Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA AROBAINI NA TANO
“Yes, nimeupenda sana huo mpango ndiyo maana huwa nakufuata wewe kwa sababu najua ni mtu ambaye una mahesabu ya mbali sana tofauti na watu wengi. Lakini kuna jambo ambalo linanitatiza hapa, vipi kama hao vijana ambao watatumwa wakikamatwa huoni kama inaweza kuwa hatari sana kwetu kama wakitutaja?”

“Tutatuma timu mbili, timu ya kwanza itakuwa kwa ajili ya kutekeleza jukumu hilo lakini timu ya pili itakuwa kwa ajili ya kuiteketeza timu ya kwanza hivyo haitajalisha kama mpango ukienda sawa au ukiharibika lakini timu ile ya kwanza ni lazima yote iuawe ili kusije kuwa na ushahidi hata hapo baadae”

“Hahaaahaaaaaaa hahaha huyu bwana mdogo anacheza na watu ambao sio levo zake, kama kweli atakuwa ndiye yeye basi ameingia sehemu mbaya sana. Mimi nikutakie usiku mwema mheshimiwa na asante sana kwa kukubali kufanya kazi na mimi” mr Mafupa aliongea kwa furaha sana huku akiwa anampa mkono mwanaume huyo na kutoka humo ndani. Mr Oscar alitabasamu sana kwani mtu huyo hakuwa na akili hivyo angemuendesha kwa namna ambayo angeona yeye inamfaa. Akiwa ameketi bado ndani humo aliingia kijana wake ambaye alionekana kuwa na taarifa ambazo alipaswa kuziwasilisha wakati huo.

“Vijana wamefanikiwa kumjua mtoto wa mr Mafupa hivyo wanasubiri amri yako kiongozi.”
“Kesho usiku wahakikishe anakufa kwa namna yoyote ile kwa sababu nina imani kwamba ndiye ambaye anampa nguvu hivyo kama mtoto huyo akifa basi hatakuwa na sehemu yoyote nyingine ya kusimamia atajikuta anakuwa mtumwa wangu kwenye siku zake zote za maisha yake” ni amri ambayo ilitakiwa kutekelezeka haraka sana kwani ilisikika na ilieleweka vizuri kabisa.

“Sawa kiongozi” alijibu kijana huyo na kutoka humo ndani huku akiwa anamuacha mwanaume huyo kwa tafakuri nzito sana ambayo ilimfanya awaze nama sahihi ya kwenda kuliendesha taifa la Tanzania kupitia mwanaume huyo ambaye alikuwa mbele yake.


Asubuhi ya siku ambayo ilikuwa inafuatia ilijaa heka heka nyingi sana ndani ya jiji la Dar es salaam kwani ndiyo siku rasmi ambayo watu waliokuwa wamechaguliwa kwenye vyama vyao kuweza kutangazwa rasmi na kuweza kuruhusiwa kuanza swala zima la kufanya kampeni. Kabla hata ya jambo hilo kufanyika watu waliamka na habari mbaya sana ya mauaji ya kutisha ya watu ambayo yalifanyika karibu kabisa na chuo cha CBE, watu hao walikuwa wamepigwa risasi vibaya sana kiasi kwamba hata hali zao zilikuwa zinatisha lakini pia mlinzi wa chuo hicho cha biashara alikuwa amepigwa risasi na kufariki hapo hapo.

Licha ya polisi kujitahidi sana kuficha jambo hilo ili kutoleta mkanganyiko kwa wananchi lakini habari hizo tayari zilikuwa zimesambaa sana kwenye mitandao ya kijamii huku watu wakianza kulaani kwamba jambo hilo halikuwa la kiungwana pia ukiangalia na aina ya matukio ya namna hiyo ambayo yalikuwa yanaendelea kutokea ndani ya nchi yalifanya watu wasiwe na imani sana na uchaguzo wao wa mwaka huo ambapo waliamini kwamba huenda kukawa na mauaji zaidi ya hayo ambayo yanatokea na huenda hiyo ilikuwa ni ishara mbaya sana kutoka kwa Mungu kuhusu uchaguzi wa mwaka huo ambao huenda ungekuwa chanzo cha maafa makubwa sana kwa watanzania.

Lakini palipo na pesa hakuna kelele za watu, kuna watu ambao walionekana kuongea sana walitafutwa haraka sana na kulipwa pesa ambapo badala ya kuanza kuwasemea wananchi na kuwatetea wanyonge walianza kuyageuza maafa hayo kuwa kama sehemu ya kampeni kwa wagombea wao huku wakidai kwamba mr Mafupa ndiye alikuwa mtu sahihi zaidi kuweza kutokomeza hayo yote ambayo yalikuwa yanatokea kwenye nchi yao.

Pesa ilinunua nafasi za watu wenye nguvu na ushawishi, pesa ilifanya sauti za wanyonge zisisikike kabisa lakini pesa ilisababisha umwagaji wa damu nyingi sana isiyo na hatia kwa sababu wale ambao walijifanya kuwa wazalendo sana na wakagoma kuungana na watu hao ili kuwapa sifa ambazo walizitaka basi hawakupewa nafasi ya pili ya kuendelea kuishi bali waliuawa muda huo huo hivyo pesa ikawa inazuia sauti za wanyonge na wasakatonge kuweza kusikika. Pesa ndicho kilikuwa kipimo cha nguvu na uwezo wa watu huku nyuma yake kukiwa na watu wenye akili kubwa ambao walikuwa wanaifanya pesa hiyo iweze kutumika kisawa sawa kutekeleza maslahi ya watu fulani.

Hivyo wananchi wenyewe walianza kupishana kwenye suala zima za kiitikadi za nchi. Lakini asubuhi hiyo hiyo wakati hayo yote yanaendelea watu wengi sana walishtushwa na taarifa nyingine kutoka kwenye ofisi ya makosa ya jinai kwa kudai kwamba kulikuwa na mkanganyiko wa taaifa za mwanzo ambapo walisema kwamba Apson Limo alikutwa na baadhi ya makosa ya jinai lakini kiuhalisia ni kwamba alikuwa ni mtu mwingine ambaye alidai kwamba Apson Limo ndiye aliyemtuma lakini baada ya uchunguzi wa kina zaidi waligundua kwamba mzee huyo hakuwa akihusika kabisa kwenye tukio hilo hivyo kama ofisi ilikuwa inaomba sana msamaha kwa familia nzima ya Apson Limo lakini kwa watanzania pia kwa huo mkanganyiko ambao ulitokea ndani ya nchi yao hususani kwenye suala zima la maamuzi.

Hiyo ilikuwa kazi ya mkurugenzi wa usalama wa taifa kama alivyokuwa ameelekezwa na Tommy kwamba kama anahitaji kutimiziwa kile ambacho alikuwa amekiomba basi kwenye moja ya masharti lilikuwa ni hilo la kumsafisha baba yake. Wakati mambo hayo yanaendelea Tommy alikuwa ndani ya chumba ambacho alikuwa amelazwa baba yake, mzee huyo hakuwa amefumbua macho lakini taarifa hiyo ni kama alikuwa anaisikia kwani alionyesha tabasamu lake kwa mbali sana ambalo lilihitaji mtu kuwa makini sana ili kuweza kuliona au kugundua kwamba mzee huyo ametabasamu.

“Baba leo tunaenda kumpumzisha mwanao wa mwisho na leo usiku lazima nimpumzishe pia ambaye amesababisha mdogo wangu kufariki. Nimekuja hapa kupata baraka zako baba nina imani nitakuona tena karibuni” mwanaume aliongea kinyonge sana huku akiwa anaigusa miguu ya baba yake na kuifanyia maombi kwa sababu alikuwa anachukua baraka zake. Alitoka humo ndani na kuelekea kwenye chumba cha daktari ambaye ndiye alimpa ile kazi ya kufanya oparesheni ya kichwa cha mdogo wake kuunganisha na kiwiliwili.
“Kazi yako imeisha vyema mheshimiwa”
“Asante sana ila kuna jambo nataka nikuombe hapa daktari”
“Lipi hilo?”
“Hili jambo hatakiwi kulijua mtu yeyote yule”
“Una maanisha nini mheshimiwa?”
“Hakuna mtu ambaye anatakiwa kujua kwamba kichwa cha mdogo wangu kimepatikana”
“Hata kwa watu wenu wa karibu?”
“Ndiyo”
“Naweza kujua kwamba ni kwanini labda?”
“Hapana siwezi kukwambia ila wewe hakikisha tu unayafanyia kazi niliyo kwambia hapa na nakuomba sana usije ukafanya kosa juu ya hili”
“Sawa mheshimiwa, kwahiyo nikifuatwa nikatae?”
“Hapana ukikataa watajua kwamba kuna kitu unakificha hivyo watakubana mpaka useme ukweli hivyo utapaswa kuwaambia kwamba umeandaa mwili ambao hauna kichwa”
“Na vipi kama nikisema ukweli” mwanaume hakuongea chochote bali aliidondoshea picha ya daktari huyo akiwa na familia yake kwenye meza yake hiyo ya kazi.
“Sitakuwa na chaguo zaidi ya kuua familia yako yote”
“Whaaaat? Umekuja kuniomba au kunilazimisha?”
“Ni ombi lakini ukiona kama nakuonea basi itakuwa ni lazima”
“Sikutegemea kama unaweza kuwa mwanadamu mshenzi sana namna hii”
“Upo sahihi ila hakikisha huu ushenzi wangu siji kuufanyia kwenye familia yako kwa sababu ujajuta sana kufanya maamuzi ya kijinga”
“Sawa nimekuelewa” alijibu huku akiwa anatokwa na jasho jingi sana kwenye mwili wake ambalo lilionyesha wazi wasiwasi mkubwa ambao alikuwa nao moyoni.
“Nipeleke kwenye hicho chumba cha mdogo wangu” hawakuwa na maneno mengine ya kuongea hapo kwa sababu mwanaume alikuwa amesha ikata hata mood ya daktari huyo ambaye moyo wake ulijawa na hofu ya kutosha. Mwanaume aliingia ndani ya chumba hicho ambacho ulifanyika upasuaji wa mdogo wake huyo akajifungia mwenyewe huko.

