashara na public services.
 
Sawa kabisa Fundi Mchundo, ila inaonekana una siku nyingi haupo tz, tuna bustani nzuri pale Ghandi hall, Rock beach na BOT conference centre, pia ufukwe wa makongoro umesafishwa. Fukwe hizi na parks zinatunzwa na mama Rwegoshora decorations services.

Mheshimiwa kikwete aliishauri city wapime viwanja vya Golf, city parks na beach resorts, tayari eneo la ufukwe la Luchelele limeshatengwa kwa kazi hiyo. Kikwete angetufanyia jambo la maana kama atamrudisha Mzee Ole Njolay kuwa RC wa Mwanza. Huyu Mwalimu wa physics haiwezi kasi ya maendeleo ya Mwanza.

Kulikuwa na shida ya car parks, PPF wametusaidia kwa kujenga car park ya ghorofa kumi na tayari reserved speces zimeshakwisha nunuliwa hata kabla jengo halijaisha.

Inaonekana NY watu hupumzika katikati ya mji, sijawahi fika NY, ila mwaka jana nilikuwa East London na Dublin africa ya kusini, watu hupunzika fukweni nje ya mji na huenda city centre kufanya shopping tu. Ofisi za serikali ziko nje ya mji pia.
 
Eddy, hizo ni gardens! Nazungumzia parks! Tofauti ni scale. Ingawa bustani ni mwanzo mzuri, tunahitaji maeneo makubwa zaidi. Dar es Salaam eneo lote la jangwani kwa mfano lingeachwa na si kubakia na botanical garden tu. Mwanza siijui vizuri kwa hiyo sina la kusema.
 
Asante Fundi, nilikosea kidogo, hiyo bustani ya Ghandi hall ni Garden, tunategemea Golf course, beach resorts na city parks ziwe nje ya mji kama alivyoshauri mh.Kikwete. Uwanja wa nyamagana hauwezi kuwa city park nipafinyu tena pembeni yake kuna railway sideway sio salama kwa watoto. Xmas nilikuwa speak bay resort km 120 kutoka city centre watu wengi walikuwa wanapumzika huko na familia zao.
 
Sometimes I really wonder hivi tunavyotembelea nchi za wenzetu huwa tunajifunza nini hasa? Jamani tusione tu vyaelea vimeundwa!
Tutakuwa washamba wa mawazo hadi lini???
 
Tukiwa nje tunatanguliza shopping ndiyo maana tunadai na sisi tuwe na malls! Malls zinajengwa nje ya mji kwa vile zinahitaji sehemu kubwa na gharama ya viwanja katikati ya miji ni bei mbovu. Malls zinachangia kufa kwa maduka asilia (corner stores, masoko ya jirani n.k.) zilizokuwa na personalised services na kuchangia kwenye community ambamo maduka hayo yalikuwemo. Nakumbuka maduka ya washihiri ambao walikuwa wanawakopesha wateja wao na kuwauzia bidhaa kwa vipimo wanavyomudu (robo kibaba, robo mche wa sabuni ya kufulia n.k). Mall zinawafaa wenye usafiri maana mteja anategemewa kununua kwa wingi. Kuwa na Mall si dalili ya maendeleo kama tunavyodhani bali ni dalili kuwa tumeingia katika mfumo wa biashara wa kimataifa. Badala ya faida kwenda kwa mshihiri inaenda kwa mwekezaji Afrika ya Kusini.
 
Kuna watu hawaitakii mema mwanza yetu, utakuta jitu aliishi mwanza, sio mbunge wa mwanza, sio diwani wa mwanza, hana biashara mwanza lakini kawa msumari wa maendeleo yetu. Mtu anasema hotel ikajengwe usagara! mbona hamkusema gome supermarket ikajengwe Mkuranga. Jinga moja linasema uwanja huu ni makumbusho! wizara husika imeshatoa shs ngapi kukarabati? nimepiga picha huu uwanja jana ila nimeshindwa kuatach hapa.

Mwaka juzi uzio wa uwanja ulianguka nusura umalize watoto. akina mama kilasiku wanaporwa pochi na simu na vibaka wanaoshinda wakivuta bangi uwanjani. ingia uwanjani utakuta simu, sight mirror za magari zinauzwa elfu mbili.

NSSF tumeshawapa kiwanja kilichokuwa josho la mbwa, viwanja 1500 kwa ajili ya housing project, waache nawengine wajenge! kama wako interested wanunue 45% share za serikali kutoka huo mradi.

Hivi inakuwaje wakazi wa mwanza wakitaka kuendeleza mji wao inakuwa kelele hivi? Mama Mongela na Magufuli wamekuwa sumu ya panya. Kupata kiwanja cha kujenga kiwanda, hotel, shule imekuwa tabu kweli kweli. Ole njolay alijaribu kufanya usafi kidogo sijui kaishia wapi, tangu atishiwe kurogwa simsikii tena.

Huyu mwalimu wa chemistry sengerema secondary anataka kuwa profesa wa mipango miji na mtaalamu wa mambo ya kale. Shenzi type.
 
Kuna watu hawaitakii mema mwanza yetu, utakuta jitu aliishi mwanza, sio mbunge wa mwanza, sio diwani wa mwanza, hana biashara mwanza lakini kawa msumari wa maendeleo yetu. Mtu anasema hotel ikajengwe usagara! mbona hamkusema gome supermarket ikajengwe Mkuranga. Jinga moja linasema uwanja huu ni makumbusho! wizara husika imeshatoa shs ngapi kukarabati? nimepiga picha huu uwanja jana ila nimeshindwa kuatach hapa.