Aliukagua mwili huo na kuona upo sawa, alikaa kwa muda akiwa anawaza mbali sana namna mdogo wake alivyokuwa akimpenda, alivyokuwa akimtania na alivyokuwa akideka kila alipokuwa akimuona kaka yake huyo. Yeye ndiye alikuwa kipenzi cha Latifa, mwanaume alijikuta taratibu anaanza kudondosha chozi lake. Alitumia saa zima kukaa humo ndani kisha zikafanyika taratibu za kuondoka na mwili ambapo walihitaji mazishi hayo yawe ya siri sana na kweli ndilo jambo ambalo liliweza kufanyika, hakuna mtu ambaye alijua kwamba familia hiyo ilikuwa inafanya mazishi siku hiyo huku wao wakiwa kwenye majonzi makubwa sana.

Ni kweli baada ya muda mfupi tangu Tommy atoke hospitalini hapo kuna wanaume waliingia na kujitambulisha kama wageni wa familia ya Apson Limo ambapo waliruhusiwa mpaka kwenye hilo eneo ambalo lilikuwa ni la watu maalumu wenye uwezo mkubwa. Wanaume hao wakiwa ndani ya suti zao walitaka kuingia ndani ya chumba ambacho alikuwa amelazwa mzee huyo lakini walikutana na ulinzi mkali sana ambapo waliambiwa kwamba kama wanahitaji kumuona mzee huyo basi walitakiwa kwanza kufanya mawasiliano na mtoto wake wa kiume jambo ambalo kwakweli hawakuwa tayari kabisa hivyo wakaaga kwa kudai kwamba wangeweza kurudi baadae.

Lakini safari yao iliishia kwenye ofisi ya daktari ambaye walipokea taarifa kwamba ndiye ambaye alikuwa anahusika na mwili wa Latifa. Wanaume hao walikuwa wapo ndani ya upelelezi mkali ili wawe na uhakika kwa asilimia mia kwamba je Tommy ndiye ambaye alikuwa nyuma ya mambo yote na mauaji ya kikatili ambayo yalikuwa yanatokea ndani ya jiji? Huo mtihani kama wangeufaulu basi walikuwa wanapata majibu ya uhakika na ndiyo maana walikuwa wamemfuata daktari huyo kwani kama angewathibitishia kwamba Tommy alikileta kichwa cha mdogo wake basi moja kwa moja angekuwa yeye ndiye mhusika lakini kama hilo jambo lisingefanikiwa basi wangehisi kwamba huenda alikuwa ni mtu mwingine ambaye alikuwa anatumia utambulisho wa Tommy ili kukamilisha mambo yake ambayo hata hawakujua lengo lake hasa ni lipi.

Baada ya kuingia humo ndani na kuweza kumhoji daktari huyo, wao walidai kwamba walikuwa ndugu na marafiki wa karibu sana wa Apson Limo hivyo walikuwa wanazihitaji taarifa hizo ili kuangalia ni namna gani walikuwa wanaweza kuyafanya mazishi ya mtoto huyo. Lakini daktari huyo alikumbuka vyema sana kuhusu vitisho ambavyo alikuw amepewa kuuliwa familia yake basi aligoma katakata na kudai kwamba mwili huo haukuwa na kichwa mpaka dakika za mwisho ambapo muda mchache tu uliopita umechukuliwa kwa ajili ya kufanyiwa mazishi na familia kwani waliona hata aibu kuweza kutangaza msiba kwa mtu ambaye hata kichwa chake hakikuwepo.

Wanaume hao baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa na kile ambacho walikifuata hapo walikikosa waliamua kuwasiliana na kiongozi wao na kumpa taarifa hiyo.

Ukurasa wa 45 unafika tamati.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA AROBAINI NA SITA
“Bosi inaonekana kama sio yeye kwa sababu daktari ambaye amehusika, ameandaa mwili tu hakukuwa na kichwa maana yake kama angekuwa ni yeye tangu jana basi angekuwa amehakikisha kinafanyiwa oparesheni usiku ili asubuhi mwili mzima uwe tayari kwa mazishi”
“Ok, tutaenda na plan B, nyie ondokeni hapo haraka sana kabla ya kushtukiwa na mtu yeyote”
“Sawa mkuu” wanaume hao baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa walitoweka hilo eneo haraka sana.

Kwenye ila nafasi ambayo alitakiwa kukaa Apson Limo alitangazwa mgombea mwingine kwa sababu mzee huyo hali yake ilikuwa mbaya sana na huenda asingeweza kupona na hata kama angepona basi ingechukua muda mrefu sana kiasi kwamba isingewezekana uchaguzi kumsubiri yeye hivyo mambo mengine yalitakiwa kuendelea kama ilivyokuwa kawaida.

Siku iliisha, hatimaye ukawa umeingia usiku mwingine tena, baadhi ya watu wakiwa wanaogopa sana neno usiku ndani ya jiji lao kwa sababu waliamini kwamba asubuhi yake wangekutana na mambo ya kutisha sana isivyokuwa kawaida na ni kweli hicho ndicho ambacho kilikuwa kinatokea kila siku kwenye jiji lao na hata usiku wa siku hiyo hayo mambo ilikuwa ni lazima yaweze kutokea tena.

Tabata.
Majira ya usiku huo, eneo la Tabata Bima ilipaki gari nyeusi sana ndani yake akiwa anatoka mwanaume ambaye pia alikuwa na mavazi meusi na usoni kwake akiwa amejifunika kitambaa cheusi. Buti lake lilikuwa linaonyesha kwamba hakuwa hilo eneo kwa bahati mbaya au kuuza sura bali kuna kazi ambayo ilikuwa imemsogeza ndani ya eneo hilo.

Mwanaume huyo alikuwa ndani ya gari yake akiwa anaziangalia kwa umakini sana nyumba ambazo zilikuwa mbele yake. Alishuka na kuingia kwenye uchochoro mmoja huku kwenye mkono wake akiwa amelishika tambara jeusi ambalo bila shaka kuna kitu alikuwa amekihifadhi hapo kiunoni akiwa na bastola mbili ambazo zilikuwa zinaning’inia bila shaka. Aliingia kwenye kichochoro hicho baada ya kusoma namba ya nyumba ambayo ilikuwa karibu na barabara huku akiamini kwamba namba ambayo alikuwa anaitafuta yeye ingekuwa nyuma ya nyumba hiyo.

Ni kweli kuhusu kile ambacho alikuwa amekiwaza kwani jengo la nyuma ya hiyo nyumba ambayo ilikuwa mbele ndilo lilikuwa na hiyo namba. Aliangalia kwa umakini sana kuweza kuona kama kuna sehemu ya kuingilia lakini hakuiona bali ukuta ndiyo ilikuwa njia pekee ya yeye kufika ndani hivyo alitulia, alikimbia kwa spidi na kugusa ukuta huo ambao aliukanyaga mara mbili tu, mara ya tatu alikuwa ametua ndani.

Eneo hilo lilionekana kuwa kimya sana ukisikika tu mziki kwa mbali ndani ya nyumba hiyo kuonyesha kwamba aliyekuwepo humo hakuwa na shaka sana na maisha yake. Mwanaume alizunguka mpaka mbele ya nyumba hiyo lakini aligundua kwamba haikuwa na mlinzi yeyote yule, alisikitika sana kuona mtu huyo anaishi kizembe sana namna hiyo wakati anajijua kabisa kwamba ni msaliti.

Alichungulia dirishani na kuona ndani mwanaume na mwanamke wakiwa wanafanya mapenzi kwa fujo sana sebuleni huku wakiwa wanahema kama kuku ambao wapo kwenye mashindano ya mbio ndefu. Mwanaume alisogea mpaka mlangoni na kuugusa mlango huo, aligundua kwamba haukufungwa hivyo aliingia kimya kimya humo ndani na kukaa kwenye sofa la upande wa pili huku watu hao wakiwa wanaendelea kufanya mapenzi na kugugumia bila yeyote kuwa na taarifa kwamba humo ndani kulikuwa na ugeni.

Mwanamke ambaye alionekana kunogewa sana na tendo hilo huku akiwa ameyafumba macho yake ndiye ambaye alikuwa mtu wa kwanza kushtuka baada ya kuona mtu humo ndani hivyo akapiga makelele na kumfanya mwanaume ambaye alikuwa juu yake kushtuka sana baada ya kuigeuza shingo yake na kutupia macho upande huo wa pili.

Alinyanyuka kwa ghadhabu sana huku akijifunga taulo lake na kujipapasa kama alikuwa na silaha ila aligundua kwamba alikuwa ameziacha chumbani, hakuwa na shaka sana kwani alikuwa mwanaume wa kazi haswa. Alitazama pembeni yake na kumuona mwanamke wake akiwa amejikunyata kwenye hilo sofa, hakuwa na shaka hata kama mtu huyo angetaka kumshambulia basi angemtumia mwanamke huyo kama ngao yake ya kuzuia risasi.

Mwanaume ambaye alikuwa emefika ndani ya hilo eneo alikuwa ni Tommy ana huyo ambaye alikuwa mbele yake alikuwa ni Luck, ambaye alikuwa ni mlinzi wa baba yake.
“Ni nani wewe ambaye unavamia kwenye nyumba za watu kama upo kwako?”
“Kwanini unakuwa msaliti Luck wakati uliaminiwa sana?”
“Nimekuuliza ni nani wewe?” aliongeza tena kuuliza kwa ghadhabu mno. Mwanaume huyo mbele yake alimwangalia sana kisha akaamua kukitoa hicho kitambaa ambacho kilikuwa usoni kwake. Kitu ambacho Luck alikiona kilimshtua mno maana hakutegemea kabisa kumuona mwanaume huyo hilo eneo.
“Tommy?”
“Nadhani utakuwa umeshangaa sana kuweza kuniona mimi hili eneo ila hata mimi nilishangaa sana nilipo gundua kwamba wewe ndiye msaliti mkubwa ambaye umesababisha mpaka mzee wangu amekuwa kwenye hali kama ile”

“Hahahaha, pesa, pesa Tommy. Usishindane na kitu kinaitwa pesa. Baada ya kulijua jambo hili nadhani ingekuwa vyema kama ungekuwa umeitafuta sehemu ya kuweza kuihifadhi familia yako lakini kujitokeza kama hivi hadharani unafanya kosa kubwa sana kwa sababu sitakuwa na namna zaidi ya kukuua”

“Nimekuuliza swali, kwanini unakuwa msaliti mtu ambaye uliaminiwa tukakufanya kama familia, nikawa mpaka nakuita kaka kwa heshima kubwa ambayo nilikuwa nakupa lakini mwisho wa siku haya ndiyo unayo tulipa kwa wema wote ambao tumekufanyia kwa sababu ya kutambia hizo pesa?”

“Mimi sijawahi kuwa upande wenu hata siku moja na hilo ndilo kosa kubwa sana ambalo mlilifanya kuniamini sana, mimi nimefanya kazi na mr Mafupa kwa muda mrefu sana na ananilipa pesa nyingi sana hivyo mimi huwa naangalia upande wenye pesa nyingi ndipo nakuwa huko. Licha ya nyie kunifanya kama familia ila yule alinilipa pesa nyingi sana ambazo nisingeweza kuzikataa hivyo wakati siku ile naondoka na baba yako nilimpatia kinywaji ambacho kilikuwa na dawa za kumpunguza nguvu na ndiyo maana hakuweza hata kufika mbali wakati anakimbia akaishia kupigwa risasi nyingi sana” alikuwa anaongea kwa majivuno sana na Tommy alikuwa anamsikiliza kwa umakini sana lakini mwanaume huyo baada ya kumaliza alitamka;

“Umeshanijua mimi hivyo lazima nikuue ili niendelee kuwa salama na familia yako iendelee kuniamini na kwa sasa nitafanya mapenzi na wale wadogo zako warembo wote mpuuzi wewe” mwanaume huyo ambaye alikuwa anajulikana kwa jina la Luck aliongea wakati huo akiwa anaipiga meza ya kioo ambayo ilikuwa mbele yake kwa mguu na kwa nguvu kubwa sana kiasi kwamba meza hiyo ilikuwa imeelekezwa alipokuwepo Tommy. Mwanaume alidunda kwnye sofa hilo akadundisha miguu yake ukutani na kutua chini ambapo meza hiyo aligonga ukuta na kupasuka vibaya sana.

Jambo ambalo alilifanya Tommy hapo hata Luck lilionekana kumshangaza sana kwani hakuwahi kujua kwamba mtu huyo anaweza kufanya tukio kama hilo licha ya kufanya kazi kwao kwa muda mrefu. Alitaka kumpima tena mwanaume huyo ambapo alisogea kwa kasi sana akiwa anakuja na mateke yake yote mawili, sofa lilinyanyuliwa kwa nguvu miguu yake iliishia hapo akadunda na kutua chini akiwa amesimama asiamini kwamba huyo ndiye alikuwa Tommy mwenyewe sasa alijua kwamba mbele yake alikuwa amesimama mtu ambaye alionekana kujiweza hivyo hakutakiwa kabisa kumchukulia kiwepesi kwani jambo hilo huenda lingekuwa hatari sana kwa maisha yake.

Luck alijaribu tena bahati yake kwa kujigeuza haraka sana na teke la kifua huku akiwa anauzungusha mkono wake mmoja ambao ungetua mwenye tumbo la Tommy, mguu wake ulipigwa ngumi nzito sana na kumfanya hata mkono wake kushindwa kabisa kumfikia Tommy pale alipokuwepo. Alihisi mguu huo unawaka moto kwani alipigwa ngumu unaweza ukadhani ni nyundo ilikuwa imepitishwa hapo.

Mguu wake aliuchezesha kidogo ili kupooza maumivu, alirusha taulo lake ambalo lilielekea usoni kwa Tommy yeye akibakia uchi kabisa na kusogea kwa kasi ambapo aliona hiyo ilikuwa ni nafasi ya kushambulia kwa umakini ila wakati amekaribia lile eneo ambalo alikuwepo Tommy alihisi kama mwili wake umekufa ganzi kwa muda maana haukuwa ukihisi kitu chochote kile na ndiyo ilikuwa sababu mpaka akawa amesimam ghafla sana.

Alivyokuja kushtuka hakuwa na mkono, yaani mkono wake mmoja wa kushoto ulikuwa chini huku damu ikiwa inamtoka kwa wingi sana. Alipiga makelele mno maana baada ya kushtuka alipata maumivu makali isivyo kawaida ambayo huenda hakutegeme kuyapata kwa wakati huo. Wakati yeye anarusha taulo hilo ni wakati ambao Tommy alilifungua lile tambara jeusi ambalo lilikuwa kwenye mkono wake ndani yake ukiwa umehifadhiwa upanga ambao ulikuwa na makali ya kutosha.

Taulo wakati linafika lilichanwa chanwa na huo upanga hali ambayo ilipelekea upanga huo kupitishwa kwa nguvu sana mpaka kwenye mkono wa Luck ambao aliurusha kwa ajili ya kushambulia hivyo mkono ulikutana na upanga na sio mwili. Kilimtokea kitu cha kutisha sana, akakaa chini akiwa anayasikilizia maumivu hayo makali. Ubaya ni kwamba huyo aliyekuwa amemfanyia ukatili huo alikuwa anamsogelea karibu na hapo alipokuwa hivyo akaamua kujizoa na kuhitataji kumvaa Tommy lakini aliyajutia hayo maamuzi yake ambapo aliona kwamba ni bora kama angebakia amekaa vile vile kwani kabla hajafika upanga huo ulirushwa kwa nguvu sana ambapo ulizama kwenye paja lake na kutokezea nyuma.

Haikuishia hapo tu mwanaume huyo alitoa bastola mbili ambapo bastola moja alimalizia risasi zote kwenye mguu mwingine wa luck hali ambayo ilimfanya kuwa kwenye hali mbaya sna huku akiwa anatoa kilio kama mtoto mdogo. Yule mwanamke ambaye alikuwa anafanya naye mapenzi alikuwa amepiga kelele mpaka sauti yake ikawa imekauka kabisa, alibakia tu akiwa anatetemeka sana kwani alikuwa anaiona hiyo kama siku yake ya mwisho.

Tommy alimpa ishara mwanamke huyo aweze kutoweka hilo eneo, hakukumbuka kwamba alikuwa anatakiwa kuzichukua nguo na muda huo alikuwa uchi, alikimbia sana mwanamke huyo kuelekea sehemu ambayo bila shaka hata yeye hakuweza kuijua ilikuwa ni wapi maana alikuwa amechanganyikiwa huku nyuma akiwaacha wanaume wawili waweze kumalizana kiume kwani walionekana kujuana kiundani sana.

Tommy alimsogelea Luck pale chini akiwa amelowa uso wake kwa machozi lakini hata mwili wake ulikuwa umeloa jasho la kutosha sana.
“Sidhani kama zile pesa ambazo ulikuwa unatambia wakati ule zinaweza kukusaidia tena kwa wakati huu Luck”
Ukurasa wa 46 unafika mwisho.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA AROBAINI NA SABA
“Naomba unisamehe sana Tommy, nimefanya kazi kwenu kwa muda mrefu sana usinifanyie hivi ndugu yangu”
“Kwahiyo muda huu ndo umegunuda kwamba mimi ni ndugu yako baada ya kuona kwamba upo kwenye hali ambayo hauwezi kutoka?”
“Hapana hapana, ilikuwa ni tamaa tu”
“Ulipewa shingapi kukamilisha lile jambo?”
“Milioni miamoja”
“Miliona mia ndiyo imekufanya umuuze baba yangu?”
“Ndiyo, ndiyo”
“Unajua wengi huwa mnakosea wapi Luck?”
“Hapana”
“Pale ambapo unahisi unajua kila kitu ndio muda sahihi wa kukaa na kujifunza kwa sababu unakuwa umewazidi tu baadhi ya watu wenye uelewa mdogo ila kuna mazingira mengine wewe unakuwa ni leaner/lena kabisa ambaye hakuna ulijualo. Hata wewe nina uhakika kwamba ulikuwa unayafanya haya kwa sababu ulijua ndani ya familia hakuna mtu ambaye anaweza kukutafuta kwa kupotea kwako na ukaona kwamba mimi ni kijana ambaye si chochote wala si lolote kwa sababu kama ungenifahamu huenda ungechukua tahadhari ambazo zingenipa mimi ugumu wa kuweza kukupata” mwanaume aliongea huku akimfanya Luck kumweza mate kwa shida sana.

“Jambo ambalo kwa sasa siwezi tena kuliruhusu Luck ni mtu mwingine kufa kwenye familia yangu, hilo kamwe halitatokea tena kuanzia hivi ninavyo ongea na wewe”

“Mimi nipo tayari kufanya lolote unalo lihitaji Tommy ila naomba unipe nafasi ya kuishi, nipe nafasi nyingine ndugu yangu nitabadilika na kuwa mtu wa tofauti kabisa, naahidi nitakuwa mtu wa mfano sana kweye jamii ambapo watu wengi watatamani kuweza kujifunza kutokwa kwangu na sitakuja kujihusisha na haya mambo tena kwenye maisha yangu mpaka nakufa” alikuwa akijitetea huku akiwa anatetemeka kuona kama anaweza kuipata huruma ya mtu huyo na kupewa nafasi nyingine tena ya maisha kwa kusingizia kwamba aliyokuwa ameyafanya zilikuwa ni tamaa tu na kuanzia siku hiyo alikuwa tayari kabisa kubadilika.

“Kwa bahati mbaya sana maisha hayakupi nafasi mbili Luck, maisha yanakupa nafasi moja tu pekee ya kuweza kuiishi kwa usahihi ambapo unatakiwa kujisahihisha kabla ya watu wengine kuja kukusahihisha kwa lazima. Kama ulikuwa na uhitaji wa kubadilika haukutakiwa kusubiri siku ambayo unakuwa hauna namna ya kuyaokoa maisha yako ndipo ufanye hivyo, hilo ni jambo ambalo ulipaswa kulifanyia maamuzi mapema sana lakini wewe umesubiri mpaka leo ndo unaniambia utabadilika? Maisha ukiyachezea mara moja tu huo ndio unakuwa mwisho wako” alimwangalia sana mtu huyo baada ya kumpa somo, kila alipokuwa anamwangalia, hasira zilikuwa zinamkaba sana kwani huyo ndiye ambaye alikuwa amesababisha baba yake kuishia kitandani maana kama angeifanya kazi yake kwa usahihi basi huenda baba yake angepona kabisa kwenye ule mtego.