Mwaka juzi uzio wa uwanja ulianguka nusura umalize watoto. akina mama kilasiku wanaporwa pochi na simu na vibaka wanaoshinda wakivuta bangi uwanjani. ingia uwanjani utakuta simu, sight mirror za magari zinauzwa elfu mbili.

NSSF tumeshawapa kiwanja kilichokuwa josho la mbwa, viwanja 1500 kwa ajili ya housing project, waache nawengine wajenge! kama wako interested wanunue 45% share za serikali kutoka huo mradi.

Hivi inakuwaje wakazi wa mwanza wakitaka kuendeleza mji wao inakuwa kelele hivi? Mama Mongela na Magufuli wamekuwa sumu ya panya. Kupata kiwanja cha kujenga kiwanda, hotel, shule imekuwa tabu kweli kweli. Ole njolay alijaribu kufanya usafi kidogo sijui kaishia wapi, tangu atishiwe kurogwa simsikii tena.

Huyu mwalimu wa chemistry sengerema secondary anataka kuwa profesa wa mipango miji na mtaalamu wa mambo ya kale. Shenzi type.

Eddy, ndiyo mimi nime suggest hiyo Usagara (na ningeweza ku-suggest sehemu nyingine tu nyingi nje ya mji ambazo zinahitaji kuendelezwa, Usagara ni mfano) kwa lengo mahili tu kuwa hiyo hotel kujengwa katikati ya mji wa Mwanza siyo suluhisho la hayo unayoyasema, sijui vibaka wanapora pochi, sijui wajinga wanataka uwe makumbusho... ooh sijui ukuta ulianguka...

Hata uwaite wajinga, ujinga wa kwanza utakao kuwepo na ni chanzo kikubwa cha huu ujinga wa sasa hivi ni hiyo hali ya kuachia kiwanja kifikie hali hiyo, kilitakiwa kiwe kimesha endelezwa zamani na kuwa katika hadhi nzuri iwapo watu kama wewe mnaojiona mnajua kuendeleza mji wa Mwanza mngelikuwepo toka awali, na hiyo akili endelevu ingelikuwemo moyoni na siyo kusubiri tamko kutoka kwa Mh. Kikwete kama unavyotaka tuamini.

Maendeleo ya Mwanza ni kwa ajili ya Watu wa Mwanza na yanabuniwa na kufanikishwa na watu wa Mwanza, hayo mambo unayotaka kutuhubiria ya kutukuza tamko la Mh. Kikwete kama nguvu ya maendeleo ya Mwanza ni kutaka kupotosha ukweli kuwa, maendeleo kama hayo yanapatikana tu iwapo yanapata baraka ya mh. Kikwete.

Pia ndugu Eddy, unataka kuendeleza kupandikiza uongo wako kuwa kubomolewa na kutokuwepo kwa hicho ni matakwa ya wakazi wa Mwanza, eti yakuwa wanataka maendeleo kwa kukibomoa ili hotel ijengwe.... spins spins spins!

Juzi tu hapa, chama cha mpira Mwanza, kimewakilisha pingamizi yake katika kubomolewa kwa hiki kiwanja, unataka kuniambia idadi ya watu wanaopinga na kuwakilishwa na chama cha mpira Mwanza ni negligible?...Bwana wee, hizo personal gain zako kutoka katika ujenzi wa hotel, usitake zi-justify ukweli kuwa hiyo sehemu ikishajengwa hotel, wakazi wengi walio mwanza mjini watakosa sehemu nafuu ya kushiriki katika michezo, na acha kuwaita watu wajinga, maana tupo hapa kutoa mapendekezo, kama huafikiani nayo eleza sababu na siyo name calling. Na kama una machungu ya kweli na mji wa Mwanza, ungelikuwa uko mstari wa mbele katika kuendeleza kupanuliwa kwa jiji la Mwanza na siyo kuli-condense kwa kusubiria directives kutoka kwa Mh. Kikwete. Ahsante.

SteveD.
 
aa usitake kuchonganisha watu, mheshimiwa hana interest na nyamagana. yeye alipokagua ujenzi wa makazi mwanza aliuliza mbona hakuna plan za maeneo ya viwanda, parks na golf course ambayo huchukua maeneo makubwa hivyo mipango inahitajika mapema.

Nasema tena mwanza tutajenga wenyewe! Hawa MRFA wanavibanda vya photocopy hawataacha kusema. Shanif namfahamu kama wanategemea mgao haupo.
 
Wapendwa muda huu kuna maandamano pale mwanza kupinga ubadilishaji wa matumizi ya uwanja wa Nyamagana. Eti mgeni rasmi ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza (mpenda vyeo) sasa wakati anahutubia na waandamaji wakitegemea kuwa atatoa tamko rasmi badala yake akawaambia wananchi wajaze saini zao kwenye daftari lililotolewa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza la kupokea maoni yao.
Waandamanaji walipomzomea akaanza kuwatishia kuwaweka ndani
 

Attachments

  • Picture 009.jpg
    Picture 009.jpg
    10.4 KB · Views: 103
  • Picture 002.jpg
    Picture 002.jpg
    9.6 KB · Views: 66
Mkuu wa mkoa wa mwanza atishia waandamani kuwaweka ndani wakimzomea wakati wa maandamano ya kupinga ubadilishaji wa matumizi ya uwanja wa nyamagana
 
Back
Top Bottom