“Ulikuwa unajua kwamba mdogo wangu angeuawa?”
“Ndiyo Tommy ila nilijua nikiwa sijafanya maamuzi ya kuacha bado kufanya kazi na hao watu ila kwa sasa naapa nimeacha”
“Mimi sijakuuliza kama umeachana nao, kwahiyo hata siku ambayo mdogo wangu anatekwa ulikuwa unajua?” mwanaume huyo alijibu kwa kubabaika sana lakini aliishia kupigwa risasi ya bega ambayo ilimfanya atoe kilio kingine.
“Ndiyo ndiyo, mimi ndiye niliye husika kukamilisha ule mpango kwa sababu nilikuwa najua kila kitu”
“Why Luck?”
“Nisamehe sana Tommy sitarudia tena ndugu yangu”
“Noelia au Sasha unamjua?”
“Ndiyo”
“Anapatikana wapi?”
“Muda mwingine huwa anakuwa pale Sea Cliff Casino”
“Na yule ambaye alikuwa anaigiza kama bibi yake anaitwaje?”
“Norah”
“Ok, Remsi muda huu yuko wapi?”
“Muda mwingi huwa anakuwa kwa baba yake Osterbay ila kwa sasa nadhani yupo kwake Kigamboni ambako ana mjengo wa siri ambao huwa anaenda kwa siri sana pale ambapo anahisi mambo yake hayaendi vizuri”
“Unaweza ukanitajia eneo na namba ya hilo jengo?”
“Ndiyo ndiyo” alijibu kwa pupa sana akiwa anayatoa maelezo hayo kwa umakini sana ambapo baada nya kukamilisha maelezo hayo mwanaume alimmiminia risasi nyingi sana kwenye kichwa chake kisha akakikata kichwa cha mwanaume huyo na kukiweka juu ya sofa. Hakukaa tena hilo eneo bali alitoweka haraka sana kwani alikuwa amempa ahadi Remsi kwamba hataweza kumaliza masaa ishirini na manne akiwa hai na huenda ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya aweze kukimbilia huko Kigamboni ili kuweza kujificha.

Tommy safari yake usiku huo ilienda kuishia Mji mwema akiwa kwenye mwendo mkali sana. Baada ya kufika eneo ambalo alikuwa amejiridhisha vyema, alishuka kwenye gari yake na kuanza kutembea kwa mguu ili kuweza kuwahi sehemu ambayo bila shaka ndiyo ilimfanya awepo saa hizo.

Alitembea haraka haraka sana mpaka karibu na jengo ambalo lilionekana kuwa kubwa sana lakini mbali kidogo na eneo hilo walionekana wanaume wanne ambapo wawili kati yao walikuwa wajapan, wanaume hao ndio wale ambao walikuwa wamepewa kazi na mr Oscar kuhakikisha kwamba wanaua kila mtu ambaye alikuwa akionekana kuwa karibu sana na mr Mafupa na usiku huo walikuwa wamemtembelea mtoto wa mzee huyo ili kuweza kummaliza kabisa ili baba yake abaki anatapa tapa ambapo atakosa msaada kabisa kitu ambacho kitamfanya awe mtumwa wa mr Oscar kwenye maisha yake yote.

Wanaume hao walikuwa nyuma ya muda kidogo kitu ambacho kilifanya Tommy aweze kuwawahi kufika ndani ya eneo hilo huenda kama wangemuwahi basi wangefanikiwa kumuua kijana huyo kabla ya Tommy. Tommy baada ya kuingia ndani ya jengo hilo alirusha kifaa kimoja ambacho kilikuwa kama bomu lakini kazi yake ilikuwa ni kutoa moshi ambao ulikuwa ni mwingi sana kitu ambacho kilipelekea mtu kutokuwa na uwezo wa kuona kile ambacho kipo mbele yake.

Mwanaume alivaa mask usoni kwake ili asiweze kuzurika na moshi huo ambao ulikuwa mbele yake, aliingia kwa sarakasi safi sana ambapo buti lake moja lilitua chini na lingine likafuatiwa. Hakuwa na maelezo mengi kila ambaye alikuwa anakutana naye mbele alikuwa anamchinja vibaya sana huku akiwa anapandisha ghorofani ndani ya jumba hilo la kifahari. Aliua walinzi wengi sana kupitia huo moshi mpaka pale ambapo ulianza kupungua ndipo alipokuwa amefika kwenye ghorofa ya juu kabisa ambapo kwa mbele aliona kuna lango kubwa likiwa limefunguliwa kuonyesha wazi kwamba ndani yake kulikuwa kuna mtu anamsubiri.

Baada ya Tommy kufika hilo eneo alikutana na mwanaume mmoja ambaye alikuwa kifua wazi akiwa amempa mgongo mithili ya mtu ambaye alikuwa amezama kwenye ibada nzito sana.
“Sikujua kwamba inaweza kuwa rahisi sana kwa mtu wa kawaida kama wewe kuweza kujua kwamba mimi nipo ndani ya hili eneo lakini inaonekana imekuwa rahisi sana kwako hata kuwaua walinzi ambao wapo nje hapo” ni sauti nzito ya mwanaume huyo ambaye alikuwa bado amekaa hapo chini akiwa amempa mgongo Tommy.

Huyo mwanaume ambaye alikuwa amekaa hapo chini ndiye ambaye alikuwa anaitwa R mwenyewe, huyo ndiye ambaye alikuwa amefanya ukatili wote kwenye familia ya Tommy hususani ule wa kuuawa kwa mdogo wake na kumteka dada yake ambapo aliishia kumbaka kwa namna ambayo ilimfaa yeye. Alinyanyuka taratibu baada ya kuona mtu ambaye alikuwa nyuma yake hakuwa akiongea jambo lolote lile, na ndipo alipo igeuza sura yake. Hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwenye maisha yao wanaume hao kuweza kuonana uso kwa uso na ndiyo ambayo ilipaswa kuwa siku ya mwisho ya mmoja kati yao.

Mwanaume huyo mwili wake ulikuwa umekatika sana kwani alikuwa kifua wazi lakini chini alikuwa peku akiwa amevaa traki nyeupe pee huku pembeni yake kukiwa na upanga ambao ulikuwa unang’aa sana.
“Una miaka mingapi?” hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza la Tommy kwenda kwa mtu huyo.
“Miaka haina umuhimu wowote ule hapa ndugu yangu zaidi tu ya kuyaokoa maisha yako. Nimesikia umeua vijana wengi sana tena kikatili, nasikia unalia lia kwa sababu ya mimi kufanya mapenzi na yule Malaya dada y……” hakumalizia sentensi yake kwani upanga ulirushwa kwa kasi ya ajabu na kumbaraza kwenye shavu lake baada ya kufanikiwa kuukwepa. Alikuwa anavuka mipaka ya kuongea na wanaume wenzake kauli kama hizo, upanga huko ulienda kujichomeka ukutani.

“Hahahaa hahahaha” alicheka kwa sauti kali sana lakini iliyo jaa kejeli, kisha alijivuta na kujizoa mpaka lile eneo ambalo alikuwepo Tommy, mwanaume huyo alizirusha ngumi zake kwa pamoja ambazo zilitua kwenye kifua cha Tommy na kumzoa mpaka nje ambapo alilazimika kuingia upya tena ndani ya chumba hicho.

R hakuwa mnyonge kabisa kwenye suala zima la urushaji wa ngumu hivyo alikuwa anashambulia kwa kasi sana hali ambayo ilionekana kuanza kumpa wakati mgumu Tommy baada ya kupokea teke la shingo ambalo lilimpeleka chini ila kwa kutumia mkono wake mmoja alijinyoosha vizuri na kuzikunja ngumu zake kwa usahihi ambazo ziliitikia vizuri kabisa. R alizunguka chini kwa mitama mikali lakini alimkosa Tommy hivyo akahitaji kujizungusha ili asimame lakini alikutana na ngumi moja nzito mno ya mdomo ambayo iliufanya mdomo huo upasuke na kuanza kutoa damu kwa wingi.

Alisimama huku akiwa anapiga makelele kwa hasira, alitishia kama anapiga kisha akarudi nyuma na kwenda kwa nguvu akihisi kwamba amempoteza mpinzani wake kumbe yeye ndiye ambaye alikuwa amepotezwa, alidakwa mkono wake ambao ulipokea kiganja kizito akatupwa mbali lakini kwa bahati nzuri wakati anarushwa mbali alikuwa amefanikiwa kuzichomoa bastola kwenye mwili wa Tommy. Kabla hajatua chini aliruhusu bastola hizo kuweza kutoa risasi lakini risasi ambayo ilitoka ilikuwa ni moja tu pekee ambayo ilizama kwenye kifua cha Tommy.

Tommy alipokea maumivu makali sana ya kifuani hali ambayo ilimfanya apige goti lake moja chini na mwanaume huyo akaishia kucheka kwa sauti na dharau sana huku yeye mwenyewe akiwa kwenye hali ambayo haikuwa nzuri. Alizitupa bastola hizo ambazo alihisi kwamba huenda mtu huyo alikuwa amezitumia na risasi ambayo ilikuwa imebakia ilikuwa ni moja tu kisha akauchomoa upanga wake pale chini ambapo alikuwa ameuhifadhi vizuri sana.

Akiwa na upanga wake mkononi alijirusha na kuushusha kwenye bega la Tommy, Tommy ni kama alichelewa kufanya maamuzi kwani upanga ulimbaraza kidogo na kumchana, akiwa bado kwenye mshangao mwanaume huyo aliuzamisha upanga huo kidogo kwenye eneo la kifua cha mwanaume huyo. Ni kama Tommy aliweza kuzinduka kutoka kwenye mshangao baada ya kurusha ngumi kali sana saba ambazo zilitua vyema kwenye mbavu za R.

Ukurasa wa 47 unafika tamati.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA AROBAINI NA NANE
Mwanaume huyo alipiga kelele sana kwa maumivu makali ambayo alikuwa anayapitia hapo na kwenda kujibamiza ukutani jirani na sehemu ambayo upanga wa Tommy ulikuwa umejichomeka. R kutokana na mauamivu makali ambayo aliyapata yalimfanya ayafumbe kabisa macho yake lakini wakati anayafumbua alipishana na buti kali sana ambalo lilifanya ukuta ubonyee hilo eneo lakini upanga ambao ulikuwa ukutani ulichomolewa kwa nguvu na kupitishwa usoni kwake ambapo alipiga yowe sana kwa maumivu ambayo alikuwa anaendelea kuyasikilizia hapo.

Alirudi nyuma akiwa ameushikilia uso wake ila hakupewa nafasi ya kuyafaidi maisha kwani alipigwa mtama mzito ambao ulifuatiwa na goti kali akawa amendoka vibaya sana chini. Akiwa hapo chini upanga ulipitishwa kwenye mguu wake mpaka ulipo katika. Alipiga sana kelele R mithili ya mwanamke ambaye alikuwa kujifungua leba lakini hata hivyo hakuachwa na mguu mwingine ulifanywa hivyo hivyo, hata mikono yake pia ilifanywa kama hivyo hivyo kwahiyo akawa amebakia na kiwili wili tu pekee.

“Wewe mpuuzi ndiye sababu kubwa ya mdogo wangu kufa na wewe mjinga ndiye sababu kubwa ya dada yangu kupotea. Wewe hapo ndiye umefanya mama yangu apate presha kubwa sana baada ya kushindwa kuzihimili taarifa ambazo alizipokea kwenye hayo matukio lakini wewe na baba yako pia ndiyo sababu kubwa sana mpaka leo hii baba yangu yupo kitandani kuipambania afya yake halafu unamwita dada yangu Malaya?” Tommy aliongea kwa sauti kali sana akiwa anamsogelea R pale chini akiwa hana mikono wala miguu anagugumia tu.

“Hahaha hahahah hahahha, hii itakuwa zawadi nzuri sana kumtumia baba yako. Kila aliye husika kwenye hili jambo atakufa kikatili sana na wewe hapo ni binadamu ambaye utakufa kikatili zaidi ya hawa wote” mwanaume alitamka wakati huo akiwa anaikata kwa upanga nguo ya mwanaume huyo ambayo ilikuwa mwilini mwake na kumuacha akiwa uchi kabisa.

“Kwahiyo wewe ndiye shababi ambaye uliutumia uume wako kuweza kumuingiza dada yangu kwenye utumwa wa kufanya akusikilize kila unacho kisema sio, uume wako si ndio unakupa sana jeuri sio?” mwanaume aliongea huku akizamisha upanga wa mbavu kwa R mwanaume huyo akiwa anajigeuza baada ya kupata maumivu makali, upanga ulipita katikati ya uume wake na kuisambaratisha vibaya sana hiyo sehemu bila huruma yoyote ile. R alitoa sauti kali huku akiwa anainuka kuiangalia sehemu hiyo ya thamani zaidi kwenye maisha ya mwanaume yeyote yule huku akiwa kama haamini kwamba hilo jambo lilikuwa likitokea kwenye maisha yake.

Huenda alitamani kuishika sehemu hiyo lakini hakuwa na uwezo maana mikono hakuwa nayo, kitu pekee ambacho alikuwa anaweza kukufanya wakati huo ni kulia tu basi.
“Ukifika huko hakikisha unapiga magoti mbele ya mdogo wangu na unaomba msamaha aweze kukusamehe kwa unyama ambao ulimtendea na usipo fanya hivyo mimi binafasi nakuahidi kwamba kwenye maisha mengine yajayo nitakutafuta na hili jambo tutalianza upya kabisa” mwanaume alitamka akiwa anazunguka zunguka humo ndani kuangalia mazingira yake huku mwenzake akiwa anaijutia dunia na wanadamu wake ambao ndio wanaishi ndani ya dunia hiyo.

“Tommy alimsogelea R pale chini na kuanza kuchimba chimba na upanga taratibu kwenye eneo lake la shingo mpaka alipo hakikisha pamechimbika huku R akiwa anabiringika lakini hakuwa na kwakwenda ni mikoromo tu ndiyo ilikuwa inasikika kwa usahihi. Mwanaume alihakikisha upanga huo umeingia vyema mtu huyo akiwa hai kisha akawa anauzungusha tatatibu kuizunguka shingo hiyo mpaka pale alipo kitenganisha kichwa na mwili na hata mwili wa R ulionekana kutulia kabisa pale kumaanisha kwamba alikuwa ameumaliza mwendo” mwanaume alikuwa kwenye hali mbaya sana kwa sababu alipigwa risasi sehemu mbaya mno.

Alianza kutoka humo ndani taratibu huku akionekana wazi kuchechemea mkononi akiwa na upanga wenye damu ambayo ilionekana kuwa mbichi tu bado. Ila kwa bahati mbaya sana wakati anafika pale kwenye uwanja mkubwa ambao ungempeleka mpaka getini alikutana na wale wanaume wanne wa kazi wakiwa ndio wanaingia ndani ya lile eneo. Kazi mpya ilizaliwa kwenye mkono wake huku akiwa kwenye hali mbaya sana.

Kwa mwonekano tu wanaume ambao walikuwa mbele yake alijua kabisa kwamba hakukuwa na mazungumzo wala maongezi ya kusema kwamba wangeweza kukubaliana kwa jambo lolote lile hivyo kitu pekee ambacho alipaswa kukifanya hapo ni kuweza kuyapigania na kuyatetea maisha yake Tommy. Alikaa kwanza kwenye ngazi za kushukia chini kabisa ya uwanja mpaka ambapo alijua kwamba yanaenda kutokea mambo mazito sana lakini hali yake ilikuwa inazidi kuwa mbaya kwani alikuwa anaishiwa nguvu kwa sababu ya ile risasi ambayo alikuwa amepigwa eneo la kifuani.

Wanaume hao wanne hawakuwa na papara kwa sababu ilionekana kwamba mtu ambaye walikutana naye ndani ya hilo eneo alitoka kuifanya kazi ambayo wao walikuwa wameijia hapo hivyo hawakutakiwa kumbakisha hata waliye mkuta hapo maana malipo ya kazi yao yalikuwa njiani hivyo walitakiwa kuhakikisha kwamba na yeye pia wanaimaliza habari yake hapo hapo muda huo.

Walianza kumsogelea taratibu Tommy pale kwenye ngazi alipokuwepo huku akiwa anahema taratibu akiwa ameyafumba macho yake. Mjapan mmoja alikunjuka na teke lake zito kwa sarakasi ya mbele kuhitaji kumshtua mwanaume huyo ambaye alionekana kuzubaa sana hapo chini alipokuwa amekaa. Ni ghafla sana Tommy aliyafumbua macho yake na kujivuta nyuma kwa nguvu, teke hilo lilitua chini ya sakafu hiyo na kuifanya uchubuke hivyo kama lingefika ni kwenye mwili wake huenda ingekuwa ni hatari nyingine ambayo ingeweza kumuweka mashakani kama sio kuiweka afya yake mashakani.

Tommy alimnyooshea mwanaume huyo upanga na kumpa alama ya kukataa kwa kichwa chake, lilikuwa ni kama onyo kumwambia kwamba hakutakiwa kabisa kumsogelea kwani ingekuwa ni hatari kwa maisha yake lakini mwanaume huyo hakuwa na muda wa kumsubiri. Alichomoa nyota mbili kwenye mfuko wake na kuzishika vizuri sana kwenye mkono wake na kumfuata Tommy kwa spidi alipokuwa amesimama.

Nyota hizo zilikuwa zinazungushwa kwa nguvu sana kiasi kamba kama Tommy angerusha vibaya ngumu zake basi angekutanishwa nazo na huenda zingemchana chana vibaya sana, licha ya kutakiwa kushambulia pia alitakiwa kuwa makini sana kwenye suala zima la kuweza kujilinda na kuhakikisha hakutani nazo kwani ingekula kwake. Aligusa kwenye kingo ya ngazi ya mwisho ambayo ilikuwa karibu na mlango na kurukia nyuma ya mwanaume yule ambaye ngumi zake zilienda kukita kwenye bawaba za mlango na kugundua kwamba mwanaume ambaye alikuwa amemfikia hapo alikuwa amerukia kwa nyuma.

Aligeuka haraka sana kuweza kushambulia ila alisahau kitu kimoja, alisahau kwamba mwenzake kwenye mkono wake alikuwa na upanga, hivyo wakati anageuka alikutanishwa na upanga kwenye tumbo lake hali ambayo ilimfanya hata yeye au wenzake wasiamini kwamba kitu hicho kilikuwa kinatokea ndani ya wakati huo. Tommy aliuchomoa upanga huo na kumdaka mwanaume huyo ambapo alimvutia upande aliokuwepo, alimpiga kichwa kikali sana mwanaume huyo alidondokea nyuma ambapo kisogo chake kilijipigiza vibaya kwenye ngazi akawa kimya, alikuwa ameumaliza mwendo mjapani huyo.

Mjapan mwenzake ni kama alikuwa ameduwaa kuweza kuona ndugu yake akiwa kwenye hali kama hiyo ambayo alihisi labda ni ndoto kwa sababu ni watu ambao walikuwa wametoka mbali sana pamoja na hakuwa amewaza kabisa kuweza kumpoteza mwenzake kwa namna kama hiyo. Alikimbia akiwa anapiga makelele akiwa amelikunja goti lake ambalo lilimkosa Tommy na kutua kwenye sakafu mpaka ardhi ikatikisika. Tommy alifanikiwa kulikwepa na kutua pembeni kidogo kisha mwanaume huyo akausogelea mwili wa mwenzake huku akiwa anatoa chozi.

Tommy akiwa chini hapo anavuta pumzi alihisi kama kuna mjongeo wa upepo unakuja upande wake, baada ya kuinama alipishana na mguu ambao ulikuwa umevalishwa kiatu ambacho kilionekana kuwa na chuma mbele yake. Kukwepa kwake mguu huo alikutanishwa na ngumi tatu ambazo zilimrudisha mita kadhaa, sasa hapo aligundua kwamba wanaume hao walikuwa wameamua kumchangia kwa pamoja. Na wakati huo pia hata yule mjapan alinyanyuka pale chini akiwa na hasira mpaka macho yake yakawa kama yanawaka moto hivi.

Tommy alijua wazi anatakiwa kuwa makini sana kwa kuwa na mahesabu makali ukizingatia afya yake kwa wakati huo ilikuwa inazidi kuwa mbovu kila sekunde moja ilivyokuwa inaenda. Sasa alizungukwa na wanaume watatu ambao kila mmoja alionekana kuwa na hasira naye sana, kazi ilikuwa kwake kuweza kujilinda dhidi yao. Akiwa anawahesabia mjapan hakuwa na muda wa kusubiri, alitishia kukimbia huku akiwa anakuja kwa mitama ya mizungusho chini lakini wakati amemkaribia Tommy alijigeuza kwa sarakasi ya nyuma ambapo mguu wake ulikuwa umelenga uso wa Tommy. Mwanaume alifanikiwa kuyapangua mateke hayo na kumshona Mjapan ngumi kali sana ya mguu ambao ulisikika kama unateguka na Mjapan akapiga kelele za maumivu lakini wakati huo huo yeye mwenyewe alichotwa mtama na wale wanaume wengine wawili na kupigwa mabuti ya tumboni ambapo alirushwa mbali sana.

Wakati anapigwa mabuti hayo aliuachia upanga wake ambao ulizama kifuani kwa mwanaume mmoja hivyo hakutaka kuumia kizembe ndiyo maana alihakikisha anashuka na mmoja kwanza ili kuwapunguza nguvu wakati ambao hata yeye nguvu zilikuwa zipo ukingoni na muda wowote kuanzia wakati huo alijua kabisa kwamba anaweza asiwe na uwezo hata wa kujilinda tena wala kuweza kuzuia mashambulizi. Mwanaume yule ambaye aliupokea upanga huo kwenye mwili wake, alikuwa amepigwa sehemu mbaya sana ambayo ilikuwa ni sentimita chache sana kutoka kwenye moyo.

Alitaka kusimama akiwa anatoa damu mdomoni lakini uhalisia ulimsaliti, mwanaume huyo alijikuta anarudi tena chini, asingeweza kuhimili hali hiyo. Mjapan naye alikuwa chini akiwa ameushika mguu wake anajaribu kuunyoosha kwa maumivu makali sana, hivyo kati ya wale wanne mwanaume ambaye alikuwa amebakia akiwa sawa kabisa alikuwa ni mmoja, wawili walikuwa wamepoteza maisha na mjapan alikuwa anaupambania kwanza mguu wake pale chini ili aweze kusimama.

Tommy alinyanyuka huku akiwa anajifuta damu yake ambayo ilikuwa inatoka mdomoni, macho yake yalikuwa kama yanaanza kupoteza nuru na eneo hilo hakuona msaada wowote ule hivyo alitakiwa kujipigania maisha yake yeye mwenyewe kwanza haraka sana kabla hajapoteza kabisa uwezo wa kuona.
Mwanaume ambaye alikuwa amebakia pekeyake ni kama alikuwa anasita sana kwenda kwa kile ambacho alifanikiwa kukishuhudia kwa wenzake lakini alishangaa mwanaume ambaye yeye alikuwa anaogopa kuweza kumfuata akiwa anakuja upande aliopo, akajikuta hana namna zaidi ya kuamua kupambana naye tu. Tommy hakuwa na uwezo wa kwenda spidi tena kwa hali ambayo alikuwa nayo hivyo alikuwa anamuendea kwa mahesabu tu.

Mwanaume huyo alichanganya miguu yake na kurusha ngumi kadhaa kisha akarudi nyuma haraka sana kwa tahadhari lakini aliona kama mteja wake alilegea maana hakuonyesha kurudisha mashambulizi asijue kama aliwekewa mtego. Alijikakamua kwa kuona ushindi ulikuwa karibu yake na kumsogelea Tommy pale alipo kwa sarakasi ambayo iligeuka kuwa majuto kwake kwani Tommy aliikwepa sarakasi ile hivyo ikawa imemkosa lakini wakati mwanaume huyo anatua chini Tommy alijisogeza kwa nguvu na kumpatia ngumi ya mbavu kisha akamdaka shingo yake na kuanza kuinyonga kwa nguvu.

Ukurasa wa 48 sina la nyongeza.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA AROBAINI NA TISA
Licha ya mwanaume huyo kufurukuta na kumpiga Tommy ngumi nyingi sana za tumboni hakuweza kuachiwa mpaka shingo hiyo ilipofanikiwa kuvunjwa. Sasa walikuwa wamebakia wanaume wawili tu humo ndani, Tommy pamoja na mjapan ambaye licha ya kujitahidi sana kuweza kuunyoosha mguu wake bado uligoma kabisa kunyooka hivyo akasimama huku akiwa anachechemea kwa maumivu. Tommy alijaribu sana kushindana na hali yake ambayo alikuwa nayo ya kukosa nguvu lakini ilionekana kumzidia kabisa.

Mjapan hiyo kwake ilikuwa ni nafasi ya dhahabu ambayo ilikuwa inampa matokeo ya ushindi hivyo alijikaza na kuanza kulisogelea hilo eneo kwa kasi huku mguu mmoja akiwa anauvuta. Tommy alikuwa kama anaona watu wawili wawili mbele yake hivyo alicho kifanya, alikitoa chuma chake mfukoni na kukirusha kwa nguvu pale alipohisi kwamba alikuwepo mjapan, kilitua kwenye mdomo wa mwanaume huyo ambaye alikuwa anakuja kwa kasi sana na kuufanya mdomo huo uchanike vibaya sana.

Alilia kwa maumivu mjapan asiamini kwamba mdomo wake umechanwa chanwa mithili ya tambi, lakini aliamua kunyanyuka kwa hasira baada ya kumuona mtu wake akiwa ametepeta sana na kupiga goti chini, Tommy hakuwa anaona kabisa kilichokuwa kinaendelea ndiyo maana alishindwa kabisa hata kuweza kusimama tena.

Mjapan akiwa kwenye mauamivu ambayo hayakuwa yakielezeka, aliamua kumaliza kazi kwa kukimbia kwa kuchechemea kwa nguvu na kujitegua kwa kutumia mguu wake mbovu ambapo alizunguka hewani na kujiviringisha ambapo mguu wake wenye ujazo wa kutosha ulikuwa unatua kwenye shingo ya Tommy ambaye kwa wakati huo hakuwa hata na uwezo wa kujitetea kwa lolote lile, na teke hilo lilikuwa linamaliza kazi.

Mwanaume huyo akiwa amebakisha sentimita chache kufikisha teke hilo hilo eneo, alipigwa risasi ya kichwa ambayo ilimfanya adondoke vibaya sana chini, alikuwa umbali wa juu kiasi hivyo kudondoka chini alidondokea vibaya sana shingo ambayo ilivunjika habari yake ikaishia hapo hapo na ni wakati huo huo ambao Tommy alikuwa analala kabisa chini na kuzimia.

Muda mchache tu alionekana mtu akiwa kwenye mavazi yake meusi, kama kawaida alikuwa ni yule mwanamke wa siku zote na mavazi yake Harper Campbell. Alikimbilia lile eneo ambalo Tommy alikuwepo akiwa na wasiwasi sana, alimgusa puani na shingoni mwanaume huyo na kugundua kwamba alikuwa ni mzima ila alipoteza fahamu na huenda alikuwa anahitaji msaada wa haraka ili kuweza kuyaokoa maisha yake. Alibeba kila kinacho mhusu mwanaume huyo ili asije kuacha ushahidi kisha akambeba na kutoweka naye hilo eneo haraka sana isivyokuwa kawaida huku wanaume wale wa mr Oscar wote wakiwa wameteketea.


Ni usiku ule ule ambao habari zilianza kusambaa kwa kasi sana kwenye mitandao ya kijamii kuhusu ile milio ya risasi ambayo ilisikika huko mji mwema Kigamboni. Ni kitu ambacho kiliwafanya polisi wafike ndani ya eneo hilo haraka sana ili kuweza kutambua kwamba shida hasa ilikuwa ni nini. Hivyo muda mchache baada ya Harper kutoweka ndani ya eneo lile, polisi walianza kuingia kwa kasi sana kwani waliambiwa kwamba wanahisi eneo hilo kuna mauaji yametokea ni baada ya wenyeji kusikia milio ya risasi na kuondoka kwa magari eneo hilo usiku huo huo.

Hizo habari zilisambaa kiasi kwamba zilianza kuleta taharuki kwa wapiga kura na kuhisi kwamba ni wagombea walikuwa wakipigana vita hususani kwenye suala zima la maslahi binafsi ambayo hayakuwa na tija yoyote ile kwa taifa. Ni wakati ambao wananchi walianza kuiogopa hata nchi yao hususani wale wakazi wa Dar es salaam kwani waliamini kwamba hayo mambo kamwe yasingeweza kuisha kuendelea kutokea na huenda huo ulikuwa ni mwanzo tu yangetokea mengine makubwa zaidi ya hayo.

“Hivi unaamini kwamba haya mauaji yamefanywa na mtanzania?” aliuliza polisi mmoja ambaye yeye na wenzake wachache ndio watu ambao walifika mapema zaidi kwenye hilo eneo.
“Sitaki kuamini lakini kuna muda naamini, hii nchi nasikia ina watu wa kutisha sana ndugu yangu na ujio wa hizi pesa umebadilisha kila kitu ambapo mwenye kisu kikali ndiye anayekula nyama”
“Sasa inawezekana vipi mtu kumuua mwenzake kikatili sana namna hii? Halafu si Mjapan asili yake huyu?” alikuwa anaangalia huku akiwa anaugeuza mdomo wa mwanaume huyo kwa namna ulivyokuwa umechanwa vibaya sana.

“Mara nyingi ukatili wa namna hii huwa unasababishwa sana na matukio mabaya ya mwanzo, kunakuwa kuna sababu kubwa sana ambayo inamfanya mtu atoke kwenye ubinadamu na kuamua kuwa mnyama kama unavyoweza kuona hapo ila nimeogopa sana” polisi hao walikuwa wanaonyesha masikitiko yao makubwa sana kwa mambo ambayo walikuwa wanayaona yanatokea kwenye nchi yao huku ikionekana kwamba hakuna jambo lolote la maana ambalo wao walikuwa wanalifanya.

Wakati wakiwa wanaendelea kuikagua miili hiyo ndipo mwenzao mmoja alipowapa ishara ya kusogea ndani, hali ilikuwa inatisha zaidi ya nje kwani njiani tu kuelekea sehemu mbayo walitakiwa kufika watu walikuwa wamechinjwa vibaya sana na kufanya damu itapakae kila mahali. Baada ya kuingia ndani ya chumba ambacho kilifanya polisi mwenzao awaite kila mtu aliyafumba macho yake. Kilichokuwa kimefanyika hata kama mtu alikukosea namna gani haikupaswa kumtendea namna ile kwa sababu ilikuwa ni kinyume hata na haki za binadamu.

Kuna askari mmoja uvumilivu ulimshinda alijikuta mpaka anashusha chozi, mwili ulikuwa umeharibiwa sana kiasi kwamba ungeweza kuhisi kwamba aliyekuwa amefanyiwa hilo tukio alikutana na shetani mwenyewe lakini hata shetani asingekuwa na ukatili wa namna hiyo hivyo kwake hakuamini kabisa kwamba hilo tukio lilifanywa na mwanadamu ambaye alikuwa yupo hai kabisa.

Wakati hayo mambo yanatokea mheshimiwa raisi alikuwa na kikao kizito sana na baadhi ya watu wakubwa serikalini akiwepo mkuu wa majeshi na DCI. Mheshimiwa alikuwa ametoka kuongea na mkuu wa majeshi kwa muda mrefu sana ambapo alikuwa amesisitiza sana kwamba mtu huyo asije hata siku moja akawaza kufanya kazi kinyume na yeye anavyo mwagiza kwa sababu ni yeye pia ambaye angehakikisha kwamba anaendelea kubakia kenye nafasi hiyo hata pale ambapo angetoka madarakani.

Walifikia makubaliano hayo japo mkuu wa majeshi hakuwahi kabisa kukubaliana na matakwa ya kiongozi wake kutoka moyoni hususani ukizingatia kwamba alikuwa amesababisha kamanda Zola kuweza kufa na familia yake ikiwa haijulikani ilipo mpaka wakati huo japo ilidaiwa kuwa kwenye mkono wa mr Oscar ambapo jambo hilo alikuwa analivutia kasi tu ila aliamini kwamba ipo siku atalifanyia kazi na wakati wowote jambo hilo lingeweza kukaa mahali ambapo aliamini kwamba lilistahili kuwa.

Baada ya mheshimiwa kukamilisha maongezi na kiongozi huyo mkuu wa jeshi kwa wakati huo alikuwa amekaa ndani ya chumba cha mkutano na DCI.
“Leo asubuhi nimeiona taarifa yako kwenye vyombo vya habari, unaweza ukaniambia labda kipi kimekufanya uende kinyume na amri yangu?”
“Kwanza nisamehe sana kiongozi wangu kwa sababu nimefanya vile kwa kuwa tu sikuwa na namna yoyote ile ila nisingeweza kwenda kinyume kabisa na kile ambacho wewe ulikuwa umenielekeza”?
“Umeshaenda kinyume tayari unanaiambiaje kwamba haukuwa tayari kwenda kinyume na mimi tena?”
“Ni mkurugenzi wa usalama wa taita mheshimiwa”
“Unajua kabisa huwa sipendi kuuliza uliza kila wakati sasa unanipaje habari nusu nusu?”
“Alikuwa amekuja kwangu na kuhitaji mimi nilisafishe jina la mzee yule Apson Limo vinginevyo angeweza kuanza kuanika mabaya ya viongozi kwenye nchi hii. Kwa hali ambayo ameniambia ni kwamba ana ushahidi wa maovu ya viongozi wengi hivyo kama ningeenda naye kinyume basi angetumaliza wote na wananchi wakajua yale ambayo tunayafanya. Hiyo ndiyo sababu ambayo imenifanya nikafikia uamuzi kama ule”

“Mhhhhhh alikuwa na taarifa za viongozi au za kwako? Mbona kama unataka jambo binafsi kulifanya lionekane la wote bwana mkubwa? Kumbuka ulishaapa kwamba mimi utanitii kwa namna yoyote ile na kwa mazingira yoyote yale sasa inakuwaje tena unanikataa na kumtii mtu ambaye naye ananitii mimi japo naye kaanza kuwa kiburi saivi?”
“Naomba nisamehe sana mheshimiwa”
“Huwa nasamehe mtu ambaye analifanya kosa bila kujua ila mtu ambaye analijua kosa na nishamuonya juu ya kosa hilo basi huwa sina nafasi yake tena kwenye maisha yangu hivyo utanisamehe sana” raisi alimaliza maongezi yake huku wakiingia wanaume wa kazi humo ndani na kumshika DCI ambapo mheshimiwa huyo alimpiga risasi nyingi sana na kuwaambia watu hao wakamtupe baharini.

“Lingson Mfwomi siku zako zinahesabika, mawazo yangu kwamba unanizunguka yalikuwa sahihi sana na kwa sasa siwezi kukupa nafasi nyingine tena ya kuishi mjinga mkubwa wewe” alitamka akiwa anahitaji kwenda kulala lakini mlinzi wake alikuja akiwa anahema sana.
“Mkuu kuna tatizo kigamboni?”
“Kuna nini?”
“Kuna mauaji ya kikatili sana yameweza kufanyika usiku huu?”
“Sasa yananihusu nini mimi?”
“Huyu ambaye ameuawa inasemekana kwamba ni mtoto wa damu kabisa wa mr Mafupa”
“Whaaat?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Ebu piga simu kwa askari waliopo huko waambie waniunganishe live moja kwa moja nahitaji kuona kila ambacho kimetokea huko” mheshimiwa aliunganishwa moja kwa moja ili kuweza kuona kila ambalo lilikuwa limetokea huko Kigamboni. Aliangalia kwa umakini sana juu ya jambo hilo ambalo lilikuwa limefanyika mpaka alipo maliza akaamua kuizima hiyo simu yake.
“Ni nani ambaye ameweza kulifanya hilo tukio?”
“Bado hajajulikana mkuu kwani wamekuta mhusika amesha ondoka eneo la tukio”
“Hilo ni jambo ambalo haliwezekani, kuna kamera za siri za watu wa usalama kule hivyo hakikisha unampigia simu mkurugenzi wa usalama wa taifa mwambie nahitaji kukutana naye sasa hivi”
“Sawa mkuu” mwanaume huyo alijibu huku akifanya kazi hiyo ambayo alipewa hapo na kiongozi wake lakini simu hiyo iliita mara moja tu kisha ikaacha kabisa kupatikana.

Ukurasa wa 49 naweka kalamu chini.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA HAMSINI
“Mkuu nadhani amezima simu”
“Huyu mpuuzi ananizimia simu mimi?”
“Ebu andaa msafara nahitaji nikaonane naye kwake muda huu” aliongea kwa ukali sana mheshimiwa kichwa kikiwa kimewaka moto haswa. Mambo yalikuwa ni mengi sana ambayo yalikuwa yanaendelea kwanza alishangazwa sana baada ya kujua kwamba eti yule kijana alikuwa ni mtoto wa mr Mafupa, aliona kama dunia haikuwa na usawa kwenye uchakataji wa taarifa na kwake mambo hayo yalikuwa kama ndoto hivi.
“Sawa mkuu”
“Nipatie na bastola zangu mbili kwa sababu sidhani kama huyu mpuuzi leo nitaweza kumuacha hai”
“Sawa kiongozi” hakukuwa na jambo la kuzubaa maana amri ya mheshimiwa ilikuwa imetoka na kilichokuwa kinafuatia hapo ulikuwa ni utekelezaji tu.


Hizo taarifa mbali na kwamba zilikuwa zimelishtua taifa lote la Tanzania hususani kwa wale watu ambao muda mwingi ungewakuta mtandanoni na walikuwa wakisambaziana taarifa hiyo kama masihara, lakini pia taarifa hizo zilimfikia mr Oscar nyumbani kwake akiwa amelala. Ni usiku sana ambapo alikuja kugongewa na mlinzi wake.

Alishangaa sana kuamshwa usiku wa manane sana kiasi hicho maana haikuwa kawaida kabisa kwa upande wake kuamshwa amshwa akiwa amelala hivyo aliamka akiwa na ghadhabu sana.
“Kuna shida gani mpaka mnanisumbua na usiku wote huu? Hamjui kama nipo na ua langu kitandani naufaidi usingizi huu mpuuzi wewe?” hakujibiwa chochote na mlinzi wake ambaye alikuwa amemuamsha muda huo zaidi ya kumkabidhi tu baadhi ya picha ambazo zilikuwa kwenye mkono wa mwanaume huyo.

Hizo ni picha ambazo zilikuwa zimepigwa eneo la tukio ambalo mauaji yalikuwa yamefanyika. Zilikuwa ni picha za wale wanaume wanne ambao yeye ndiye aliwapa kazi ya kuweza kuua kila mtu ambaye angeonekana kuwa karibu na mr Mafupa ili kuweza kumfanya kukosa nguvu kabisa na kuwa tegemezi.
“Nini kimetokea?”
“Moja kati ya mapolisi wetu ambao tunafanya nao kazi ametutumia hizo picha na kusema kwamba wamekuta watu hao wakiwa wameuliwa kikatili sana lakini pia mtu ambaye walienda kumuua hapo alikuwa amekufa tayari”
“Ohhhhhh shiiiiit! Ina maana hawa vijana wameuliwa kabla hawajamfikia mhusika sio?”
“Ndiyo mheshimiwa maana inaonekana kwamba ndiyo walikuwa wanafika ila walikuwa wamechelewa hivyo kuna muuaji ambaye alitangulia kabla yao wakati wa kutoka ndipo akakutana nao wakiwa wanaingia hivyo nao akawaua wote na kuondoka”
“Wamefanikiwa kujua kwamba muuaji alikuwa ni nani?”
“Hapana mheshimiwa, kuhusu hilo hakuna mtu hata mmoja ambaye anajua kabisa”
“Huyu mpuuzi ni nani ambaye kila siku anakuja na mambo mapyaaaaaaaa?” aliongea kwa jazba sana kiasi kwamba hata mlinzi wake alilazimika kurudi nyuma, kama angeendelea kukaa karibu na mtu huyo basi angeishia kupokea vibao vikali sana.

“Namhitaji huyu mtoto, nendeni mkaniletee huyu mtoto kwa gharama yoyote ile na hata kama itashindikana kumpata basi hakikisheni maniletea baba yake mzazi hapa kwa sababu najua kama mkimpata baba yake basi atakuja tu hawezi kuvumilia hilo jambo litokee kwenye maisha yake. Namtaka akiwa hai, nitamuua kwa mkono wangu mpuuzi huyu. Anajikuta nani kwenye nchi ambayo hajui hata ilikotoka?” aliongea kwa kufoka sana mheshimiwa huku akiwaruhusu watu hao wakamtafute kwa gharama yoyote ile na mahali popote pale ambapo angekuwepo.


Mr Mafupa taarifa hiyo ilimkutia juu ya kiuno cha Malaya mmoja ambaye alikuwa naye majira hayo ya usiku wakionyeshana namna walivyokuwa wanajua kucheza na viuno vyao na kuihamishia sanaa ya mchezo wa ngono kitandani. Akiwa anaendelea kugugumia kwa raha ambazo zilikuwa zinaikonga nafsi yake na kumkosha sana alisikia mlango wa chumba hicho ukiwa unagongwa kwa fujo sana hali ambayo ilimfanya aishie kusonya kwa nguvu akionekana kabisa kwamba hakuridhika na hilo jambo la kukatishwa starehe yake hiyo hivyo alivaa taulo na kuchukua bastola yake na kusogea mlangoni hapo.
“Mzee kuna taarifa ambazo sio nzuri sana”
“Sitaki kuongea lolote saivi, kamchukue luck haraka sana huenda yupo kwenye hatari. Huyu ndiye pekee ambaye nadhani anajua wapi mwanangu yupo wakati huu hivyo kama kuna hatari yoyote ile kwake basi hata mwanangu anaweza kuwa kwenye hatari kubwa sana”
“Lakini mzee”
“Lakini nini? Fanya nilicho kuagiza na ukiona kwamba kuna ugumu wowote wa kumleta hapa basi hakikisha mnamuua haraka sana” Semzaba kusema kwamba Mapenzi ni kitovu cha uzembe hakukosea hata pointi moja, alikuwa sahihi pakubwa sana kwani mzee huyo licha ya uwepo wa taarifa ambazo zilikuwa ni nyeti sana lakin hakutaka hata kuzisikia zaidi ya kuhitaji kuendelea kupewa mambo mazuri kitandani.

Baada ya kutoa amri hiyo alirudi tena kitandani ili kuufurahia ulimwengu, angemuogopa nani na kila kitu kilikuwa mkononi mwake na siku kadhaa ambazo zilikuwa zinafuatia alikuwa anaingia Ikulu na kuwa raisi wa Tanzania moja kwa moja? Amani ilitakiwa kuitakasa nafsi yake kwa kupata mambo mazuri sana kama hayo ambayo alikuwa anayapitia wakati huo.

Lakini ndani ya nusu saa baadae aligongewa tena mlango huo ambapo alitukana na kuikoki bastola yake kabisa kujiandaa kumpiga nayo kijana wake ambaye alionekana kuwa msumbufu sana kwa upande wake. Baada ya kufungua mlango alimnyooshea moja kwa moja bastola hiyo akiwa anajiandaa kuiachia alipokea taarifa ambayo ilimfanya yeye mwenyewe aishushe chini.
“Bosi Luck amekutwa ameuawa na kichwa kimetenganishwa na mwili wake”
“Unasemaje wewe?”
“Luck ameuawa” kijana huyo alitoa simu yake ili kumuonyesha bosi wake video ambayo ilitumwa na vijana waliokuwa wameelekea huko ambako ndiko ilisemekana kwamba tukio hilo liliweza kutokea.

“Mungu wangu!” aliongea kwa pupa mpaka taulo lake likadondoka hali ambayo ilimfanya mlinzi huyo ageukie upande mwingine lakini mzee huyo hakuwa akijali kabisa kuhusu hilo. Alikimbilia mezani na kuchukua simu yake na kuanza kupiga namba ya mwanae ambayo haikuwa ikipatikana kabisa mpaka wakati huo. Alipiga zaidi ya mara tano lakini namba hiyo hata haikupatikana kabisa, akalazimika kumsogelea tena yule mlinzi wake.
“Ndo hii taarifa ambayo ulitaka kunipa mara ya kwanza?”
“Hapana bosi”
“Ni ipi hiyo?” Aliuliza akiwa anatetemeka sana
“Ni kuhusu mwanao”
“Enhe! kafanyaje?”
“Ameuawa” kauli hiyo ilimfanya mzee huyo akae chini akiwa uchi vile vile, hakuwa akihitaji kuamini kwamba taarifa hizo zilikuwa za kweli lakini aliona hata kama akisema ataanza kubisha huenda yeye ndiye atakuwa mjinga kwani uhalisia usingeweza kubadilika. Huyo ndiye mtoto pekee ambaye yeye alikuwa amebahatika kumpata enzi za ujana wake na ndiye huyo ambaye alikuwa anamtegemea kwa kila kitu hususani kwenye kutekeleza kila jambo ambalo alikuwa analihitaji halafu usiku huo alikuwa anapewa taarifa kwamba huyo mtoto hakuwa hai, alichanganyikiwa sana mr Mafupa.

Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu. Ni methali ambayo aliisahau kabisa kwenye maisha yake, hakuwahi kuamini kwamba ukiua kwa upanga basi na wewe lazima utakufa kwa upanga, hakujua kwamba ukipenda vya kunyonga basi na wewe lazima utanyongwa. Alinyanyuka na kutembea kama mtu ambaye amechanganyikiwa na kuingia ndani ya chumba kingine ambako alijifungia.

Aliifungua droo moja ndani ya chumba hicho, kwenye droo hiyo kulikuwa na picha ya mtoto mdogo na ndiye huyo Remsi wake. Alivuta kumbukumbu ndefu sana namna alivyoweza kumpata mtoto huyo. Ni siku moja miaka ya nyuma sana majira ya usiku akiwa kwenye gari yake, alikuwa ametoka kwenye mambo ya kampeni akiwa ana mawazo sana baada ya kuikosa nafasi ambayo alikuwa anaihitaji kwenye chama yake.

Akiwa kwenye safari ya kurudi nyumbani kwake wakati huo ambao hata walinzi hakuwa nao, alikutana na mwanamke ambaye bila shaka alikuwa anajiuza na eneo hilo alikuwa mwenyewe kabisa. Alisimamisha gari yake ili kuweza kumthaminisha mwanamke huyo kama angeweza kumfaa kwa usiku huo ili apunguze mawazo. Baada ya kuona ni mwanamke mrembo sana aliamua kushusha kioo cha gari yake ili wafanye biashara.

Mwanamke huyo alianza kujizungusha huku akiwa anafunua vifungo vya nguo yake na kumfanya kila kitu kionekane na mheshimiwa akajikuta anavamiwa na pepo kali sana la ngono kiasi kamba hata akili ilimtoka. Alimvutia ndani mwanamke huyo na kuanza kufanya naye mapenzi kwa fujo sana na hali hiyo ikawa ni mazoea kwao kwani ilifika mahali Malaya huyo akawa kama ni mali ya mheshimiwa kwani angenda naye popote na angemuita muda wowote ule ambao yeye angemhitaji mpaka siku ambayo zilikuja taarifa kutoka kwa mwanamke huyo kwamba ana mimba.

Mheshimiwa aliweza kugoma kabisa kwa kudai kwamba mimba hiyo haikuwa yake lakini mwanamke huyo alimthibitishia kwamba tangu aanze kufanya naye mapenzi yeye hakuwahi kukutana kimwili na mwanaume mwingine yeyote yule hivyo mimba hiyo ilikuwa ni yake basi mheshimiwa akaamua kuikubali japo kishingo upande.

Baada ya muda mrefu kupita hatimaye mwanamke huyo aliweza kujifungua na kujifungua kwake kulibadilisha mambo mengi sana kwani ujio wa mtoto yule ukawa kama ni baraka kwa kiongozi huyo ambapo mambo yake mengi sana yalianza kwenda kama vile alivyokuwa anahitaji na alivyokuwa amepanga. Lakini kwa baadae aliona kwamba uwepo wa mwanamke huyo kwenye maisha yake ambaye historia yake ya nyuma alikuwa anajiuza ingemharibia sana hivyo akaamua kumuua na kubakia na mtoto pekee huku akiizika hiyo siri kwenye moyo wake japo kuna watu ilikuja kuwafikia kwa baadae.

Tangu hapo alimlea kwa siri sana huyo mtoto na hakutaka kabisa dunia iweze kutambua kwamba alikuwa na mtoto ambaye anaishi hivyo akapanga kumtumia mtoto huyo kuwa kama silaha yake ya siri ambapo alimtengeneza kwa gharama kubwa sana na baadae akaanza kumrahisishia kazi zake nyingi sana lakini siku hiyo mtoto huyo alikuwa amepotea kiwepesi sana na kuuliwa na watu ambao alikuwa anawahisi tu huku asiwe na uhakika kama kweli ndio ambao walikuwa wanahusika na jambo hilo.
Ukurasa wa 50 nafika mwisho.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom