Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

FEBIANI BABUYA

JF-Expert Member
Mar 5, 2022
1,035
1,925
Kama wewe ni mpenzi wa simulizi kali sana za kijasusi na kipelelezi, kama unapenda simulizi zinazohusu michezo ya siasa na namna watu wanavyo iishi siasa kikatili.

Kama wewe ni mpenzi wa simulizi ambazo nafsi moja inaishi kwa watu zaidi ya mmoja.

Kama wewe ni mpenzi wa simulizi kali za mapigano na stori kali sana.......BASI UWANJA NI WAKO TWENDE SAWA KWENYE MOJA YA SIMULIZI BORA SANA AMBAZO UTAFUNGA NAZO MWAKA HUU.

SAKATA LA UCHAGUZI-PESA KWENYE DAMU.

Kwenye kalamu ni mimi mwenyewe FEBIANI BABUYA.

Wao wapenda kuniita Bux the storyteller.

Wasalaam.


1700125076950.jpg
FB_IMG_1699421352434.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA KWANZA
Ndani ya ofisi moja kubwa sana, alikuwa anaonekana tajiri mmoja ambaye bila shaka umri wake ulikuwa umeenda kiasi cha kutosha. Mzee huyo mwenye kitambi cha wastani ambacho kiliashiria ukwasi ambao alikuwa nao, alikuwa ameketi kwenye meza yake ghorofa ya juu zaidi ndani ya ofisi yake hiyo.

Meza yake upande wa mbele ilikuwa imeandikwa CHAIRMAN kwa maandishi makubwa kisha likafuatia jina lake ambao lilisomeka kama Apson Limo, bila shaka yeye ndiye ambaye alikuwa mmliki wa hizo ofisi kama sio kampuni kwa namna ilivyokuwa inaonekana humo ndani. Ofisi ilikuwa imepambwa kwa vitu vya gharama sana huku ukutani kukiwa na picha kubwa mbili ambazo zilionekana kwa usahihi sana.

Kulikuwa na picha moja ya kawaida ya muasisi wa taifa la Tanzania hayati Julius Kambarage Nyerere lakini pia upande wake wa juu palikuwa na picha kubwa sana ambayo bila shaka ilikuwa ni ya familia. Kwenye picha hiyo alikuwa anaonekana yeye, mama mmoja ambaye bila shaka alikuwa ni mkewe lakini pia walikuwa wanaonekana watoto watano ambapo kati ya hao watoto watano, mmoja tu pekee ndiye alikuwa ni mtoto wa kiume kati yao. Ni picha ambayo ilikuwa inaonyesha namna familia hiyo ilivyokuwa kwenye furaha kubwa sana maana wote walikuwa ndani ya tabasamu zito mno ambalo usingeweza hata kujisumbua kulielezea kwani mtu angeiona tu picha hiyo angeelewa ni kwa namna gani familia hiyo ilikuwa kwenye hiyo furaha kubwa.

Upande wa mkono wa kulia mwa ofisi hiyo ukutani, kulikuwa na maneno makubwa ambayo yalikuwa yanang’aa sana yakiwa yapo chini ya nembo ya kampuni hiyo yakiwa yanasomeka LIMO INVESTMENTS. Ofisi hiyo kubwa ilikuwa pia imenakshiwa kwa vito vya thamani sana ikiwemo na samani za kutosha huku ikiwa na sehemu nzuri sana ya wageni kuweza kukaa na sehemu ya kufanyia mazungumzo ambayo yangekuwa ya mhimu na kumfanya mhusika aongee na tajiri huyo moja kwa moja.

Mzee huyo akiwa ametulia kwenye hilo eneo anaangalia kwa umakini sana jina la kampuni yake ukutani na kuwaza namna alivyoweza kutoka mbali na kampun hiyo mpaka ikaja kusimama vyema na kuwa moja kati ya makampuni makubwa sana nchini, simu yake ya mezani ilimshtua kutoka kwenye mawazo baada ya kuanza kupiga kelele kwa nguvu, akaipokea.

“Mruhusu aingie” ni kauli moja tu ambayo aliitamka bila shaka aliipokea simu ya ugeni kutoka kwa katibu wake ambaye alimpa ruhusa kuweza kumruhusu mtu ambaye alikuwa amefika hapo. Ndani ya muda mfupi mlango ulifunguliwa, aliingia mwanaume mmoja ambaye naye umri ulikuwa umemtupa mkono kidogo akiwa ndani ya suti ya gharama mno na fimbo yake mkononi bila shaka.

“Karibu sana Mr Mafupa” alimkaribisha mgeni wake huku akiwa ananyanyuka kwenye kiti chake na kumpa mtu huyo mkono na ilionekana kwamba walikuwa wakijuana sana.

“Nadhani sio waafrika wote ambao hawajastaarabika, kuna watu mpo safi sana na huo ndio utamaduni wetu waafrika bwana lazima tusalimiane kwanza hata kama hatupo sawa” Mr Mafupa alijibu naye huku akiwa anaukutanisha mkono wake na mheshimiwa Apson Limo.

“Ujinga wa mtu mmoja usiujumlishe kwa waafrika wote, sio kawaida sana wewe kuja hapa, nilivyo ipata taarifa kwamba unahitaji kuniona nilishtuka kidogo kwamba kwanini usingesubiri sehemu nyingine nje na hapa tukakutana ila nikaamua kukubali kwa sababu nilijua huenda una shida ya mhimu sana” mr Apson aliongea akiwa anaketi baada ya kuhakikisha pia mgeni wake ameketi chini kwa ajili ya mazungumzo.

“Mhhhh sehemu yoyote ile inafaa kwa mazungumzo hususani kwa wanasiasa na wafanya biashara kama mimi na wewe, vipi mwanao alisharudi kutoka masomoni? Maana ni muda sana naskia yupo nje ya nchi”

“Sio muda anarudi nadhani kwa sasa amemaliza masomo yake”

“Kwahiyo anakuja kumsaidia baba yake kwenye mambo ya kampeni? Maana ndiye mtoto wa pekee wa kiume uliye naye”

“Ni vizuri kama ungeenda moja kwa moja kwenye maada ambayo imekuleta hapa sidhani kama mambo ya familia yangu yanakuhusu sana au yana umuhimu kwa hapa tulipo”

“Sawa ila yanaweza kuwa na umuhimu mkubwa sana kwa hapo baadae ndiyo maana nakuuliza usidharau sana. Lengo la mimi kuja mpaka hapa kwenye ofisi yako kuna makubaliano ambayo nahitaji tuyafanye mimi na wewe. Ni makubaliano ya mhimu sana ambayo yanakubidi wewe ufanye maamuzi ya kiume, narudia tena ni ya mhimu sana mr Apson”

“Nenda moja kwa moja kwenye hoja ya msingi acha kuzunguka mr Mafupa”

“Nahitaji ujitoe kwenye mbio za kugombea uraisi”

“Hahahaha Mr Mafupa nadhani uliko toka umelewa sio? Hivi unajua hata kuja hapa nimekukubalia tu kwa sababu nakuheshimu sana, huu muda mimi na wewe ni wapinzani sidhani kama ni sahihi kukutana kutana kirahisi sana namna hii maana wananchi wakijua wanaweza kuanza kuwaza mambo mabaya, nadhani kama hauna jambo la mhimu la kuongea na mimi ni vizuri zaidi kama utanyanyuka na kutoka nje ya ofisi yangu kisha usije ukarudi tena hapa maana nitafanya kama sijawahi kukufahamu”

“Najua mr Apson, najua kwamba ndani yako kuna moto unawaka sana hususani pale ambapo unakuwa unaiwaza ile Ikulu, unawaza namna watu wanavyo yasimulia maisha ya pale ukiwa kama ndiye kiongozi mkuu maana hata baadhi ya vikao vingi na mialiko mikubwa ulikuwa unaipata ila nimekuja kukuomba kistaarabu sana achia hiyo nafasi na awekwe mtu ambaye ni dhaifu na hawezi kuniyumbisha kwa sababu mimi nahitaji kuingia pale Ikulu kisha kuna makubaliano ambayo mimi na wewe tutaingia hata nikiingia Ikulu utakuwa kama mkono wangu wa kulia”

“Makubaliano yapi hayo Mr Mafupa ambayo unahisi yatanishawishi mimi kukubali kuwasaliti wananchi wangu ambao wameniamini na kuniruhusu mimi kuingia Ikulu na kuahidi kunipa kura zao za ndiyo na kwa sababu ipi hasa?”

“Kuna mpango ambao nimeuandaa, sababu tutatengeneza ugonjwa feki na kudai kwamba utakuwa nje ya nchi hospitali kwa mwaka mzima ambapo uchaguzi utakuwa umekamilika na hauwezi kuchaguliwa mtu ambaye upo hospitali hivyo watatakiwa kusubiri mpaka upone. Mwaka ukiisha mimi nitakuwa tayari Ikulu na wewe nitakuteua uwe makamu wangu kwa kuwaahidi wananchi kwamba utaingia Ikulu kama wanavyo hitaji kwenye uchaguzi ambao unafuata huku wakihisi kwamba hakuna tatizo baina yetu ni upendo tu umetawala ndiyo maana nimekupa nafasi kubwa ya umakamu wa raisi na hayo mambo inabidi uyathibitishe wewe mwenyewe kwenye vyombo vya habari. Ukikubali tu kutoka kwenye hiyo nafasi, utaingiziwa bilioni mia moja kwenye akaunti yako maana mimi najua namna ya kuzirudisha nikiingia Ikulu kisha tutaingia mikataba ya kibiashara mimi na wewe ambayo itatusaidia kutengeneza pesa kadri tutakavyo na kutufanya kuwa miongoni mwa watu matajiri sana hapa Afrika”

“Kwahiyo unahisi bilioni mia moja na hiyo mikataba ndiyo itanifanya mimi niuze uzalendo wangu na kuwasaliti wananchi wangu na kuuza utu wangu? Mr Mafupa tangu unatoka kwako ulitakiwa kuwaza kwa umakini aina ya mtu ambaye unaenda kuongea nae. Kwahiyo umeona kwamba mimi nina njaa sana na unaweza kuninunua kwa hiyo pesa? Umekosea sana, nitafanya kama hili hujaliongea naomba utoke kwenye ofisi yangu”

“Koh, koh, Mr Apson mimi huwa ni mara chache sana kumuomba mtu jambo ambalo naweza kulifanya hata kwa lazima bila mapenzi yake, mpaka nakuja kukuomba hapa ni kwa sababu nimeamua kukuheshimu kama rafiki tu japo hatujawahi kuwa karibu. Mimi Ikulu naingia kwa gharama yoyote ile na haujui kwanini naihitaji sana ile Ikulu. Hivi umewaza labda kwamba kwanini nimekubali kuingia kwenye kinyang’anyiro na mheshimiwa raisi ambaye yupo madarakani wakati nipo naye chama kimoja? Ungejua hayo basi hiyo nafasi ungeiachia mwenyewe bila kulazimishwa. Unaongelea uzalendo kwenye nchi hii ambayo wananchi wakipewa hata noti moja tu wanauza utu wao? Uzalendo upi labda ambao unakufanya ujione wewe ndiye ulizaliwa kwa ajili ya hii nchi? Jambo la msingi zaidi ambalo wewe unapaswa kuliwaza sana kabla ya kufanya maamuzi yoyote yale ni familia ndugu yangu. Nitajisikia vibaya sana kama itafikia hatua ya kunilazimu niingie mpaka upande wa familia wakati una nafasi ya kufanya maamuzi sahihi, una wanao ambao ni waz…….”

“Stooop! mjinga wewe, una jeuri gani ya kuiongelea familia yangu mbele yangu kirahisi sana namna hiyo? Nitakupiga risasi nikuzike humu humu ndani kwangu. Nisije nikakusikia tena ukiwa unaitaja familia yangu kirahisi sana namna hiyo, mimi siyo kama wewe ambaye unashinda na hao wanawake ambao unawabadilisha kila siku kama nguo kwenye makasino. Tena ukija kutaja neno familia kwangu basi nitakuua hapo hapo” alikuwa amesimama mr Apson akiwa ameitoa bastola yake amemnyooshea mwanaume mwenzake huyo ambaye alionekana kwamba alikuwa ni mgombea mwenzake kwenye nafasi ya uraisi wa nchi ya Tanzania. Mwenzake huyo baada ya kushindwa kumshawishi aliamua kuitumia familia kama ngao ya kumdhoofisha na ndiyo sababu ya mr Apson kumnyooshea bastola mr Mafupa kwani kwake familia ndilo lilikuwa jicho lake aliipenda mno. Mr Mafupa alijikohoza kidogo na kumfungukia;

“Huo uwezo wa wewe kunipiga risasi mimi hauna kwa sababu watu wameniona naingia hapa hivyo nisipo toka lazima wewe ndiye utakuwa mhusika namba moja na kesho tu asubuhi magazeti na vyombo vya habari vitaandika kwamba umemuua mgombea mwenzako ili uingie Ikulu, unadhani nani atakuamini tena? Nani atatamani kukupigia kura tena wakati wewe ni muuaji na una tamaa ya madaraka? Hahahaha utakuwa unaisubiria jela wakati huo na familia yako haitakuwa na msaada wowote ule hivyo huo ubavu hauna wa kuiacha familia yako maana unaipenda mno, mpaka hapo nipo salama na hauwezi kunifanya lolote” alitulia kidogo kuacha maneno yamuingie vyema mr Apson kisha akaendelea.

“Mimi nimekuomba kistaarabu lakini umeishia kunidharau, unajua kuna maongezi ya wanaume yanatakiwa kufanywa kiume hata maamuzi yake yanatakiwa kwenda kiume pia na hivyo ndivyo siasa inavyotakiwa kuwa lakini kwa sababu hautaki kwenda kistaarabu basi mimi nitakuonyesha namna sahihi ya kuweza kuyafanya maamuzi magumu ukiwa hauna namna na huenda kwa wakati huo hautakuwa na namna zaidi ya kutoa kilio. Likumbuke neno familia kwenye kichwa chako mr Apson na ujue tu kwamba nitarudi na kwa sasa sitarudi kukubembeleza bali nitarudi na kukufanya ulie huku ukija mwenyewe mbele yangu kunipigia magoti na kuniomba kwamba umekubali masharti yangu ila huenda utakuwa umechelewa tayari”

“Out” aliongea kwa sauti kali yenye uchungu sana baada ya mr Mafupa kumaliza kujigamba mbele yake na kuitishia familia yake huku akiwa anaikoki bastola yake, mr Mafupa alitabasamu na kutoka humo ndani kwa dharau kubwa mno.

Mr Apson alipigiza bastola yake chini kwa hasira sana huku akiwa anahema kwa nguvu mno, aligeukia ukutani na kuangalia picha ya familia yake ambayo ilikuwa kwenye tabasamu zuri sana, moyo wake ulizidi kumuenda mbio isivyo kawaida. Alikusanya begi lake na kutoka haraka sana humo ndani, alitaka kuwahi nyumbani kwanza aione familia yake maana vile vitisho ambavyo alipewa pale alihisi huenda familia yake ilikuwa kwenye matatizo huku akiwa anaendelea kumpigia simu mkewe ambaye naye hakuwa akipokea basi alizidisha wasiwasi sana kwenye nafsi yake, siasa ilianza kumtokea puani mapema sana.

Ukurasa wa kwanza naweka nukta hapa. Niseme tu karibu sana tuweza kujumuika kwa pamoja ndani ya simulizi hii ili tuweze kujua kwamba imetuandalia nimi haswa ndani yake. Unataka kujua hilo salata la uchaguzi linahusiana vipi na hizo pesa kwenye damu? Basi usibanduke twende sawa.

Kwenye kalamu nipo mwenyewe, mwapenda kuniita Bux the storyteller lakini jina langu waweza kuniita;

FEBIANI BABUYA.

Wasalaam.
1700125076950.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA PILI
Mr Apson baada ya safari yake ya muda mfupi ambao aliutumia kuendesha gari yake kwa kasi isiyo ya kawaida alifanikiwa kufika nyumbani akiwa anahema kwa nguvu mno, walinzi wake walibaki wanamshangaa kiongozi huyo maana hakuwahi kuwa kwenye hali kama hiyo siku zote za maisha yake hata ule msafara wake ambao ulikuwa unamlinda ulikuwa unamshangaa kiongozi huyo kwani hakuwa akiendesha gari bali alikuwa akiendeshwa siku zote lakini siku hiyo alitoka ofisini na kuingia kwenye gari akaitoa kwa kasi bila taarifa hali ambayo ilipelekea walinzi wake kumfuata nyuma na magari mengine.

Alikuwa anaishi maisha ya kifahari sana mheshimiwa Apson kwani hata jumba lake tu lilielezea namna alivyokuwa na maisha mazuri. Aliwapita walinzi wake kama vile hakuwa akiwaona huku gari akiwa ameiacha nje. Alikimbilia mpaka ndani lakini hakukuta mtu ila alisikia kelele upende wa pili ambako aliwaona watoto wake wakiwa wanacheza na mkewe, alijikuta anatabasamu na kukaa kwenye korido ya kushukia eneo hilo ambalo lilikuwa na bustani nzuri na bwana la kuogelea akiwa anaiangalia familia yake.

Kwake familia ilikuwa kila kitu, hakuwa na kitu ambacho angeweza kukiweka sawa na hiyo familia akakilinganisha kwenye mzani mmoja. Mkewe alikuwa ni rafiki mkubwa sana kwa wanae hususani yule mtoto wa mwisho ambaye ndiye alionekana kupendwa kuliko wengine wote. Baada ya kuona watu hao hawana muda naye kabisa ikabidi ajikohoze kidogo ili kuwashtua na ndipo hapo walipo tulia kwanza na kugeukia upande ambao yeye alikuwepo.

Mtu wa kwanza kumkimbilia alikuwa ni mwanae wa mwisho wa kike ambaye ndiye alikuwa kipenzi chake, alimkumbatia baba yake huku akidai zawadi zake lakini tajiri huyo hakuwa na zawadi kwa muda huo kwani aliondoka kwa kasi tu kuweza kuwahi nyumbani hakuwa hata na muda wa kubeba zawadi yoyote ile hivyo akamuahidi mwanae kwamba angemletea baadae maana ameagiza tayari.

Watoto wote walimkumbatia kwa mapenzi mazito mno kuonyesha ni familia ambayo ilikuwa na raha mstarehe isivyo kawaida, mtu wa mwisho kabisa alikuwa mkewe ambaye alimkumbatia baada ya watoto kuondoka na kwenda ndani. Akiwa kwenye kifua cha mmewe aliinua uso wake na kumtazama mwanaume huyo kwenye uso wake

“Una hofu sana, nini shida baba?” kitu ambacho hakuwa na uwezo wa kukificha ni uhalisia wake kwa mwanamke huyo ambaye alikuwa anamjua vizuri sana, kumkumbatia tu kidogo aligundua kwamba mumewe alikuwa na wasiwasi isiyo ya kawaida.

“Nawaza sana kuhusu mustakabali wa maisha yangu kuhusu siasa, siasa naiona kabisa kama sio sehemu salama kwangu, nadhani ile siku ambayo nilikubali kuwa mwanasiasa ndiyo siku ambayo niliamua kuitoa sadaka familia yangu. Naomba unisamehe mke wangu, naogopa sana” aliongea huku akiwa anaketi chini kwenye hizo korido lakini mkewe alimkumbatia na kukilaza kichwa cha mumewe kwenye mapaja yake.

“Hili unalo lifanya ndilo limeifanya familia hii kuwa yenye furaha kubwa sana, watoto huwa wanajivunia sana kuwa na baba kama wewe hususani unapokuwa mbele ya vyombo vya habari ukiwa unaongea, namna unavyo tengeneza hoja fikirishi, namna ulivyokuwa mtu wa kuwaza mambo makubwa na mambo ambayo yanajenga fikra za mtu yeyote hivyo hauna haja ya kutuomba sisi msamaha bali unatufanya tujivunie kuwa na wewe. Najua siasa ina mambo mengi sana na sio hapa tu bali duniani kote kwani unakuwa na maadui wengi sana na ndiyo maana wewe hapo una mke ili pale unapokuwa kwenye hali kama hii mimi nipo kukuweka sawa. Kitu ambacho unatakiwa kukifanya popote ulipo kifanye kwa ukubwa hata kama utakutana na changamoto gani kwa sababu unatakiwa kujua kwamba mkeo ndiyo mshabiki wako namba moja ambaye anakupenda sana kama kiongozi wake lakini pia anakupenda na kukuheshimu kama mumewe” alitabasamu mr Apson na hiyo ndiyo sababu ambayo mara nyingi sana ilikuwa ikimfanya amuwaze mkewe kila anapokuwa mbali naye. Huyo mwanamke alikuwa chanzo kikubwa sana cha furaha kwake, ambapo angehisi kuchanganyikiwa basi akiwa mbele ya mwanamke huyo alikuwa anakuwa sawa. Mawazo yake yote yaliisha ndani ya dakika moja wakajikuta wote wanacheka sana huku wakitaniana na mkewe alimtaka mwanaume huyo akaoge kisha wakapate chakula pamoja.

“Dady nataka kumuona kaka, nimemmiss” ilikuwa ni sauti ya Latifa ambaye alikuwa ndiye mtoto wa mwisho kabisa wa mr Apson, aliongea wakati wakiwa wanaendelea kupata chakula. Kauli yake aliiongea kwa masikitiko sana, alikuwa ni mtoto wa mwisho ambaye alipendwa sana hivyo wazazi walikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili yake yeye. Ndani ya familia hiyo kulikuwa na mtoto wa kiume mmoja tu ambaye alikuwa anaelewana sana na Latifa na ndiyo sababu alikuwa akimkumbuka sana kaka yake kwani ndiye aliyekuwa akimpenda sana kuliko ndugu zake wengine wote.

Mr Apson aligeukia upande wa ukutani akiwa kwenye tabasamu zito, ukutani palikuwa na picha kubwa sana ya wanaume wawili wakiwa ndani ya suti za blue ambazo zilikuwa zinafanana kwa kila kitu. Wanaume hao walikuwa wanafanana mno ila kilichokuwa kinawatofautisha ni umri, upara na kitambi. Mr Apson kwenye hiyo picha ndiye alikuwa na umri mkubwa zaidi, na ndiye ambaye alikuwa na kitambi pamoja na upara ila ilikuwa ni tofauti kwa huyo mwanaume mwingine ambaye bila shaka alikuwa ni mwanae wa damu kwani alikuwa anafanana naye utadhani alijitoa kopi yake.

Huyo ndiye alikuwa mwanae pekee wa kiume ambaye ndiye alikuwa mrithi wake kwa kila kitu hivyo mwanae huyo wa kike kudai anataka kumuona kaka yake, alitabasamu sana baada ya kuiona ile picha kisha akatamka

“That’s my boy” aliongea akiwa na cheko la furaha kisha akaitoa simu yake na kupiga video call kwa mtu huyo ambaye alionekana kuwa nje ya nchi ili mdogo wake huyo aweze kumuona. Kweli simu iliita kwa muda mfupi kisha ikapokelea na mtu ambaye ungehisi ni yeye mwenyewe kwa namna walivyokuwa wanafanana. Hawakuongea lolote zaidi ya kumpa simu kwanza Latifa maana angeanza kusalimiana na wengine hapo ingekuwa kesi nyingine hiyo. Alifurahi sana kumuona kaka yake ambaye alimpenda mno kisha kijana huyo akawasalimia na wengine kisha akakata simu yake huku akiahidi kwamba muda mfupi ambao ulikuwa unakuja angeweza kurudi nchini maana amemaliza masomo na kwa wakati huo alikuwa anatalii kabla ya kuianza safari.

“Mwanangu arudi tu nimemkumbuka sana, ni muda sana sijampikia chakula change, watakuwa wanamlisha mavyakula ya hovyo ya dukani huko maana naona amepungua sana” aliongea mama yake akiwa amemkazia macho mumewe kama kumwambia hakikisha mtoto anarudi haraka namtaka nyumbani hapa. Mzee Apson ilibidi ajikohoze maana mkewe alimpiga jicho kali mpaka yeye mwenyewe ikabidi azuge kwa kubadilisha maada ya hapo.

“Linda yuko wapi?” aliuliza swali kuhusu uwepo wa binti yake mkubwa ambaye ndiye alikuwa mtoto wa kwanza kuzaliwa kwenye familia.

“Atakuwa kwenye biashara zake huko maana alisema kwamba amepata watu wa nje wa kufanya nao kazi nadhani atakuwa anamalizana nao kwenye masuala mazima ya mikataba” mkewe alimjibu kwa ufupi ili kumridhisha maana mzee huyo kwa namna alivyokuwa anawapenda wanae kama asingepewa taarifa ya maana angeacha hata kula hapo akamtafute mwanae.

“Hahahaha my princess, anapambana sana ndiyo maana najivunia yeye kuwa wa kwanza kuzaliwa kwani anakuwa mfano kwa wenzake kila inapo itwa leo. Nataka nimfungulie kampuni kubwa zaidi ya mitindo maana ile aliyo nayo kwa sasa ana uwezo wa kuisimamia vizuri hahahaha nataka mwanangu awe malkia wa mitindo kwenye hili bara zima la Afrika” aliongea kwa kutamba mzee huyo akiwa ananyanyuka na kucheza kidogo kitu kilicho pelekea wote kulipuka kwa kicheko maana mzee huyo alikuwa mwenye furaha sana na alipenda wakati wote familia yake iwe ina furaha.

“Na mimi sasa unitafutie biashara kubwa nyingine sio unawawaza wanao tu unamsahau mkeo aliyekuletea hao watoto, yaani nyie wanaume mkiwa na watoto tu hata mke unamsahau sijui mlirogwa na nani” mkewe aliongea huku akiwa anacheka kitu kilichofanya watoto wote wamzunguke kumcheka.

“Mama unawaonea wivu hadi wanao hahahahaha” wanae walikuwa wanamcheka huku wakiwa wanamtekenya, walianza kukimbizana humo ndani huku mumewe akikimbilia bwawani kuogelea. Ilikuwa ni moja ya familia ambazo zilikuwa kwenye furaha kubwa sana.


Ndani ya jengo lingine kubwa la kifahari majira ya usiku, alionekana mr Mafupa akiwa anavuta sigara yake ya bei ghali akiwa ametulia sehemu ambayo bila shaka ilikuwa ni mapokezi akiwa anasubiria kukutana na mwenyeji wake. Baada ya dakika tano za kusubiri akiwa anaivuta sigara yake, alikuja mwanaume mmoja ambaye alikuwa amejaa sana kwenye mwili wake na kumtaka asimame. Hakuwa na usumbufu wowote kwani alisimama na kuikabidhi sigara hiyo kwa kijana wake ambaye alikuwa amemshikia mkoba wake kisha akasimama na kuanza kusachiwa kama ana silaha yoyote kwenye mwili wake na baada ya kuonekana kwamba hana shida, mwanaume huyo alimpa ishara ya kumfuata ili akakutane na mtu ambaye alikuja kumuona huku mlinzi wake akibakia nje sehemu ya mapokezi.

Baada ya kuingia ndani alikutana na mtu mmoja ambaye alikuwa amesimama kageukia ukutani akiwa anaangalia picha kubwa nzuri za gharama ambazo zilikuwa zimepambwa ukutani mwili wake ukiwa ndani ya kanzu ndefu sana nyeupa na kichwa chake kikiwa wazi kabisa.

“Samahani sana kwa kukuingilia kiongozi, naona unajikumbushia mbali sana kwa kuangalia picha nzuri za kihistoria” Mr Mafupa aliongea huku akiwa anautua mkoba wake chini na kubaki amesimama kama alivyo ingia maana hakuona kama ni sahihi kukaa kabla ya kukaribishwa ingali mwenyeji wake naye bado amesimama.

“Unajua watu wengi mpaka leo bado hawajui kwamba hii ni moja ya nchi zilizo barikiwa kila kitu. Huwezi kuamini kwamba haya mazingira yapo hapa hapa Tanzania na hata mchoraji ni mtanzania, hizi ni miongoni mwa picha adimu sana kupatikana duniani hata nikiamua kusema nazipeleka kwenye minada huko kwa wenzetu naweza kutengeneza pesa ambayo nitakula mpaka nakufa na bado nitaiacha”

“Mhhhhh sasa kwanini hauziuzi?”

“Kuna muda kwenye maisha yako hakikisha kwenye mkono wako una vitu vya thamani ambavyo ni adimu kupatikana hiyo itakufanya upate heshima kubwa sana kwenye maisha yako yote na ndiyo maana hizi huwezi kuzikuta popote pale zaidi ya kwangu tu kwani hata mchoraji alikufa miaka mingi sana iliyo pita. Wamekuja wachoraji wengi sana wamejitahidi ila bado hakuna ambaye anaweza kuingia ligi moja na aliye zichora picha hizi na ndiyo maana zinabaki kuwa picha bora sana kuwahi kuchorwa ndani ya nchi ya Tanzania” mzee huyo aliongea akiwa anampa ishara mgeni wake aweze kuketi chini, haikuwa sawa kufanya mazungumzo wakiwa wamesimama wakati walitakiwa kupata vinywaji kidogo.

“Mr Oscar, kila nikiyaona matendo yako, nikisikia maneno yako kama hayo lakini pia nikitulia na kuisoma akili yako pamoja na misimamoyako basi naishia kumkumbuka sana wajina wako na nawaza sana kwamba kwanini uliishia tu kuwa waziri mkuu wakati kwa uwezo wako ulikuwa unaweza kuingia mpaka Ikulu kabisa?”

“Mhhhh usiniambie kwamba unamzungumzia Oscar ambaye ni miongoni mwa waasisi wa TANU?”

“Ndiyo mheshimiwa”

“Maisha hayakupi unacho kitaka wewe na kuna muda akili ikizidi sana matatizo makubwa yanaweza kutokea na ndiyo sababu hakuwa na mwisho mzuri sana. Tuachane na hayo unaweza ukaniambia sababu ya msingi ya mimi kukutana na wewe?”

“Nahitaji kuingia Ikulu”

“Sasa mimi nahusikaje hapo wakati ni suala la wewe kuwa na ushawishi mkubwa tu ili uchaguliwe na kuungwa mkono na wananchi pamoja na watu wa chama chako?”

“Mpaka nakuja kwako nina uhakika unaelewa vyema namna siasa ilivyo, unaelewa vizuri kwamba ninashindana na raisi wangu lakini pia nina uhakika wewe unaelewa namna siasa inavyo fanya kazi, kuna muda Ikulu sio wananchi wanao kuweka bali watu kama wewe hapo ndio ambao wana uwezo wa kumuweka mtu Ikulu au kumtoa Ikulu kwani hii nchi nyie mnaijua kuliko mtu mwingine yeyote yule”

“Mhhhhh unahisi ni sababu gani labda ambayo itanishawishi mimi kukusaidia wewe uingie Ikulu kama unavyo hitaji?”

Naam ukurasa wa pili nafika mwisho, ungana na mimi kwenye ukurasa wa tatu ambao unafuatia.

Wasalaam,

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kama wewe ni mpenzi wa simulizi kali sana za kijasusi na kipelelezi, kama unapenda simulizi zinazohusu michezo ya siasa na namna watu wanavyo iishi siasa kikatili.

Kama wewe ni mpenzi wa simulizi ambazo nafsi moja inaishi kwa watu zaidi ya mmoja.

Kama wewe ni mpenzi wa simulizi kali za mapigano na stori kali sana.......BASI UWANJA NI WAKO TWENDE SAWA KWENYE MOJA YA SIMULIZI BORA SANA AMBAZO UTAFUNGA NAZO MWAKA HUU.

SAKATA LA UCHAGUZI-PESA KWENYE DAMU.

Kwenye kalamu ni mimi mwenyewe FEBIANI BABUYA.

Wao wapenda kuniita Bux the storyteller.

Wasalaam.


View attachment 2818481View attachment 2818482

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Dogo ungemaliza kwanza stori zako zingine ambazo hazijaisha. Sioni kama ni busara kujaza ma hadithi kibao ambayo yapo robo robo!
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA TATU
“Wakati ukiwa kiongozi, ulikuwa ni moja ya watu wa mfano kwangu hali ambayo ilinifanya mimi nikufuatilie wewe kwa ukaribu sana, kwenye kukufuatilia kwa umakini nilijifunza vitu vingi sana kwako lakini sikuishia hapo tu bali niliyajua mengi sana ambayo yalikuwa kwako na yalikuwa yakikuzunguka” mr Mafupa alijikohoza kidogo kisha akaendelea tena.

“Huko Kahama kuna migodi yako ambayo ilikuwa inakuingizia pesa nyingi sana ila kwa bahati mbaya ikaja kubinafsishwa na serikali ikakutishia kukupatia kesi ya uhujumu uchumi kama utakuja kuifuatilia tena kitu ambacho kilikupelekea wewe kuingia hasara kubwa sana mpaka mwisho wa siku ukawa kama umeikatia tamaa kabisa. Sasa nahitaji hivyo vitu nivirudishe kwenye mikono yako lakini pia utakuwa mtu wangu wa karibu sana hali ambayo itapelekea wewe kuweza kufanya biashara yoyote ile ambayo utajisikia ndani ya nchi hii na hakuna mtu yeyote yule ambaye atakugusa. Hayo yote hayawezi kufanyika mimi nikiwa nje huku na ndiyo sababu ni lazima uhakikishe naingia Ikulu ili haya yote yaweze kutimia kwa urahisi zaidi” Mr Mafupa baada ya kumaliza maelezo yake alitulia kwanza na kuhema akiwa anamsikilizia kigogo huyo aweze kuongea lolote.

Mr Oscar alimwangalia sana mwanaume huyo ambaye alionekana kuwa na moto usio wa kawaida kuweza kuingia Ikulu, aliinyanyua pombe kwenye chupa na kuinywa yote, akatikisa kichwa chake na kuuinua uso wake kumwangalia tena Mr Mafupa kwa umakini akiwa kama anapima jambo kwenye macho yake.

“Wakati unaingizwa kwenye baraza la mawaziri nilijua kabisa nchi imepata kirusi kipya ambacho kitakuwa ni hatari sana kwa taifa hili. Ni hatari sana kama nchi inaanza kuwa na viongozi wenye tamaa kubwa sana namna hiyo kushika madaraka kwani kinachokuwa kinawapeleka pale ni maslahi yao tu na sio kuipigania nchi, hali hii inanifanya niwaonee sana huruma watu maskini japo sio biashara yangu hivyo inabidi tu wapambane na hali zao maana mimi hayanihusu. Mimi nitakusaidia wewe kukichukua hicho kiti lakini kama ukija kwenda nje na maneno yako au ukanisaliti basi wewe na familia yako ambayo huwa unaificha na kuwadanganya watu kwamba hauna, nitawafanyia kitu kibaya sana. Nina imani kama ulinichunguza basi utakuwa unajua mimi ni mtu wa namna gani hususani pale anapo tokea mtu na kunisaliti” aliongea kwa msisitizo sana maneno ambayo aliamini kwamba Mr Mafupa alikuwa akiyasikia vyema kabisa kwenye ngoma za maskio yake.

“Nakuelewa mheshimiwa, mpaka nakuja hapa nakuamini sana hivyo siwezi kupoteza imani kwa mtu anaye niamini kwa sababu siku nyingine yakinikuta nitakuwa sina pa kukimbilia, hivyo nakupa maneno yangu siwezi kwenda nje na makubaliano yetu”

“Mimi nakusaidia lakini kwa sharti kubwa moja”

“Nakusikiliza mheshimiwa”

“Mimi nataka kuwa nje kabisa ya haya mambo”

“Unamaanisha hautaki kujulikana kama umenisaidia wala kuwa na mimi upande mmoja?”

“Safi, kumbe umekomaa kisiasa na tunaongea lugha moja. Mimi sitaki kabisa kujulikana kwamba nipo kwenye hii michezo, mimi sitaki kutajwa tajwa kwenye vyombo vya habari, mimi sitaki kabisa hata wewe ujulikane kwamba huwa tunakutana au kuwasiliana. Mimi nitakuwa kama kivuli tu kwako na hili jambo hatakiwi kulijua mtu yeyote yule kwamba mimi nilikuwa nyuma yako maana inaweza kuwa na athari baadae hata ukikichukua kiti wananchi watakuwa hawakuamini kabisa kwa kujua kwamba una uwezo mdogo sana ndiyo maana uliwategemea watu wengine ili kupata nafasi. Kama nikija kujua kwamba maongezi yangu mimi na wewe yapo kwa mtu mwingine au kukutana kwetu kuna mtu mwingine anajua nadhani unajua ni kipi ambacho nitakifanya kwako na kwa watu wako wanao kuzunguka”

“Nimekuelewa vizuri mheshimiwa”

“Una mpango gani kwa sasa?”

“Nataka kwanza niipate imani ya wananchi”

“Unaipataje”

“Nadhani nitumie pesa nyingi sana kwa sasa kuweza kuziridhisha nafsi zao”

“Huwa unafikiria kweli kabla ya kufanya maamuzi? Mbona unakurupuka sana? Una miaka mingapi kwenye siasa?”

“Ni zaidi ya miaka ishirini”

“Haukutakiwa kuwepo huku, bado una akili za darasa la saba. Kwa miaka yote hiyo ambayo ulikuwa kwenye siasa kuna jambo gani la maana ambalo umewafanyia wananchi kiasi kwamba wakukumbuke wewe au kukupa imani?”

“Sina imani sana kama lipo”

“Usiwe na mawazo kama mtoto mdogo. Wananchi huwezi kuzishinda imani zao kwa kuwapa pesa japo haimaanishi kwamba watazikataa pesa zako, dunia hii hakuna mtu anazikataa pesa ila unahisi hata baada ya kupata pesa hizo ndo watakupigia kura? Hapana hata wao wanajua wewe ni mtu mjinga tu ambaye hauna huo uwezo wa kuiendesha nchi hii hivyo kwa kutupia pesa tu pekee hakuna utakacho kipata zaidi ya kupoteza tu, akili inatakiwa kuanza kwanza ndipo pesa inafuata na hivyo ndivyo jinsi siasa inavyofanya kazi”
“Unaweza ukanipa maelezo zaidi kiongozi?”

“Kitu pekee ambacho unatakiwa kukifanya wewe ni kuhakikisha kwamba wananchi hawana chaguo lingine zaidi ya kukuchagua wewe, ndiyo njia ambayo utaitumia kuweza kuingia Ikulu kirahisi sana”

“Unamaanisha kwamba niwaue wapinzani wangu ili mwenye nguvu nibaki mwenyewe?” Mr Mafupa aliuliza akiwa ana hamu kubwa sana ya kuweza kujua kwani alikuwa mbele ya mtu ambaye alikuwa ni mkongwe mkubwa sana wa siasa na alikuwa na uzoefu kuliko yeye hivyo hata nchi yeye ndiye alikuwa anaijua zaidi yake hata namna siasa ilivyokuwa inafanya kazi kwa sababu aliwahi kuwa waziri mkuu wa nchi. Mr Oscar alitabasamu na kunywa pombe nyingine ili kuendelea kukiweka kichwa sawa kuweza kutengeneza hoja kwenye hilo eneo ambalo aliona moja kwa moja lina maslahi makubwa sana kwake.

“Moja kati ya njia nzuri zaidi ya kumshinda adui yako sio kuwa na mipango hatari zaidi bali ni kuidhoofisha mipango yake yeye, ndiyo sababu kubwa huwa unaona kwenye masoko kampuni zinazo fanikiwa sana ni zile ambazo zinawekeza sana kumsoma mpinzani wake, wanakuwa wanajua huyu mjinga atatoka hapa ataenda pale hivyo sisi tunageuza kete tu kuiweka pale ushindi tunachukulia mezani kirahisi sana. Hata kwenye siasa ipo hivyo ukiujua udhaifu mkubwa wa mpinzani wako hata ukikurupuka saa tisa usiku basi mchezo utakao ucheza unashinda ndani ya dakika kumi tu za mwanzo na sio tisini” Mr Oscar alimtazama Mr Mafupa ambaye alikuwa makini sana kuisikiliza kila sentensi ambayo ilikuwa inatamkwa pale. Baada ya utulivu huo wa muda mfupi kupita Mr Oscar aliendelea;

“Kumfanya mtu asiwe na chaguo, ina maana atafanya lile lililo mbele yake hata kama halipendi au halihitaji. Ni sawa na mtu mwenye njaa kali na hapendi aina fulani ya chakula, kama chakula ambacho kipo ndicho pekee kinachoweza kuituliza njaa yake hata kama atakula kwa manung’uniko ila bado atakuwa amekula tu. Kwa maana hiyo inatakiwa ucheze na udhaifu wa wenzako. Tafuta udhaifu wao mkubwa kisha utumie kuwateketeza maana siasa haitaki huruma, siasa inataka wanaume ambao huwa tunasema kwamba wanakuwa wameaga kwao”

“Jambo la pili ukisha ujua udhaifu wao na kuutumia ili kuwafanya wananchi wasiwe na namna hakikisha una watu wa kukulinda endapo kuna mambo mabaya yataanza kujitokeza kwa baadae. Najua utapata kiburi kwa sababu upo na mimi ila hapa nazungumzia kwamba unatakiwa kuishinda mioyo wa wale viongozi wa ngazi za juu zaidi kwenye jeshi la polisi, jeshi la nchi pamoja na wale watu wa usalama. Hawa watu ukiingia Ikulu watakuwa chini yako ndiyo na wewe ndiye unaye wateua na kuwatoa pale unapo jisikia mwenyewe lakini kuwa chini yako haimaanishi kwamba watakuwa waaminifu kwako au watakuwa wanakusikiliza, ili wakusikilize inatakiwa uishinde mioyo yao na kuwafanya wawe waaminifu sana kwako kwa kila jambo na kila hatua. Sasa wanakuwaje waaminifu kwako?” mheshimiwa alitulia tena na kutoa bunda la noti kisha akaliweka mezani. Akaendelea;

“Hawa inatakiwa ule nao vizuri tu, yaani wape wanacho kihitaji na kwa sababu moyo wa mwanadamu umeumbwa na matamanio basi pesa itakuwa ndiyo njia nzuri zaidi ya kuwashawishi wao kuwa upande wako yaani unakuwa kama mfuga mbwa na namna mbwa ambavyo anakuwa anakutii kwa sababu wewe ndiye unamlisha. Ukifanya hivyo hawa watakusikiliza sana na ndio ambao watakuwa wanakuletea habari zote na kukufanyia kazi zote chafu ambazo wewe hutataka kuhusika moja kwa moja wala kutaka kujulikana kama ulikuwa unahusika nazo. Lakini ukiishi na hawa vibaya wanaweza hata kukutoa kwenye hicho kiti na usiwe na la kufanya hususani wakiamua kuungana pamoja hivyo hawatakiwi kuwa karibu sana hawa watu wao kwa wao kwa gharama yoyote ile”

“Kitu ambacho unatakiwa kukikumbuka sana ni namna unavyo itumia akili yako kuwaweka hawa watu kwenye mikono yako, sio kila sehemu itatumika pesa na sio kila sehemu yatahitajika mabavu ila kuna sehemu itahitajika zaidi akili. Hawa watu kabla ya kuwapa hiyo ofa ya maisha mazuri hakikisha kwanza umewatafiti na kujua kila mmoja anavutiwa sana na nini na hicho ndicho utakacho kitumia kumkamatia, kirahisi sana atakuwa kwenye mkono wako”

“Kama ukiona kuna mmoja wapo anaanza kwenda tofauti na unavyo hitaji wewe basi hakikisha anakuwa wa kwanza kumezwa na udongo yaani umuue haraka sana kwa sababu ukichelewa tu itakugeukia wewe mwenyewe, ila hiyo hali ya kumuua inatakiwa kuwa ya mwisho kabisa pale ambapo njia zingine zinakuwa zimeshindikana kabisa kutumika na hakuna namna nyingine zaidi ya hiyo. Hapo nadhani umejifunza jambo kwamba ni mhimu hizo nafasi nyeti uwape watu wako ambao unawaamini kana kwamba likitokea tatizo watakulinda maana sio kila kiongozi ana tamaa ya pesa, kuna watu ni wazalendo isivyo kawaida yaani kwao pesa sio chochote sasa ukijichanganya kumpa mtu kama huyo nafasi wakati unajijua wewe sio mzalendo ndipo utakapo anza kuona hicho kiti ni kichungu sana.” Mr Oscar aliendelea kumpa somo Mr Mafupa kama alivyokuwa anahitaji kisha akaendela;

“Unamjua mshindani wako mkubwa?”

“Ndiyo, ndiyo namjua, ni Mr Apson Limo”

“Kwanini unahisi hivyo?”

“Kwa sababu anapendwa sana na wananchi na ndiye kipenzi cha wananchi ambaye wananchi ndio walimuomba aweze kuingia Ikulu”

“Umeona namna wenzako wanavyokuwa wanazipata imani za wananchi eeh”

“Mhhhhh sijui aliwezaje kufanya hivi”

“Ni namna unavyokuwa unajiweka, ukiwa na malengo ya mbali na ndivyo unavyokuja kuwa. Hauwezi ukawa kibaka mtaani halafu unajua kabisa baadae unataka kuwa kiongozi, unadhani nani atakupa nchi? Lakini ukijiweka kwa namna inayo takiwa basi wananchi wenyewe watakuomba uwe mtu fulani na ndicho kinacho tokea kwa Apson, tangu zamani amekuwa mtu wa kusaidia sana jamii, mtu safi hata kwenye wizara akili yake imebadilisha sana mambo mengi ya nchi, sasa unahisi mtu kama yule unaweza kushindana naye wewe?”

“Hapana hapana”

“Ndiyo maana nimekwambia unatakiwa kuwafanya wananchi wasiwe na chaguo lingine”

“Kwahiyo unataka nimuue Apson Limo”

“Mimi siwezi kukupangia cha kufanya ila kitu cha kwanza unatakiwa kuutafuta udhaifu wake mkubwa ulipo. Mara nyingi mtu anakuwa sawa pale ambapo vitu anavyo vipenda vipo sawa ila visipokuwa sawa hata ile nguvu ya kupambana huwezi ukaiona tena kwake hiyo inakuwa ni nafasi yako kubwa ya wewe kushinda huku ukiwa na hao watu wa mamlaka na nafasi kubwa za ulinzi na usalama basi unakuwa unafanya unacho kitaka”

“Mr Limo udhaifu wake mkubwa sana ni familia yake, kwake familia ni kila kitu na ndiyo ambayo inampa nguvu kubwa sana ya mapambano hivyo kama ukiiyumbisha familia yake basi atakuwa kwenye hali mbaya sana kitu ambacho kitamfanya awe anafanya maamuzi ya kukurupuka na kila kitu hakikisha wananchi wanakijua. Itafika wakati wataona kwamba mtu ambaye wanampenda hayupo sawa kutokana na matatizo ambayo yanampata na wakisema wampe Ikulu huenda itakuwa hatari kubwa sana hivyo wataamua kumpatia mtu wa pili ambaye utakuwa ni wewe hapo. Ila kama ikishindikana basi muue” maelezo hayo ya Mr Oscar yalilichanua tabasamu kwa mr Mafupa na ndiyo maana alimfuata mzee huyo kwani hakukosea kabisa.

“Hahahaha hahahaa sikufanya kabisa makosa kukuchagua wewe kuwa role model wangu maana ni mtu mwenye mawazo mapana na unaona mbali sana. Hili ni jambo ambalo nilikuwa naliwaza tangu muda sana kwamba huenda mambo yatakuwa hivi, hivyo kuna jambo ambalo nililifanya mapema kama kujilinda tu sasa naanza kuuona umuhimu wake” Mr Mfupa aliongea kwa furaha sana

“Lipi hilo?”

“Nilisha ingia tayari kwenye familia yake”

“Una maanisha nini?”

“Unajua kwenye ujana wangu nilikuwa na mambo mengi sana hivyo kuna mtoto ambaye nilimpata kwa siri na huwa sipendi sana ajulikane kwamba ni wangu ila namtunza kwa kila kitu na ndiye ambaye anafanya kazi zangu nyingi sana kwa siri na ndiye ambaye nilimtumia kumuingiza kwenye ile familia”
“Usiniambie kwamba ndiye mpenzi wa yule binti mkubwa wa mr Apson?”

“Ndiyo mheshimiwa” jibu la Mr Mafupa lilimfanya mr Oscar kucheka sana

“Hahahah hahahah wewe mjinga kumbe kuna muda huwa una akili kidogo, hilo ni moja kati ya jambo bora sana kuwahi kulifanya kwenye maisha yako, enhe ni mpango upi ambao unafuata kwenye akili yako”

“Kama ulivyo nipa ushauri nataka nimdhoofishe kupitia familia yake huku nikijiweka mbali sana na masuala ya ugomvi ili yakitokea nisije nikaonekana nahusika kwa lolote. Nataka nimuue binti yake wa mwisho ambaye ndiye kipenzi cha familia kwa sababu ndiye ambaye anapendwa sana, kufa kwake litakuwa pengo kubwa sana kwao hivyo lazima familia itayumba pakubwa sana lakini wakati hilo likifanyika basi nitampoteza na binti yake mkubwa kupitia mwanangu hivyo hakuna ambaye atajua yupo wapi sasa hapo ndipo nitaamua kutokana na hali atakayo kuwa nayo Mr Apson kama nimuue au nifanyaje”

Unayaamini maneno ya Mr Mafupa? Mimi sijui ila ukurasa wa tatu naishia hapa.

Wasalaam,

Febiani Babuya.
FB_IMG_1704084797132.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA NNE
“Wazo lako ni zuri, nakuunga mkono lakini umewaza kuhusu mwanae wa kiume huyo bwana mdogo ambaye alikuwa na akili sana mpaka akaliongozea taifa kwenye masomo yake na kudaiwa kwamba ni miongoni mwa wale binadamu wachache sana wenye akili zaidi hapa duniani?”

“Ndiyo mheshimiwa, yule bwana mdogo hana madhara yoyote kwani hata siasa haijui, ni mtu wa kushinda na wino tu kwenye makaratasi, yaani ni yeye na kitabu kitabu na yeye hivyo hayupo kwenye mipango yangu kabisa maana hatakuwa na la kufanya zaidi ya kubaki mkiwa huenda hata nchi atahama na kuhamia huko huko ambako ndiko anasomea”

“Mhhhh kuna kauli wahenga waliwahi kusema kwamba samaki mkunje angali mbichi maana akikauka atavunjika, usije ukakumbuka kumwagilia bustani wakati imesha komaa tayari bwana Mafupa” mheshimiwa alimtahadharisha mapema ili baadae asije akaanza kuwalaumu watu.

“Nipo makini sana kwenye hilo jambo. Naomba niende ili nianze kuyafanyia kazi mambo yote kwa haraka sana ila naomba unisaidie jambo moja la mhimu sana mheshimiwa” Mr Oscar alikuwa anamtazama Mr Mafupa kwa umakini kama kumpa ruhusa kuongea hicho ambacho alionekana kuwa nacho na kuhitaji kukitoa moyoni hivyo akaendelea baada ya kuona kama ameruhusiwa.

“Naomba ushughulike na suala la raisi ambaye yupo madarakani naona bado anahitaji kuendelea kubaki”
“Nitakusaidia ila kwa sharti moja”

“Lipi hilo mheshimiwa?”

“Ukiingia Ikulu, utafanya kazi chini yangu” Mr Mafupa alimwangalia sana Mr Oscar baada ya kuongea kauli hiyo lakini mwisho alimpa mkono na kutamka neno

“Deal” kisha akatoka humo ndani. Alifika mpaka nje kabisa akiwa na mlinzi wake, akageuka kuliangalia jengo hilo kubwa akiwa na tabasamu la kutosha kwenye uso wake kisha akatamka.

“Siasa ni mchezo ambao unachezwa tofauti na watu wanavyo hitaji uchezwe au wanavyo uelewa na hapo ndipo inakuja tofauti kubwa sana kati ya siasa na michezo mingine yeyote. Hii nchi naenda kuiweka kwenye mkono wangu mimi na nitaiendesha kwa namna ninavyo hitaji mimi na kwa atakaye jitokeza mbele yangu basi nitamuonyesha namna siasa ilivyo kwa upande mwingine mbali na ule ambao wanauona wanasiasa wakijinadi nao kwenye mitandao ya kijamii na kwenye uombaji wa kura wanapokuwa wanawadanganya wananchi” Kisha akapanda kwenye gari na kutoweka hilo eneo na mlinzi wake.

“Bosi, una uhakika kweli unatataka kumsaidia huyu mtu? Anaonekana ana tamaa sana” aliongea mlinzi wa Mr Oscar baada ya mgeni wao kuondoka, aliingia ndani ili kuhakikisha kama mheshimiwa alikuwa salama huku mzee huyo akiwa dirishani anaangalia upande wa nje ambako alitokea Mr Mafupa. Alitabasamu na kugeuka baada ya kusikia swali kutoka kwa huyo mfanyakazi wake.

“Unahisi kwanini amekuja kuniomba msaada mimi na sio watu wengine?”

“Kwa sababu wewe ni mtu mwenye nguvu kubwa sana hivyo ana imani kwamba unaweza kufika sehemu yoyote ile hivyo uwepo wako ana imani kwamba utampitisha popote pale ambapo atataka kwenda”

“Umejibu sahihi sana na hivyo ndivyo ambavyo siasa mara nyingi inafanya kazi. Hawa watu wakiwa na shida huwa wanakuwa wapole sana hata ukihitaji apige magoti hapo atapiga tu lakini ikifika wakati ambao wanakuwa wamemaliza shida zao na wakapata nafasi kubwa huwa wanabadilika sana na kuwa watu wengine. Nakumbuka hata mimi wakati najitafuta kwenye siasa nilikuwa mpole sana, nilikuwa tayari hata kuwafuta watu viatu ili tu wanipe nafasi ya kunisikiliza lakini baada ya kuwa hapa juu nilitamani nianze kuwaendesha hata wao jambo ambalo walilipinga sana nikaishia kuwaua wote. Huyu ana tamaa sana ya madaraka hivyo haoni shida kufanya jambo lolote lile ili atimize tu malengo yake ila amekosa akili. Sasa kwa sababu hana akili mimi nitaweza kumuendesha kwa namna nitakavyo hitaji mimi na kama akiniletea uswahili kama anavyo hitaji kuwafanyia wenzake basi hata yeye sitaona shida kubwa kuweza kumuua maana atakuwa hana umuhimu wowote ule. Jambo ambalo nahitaji wewe ulifanye ni kuzifuatilia hatua zake zote bila kusahau nahitaji hiyo ripoti ya huyo mtoto wake wa siri wa kiume ili nijue naanzia wapi kudili naye”

“Nimekuelewa bosi, na hilo suala la mheshimiwa raisi ambaye bado yupo madarakani utalimaliza vipi? Kwa sababu hata yeye hayupo tayari kuyaachia madaraka”

“Huyo nitaenda kuongea naye na kuweka naye makubaliano, kama akishindwa kunisikiliza akaamua kuwa mbishi basi itabidi tufanye kama anavyo hitaji yeye ili aondoke pale kwa lazima”

“Lakini naona kama itakuwa ni hatari sana, yule ni raisi wa nchi hivyo hata kumtoa kwenye ile nafasi sio rahisi sana bosi, kunaweza kuwa na madhara makubwa sana kwa hapo baadae”

“Jambo lolote zuri ni lazima nyuma yake kuwa na hatari kubwa sana, ukiona jambo kubwa unalifanikisha kiwepesi basi jihadhari sana kuyapokea matokeo mabaya lakini ukiona jambo la hatari ukalifanikisha kwa ugumu basi hata matokeo yake yatakuwa mazuri japo wakati wa kulifanikisha kunaweza kutokea madhara ambayo kama usipokuwa makini yanaweza yakasababisha matatizo mengi makubwa hivyo cha kukifanya wewe hapo ni kudili na hayo matatizo ambayo yatajitokeza wakati unalishughulikia”

“Sawa bosi” mlinzi huyo alimaliza maelezo yake na kutoka humo ndani akimwacha mheshimiwa huyo kwenye uso wa tabasamu kiasi kwamba alikuwa anashangilia kwa hatua kubwa sana ambazo alikuwa amezipiga, alikuwa anaenda kurudisha migodi yake ambayo ilipotelea kwenye mikono ya serikali lakini pia alikuwa anaenda kumshika kwenye mkono wake mwanaume ambaye alikuwa anaingia Ikulu hivyo kiufupi yeye ndiye ambaye alikuwa anaenda kuiendesha nchi na huyo ambaye angeingia madarakani yeye angekuwa kama kivuli tu maana shida yake yeye ilikuwa pesa tu hivyo kama angepata pesa basi asingekuwa na uhitaji na jambo lingine lolote lile.


IKULU
Mheshimiwa Boniphace Wala wala ambaye ndiye alikuwa raisi wa nchi ya Tanzania, majira hayo ya usiku alikuwa ndani ya Ikulu kwenye ofisi yake. Alikaa kwa zaidi ya dakika sabini na tano akiwa anaizungusha kalamu yake ya wino kwenye mkono wake mbele yake akiwa ameziweka picha mbili ambazo zilikuwa zimechorwa kwa ustadi mkubwa sana pembeni yake pakiwa na maelezo ya kutosha kuhusu picha hizo.

Picha ya kwanza ilikuwa ni picha ya Apson Limo ambayo iliandikwa kwa maandishi yaliyo kolezwa kama Mwanasiasa na muanzilishi na mmiliki wa kampuni zote za LIMO INVESTMENTS, mwanamapinduzi lakini ni msaidia jamii kwa kiasi kikubwa sana akiwa amehudumu kwenye wizara ya mambo ya nje ya nchi kwa miaka mitano lakini kwa sasa alikuwa anawania nafasi ya kuwa raisi wa nchi ya Tanzania. Hayo ndiyo yalikuwa maelezo ya mhimu zaidi kwake kuweza kuyapitia wakati huo kwani yaliyokuwa yanaendelea chini yake yalikuwa yakizungumzia kuhusu maisha yake binafsi na familia kwa ujumla.

Picha ya pili ilikuwa na picha ya Mr Mafupa ambaye alikuwa amewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani wa nchi ya Tanzania, akahudumu kama mbunge bila kusahau aliwahi kufanya kazi kama mwanadiplomasia kwa miaka isiyo pungua kumi ila kwa wakati huo naye alikuwa anahitaji kuiwania nafasi hiyo ya kuweza kuingia Ikulu.

Hizo picha ndizo ambazo zilimfanya mheshimiwa atumie hizo dakika sabini na tano kuweza kuzitafakari huku kichwani kwake yakiwa yanakuja mambo mengi sana na kupotea kwani hakuwa akielewa kama hayo mambo hatima yake ingekuwa ni ipi. Picha moja ndiyo ilikuwa inampa sana wasiwasi zaidi ambayo ilikuwa ni ya Apson Limo, mtu huyo alikuwa akipendwa sana na watu pamoja na jamii ambayo ilikuwa ikimzunguka kwa ujumla kwa namna alivyokuwa anawapigania wananchi hususani wale maskini sana. Wananchi walimpa dhamana mtu huyo kwa kumuahidi kwamba ni lazima aingie Ikulu ili akaibadilishe nchi ambayo ilionekana kujaa rushwa na ubadhilifu mkubwa sana wa mali za uma ambazo wananchi walitegemea kwamba zingetumika kutengenezea miundombinu na huduma za kijamii.

Kukubalika sana kwa mtu huyo ilikuwa ni hatari kubwa sana kwake kwa sababu kama angekaa vibaya basi angekipoteza hicho kiti chake ambacho kiuhalisia hakuwa tayari kabisa kukiachia kwa namna yoyote ile. Kuhusu mtu wa pili ambaye alikuwa ni Mr Mafupa, hakuwa na wasiwasi naye sana kwa sababu alikuwa wa chama chake hivyo alijua kwamba hata kwenye ule mchujo wa ndani ya chama chake lazima jina lake lingetoka tu na huyo mwenzake angeshindwa kutimiza kile ambacho alikuwa anakitaka kwa kuamini kwamba ndani ya chama chake watu wengi sana walikuwa upande wake hivyo akaamua kumpuuza sana Mr Mafupa.

Akiwa hapo ndani, aliingia mzee mmoja ambaye alikuwa na mkoba wake akiwa ndani ya suti nzuri ambayo ilimpendeza sana. Alifika hapo na kutoa heshima kwa raisi wake, baada ya hapo aliruhusiwa kukaa chini.

“Kwema kiongozi? Maana nimetoka hapa muda ule nafika tu nyumbani napata ujumbe kwamba unanihitaji tena Ikulu. Nini shida kiongozi wangu! maana nakuona kabisa kwamba haupo sawa” Aliongea mzee huyo ambaye ndiye alikuwa mshauri mkuu wa raisi Boniphace Wala wala.

“Ni kweli kabisa, tena upo sahihi sana, mimi sipo sawa tena sipo sawa kabisa. Najua wewe ni mzee mwenzangu japo kiumri umenizidi parefu tu huenda ndiyo maana ukawa mshauri wangu. Hivyo nina imani kwamba kwa namna moja ama nyingine hata kama mimi ni raisi wa nchi utakuwa unanizidi akili hata kidogo tu kwahiyo nimekuita hapa ili unipe ushauri fulani kuhusu hili sakata la uchaguzi ambalo linaenda kutokea siku za hapa karibuni”

“Mheshimiwa mimi siku zote nipo hapa kwa ajili yako, kazi yangu ni kukushauri yale ambayo ni sawa kwako na yatakuwa na umuhimu mkubwa sana kwa upande wako. Nakusikiliza kiongozi wangu, niulize chochote au niambie chochote kile mimi nitakishughulikia kwa nguvu zangu zote” mzee huyo alongea kwa unyenyekevu mkubwa sana kuonyesha kwamba alikuwa akimtii sana raisi wake.

“Kwa hii nafasi yangu unahisi ni jambo gani ambalo linaweza kuwa kama tishio kwangu au ni kitu gani ambacho hakitakiwi kutokea ili nibaki salama?” mheshimiwa aliuliza swali hilo huku akiwa amemkazia macho mshauri wake na kusubiria jibu ambalo alihisi huenda likampa utatuzi wa mambo mengi sana ambayo yalikuwa yanapita kwenye kichwa chake kwa wakati huo. Mzee huyo alikohoa kidogo ili kuliweka koo lake sawa maana hakutaka kumjibu mheshimiwa kwa kukurupuka kisha akakifungua kinywa chake.

Ukurasa wa nne hauna cha kukuongezea mpaka wakati ujao.

Febiani Babuya.
FB_IMG_1704253516066.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA TANO
“Unajua wewe ndiye mtu namba moja ndani ya nchi hii, wewe ndiye mtu mwenye nguvu zaidi ndani ya taifa hili lakini pia wewe ndiye mtu ambaye kauli yako ina nguvu na maamuzi ya mwisho ndani ya hii nchi. Lakini ukiacha hayo yote jambo la hatari zaidi kwako ni uwepo wa watu wenye nguvu zaidi ndani ya nchi yako nadhani hiyo ndiyo inaweza kuwa hatari kubwa zaidi kwako” Mzee huyo alitamka sentensi fupi ambayo ilikuwa na maana kubwa sana na alikuwa na uhakika kwamba mheshimiwa lazima angeielewa vizuri tu.

“Una maanisha nini kusema hivyo?”

“Mheshimiwa kitu ambacho kinampa jeuri mtu yeyote yule ni nguvu, mtu anapokuwa na nguvu kubwa sana anakuwa anajihisi kwamba yeye anaweza kufanya jambo lolote lile na hakuna mtu yeyote yule wa kuweza kumzuia wala kitu chochote kile cha kutokea kati kati na kuweza kumuyumbisha hivyo anaanza kujikuta hata mamlaka haziheshimu kwani anaamini hata hao ambao wapo kwenye mamlaka anaweza kuwaendesha atakavyo yeye na mgawanyiko huwa unaanzia hapo” aliongea na kuhitaji kuendelea lakini alitulia baada ya kuona kama mheshimiwa anahitaji kuongea, hakuwa tayari kumzuia bosi wake

“Unataka kusema kwamba?”

“Mheshimiwa nadhani unamkumbuka vizuri Mr Pandei Santo”

“Ndiyo namkumbuka vizuri sana, anahusikaje na swali langu?”

“Yule bwana ni wewe mwenyewe ndiye uliuondoa utawala wake kwa ushauri wangu mimi hapa, nadhani unakumbuka baada ya kuwa na pesa nyingi sana alianza kuleta jeuri hadharani kwa kuhisi kwamba mamlaka zote zipo chini yake na anaweza kuyafanya yale ambayo anajisikia yeye mwisho wa siku akaanza kukukosea heshima mpaka wewe tena hadharani lakini kwa kile ambacho ulimfanyia kilitosha kurudisha heshima yako na kuitoa hatari ambayo alikuwa anaitengeneza kwako. Sasa kwenye nchi wakiwepo watu kama wale tena wakiwa wengi linakuwa sio jambo zuri kwani muda wowote wanaweza kufanya jambo lolote kwa sababu wanakuwa na pesa na pesa inaweza kuinunua nafsi ya mtu yeyote yule”

“Mbali na hilo jambo ambalo ni hatari zaidi kwa nafasi yako ni pale ambapo wanakuwepo watu wenye uwezo mkubwa zaidi kichwani kukuzidi wewe halafu hawapo upande wako. Ni vyema kama kuna watu wana kuzidi uwezo wewe hakikisha wanakuwa upande wako na wanakuwa chini yako hivyo wewe unazitumia akili zao kuweza kukamilisha mambo yako. Akili ndiyo inaweza kumuendesha mtu, akili ndiyo inaweza ikakuweka kwenye hicho kiti chako na akili ndiyo inaweza kukufanya ukatolewa kwenye hiyo nafasi yako. Sasa ukikutana na mtu ambaye ana nguvu kubwa ya pesa na akili tena wengine wanakuwa wanabarikiwa unakuta pia ana nguvu kubwa ya ushawishi kwa watu wanao mzunguka na wananchi kwa ujumla, kukutoa kwenye nafasi yako au kukutawala linakuwa ni suala la muda tu mheshimiwa”

“Mhhhhh, mhhhhhhh umenipa jambo kubwa sana ambalo sikulifikiria kwa wakati huu, unahisi ni kitu gani unatakiwa kukifanya unapo fanikiwa kuwapata au kuwajua watu wa namna hiyo?”

“Hapo ndipo unatakiwa kuyafanya maamuzi kama uliyo yachukua kwa Pandei Santo mheshimiwa”

“Hahahahah hahahaha hahaha naomba ukapumzike, kwa leo inatosha. Kuna namna unanifanya nijivunie sana kuwa na mshauri kama wewe hakika sikufanya makosa kukuweka karibu yangu, kwa sasa hili jambo niachie mimi wewe waweza kwenda ila kabla ya kufanya hivyo peleka taarifa kwa watu wangu wawasiliane na mkurugenzi wa usalama wa taifa apewe maagizo kwamba nahitaji kuonana naye ndani ya masaa mawili yajayo. Unaweza kwenda, asante sana kwa ushauri wako” mheshimiwa raisi alicheka sana kwani alikuwa amefunguliwa akili kwa jambo ambalo alihisi lilikuwa linamuumiza kichwa wakati alikuwa na uwezo wa kulimaliza kwa njia rahisi sana.

Mzee huyo ambaye alikuwa mshauri wake, alitoka mpaka nje ya ofisi hiyo, aligeuka na kuangalia mlango wa kuingilia ndani kabisa ya ofisi hiyo kisha akatingisha kichwa kwa masikitiko sana, baada ya hapo aliondoka kwenda kuyafanyia kazi maagizo ya bosi wake na kisha arudi nyumbani kwake ambako alitoka kwa muda mfupi ambao ulikuwa umepita.


Ilikuwa ni usiku sana tayari lakini hiyo haikuwa sababu ya kumfanya aukatae wito wa bosi wake Ikulu, Mr Lingson Mfwomi ambaye ndiye alikuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa wa nchi ya Tanzania aliweza kufika Ikulu kama alivyo agizwa, hakuelewa majira ya usiku wote huo kiongozi wake alikuwa anahitaji nini ambacho alishindwa kumwambia kwenye simu au kuhitaji kuongea naye hata siku ya kesho yake? Hakujua ila huenda uwepo wake hapo kwa wakati huo ungemfanya aelewe vizuri sana. Alinyoosha moja kwa moja kuelekea kwenye ofisi kiuu ya raisi ambapo aliongozana na walinzi wa raisi walio mpa maelekezo juu ya kusubiriwa kwake na bosi wake.

“Heshima yako kiongozi wangu” alimpa heshima yake mheshimiwa raisi huku akiwa anaketi kwenye kiti chake ambacho mgeni yeyote angekikalia anapo ingia humo ndani.

“Lingson nyumbani kwema?”

“Kwema kiongozi japo wasiwasi wangu mkubwa ni juu yako tu maana sio kawaida sana kuniita ghafla hivi bila taarifa ya awali na leo nimeshangaa natafutwa na watu wengine wakati huwa unanipigia wewe mwenyewe moja kwa moja pale unapokuwa unauhitaji uwepo wangu hapa!”

“Ni kweli kabisa, mpaka nawaagiza watu wengine basi ujue kwamba mimi sipo sawa na ndiyo maana nikakuhitaji uje hapa wakati huu ili tujue tunafanya nini maana wewe ndiye kiongozi wa usalama namba moja ndani ya nchi hii” mheshimiwa aliongea akiwa anaifungua droo yake na kuitoa bahasha moja ambayo aliifungua na kumrushia mkurugenzi huyo. Bahasha hiyo ilikuwa inaonyesha kama mfumo wa uongozi kwenye taasisi fulani lakini uliandikwa kwa code maalumu ambao ilikuwa ni ngumu sana kuutafsiri kiwepesi mpaka mtu akupe maelekezo yake.

“Mheshimiwa unajaribu kumaanisha nini kunipatia hii?”

“Huo ni mfumo mzima wa namna Ikulu ilivyo, nina uhakika unaujua vyema. Baada ya ofisi yangu ofisi ambayo ipo karibu hapo kwenye huo mchoro ni ya makamu wa raisi kisha ni ofisi yako. Unajua maana yake?”

“Ndiyo mheshimiwa”

“Inamaanisha nini?”

“Ina maanisha kwamba mimi ni mtu wa karibu zaidi ambaye natakiwa kuhakikisha kwamba ofisi yako, Ikulu pamoja na nchi kwa ujumla ipo salalama wakati wote”

“Safi sana, watu wangu mnanifurahisha sana kwa sababu nimewaweka watu ambao mna uwezo mkubwa sana wa kuweza kufikiria na kuweza kuyachanganua mambo” aliongea mheshimiwa kisha akaendelea;

“Unajua kwenye mifumo ya ulinzi wa nchi, kuna mambo mengi sana ambayo yanawekwa ili mfumo mmoja unapo shindwa kufanya kazi vizuri basi mfumo mwingine unasaidia kuweza kuziba hilo kosa, hapo ndipo unapata jeshi la polisi, unalipata jeshi la nchi la kujenga taifa, utakutana na jeshi la majini, na mengine lakini hayo yote yanategemea zaidi idara yako ya usalama wa taifa. Ni rahisi sana kwa wewe hapo kwenda jeshini kumchukua mtu ambaye unahisi anafaa na kumleta kwenye ofisi yako ila huwezi ukakuta mtu anatoka kwako anaenda sehemu nyingine ya ulinzi kama jeshi la kujenga taifa, jeshi la wananchi au hata jeshi la polisi isipokuwa kama kuna kazi maalumu ambayo inampeleka kule kwa wakati huo”

“Hiyo inamaanisha idara ya usalama wa taifa ndiyo taasisi nyeti zaidi kuhakikisha nchi inakuwa salama, ndiyo taasisi ambayo inaendesha nchi na ndiyo taasisi ambayo nchi inaitegemea zaidi kwenye kila sekta kuanzia kwenye uchumi, kisiasa, kidiplomasia lakini hata kiteknolojia pia kwani tunategemea taarifa zenu ambazo mtazikusanya ndani na nje ya nchi ndizo tuzitumie kuweza kuijenga nchi yetu”

“Wakati mimi nasoma pale Tabora boys, kuna waalimu pale sikuwahi kujua kama ni majasusi na walishafanya kazi nyingi sana za nje ya nchi ambazo zingine zilikuwa ni hatari sana ila siku ambayo nilikuja kujua hilo jambo nilivutiwa sana na hii idara baada ya kugundua kumbe huwa wapo pale ili kuwatafuta wanafunzi ambao wanafaa kabisa kuingia kwenye idara ya usalama wa taifa na kuja kulikomboa taifa baadae na ndio wengine mpo huko pamoja na vijana wako”

“Umenielewa Mr Lingson?” mheshimiwa raisi aliyatoa maelezo mengi sana lakini akakatisha na kuuliza swali ambalo bila shaka hata mkurugenzi lilimuacha kinywa wazi

“Yote uliyo yaongea ni sahihi sana mheshimiwa lakini sijajua pointi yako ni ipi hasa mpaka uyaongee yote hayo?”

“Maana yangu ni kwamba wewe ni moja kati ya watu wa mhimu sana ambao mimi nawategemea kwenye taifa hili kwa sababu wewe ndiye ambaye una mamlaka makubwa zaidi ya ulinzi ambayo nimekupa. Kuna watu huwa wanahisi mkuu wa majeshi pamoja na kapteni wa jeshi ndiyo ambao wana nguvu sana kwenye nchi kuhusu ulinzi ila sio kweli, huyo hata akihitaji kuipindua nchi kama hana mawasiliano mazuri na wewe hapo basi hana uwezo wa kufanya hivyo. Kwahiyo nahitaji sana uujue umuhimu wako kwanza kwenye hiyo nafasi ambayo nimekuweka japo ipo chini ya ofisi yangu ila wewe ni mtu mhimu sana kwangu”

“Kuna hili sakata la uchaguzi ambalo linaenda kutokea siku za usoni hapa kwanza nahitaji ule kiapo mbele yangu kwamba hautafanya jambo lolote lile la kijinga na utakuwa makini sana kuhakikisha mambo yangu yanaenda kama nilivyo panga mimi na utafuata yale yote ambayo mimi nayasema” mheshimiwa alimeza mate na kuendelea akiwa amemkazia macho mkurugenzi.

“Nahisi kuna mambo ambayo yanaendelea chini chini kuhusu hili sakata sasa nahitaji nizipate taarifa zote na kila hatua ambayo inapigwa hususani na washindani wangu na kila siku niwe naipata ripoti ya mambo yao yote, ratiba zao zote pamoja na mambo yote ambayo yanaendelea kwenye familia zao” alitulia baada ya kuongea hayo.

“Mheshimiwa mimi nilisha apa kufanya yale ambayo unayahitaji, wewe ndiye ambaye uliniweka mimi kwenye hii nafasi na wewe ndiye ambaye una uwezo wa kunitoa hivyo nitayatoa hata maisha yangu kukusaidia wewe kwa kila hali. Muda wowote nipo kwa ajili yako hivyo unaweza ukanituma lolote lile na nikalitekeleza kwa namna unavyo hitaji wewe. Kama hilo ndilo linakutatiza basi limeisha kiongozi wangu, kesho tu asubuhi naamka nalo ofisini kwangu linaanza kufanyiwa kazi” maelezo ya mkurugenzi yalimfanya atabasamu na kumimina pombe kwenye bilauri mbili ambapo moja alimpa kiongozi huyo.

“Sisi tuna historia kubwa sana ndugu yangu, historia ya baba zetu. Nakumbuka historia ya baba yangu kumsaidia baba yako wakiwa jeshini ambapo bila baba yangu huenda baba yako angekufa na wewe usinge zaliwa kabisa hivyo najisikia fahari sana na mimi pia kuja kukusaidia kwa baadae kisha na wewe unaenda kuwa msaada mkubwa kwangu. Haujawahi kuniangusha kwenye majukumu ambayo nakutuma na ndiyo sababu ambayo inanifanya niendelee kukuamini zaidi na kukupa hiyo nafasi hivyo nitafurahi kama msaada wa baba yangu kwa familia yako na msaada wangu kwako ukaulipa kwa moyo wote. Nahitaji ufanye kazi yangu kama ninavyokutuma ili tubakie Ikulu kwani hatujui mtu mwingine ambaye ataingia atakuwa na upepo gani, kama tukicheza vibaya hata wewe unaweza ukaipoteza hiyo nafasi yako na ukaishia kupewa hata kesi ambazo haukuhusika nazo ukaishia jela. Unaweza kwenda mr Lingson” kiongozi huyo aliongea kwa msisitizo sana kisha akamruhusu mwanaume huyo aondoke bila kutoa jibu la mwisho.

Mr Lingson Mfwomi aliinama kutoa heshima kabla ya kutoka humo ndani, baada ya hapo alitoka na kubaki kwenye mshangao mkubwa sana maana ilikuwa ni ghafla sana kuambiwa maneno mazito kama hayo na kiongozi wake, alijua kabisa kulikuwa na mambo ambayo hayakuwa sawa hata bosi wake hakuonekana kabisa kuwa sawa hivyo aliondoka kichwa chake kikiwa na mashaka mengi sana. Kwanini raisi alikuwa anasisitiza sana kulindwa yeye na sio nchi au ofisi yake? Maana yake alikuwa anajijali yeye zaidi kuliko maslahi ya nchi? Alisikitika na kutoweka hilo eneo haraka sana.

Ukurasa wa tano unafika mwisho.

Febiani Babuya.
FB_IMG_1704516790884.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA KWANZA
Ndani ya ofisi moja kubwa sana, alikuwa anaonekana tajiri mmoja ambaye bila shaka umri wake ulikuwa umeenda kiasi cha kutosha. Mzee huyo mwenye kitambi cha wastani ambacho kiliashiria ukwasi ambao alikuwa nao, alikuwa ameketi kwenye meza yake ghorofa ya juu zaidi ndani ya ofisi yake hiyo.

Meza yake upande wa mbele ilikuwa imeandikwa CHAIRMAN kwa maandishi makubwa kisha likafuatia jina lake ambao lilisomeka kama Apson Limo, bila shaka yeye ndiye ambaye alikuwa mmliki wa hizo ofisi kama sio kampuni kwa namna ilivyokuwa inaonekana humo ndani. Ofisi ilikuwa imepambwa kwa vitu vya gharama sana huku ukutani kukiwa na picha kubwa mbili ambazo zilionekana kwa usahihi sana.

Kulikuwa na picha moja ya kawaida ya muasisi wa taifa la Tanzania hayati Julius Kambarage Nyerere lakini pia upande wake wa juu palikuwa na picha kubwa sana ambayo bila shaka ilikuwa ni ya familia. Kwenye picha hiyo alikuwa anaonekana yeye, mama mmoja ambaye bila shaka alikuwa ni mkewe lakini pia walikuwa wanaonekana watoto watano ambapo kati ya hao watoto watano, mmoja tu pekee ndiye alikuwa ni mtoto wa kiume kati yao. Ni picha ambayo ilikuwa inaonyesha namna familia hiyo ilivyokuwa kwenye furaha kubwa sana maana wote walikuwa ndani ya tabasamu zito mno ambalo usingeweza hata kujisumbua kulielezea kwani mtu angeiona tu picha hiyo angeelewa ni kwa namna gani familia hiyo ilikuwa kwenye hiyo furaha kubwa.

Upande wa mkono wa kulia mwa ofisi hiyo ukutani, kulikuwa na maneno makubwa ambayo yalikuwa yanang’aa sana yakiwa yapo chini ya nembo ya kampuni hiyo yakiwa yanasomeka LIMO INVESTMENTS. Ofisi hiyo kubwa ilikuwa pia imenakshiwa kwa vito vya thamani sana ikiwemo na samani za kutosha huku ikiwa na sehemu nzuri sana ya wageni kuweza kukaa na sehemu ya kufanyia mazungumzo ambayo yangekuwa ya mhimu na kumfanya mhusika aongee na tajiri huyo moja kwa moja.

Mzee huyo akiwa ametulia kwenye hilo eneo anaangalia kwa umakini sana jina la kampuni yake ukutani na kuwaza namna alivyoweza kutoka mbali na kampun hiyo mpaka ikaja kusimama vyema na kuwa moja kati ya makampuni makubwa sana nchini, simu yake ya mezani ilimshtua kutoka kwenye mawazo baada ya kuanza kupiga kelele kwa nguvu, akaipokea.

“Mruhusu aingie” ni kauli moja tu ambayo aliitamka bila shaka aliipokea simu ya ugeni kutoka kwa katibu wake ambaye alimpa ruhusa kuweza kumruhusu mtu ambaye alikuwa amefika hapo. Ndani ya muda mfupi mlango ulifunguliwa, aliingia mwanaume mmoja ambaye naye umri ulikuwa umemtupa mkono kidogo akiwa ndani ya suti ya gharama mno na fimbo yake mkononi bila shaka.

“Karibu sana Mr Mafupa” alimkaribisha mgeni wake huku akiwa ananyanyuka kwenye kiti chake na kumpa mtu huyo mkono na ilionekana kwamba walikuwa wakijuana sana.

“Nadhani sio waafrika wote ambao hawajastaarabika, kuna watu mpo safi sana na huo ndio utamaduni wetu waafrika bwana lazima tusalimiane kwanza hata kama hatupo sawa” Mr Mafupa alijibu naye huku akiwa anaukutanisha mkono wake na mheshimiwa Apson Limo.

“Ujinga wa mtu mmoja usiujumlishe kwa waafrika wote, sio kawaida sana wewe kuja hapa, nilivyo ipata taarifa kwamba unahitaji kuniona nilishtuka kidogo kwamba kwanini usingesubiri sehemu nyingine nje na hapa tukakutana ila nikaamua kukubali kwa sababu nilijua huenda una shida ya mhimu sana” mr Apson aliongea akiwa anaketi baada ya kuhakikisha pia mgeni wake ameketi chini kwa ajili ya mazungumzo.

“Mhhhh sehemu yoyote ile inafaa kwa mazungumzo hususani kwa wanasiasa na wafanya biashara kama mimi na wewe, vipi mwanao alisharudi kutoka masomoni? Maana ni muda sana naskia yupo nje ya nchi”

“Sio muda anarudi nadhani kwa sasa amemaliza masomo yake”

“Kwahiyo anakuja kumsaidia baba yake kwenye mambo ya kampeni? Maana ndiye mtoto wa pekee wa kiume uliye naye”

“Ni vizuri kama ungeenda moja kwa moja kwenye maada ambayo imekuleta hapa sidhani kama mambo ya familia yangu yanakuhusu sana au yana umuhimu kwa hapa tulipo”

“Sawa ila yanaweza kuwa na umuhimu mkubwa sana kwa hapo baadae ndiyo maana nakuuliza usidharau sana. Lengo la mimi kuja mpaka hapa kwenye ofisi yako kuna makubaliano ambayo nahitaji tuyafanye mimi na wewe. Ni makubaliano ya mhimu sana ambayo yanakubidi wewe ufanye maamuzi ya kiume, narudia tena ni ya mhimu sana mr Apson”

“Nenda moja kwa moja kwenye hoja ya msingi acha kuzunguka mr Mafupa”

“Nahitaji ujitoe kwenye mbio za kugombea uraisi”

“Hahahaha Mr Mafupa nadhani uliko toka umelewa sio? Hivi unajua hata kuja hapa nimekukubalia tu kwa sababu nakuheshimu sana, huu muda mimi na wewe ni wapinzani sidhani kama ni sahihi kukutana kutana kirahisi sana namna hii maana wananchi wakijua wanaweza kuanza kuwaza mambo mabaya, nadhani kama hauna jambo la mhimu la kuongea na mimi ni vizuri zaidi kama utanyanyuka na kutoka nje ya ofisi yangu kisha usije ukarudi tena hapa maana nitafanya kama sijawahi kukufahamu”

“Najua mr Apson, najua kwamba ndani yako kuna moto unawaka sana hususani pale ambapo unakuwa unaiwaza ile Ikulu, unawaza namna watu wanavyo yasimulia maisha ya pale ukiwa kama ndiye kiongozi mkuu maana hata baadhi ya vikao vingi na mialiko mikubwa ulikuwa unaipata ila nimekuja kukuomba kistaarabu sana achia hiyo nafasi na awekwe mtu ambaye ni dhaifu na hawezi kuniyumbisha kwa sababu mimi nahitaji kuingia pale Ikulu kisha kuna makubaliano ambayo mimi na wewe tutaingia hata nikiingia Ikulu utakuwa kama mkono wangu wa kulia”

“Makubaliano yapi hayo Mr Mafupa ambayo unahisi yatanishawishi mimi kukubali kuwasaliti wananchi wangu ambao wameniamini na kuniruhusu mimi kuingia Ikulu na kuahidi kunipa kura zao za ndiyo na kwa sababu ipi hasa?”

“Kuna mpango ambao nimeuandaa, sababu tutatengeneza ugonjwa feki na kudai kwamba utakuwa nje ya nchi hospitali kwa mwaka mzima ambapo uchaguzi utakuwa umekamilika na hauwezi kuchaguliwa mtu ambaye upo hospitali hivyo watatakiwa kusubiri mpaka upone. Mwaka ukiisha mimi nitakuwa tayari Ikulu na wewe nitakuteua uwe makamu wangu kwa kuwaahidi wananchi kwamba utaingia Ikulu kama wanavyo hitaji kwenye uchaguzi ambao unafuata huku wakihisi kwamba hakuna tatizo baina yetu ni upendo tu umetawala ndiyo maana nimekupa nafasi kubwa ya umakamu wa raisi na hayo mambo inabidi uyathibitishe wewe mwenyewe kwenye vyombo vya habari. Ukikubali tu kutoka kwenye hiyo nafasi, utaingiziwa bilioni mia moja kwenye akaunti yako maana mimi najua namna ya kuzirudisha nikiingia Ikulu kisha tutaingia mikataba ya kibiashara mimi na wewe ambayo itatusaidia kutengeneza pesa kadri tutakavyo na kutufanya kuwa miongoni mwa watu matajiri sana hapa Afrika”

“Kwahiyo unahisi bilioni mia moja na hiyo mikataba ndiyo itanifanya mimi niuze uzalendo wangu na kuwasaliti wananchi wangu na kuuza utu wangu? Mr Mafupa tangu unatoka kwako ulitakiwa kuwaza kwa umakini aina ya mtu ambaye unaenda kuongea nae. Kwahiyo umeona kwamba mimi nina njaa sana na unaweza kuninunua kwa hiyo pesa? Umekosea sana, nitafanya kama hili hujaliongea naomba utoke kwenye ofisi yangu”

“Koh, koh, Mr Apson mimi huwa ni mara chache sana kumuomba mtu jambo ambalo naweza kulifanya hata kwa lazima bila mapenzi yake, mpaka nakuja kukuomba hapa ni kwa sababu nimeamua kukuheshimu kama rafiki tu japo hatujawahi kuwa karibu. Mimi Ikulu naingia kwa gharama yoyote ile na haujui kwanini naihitaji sana ile Ikulu. Hivi umewaza labda kwamba kwanini nimekubali kuingia kwenye kinyang’anyiro na mheshimiwa raisi ambaye yupo madarakani wakati nipo naye chama kimoja? Ungejua hayo basi hiyo nafasi ungeiachia mwenyewe bila kulazimishwa. Unaongelea uzalendo kwenye nchi hii ambayo wananchi wakipewa hata noti moja tu wanauza utu wao? Uzalendo upi labda ambao unakufanya ujione wewe ndiye ulizaliwa kwa ajili ya hii nchi? Jambo la msingi zaidi ambalo wewe unapaswa kuliwaza sana kabla ya kufanya maamuzi yoyote yale ni familia ndugu yangu. Nitajisikia vibaya sana kama itafikia hatua ya kunilazimu niingie mpaka upande wa familia wakati una nafasi ya kufanya maamuzi sahihi, una wanao ambao ni waz…….”

“Stooop! mjinga wewe, una jeuri gani ya kuiongelea familia yangu mbele yangu kirahisi sana namna hiyo? Nitakupiga risasi nikuzike humu humu ndani kwangu. Nisije nikakusikia tena ukiwa unaitaja familia yangu kirahisi sana namna hiyo, mimi siyo kama wewe ambaye unashinda na hao wanawake ambao unawabadilisha kila siku kama nguo kwenye makasino. Tena ukija kutaja neno familia kwangu basi nitakuua hapo hapo” alikuwa amesimama mr Apson akiwa ameitoa bastola yake amemnyooshea mwanaume mwenzake huyo ambaye alionekana kwamba alikuwa ni mgombea mwenzake kwenye nafasi ya uraisi wa nchi ya Tanzania. Mwenzake huyo baada ya kushindwa kumshawishi aliamua kuitumia familia kama ngao ya kumdhoofisha na ndiyo sababu ya mr Apson kumnyooshea bastola mr Mafupa kwani kwake familia ndilo lilikuwa jicho lake aliipenda mno. Mr Mafupa alijikohoza kidogo na kumfungukia;

“Huo uwezo wa wewe kunipiga risasi mimi hauna kwa sababu watu wameniona naingia hapa hivyo nisipo toka lazima wewe ndiye utakuwa mhusika namba moja na kesho tu asubuhi magazeti na vyombo vya habari vitaandika kwamba umemuua mgombea mwenzako ili uingie Ikulu, unadhani nani atakuamini tena? Nani atatamani kukupigia kura tena wakati wewe ni muuaji na una tamaa ya madaraka? Hahahaha utakuwa unaisubiria jela wakati huo na familia yako haitakuwa na msaada wowote ule hivyo huo ubavu hauna wa kuiacha familia yako maana unaipenda mno, mpaka hapo nipo salama na hauwezi kunifanya lolote” alitulia kidogo kuacha maneno yamuingie vyema mr Apson kisha akaendelea.

“Mimi nimekuomba kistaarabu lakini umeishia kunidharau, unajua kuna maongezi ya wanaume yanatakiwa kufanywa kiume hata maamuzi yake yanatakiwa kwenda kiume pia na hivyo ndivyo siasa inavyotakiwa kuwa lakini kwa sababu hautaki kwenda kistaarabu basi mimi nitakuonyesha namna sahihi ya kuweza kuyafanya maamuzi magumu ukiwa hauna namna na huenda kwa wakati huo hautakuwa na namna zaidi ya kutoa kilio. Likumbuke neno familia kwenye kichwa chako mr Apson na ujue tu kwamba nitarudi na kwa sasa sitarudi kukubembeleza bali nitarudi na kukufanya ulie huku ukija mwenyewe mbele yangu kunipigia magoti na kuniomba kwamba umekubali masharti yangu ila huenda utakuwa umechelewa tayari”

“Out” aliongea kwa sauti kali yenye uchungu sana baada ya mr Mafupa kumaliza kujigamba mbele yake na kuitishia familia yake huku akiwa anaikoki bastola yake, mr Mafupa alitabasamu na kutoka humo ndani kwa dharau kubwa mno.

Mr Apson alipigiza bastola yake chini kwa hasira sana huku akiwa anahema kwa nguvu mno, aligeukia ukutani na kuangalia picha ya familia yake ambayo ilikuwa kwenye tabasamu zuri sana, moyo wake ulizidi kumuenda mbio isivyo kawaida. Alikusanya begi lake na kutoka haraka sana humo ndani, alitaka kuwahi nyumbani kwanza aione familia yake maana vile vitisho ambavyo alipewa pale alihisi huenda familia yake ilikuwa kwenye matatizo huku akiwa anaendelea kumpigia simu mkewe ambaye naye hakuwa akipokea basi alizidisha wasiwasi sana kwenye nafsi yake, siasa ilianza kumtokea puani mapema sana.

Ukurasa wa kwanza naweka nukta hapa. Niseme tu karibu sana tuweza kujumuika kwa pamoja ndani ya simulizi hii ili tuweze kujua kwamba imetuandalia nimi haswa ndani yake. Unataka kujua hilo salata la uchaguzi linahusiana vipi na hizo pesa kwenye damu? Basi usibanduke twende sawa.

Kwenye kalamu nipo mwenyewe, mwapenda kuniita Bux the storyteller lakini jina langu waweza kuniita;

FEBIANI BABUYA.

Wasalaam.View attachment 2818483

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Ehe
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA TANO
“Unajua wewe ndiye mtu namba moja ndani ya nchi hii, wewe ndiye mtu mwenye nguvu zaidi ndani ya taifa hili lakini pia wewe ndiye mtu ambaye kauli yako ina nguvu na maamuzi ya mwisho ndani ya hii nchi. Lakini ukiacha hayo yote jambo la hatari zaidi kwako ni uwepo wa watu wenye nguvu zaidi ndani ya nchi yako nadhani hiyo ndiyo inaweza kuwa hatari kubwa zaidi kwako” Mzee huyo alitamka sentensi fupi ambayo ilikuwa na maana kubwa sana na alikuwa na uhakika kwamba mheshimiwa lazima angeielewa vizuri tu.

“Una maanisha nini kusema hivyo?”

“Mheshimiwa kitu ambacho kinampa jeuri mtu yeyote yule ni nguvu, mtu anapokuwa na nguvu kubwa sana anakuwa anajihisi kwamba yeye anaweza kufanya jambo lolote lile na hakuna mtu yeyote yule wa kuweza kumzuia wala kitu chochote kile cha kutokea kati kati na kuweza kumuyumbisha hivyo anaanza kujikuta hata mamlaka haziheshimu kwani anaamini hata hao ambao wapo kwenye mamlaka anaweza kuwaendesha atakavyo yeye na mgawanyiko huwa unaanzia hapo” aliongea na kuhitaji kuendelea lakini alitulia baada ya kuona kama mheshimiwa anahitaji kuongea, hakuwa tayari kumzuia bosi wake

“Unataka kusema kwamba?”

“Mheshimiwa nadhani unamkumbuka vizuri Mr Pandei Santo”

“Ndiyo namkumbuka vizuri sana, anahusikaje na swali langu?”

“Yule bwana ni wewe mwenyewe ndiye uliuondoa utawala wake kwa ushauri wangu mimi hapa, nadhani unakumbuka baada ya kuwa na pesa nyingi sana alianza kuleta jeuri hadharani kwa kuhisi kwamba mamlaka zote zipo chini yake na anaweza kuyafanya yale ambayo anajisikia yeye mwisho wa siku akaanza kukukosea heshima mpaka wewe tena hadharani lakini kwa kile ambacho ulimfanyia kilitosha kurudisha heshima yako na kuitoa hatari ambayo alikuwa anaitengeneza kwako. Sasa kwenye nchi wakiwepo watu kama wale tena wakiwa wengi linakuwa sio jambo zuri kwani muda wowote wanaweza kufanya jambo lolote kwa sababu wanakuwa na pesa na pesa inaweza kuinunua nafsi ya mtu yeyote yule”

“Mbali na hilo jambo ambalo ni hatari zaidi kwa nafasi yako ni pale ambapo wanakuwepo watu wenye uwezo mkubwa zaidi kichwani kukuzidi wewe halafu hawapo upande wako. Ni vyema kama kuna watu wana kuzidi uwezo wewe hakikisha wanakuwa upande wako na wanakuwa chini yako hivyo wewe unazitumia akili zao kuweza kukamilisha mambo yako. Akili ndiyo inaweza kumuendesha mtu, akili ndiyo inaweza ikakuweka kwenye hicho kiti chako na akili ndiyo inaweza kukufanya ukatolewa kwenye hiyo nafasi yako. Sasa ukikutana na mtu ambaye ana nguvu kubwa ya pesa na akili tena wengine wanakuwa wanabarikiwa unakuta pia ana nguvu kubwa ya ushawishi kwa watu wanao mzunguka na wananchi kwa ujumla, kukutoa kwenye nafasi yako au kukutawala linakuwa ni suala la muda tu mheshimiwa”

“Mhhhhh, mhhhhhhh umenipa jambo kubwa sana ambalo sikulifikiria kwa wakati huu, unahisi ni kitu gani unatakiwa kukifanya unapo fanikiwa kuwapata au kuwajua watu wa namna hiyo?”

“Hapo ndipo unatakiwa kuyafanya maamuzi kama uliyo yachukua kwa Pandei Santo mheshimiwa”

“Hahahahah hahahaha hahaha naomba ukapumzike, kwa leo inatosha. Kuna namna unanifanya nijivunie sana kuwa na mshauri kama wewe hakika sikufanya makosa kukuweka karibu yangu, kwa sasa hili jambo niachie mimi wewe waweza kwenda ila kabla ya kufanya hivyo peleka taarifa kwa watu wangu wawasiliane na mkurugenzi wa usalama wa taifa apewe maagizo kwamba nahitaji kuonana naye ndani ya masaa mawili yajayo. Unaweza kwenda, asante sana kwa ushauri wako” mheshimiwa raisi alicheka sana kwani alikuwa amefunguliwa akili kwa jambo ambalo alihisi lilikuwa linamuumiza kichwa wakati alikuwa na uwezo wa kulimaliza kwa njia rahisi sana.

Mzee huyo ambaye alikuwa mshauri wake, alitoka mpaka nje ya ofisi hiyo, aligeuka na kuangalia mlango wa kuingilia ndani kabisa ya ofisi hiyo kisha akatingisha kichwa kwa masikitiko sana, baada ya hapo aliondoka kwenda kuyafanyia kazi maagizo ya bosi wake na kisha arudi nyumbani kwake ambako alitoka kwa muda mfupi ambao ulikuwa umepita.


Ilikuwa ni usiku sana tayari lakini hiyo haikuwa sababu ya kumfanya aukatae wito wa bosi wake Ikulu, Mr Lingson Mfwomi ambaye ndiye alikuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa wa nchi ya Tanzania aliweza kufika Ikulu kama alivyo agizwa, hakuelewa majira ya usiku wote huo kiongozi wake alikuwa anahitaji nini ambacho alishindwa kumwambia kwenye simu au kuhitaji kuongea naye hata siku ya kesho yake? Hakujua ila huenda uwepo wake hapo kwa wakati huo ungemfanya aelewe vizuri sana. Alinyoosha moja kwa moja kuelekea kwenye ofisi kiuu ya raisi ambapo aliongozana na walinzi wa raisi walio mpa maelekezo juu ya kusubiriwa kwake na bosi wake.

“Heshima yako kiongozi wangu” alimpa heshima yake mheshimiwa raisi huku akiwa anaketi kwenye kiti chake ambacho mgeni yeyote angekikalia anapo ingia humo ndani.

“Lingson nyumbani kwema?”

“Kwema kiongozi japo wasiwasi wangu mkubwa ni juu yako tu maana sio kawaida sana kuniita ghafla hivi bila taarifa ya awali na leo nimeshangaa natafutwa na watu wengine wakati huwa unanipigia wewe mwenyewe moja kwa moja pale unapokuwa unauhitaji uwepo wangu hapa!”

“Ni kweli kabisa, mpaka nawaagiza watu wengine basi ujue kwamba mimi sipo sawa na ndiyo maana nikakuhitaji uje hapa wakati huu ili tujue tunafanya nini maana wewe ndiye kiongozi wa usalama namba moja ndani ya nchi hii” mheshimiwa aliongea akiwa anaifungua droo yake na kuitoa bahasha moja ambayo aliifungua na kumrushia mkurugenzi huyo. Bahasha hiyo ilikuwa inaonyesha kama mfumo wa uongozi kwenye taasisi fulani lakini uliandikwa kwa code maalumu ambao ilikuwa ni ngumu sana kuutafsiri kiwepesi mpaka mtu akupe maelekezo yake.

“Mheshimiwa unajaribu kumaanisha nini kunipatia hii?”

“Huo ni mfumo mzima wa namna Ikulu ilivyo, nina uhakika unaujua vyema. Baada ya ofisi yangu ofisi ambayo ipo karibu hapo kwenye huo mchoro ni ya makamu wa raisi kisha ni ofisi yako. Unajua maana yake?”

“Ndiyo mheshimiwa”

“Inamaanisha nini?”

“Ina maanisha kwamba mimi ni mtu wa karibu zaidi ambaye natakiwa kuhakikisha kwamba ofisi yako, Ikulu pamoja na nchi kwa ujumla ipo salalama wakati wote”

“Safi sana, watu wangu mnanifurahisha sana kwa sababu nimewaweka watu ambao mna uwezo mkubwa sana wa kuweza kufikiria na kuweza kuyachanganua mambo” aliongea mheshimiwa kisha akaendelea;

“Unajua kwenye mifumo ya ulinzi wa nchi, kuna mambo mengi sana ambayo yanawekwa ili mfumo mmoja unapo shindwa kufanya kazi vizuri basi mfumo mwingine unasaidia kuweza kuziba hilo kosa, hapo ndipo unapata jeshi la polisi, unalipata jeshi la nchi la kujenga taifa, utakutana na jeshi la majini, na mengine lakini hayo yote yanategemea zaidi idara yako ya usalama wa taifa. Ni rahisi sana kwa wewe hapo kwenda jeshini kumchukua mtu ambaye unahisi anafaa na kumleta kwenye ofisi yako ila huwezi ukakuta mtu anatoka kwako anaenda sehemu nyingine ya ulinzi kama jeshi la kujenga taifa, jeshi la wananchi au hata jeshi la polisi isipokuwa kama kuna kazi maalumu ambayo inampeleka kule kwa wakati huo”

“Hiyo inamaanisha idara ya usalama wa taifa ndiyo taasisi nyeti zaidi kuhakikisha nchi inakuwa salama, ndiyo taasisi ambayo inaendesha nchi na ndiyo taasisi ambayo nchi inaitegemea zaidi kwenye kila sekta kuanzia kwenye uchumi, kisiasa, kidiplomasia lakini hata kiteknolojia pia kwani tunategemea taarifa zenu ambazo mtazikusanya ndani na nje ya nchi ndizo tuzitumie kuweza kuijenga nchi yetu”

“Wakati mimi nasoma pale Tabora boys, kuna waalimu pale sikuwahi kujua kama ni majasusi na walishafanya kazi nyingi sana za nje ya nchi ambazo zingine zilikuwa ni hatari sana ila siku ambayo nilikuja kujua hilo jambo nilivutiwa sana na hii idara baada ya kugundua kumbe huwa wapo pale ili kuwatafuta wanafunzi ambao wanafaa kabisa kuingia kwenye idara ya usalama wa taifa na kuja kulikomboa taifa baadae na ndio wengine mpo huko pamoja na vijana wako”

“Umenielewa Mr Lingson?” mheshimiwa raisi aliyatoa maelezo mengi sana lakini akakatisha na kuuliza swali ambalo bila shaka hata mkurugenzi lilimuacha kinywa wazi

“Yote uliyo yaongea ni sahihi sana mheshimiwa lakini sijajua pointi yako ni ipi hasa mpaka uyaongee yote hayo?”

“Maana yangu ni kwamba wewe ni moja kati ya watu wa mhimu sana ambao mimi nawategemea kwenye taifa hili kwa sababu wewe ndiye ambaye una mamlaka makubwa zaidi ya ulinzi ambayo nimekupa. Kuna watu huwa wanahisi mkuu wa majeshi pamoja na kapteni wa jeshi ndiyo ambao wana nguvu sana kwenye nchi kuhusu ulinzi ila sio kweli, huyo hata akihitaji kuipindua nchi kama hana mawasiliano mazuri na wewe hapo basi hana uwezo wa kufanya hivyo. Kwahiyo nahitaji sana uujue umuhimu wako kwanza kwenye hiyo nafasi ambayo nimekuweka japo ipo chini ya ofisi yangu ila wewe ni mtu mhimu sana kwangu”

“Kuna hili sakata la uchaguzi ambalo linaenda kutokea siku za usoni hapa kwanza nahitaji ule kiapo mbele yangu kwamba hautafanya jambo lolote lile la kijinga na utakuwa makini sana kuhakikisha mambo yangu yanaenda kama nilivyo panga mimi na utafuata yale yote ambayo mimi nayasema” mheshimiwa alimeza mate na kuendelea akiwa amemkazia macho mkurugenzi.

“Nahisi kuna mambo ambayo yanaendelea chini chini kuhusu hili sakata sasa nahitaji nizipate taarifa zote na kila hatua ambayo inapigwa hususani na washindani wangu na kila siku niwe naipata ripoti ya mambo yao yote, ratiba zao zote pamoja na mambo yote ambayo yanaendelea kwenye familia zao” alitulia baada ya kuongea hayo.

“Mheshimiwa mimi nilisha apa kufanya yale ambayo unayahitaji, wewe ndiye ambaye uliniweka mimi kwenye hii nafasi na wewe ndiye ambaye una uwezo wa kunitoa hivyo nitayatoa hata maisha yangu kukusaidia wewe kwa kila hali. Muda wowote nipo kwa ajili yako hivyo unaweza ukanituma lolote lile na nikalitekeleza kwa namna unavyo hitaji wewe. Kama hilo ndilo linakutatiza basi limeisha kiongozi wangu, kesho tu asubuhi naamka nalo ofisini kwangu linaanza kufanyiwa kazi” maelezo ya mkurugenzi yalimfanya atabasamu na kumimina pombe kwenye bilauri mbili ambapo moja alimpa kiongozi huyo.

“Sisi tuna historia kubwa sana ndugu yangu, historia ya baba zetu. Nakumbuka historia ya baba yangu kumsaidia baba yako wakiwa jeshini ambapo bila baba yangu huenda baba yako angekufa na wewe usinge zaliwa kabisa hivyo najisikia fahari sana na mimi pia kuja kukusaidia kwa baadae kisha na wewe unaenda kuwa msaada mkubwa kwangu. Haujawahi kuniangusha kwenye majukumu ambayo nakutuma na ndiyo sababu ambayo inanifanya niendelee kukuamini zaidi na kukupa hiyo nafasi hivyo nitafurahi kama msaada wa baba yangu kwa familia yako na msaada wangu kwako ukaulipa kwa moyo wote. Nahitaji ufanye kazi yangu kama ninavyokutuma ili tubakie Ikulu kwani hatujui mtu mwingine ambaye ataingia atakuwa na upepo gani, kama tukicheza vibaya hata wewe unaweza ukaipoteza hiyo nafasi yako na ukaishia kupewa hata kesi ambazo haukuhusika nazo ukaishia jela. Unaweza kwenda mr Lingson” kiongozi huyo aliongea kwa msisitizo sana kisha akamruhusu mwanaume huyo aondoke bila kutoa jibu la mwisho.

Mr Lingson Mfwomi aliinama kutoa heshima kabla ya kutoka humo ndani, baada ya hapo alitoka na kubaki kwenye mshangao mkubwa sana maana ilikuwa ni ghafla sana kuambiwa maneno mazito kama hayo na kiongozi wake, alijua kabisa kulikuwa na mambo ambayo hayakuwa sawa hata bosi wake hakuonekana kabisa kuwa sawa hivyo aliondoka kichwa chake kikiwa na mashaka mengi sana. Kwanini raisi alikuwa anasisitiza sana kulindwa yeye na sio nchi au ofisi yake? Maana yake alikuwa anajijali yeye zaidi kuliko maslahi ya nchi? Alisikitika na kutoweka hilo eneo haraka sana.

Ukurasa wa tano unafika mwisho.

Febiani Babuya.View attachment 2863215

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Malizia
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA SITA

Asubuhi kulikuwa kumekucha salama kabisa na shughuli za kila siku zilikuwa zikiendelea kama ilivyokuwa kwa watafutaji na wasaka tonge ambao hawajawahi kuamini kufanikiwa kwa miujiza zaidi ya kuzitumia nguvu zao vizuri ili kuyafikia malengo yao. Ndani ya jiji la Dar es salaam, asubuhi hiyo watu walikuwa na pilika pilika zao lakini usingekosa kuwakuta watu kadhaa wakiwa wamekaa sehemu wakiteta jambo kuhusu siasa kwa sababu maandaliza ya uchaguzi mpya yalikuwa yanaanza taratibu.

Kuna watu ambao muda wao mwingi waliutumia kwenye kusoma magazeti ambayo yalikuwa na zile habari moto moto zilizokuwa zinasubiriwa kwa hamu na wengi hivyo ilipelekea watu kuwa na mengi sana ya kuyazungumza kuhusu siasa.

Maeneo ya mabibo sokoni, wengi huwa wanapaita mahakama ya ndizi. Ni eneo ambalo linayabeba maisha ya sehemu kubwa sana ya jiji la Dar es salaam kama sio lote kwa ujumla kwani sehemu hiyo vinapatikana vyakula kwa bei rahisi sana ambavyo vinatoka moja kwa moja mashambani na kuletwa mjini kwa ajili ya wananchi kunufaika na moja kati ya uwekezaji bora ambao unafanywa kwenye kilimo. Watu wengi sana huvutiwa kufika ndani ya soko hilo kwa sababu mahitaji yanapatikana kwa bei rahisi sana basi huwa inapelekea kuwa na msongamano mkubwa sana wa magari pamoja na watu kiujumla bila kusahau wale wanachuo ambao wanasoma ndani ya chuo cha taifa cha usafirishaji ambacho kipo jirani sana na eneo hilo.

Asubuhi hiyo wakati hizo pilika pilika zikiwa zinaendelea ndani ya eneo hilo, walikuwa wamekati watu wakiwa wanabishana sana kuhusu siasa ya nchi yao yaani ungehisi kwamba wao ndio ambao walikuwa wanaiendesha nchi kwa namna walivyokuwa wanajinasibu huku kila mtu akijinadi kwamba yeye ndiye ambaye alikuwa na taarifa za kweli kabisa kuhusu uhalisia wa nchi ya Tanzania kwani hata babu yake alikuwa akimsimulia sana.

“Nisikilize Chande wewe umekuja juzi tu hapa kutoka huko kwenu Mtwara kulima korosho, hakuna jambo ambalo unalijua kuhusu nchi hii zaidi ya majirani zako wa Msumbiji huko. Tumekupokea wenyewe ndani ya jiji hili utatuambia nini kuhusu siasa ya hapa wewe? Tukikwambia hata utupe historia ya mwenge wa uhuru ya Forojo Ganze unaijua wewe? Tukikwambia kwamba utume tafsiri ya ile namba miamoja kumi na tano (115) ambayo kwa baadae ilikuja kutafsiriwa na shekhe Yahya kwa mwalimu Nyerere unaijua wewe? Hahahaha sasa utatuambia nini kuhusu nchi hii wewe na siasa zake? Acha kutupigishia kelele sisi wakubwa tunapokuwa tunaongea wewe unatulia na kula somo”

“Na wewe Ismail acha kumtisha mwenzako kwa historia ambayo imeandikwa na unaweza hata kwenda kuisoma, wewe mwenyewe mweupe tu basi uliibahatisha hiyo ukaanza kutupigia makelele hapa. Hata wewe nikikuuliza unipe historia ya TAA na TANU hauzijui, hata tu vyama vya sasa na sera zake huzijui, unapata wapi nguvu ya kumtishia mwenzako na kumwambia anyamaze? Vijana wa siku hizi mnatanguliza majigambo kuliko uhalisia wa mambo yalivyo” ni mzee mmoja mwenye busara alimjibu kijana ambaye aliitwa Ismail aliyekuwa anamkosoa na kumsema vibaya mwenzake kwa kudai kwamba hajui lolote. Aliambiwa ukweli basi naye akajikuta anakuwa mpole maana angedhalilika kama angeendelea kubishania kitu ambacho hakukijua.

Kijana Chande baada ya kuona hata mtesi wake naye pia alipewa vidonge vyake, alitabasamu sana na kumgeukia mzee huyo.

“Mzee wangu asante sana kwa busara zako, naomba kukuuliza hivi kwa sasa unahisi ni kiongozi gani anaweza kuingia madarakani na kwa sababu zipi ambazo unahisi zitamfanya apate hicho kiti?” aliuliza na kukohoa kidogo na kutega sikio ili kumpa nafasi mzee huyo kuweza kujibu.

“Kwa bahati mbaya sana nchi haiongozwi kama unavyo hisi wewe au kama unavyotaka wewe iwe. Hii nchi kuna watu ambao wanaamua kipi kiwe kipi au nani awe nani hivyo kukujibu swali lako ni kwamba wataamua wao kwamba ni nani ambaye anafaa kuwa Ikulu na sio mimi kukueleza maana hata nikikupa sababu za mtu kuingia huko haitakuwa na maana yoyote ile” mzee huyo aliongea kwa ufupi sana huku akiwa analikunjua gazeti lake ili aweze kuzipata habari

“Mzee sijakuelewa unamaanisha nini, unasema wao ndio wanaamua nani awe nani! Kwani unawazungumzia akina nani hao?” mzee huyo alimwangalia sana Chande

“Wewe bado ni mdogo sana kuna mambo hautakiwi kuyajua kwenye maisha yako kwa sababu yanaweza kuwa hatari sana kwako. Mimi nimeishi miaka mingi sana kwenye nchi hii na niliwahi kuwa pia ndani ya jeshi hivyo kuna baadhi ya mambo nayajua vizuri sana japo siwezi kukueleza. Kitu ambacho unatakiwa kuwa nacho kichwani mwako ni kwamba duniani hakuna demokrasia na haitakuja kuwepo kama ambavyo wewe huwa unaambiwa kwamba demokrasia ipo, hivyo ambao wanaamua nani awe pale ni wenye mamlaka na sio wewe hapo. Vijana mimi nawahi nyumbani muwe na asubuhi njema” mzee huyo aliongea jambo ambalo wote liliwaacha njiapanda wasielewe anamaanisha nini na mzee huyo baada ya kuona kwamba vijana hao wanaanza kumchimba sana aliamua kuondoka tu kwani yangekuwa mengine hapo mwisho wa siku waanze kuongelea habari ambazo huenda zingewaingiza kwenye matatizo.

Hayo yalikuwa maisha ya kawaida tu mtaani hapo watu wakiwa wanaendelea na maisha yao ya kila siku na vijana hao wa vijiweni wakiwa wanaendelea kupiga hadithi ambazo hawakuwa hata na uhakika nazo. Pembeni mwa hicho kijiwe cha hao vijana ambao walikuwa wanapiga hizo stori na mzee huyo palikuwa na mwanaume mmoja ambaye kwa mavazi yake tu ambayo yalikuwa mwilini, ungegundua kwamba alikuwa ni mbeba mizigo wa hapo sokoni.

Alikuwa makini sana isivyo kawaida kusikiliza hayo majibizano ya watu hao hapo japo alijfanya kama mtu mwenye mawazo mengi sana kwenye kichwa chake. Baada ya mzee huyo kuondoka naye alizuga zuga na kuanza kutoka hiyo sehemu huku akiwa anasogelea taratibu karibu na eneo la kuchezea michezo ya kubashiri ambalo lipo karibu sana na eneo hilo.

Alisimama hapo na kuangalia namna vijana walivyokuwa wanapishana wakiingia na kutoka ndani ya jumba hilo la michezo ya kubashiri na kusikitika namna vijana walivyokuwa wanautumia muda wao kuamini kwamba wanaweza kuchota pesa kwa zile namba ambazo zilikuwa zinabandikwa kwenye makaratasi huku wao wakiwa wanatoa vile vidogo ambavyo walikuwa wanavisaka kwa jasho sana.

“Naona unajaribu kuangalia namna namba za kusadikika zinavyo wapumbaza wenzako mpaka wanakuwa kama wajinga wa kushindwa kupambana huku wakiamini kwamba wanaweza kupata utajiri bila kufanya kazi” ilikuwa ni sauti ya mzee mmoja ambayo ilimshtua kutoka kwenye hiyo tafakuri yake.

“Ndiyo mzee, hawa watu wa nje wamefanikiwa sana kwenye suala la kuwageuza vijana wengi kuwa wajinga. Yaani mtu anaamka kwake anakuja hapa akiwa ana amini kwamba anaweza kuchota hizi pesa kirahisi sana namna hii kwa sababu anaona namba zimebandikwa ukutani. Matokeo yake unaweza ukaondoka miaka kumi, ukarudi na bado utamkuta anazunguka hapo hapo na makaratasi mkononi akiamini miujiza. Nadhani nchi ina hasara kubwa sana kuwa na idadi kubwa ya vijana ambao wana akili za kijinga sana namna hii”

“Shida ya vijana wa siku hizi wanaamini kwamba wao ndio wajanja sana, wanaamini kwamba wao ndio wanayajua mambo mengi sana zaidi yetu. Ukiwashauri wanakwambia umepitwa na wakati hivyo unawaacha tu umri na muda utakuja kuwahukumu vibaya sana na ndo hapo wanaanza kuwachukia watu wenye mafanikio na kuwasingizia kwamba wao wana pesa mara za manyoka, utasikia za mashetani, hayo ndiyo mawazo pekee ambayo watu maskini huwa wanahisi yanawafariji bila kujua kwamba wanaudumaza uwezo wao wa akili kufikiria mambo makubwa. Kwa umri wako wewe bado ni kijana sana, jitahidi upambane mno, jitahidi uwekeze sana kwani kuna muda utafika utakuwa hauna uwezo wa kupambana tena, kuna wakati utafika mwili hautakuwa na uwezo wa kunyanyua hata mfuko wa unga sasa hapo kama ulijiwekeza vizuri basi hautapata shida yoyote ile ila kama ulicheza vibaya utaanza kuwachukia watu na kulia lia kwamba hawakusaidii. Nawahi nyumbani kijaja wangu, nilikuwa kuhemea kidogo sokoni hapo Mungu akubariki sana kwa kujielewa na kujua kwamba hivyo vitu ni jela kubwa sana” mzee huyo baada ya kumaliza mawaidha yake kwa mwanaume huyo alimuaga na kuondoka, aligeuka na kumwangalia sana mzee huyo akaishia kutabasamu tu kwani aliongea mambo ya maana sana japo hawakuwa wakifahamiana ila alimuelewa sana.

Mwanaume huyo aliangalia saa yake kisha akajichanganya ndani ya soko ambako alitumia dakika ishirini tu pekee akatoka tena mpaka barabarani. Alisogea pembeni kabisa akaruka mtaro na kwenda kukaa katikati ya uwanja ambao unatenganisha kati ya soko hilo na chuo cha taifa cha usafirishaji, aliitoa simu yake ndogo sana ambayo ilikuwa imechoka mfukoni na kuipiga mahali ambapo iliita kwa sekunde kumi na tano tu kisha ikapokelewa.

“Mkuu nimemaliza kutega kamera kila sehemu ya mhimu ya soko hivyo tutakuwa tunaona na kupata kila habari mpya ambayo inaendelea lakini pia hata sehemu za mhimu kama sehemu zenye majumba ya michezo ya kubashiri pia nimeweka ili tuwe tunajua mitazamo ya wananchi juu ya jambo hili na kila kitakachokuwa kinaendelea, nadhani hiyo itaturahishia sana kuchukua hatua za haraka pale itakapo bidi”

“Safi sana, kwa sasa una kazi moja kubwa sana, hakikisha unaifuatilia familia ya Mr Apson Limo. Kuanzia asubuhi wanapo amka mpaka usiku wanapo enda kulala na kama kuna mtu atakushtukia kwenye hayo mambo yako basi haraka sana hakikisha unampoteza ili kutoacha ushahidi eneo lolote lile”

“Sawa mkuu” kisha simu ikakatwa. Mwanaume huyo alisonya kwa hasira baada ya simu hiyo kukatwa kwani kwa wakati huo alikuwa anaongea na kiongozi wake ambaye ndiye alikuwa amempa hiyo kazi. Mwanaume alikuwa ni shushushu aliyekuwa akizikusanya taarifa mbali mbali ndani ya nchi lakini pia alikuwa ni jasusi mbobevu sana ambaye alikuwa amefanya kazi nyingi sana za nje.

“Ndiyo maana siipendi kabisa siasa mimi, yaani juzi tu nimetoka kufanya kazi ngumu huko Kongo hata sijapumzika napewa kazi nyingine tena halafu wenyewe wapo na wake zao ndani wamelala tu wanasubiri ukosee waje kukulaumu na vitambi vyao, pumbavu sana. Wana siasa ni watu wa hovyo sana muda mwingine” aliongea kwa kulalamika sana kwa sababu hakupewa muda wa kupumzika, kupewa kazi hiyo ya kumfuatilia mwana siasa huyo kwake hakuona kama ni sawa kwa sababu yalikuwa ni maslahi binafsi na sio nchi ila hakuwa na namna kwa sababu ni kazi ambayo alipewa na kiongozi wake hivyo hakuwa hata na nguvu ya kuhoji au kukataa.

Alikuwa anaitwa Matiasi Ndugu mwanaume wa shoka huyo. Alikuwa amepewa kazi ambayo aliijua moja kwa moja kwamba ilikuwa ni ngumu na ni hatari sana endapo kama ingetokea siku akaweza kukamatwa. Aliondoka hilo eneo kishingo upande baada ya kumaliza kutega vifaa vyake hayo maeneo ambavyo vingempa urahisi sana wa kupata taarifa ambazo wangezihitaji wakubwa wake kuhusu yale yanayo endelea mtaani. Sasa kazi iliyokuwa mbele yake ilikuwa ni kuzikusanya taarifa zote za Apson Limo pamoja na familia yake kuanzia asubuhi mpaka usiku.

Ukurasa wa sita naweka nukta hapa. Tukutane tena wakati ujao.

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA SITA

Asubuhi kulikuwa kumekucha salama kabisa na shughuli za kila siku zilikuwa zikiendelea kama ilivyokuwa kwa watafutaji na wasaka tonge ambao hawajawahi kuamini kufanikiwa kwa miujiza zaidi ya kuzitumia nguvu zao vizuri ili kuyafikia malengo yao. Ndani ya jiji la Dar es salaam, asubuhi hiyo watu walikuwa na pilika pilika zao lakini usingekosa kuwakuta watu kadhaa wakiwa wamekaa sehemu wakiteta jambo kuhusu siasa kwa sababu maandaliza ya uchaguzi mpya yalikuwa yanaanza taratibu.

Kuna watu ambao muda wao mwingi waliutumia kwenye kusoma magazeti ambayo yalikuwa na zile habari moto moto zilizokuwa zinasubiriwa kwa hamu na wengi hivyo ilipelekea watu kuwa na mengi sana ya kuyazungumza kuhusu siasa.

Maeneo ya mabibo sokoni, wengi huwa wanapaita mahakama ya ndizi. Ni eneo ambalo linayabeba maisha ya sehemu kubwa sana ya jiji la Dar es salaam kama sio lote kwa ujumla kwani sehemu hiyo vinapatikana vyakula kwa bei rahisi sana ambavyo vinatoka moja kwa moja mashambani na kuletwa mjini kwa ajili ya wananchi kunufaika na moja kati ya uwekezaji bora ambao unafanywa kwenye kilimo. Watu wengi sana huvutiwa kufika ndani ya soko hilo kwa sababu mahitaji yanapatikana kwa bei rahisi sana basi huwa inapelekea kuwa na msongamano mkubwa sana wa magari pamoja na watu kiujumla bila kusahau wale wanachuo ambao wanasoma ndani ya chuo cha taifa cha usafirishaji ambacho kipo jirani sana na eneo hilo.

Asubuhi hiyo wakati hizo pilika pilika zikiwa zinaendelea ndani ya eneo hilo, walikuwa wamekati watu wakiwa wanabishana sana kuhusu siasa ya nchi yao yaani ungehisi kwamba wao ndio ambao walikuwa wanaiendesha nchi kwa namna walivyokuwa wanajinasibu huku kila mtu akijinadi kwamba yeye ndiye ambaye alikuwa na taarifa za kweli kabisa kuhusu uhalisia wa nchi ya Tanzania kwani hata babu yake alikuwa akimsimulia sana.

“Nisikilize Chande wewe umekuja juzi tu hapa kutoka huko kwenu Mtwara kulima korosho, hakuna jambo ambalo unalijua kuhusu nchi hii zaidi ya majirani zako wa Msumbiji huko. Tumekupokea wenyewe ndani ya jiji hili utatuambia nini kuhusu siasa ya hapa wewe? Tukikwambia hata utupe historia ya mwenge wa uhuru ya Forojo Ganze unaijua wewe? Tukikwambia kwamba utume tafsiri ya ile namba miamoja kumi na tano (115) ambayo kwa baadae ilikuja kutafsiriwa na shekhe Yahya kwa mwalimu Nyerere unaijua wewe? Hahahaha sasa utatuambia nini kuhusu nchi hii wewe na siasa zake? Acha kutupigishia kelele sisi wakubwa tunapokuwa tunaongea wewe unatulia na kula somo”

“Na wewe Ismail acha kumtisha mwenzako kwa historia ambayo imeandikwa na unaweza hata kwenda kuisoma, wewe mwenyewe mweupe tu basi uliibahatisha hiyo ukaanza kutupigia makelele hapa. Hata wewe nikikuuliza unipe historia ya TAA na TANU hauzijui, hata tu vyama vya sasa na sera zake huzijui, unapata wapi nguvu ya kumtishia mwenzako na kumwambia anyamaze? Vijana wa siku hizi mnatanguliza majigambo kuliko uhalisia wa mambo yalivyo” ni mzee mmoja mwenye busara alimjibu kijana ambaye aliitwa Ismail aliyekuwa anamkosoa na kumsema vibaya mwenzake kwa kudai kwamba hajui lolote. Aliambiwa ukweli basi naye akajikuta anakuwa mpole maana angedhalilika kama angeendelea kubishania kitu ambacho hakukijua.

Kijana Chande baada ya kuona hata mtesi wake naye pia alipewa vidonge vyake, alitabasamu sana na kumgeukia mzee huyo.

“Mzee wangu asante sana kwa busara zako, naomba kukuuliza hivi kwa sasa unahisi ni kiongozi gani anaweza kuingia madarakani na kwa sababu zipi ambazo unahisi zitamfanya apate hicho kiti?” aliuliza na kukohoa kidogo na kutega sikio ili kumpa nafasi mzee huyo kuweza kujibu.

“Kwa bahati mbaya sana nchi haiongozwi kama unavyo hisi wewe au kama unavyotaka wewe iwe. Hii nchi kuna watu ambao wanaamua kipi kiwe kipi au nani awe nani hivyo kukujibu swali lako ni kwamba wataamua wao kwamba ni nani ambaye anafaa kuwa Ikulu na sio mimi kukueleza maana hata nikikupa sababu za mtu kuingia huko haitakuwa na maana yoyote ile” mzee huyo aliongea kwa ufupi sana huku akiwa analikunjua gazeti lake ili aweze kuzipata habari

“Mzee sijakuelewa unamaanisha nini, unasema wao ndio wanaamua nani awe nani! Kwani unawazungumzia akina nani hao?” mzee huyo alimwangalia sana Chande

“Wewe bado ni mdogo sana kuna mambo hautakiwi kuyajua kwenye maisha yako kwa sababu yanaweza kuwa hatari sana kwako. Mimi nimeishi miaka mingi sana kwenye nchi hii na niliwahi kuwa pia ndani ya jeshi hivyo kuna baadhi ya mambo nayajua vizuri sana japo siwezi kukueleza. Kitu ambacho unatakiwa kuwa nacho kichwani mwako ni kwamba duniani hakuna demokrasia na haitakuja kuwepo kama ambavyo wewe huwa unaambiwa kwamba demokrasia ipo, hivyo ambao wanaamua nani awe pale ni wenye mamlaka na sio wewe hapo. Vijana mimi nawahi nyumbani muwe na asubuhi njema” mzee huyo aliongea jambo ambalo wote liliwaacha njiapanda wasielewe anamaanisha nini na mzee huyo baada ya kuona kwamba vijana hao wanaanza kumchimba sana aliamua kuondoka tu kwani yangekuwa mengine hapo mwisho wa siku waanze kuongelea habari ambazo huenda zingewaingiza kwenye matatizo.

Hayo yalikuwa maisha ya kawaida tu mtaani hapo watu wakiwa wanaendelea na maisha yao ya kila siku na vijana hao wa vijiweni wakiwa wanaendelea kupiga hadithi ambazo hawakuwa hata na uhakika nazo. Pembeni mwa hicho kijiwe cha hao vijana ambao walikuwa wanapiga hizo stori na mzee huyo palikuwa na mwanaume mmoja ambaye kwa mavazi yake tu ambayo yalikuwa mwilini, ungegundua kwamba alikuwa ni mbeba mizigo wa hapo sokoni.

Alikuwa makini sana isivyo kawaida kusikiliza hayo majibizano ya watu hao hapo japo alijfanya kama mtu mwenye mawazo mengi sana kwenye kichwa chake. Baada ya mzee huyo kuondoka naye alizuga zuga na kuanza kutoka hiyo sehemu huku akiwa anasogelea taratibu karibu na eneo la kuchezea michezo ya kubashiri ambalo lipo karibu sana na eneo hilo.

Alisimama hapo na kuangalia namna vijana walivyokuwa wanapishana wakiingia na kutoka ndani ya jumba hilo la michezo ya kubashiri na kusikitika namna vijana walivyokuwa wanautumia muda wao kuamini kwamba wanaweza kuchota pesa kwa zile namba ambazo zilikuwa zinabandikwa kwenye makaratasi huku wao wakiwa wanatoa vile vidogo ambavyo walikuwa wanavisaka kwa jasho sana.

“Naona unajaribu kuangalia namna namba za kusadikika zinavyo wapumbaza wenzako mpaka wanakuwa kama wajinga wa kushindwa kupambana huku wakiamini kwamba wanaweza kupata utajiri bila kufanya kazi” ilikuwa ni sauti ya mzee mmoja ambayo ilimshtua kutoka kwenye hiyo tafakuri yake.

“Ndiyo mzee, hawa watu wa nje wamefanikiwa sana kwenye suala la kuwageuza vijana wengi kuwa wajinga. Yaani mtu anaamka kwake anakuja hapa akiwa ana amini kwamba anaweza kuchota hizi pesa kirahisi sana namna hii kwa sababu anaona namba zimebandikwa ukutani. Matokeo yake unaweza ukaondoka miaka kumi, ukarudi na bado utamkuta anazunguka hapo hapo na makaratasi mkononi akiamini miujiza. Nadhani nchi ina hasara kubwa sana kuwa na idadi kubwa ya vijana ambao wana akili za kijinga sana namna hii”

“Shida ya vijana wa siku hizi wanaamini kwamba wao ndio wajanja sana, wanaamini kwamba wao ndio wanayajua mambo mengi sana zaidi yetu. Ukiwashauri wanakwambia umepitwa na wakati hivyo unawaacha tu umri na muda utakuja kuwahukumu vibaya sana na ndo hapo wanaanza kuwachukia watu wenye mafanikio na kuwasingizia kwamba wao wana pesa mara za manyoka, utasikia za mashetani, hayo ndiyo mawazo pekee ambayo watu maskini huwa wanahisi yanawafariji bila kujua kwamba wanaudumaza uwezo wao wa akili kufikiria mambo makubwa. Kwa umri wako wewe bado ni kijana sana, jitahidi upambane mno, jitahidi uwekeze sana kwani kuna muda utafika utakuwa hauna uwezo wa kupambana tena, kuna wakati utafika mwili hautakuwa na uwezo wa kunyanyua hata mfuko wa unga sasa hapo kama ulijiwekeza vizuri basi hautapata shida yoyote ile ila kama ulicheza vibaya utaanza kuwachukia watu na kulia lia kwamba hawakusaidii. Nawahi nyumbani kijaja wangu, nilikuwa kuhemea kidogo sokoni hapo Mungu akubariki sana kwa kujielewa na kujua kwamba hivyo vitu ni jela kubwa sana” mzee huyo baada ya kumaliza mawaidha yake kwa mwanaume huyo alimuaga na kuondoka, aligeuka na kumwangalia sana mzee huyo akaishia kutabasamu tu kwani aliongea mambo ya maana sana japo hawakuwa wakifahamiana ila alimuelewa sana.

Mwanaume huyo aliangalia saa yake kisha akajichanganya ndani ya soko ambako alitumia dakika ishirini tu pekee akatoka tena mpaka barabarani. Alisogea pembeni kabisa akaruka mtaro na kwenda kukaa katikati ya uwanja ambao unatenganisha kati ya soko hilo na chuo cha taifa cha usafirishaji, aliitoa simu yake ndogo sana ambayo ilikuwa imechoka mfukoni na kuipiga mahali ambapo iliita kwa sekunde kumi na tano tu kisha ikapokelewa.

“Mkuu nimemaliza kutega kamera kila sehemu ya mhimu ya soko hivyo tutakuwa tunaona na kupata kila habari mpya ambayo inaendelea lakini pia hata sehemu za mhimu kama sehemu zenye majumba ya michezo ya kubashiri pia nimeweka ili tuwe tunajua mitazamo ya wananchi juu ya jambo hili na kila kitakachokuwa kinaendelea, nadhani hiyo itaturahishia sana kuchukua hatua za haraka pale itakapo bidi”

“Safi sana, kwa sasa una kazi moja kubwa sana, hakikisha unaifuatilia familia ya Mr Apson Limo. Kuanzia asubuhi wanapo amka mpaka usiku wanapo enda kulala na kama kuna mtu atakushtukia kwenye hayo mambo yako basi haraka sana hakikisha unampoteza ili kutoacha ushahidi eneo lolote lile”

“Sawa mkuu” kisha simu ikakatwa. Mwanaume huyo alisonya kwa hasira baada ya simu hiyo kukatwa kwani kwa wakati huo alikuwa anaongea na kiongozi wake ambaye ndiye alikuwa amempa hiyo kazi. Mwanaume alikuwa ni shushushu aliyekuwa akizikusanya taarifa mbali mbali ndani ya nchi lakini pia alikuwa ni jasusi mbobevu sana ambaye alikuwa amefanya kazi nyingi sana za nje.

“Ndiyo maana siipendi kabisa siasa mimi, yaani juzi tu nimetoka kufanya kazi ngumu huko Kongo hata sijapumzika napewa kazi nyingine tena halafu wenyewe wapo na wake zao ndani wamelala tu wanasubiri ukosee waje kukulaumu na vitambi vyao, pumbavu sana. Wana siasa ni watu wa hovyo sana muda mwingine” aliongea kwa kulalamika sana kwa sababu hakupewa muda wa kupumzika, kupewa kazi hiyo ya kumfuatilia mwana siasa huyo kwake hakuona kama ni sawa kwa sababu yalikuwa ni maslahi binafsi na sio nchi ila hakuwa na namna kwa sababu ni kazi ambayo alipewa na kiongozi wake hivyo hakuwa hata na nguvu ya kuhoji au kukataa.

Alikuwa anaitwa Matiasi Ndugu mwanaume wa shoka huyo. Alikuwa amepewa kazi ambayo aliijua moja kwa moja kwamba ilikuwa ni ngumu na ni hatari sana endapo kama ingetokea siku akaweza kukamatwa. Aliondoka hilo eneo kishingo upande baada ya kumaliza kutega vifaa vyake hayo maeneo ambavyo vingempa urahisi sana wa kupata taarifa ambazo wangezihitaji wakubwa wake kuhusu yale yanayo endelea mtaani. Sasa kazi iliyokuwa mbele yake ilikuwa ni kuzikusanya taarifa zote za Apson Limo pamoja na familia yake kuanzia asubuhi mpaka usiku.

Ukurasa wa sita naweka nukta hapa. Tukutane tena wakati ujao.

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA SABA
Wakati huo kwenye hoteli moja kubwa sana mapema ya asubuhi hiyo walikuwa wanaonekana watu wawili ambao hawakuhitaji maelezo mengi kuweza kujieleza kwamba wao walikuwa kwenye penzi zito sana. Mwanaume alivaa bukta tu huku mwanamke pia akiwa ndani ya bikini tu, walikuwa wanapata chai huku wakiwa wanapeana mahaba ya wazi wazi.

“Mpenzi ni lini utafika nyumbani kwa ajili ya kujitambulisha?” ilikuwa sauti ya mwanamke akiongea kwa mahaba ya wazi wazi kwani hata macho yake yalikuwa yakiongea jambo hilo. Alikuwa ni Patrina Apson Limo ambaye alikuwa binti mkubwa wa mwana siasa na tajiri Apson Limo.

“Mzee wako kwa sasa anajiandaa na mambo ya uchaguzi, sioni kama ni muda sahihi sana, hili likipita tu mimi nakuja kwenu na kukuvisha pete kabisa inabaki harusi tu” Ni lugha safi ambayo aliipata kutoka kwa mwanaume ambaye alikuwa akimpenda sana.

“Basi usije ukanidanganya maana nitajisikia vibaya sana kwa sababu mimi nakupenda sana” aliongea akiwa na furaha sana Patrina lakini wakati huo huo simu ya mwanaume huyo ilianza kuita, alivyo angalia namba hiyo ya mpigaji, alitoka haraka sana hilo eneo na kwenda nje kabisa ya kile chumba.

“Ndiyo baba”

“Mpango ukikamilika tu niambie nilitekeleze hilo haraka sana maana hata muda huu nipo naye hotelini”

“Sawa baba” mwanaume huyo aliikata simu yake na kurudi ndani akisingizia kwamba alikuwa naongea na simu ya biashara zake binafsi, na mwanamke huyo kwa sababu alikuwa akimuamini sana basi hakuona kama ilikuwa ni busara sana kuanza kubishana naye, uwepo tu wa mwanaume huyo ulikuwa unamridhisha sana asijue mwenzake alikuwa na mipango ipi juu yake maana hata dakika hizo hizo alitoka kumwongelea ikionekana wazi kwamba kuna mpango mzito sana ambao ulikuwa unaandaliwa kwa ajili yake yeye.

Majira ya usiku wa mapema Mr Apson Limo alikuwa na familia yake nyumbani kama ilivyokuwa kawaida yake, alichagua kuwa baba bora wa familia yake na kuyabeba majukumu vile inavyo takikana. Akiwa hapo sebuleni majira hayo anacheza na mwanae wa mwisho alimuona moja kati ya walinzi wake wa getini anakuja kwa spidi sana akiwa anahema kama mtu ambaye alijaa hofu sana ndani yake, alimgeukia na kumwangalia kwa macho ya kumuuliza kuhusu kile ambacho kilikuwa kinaendelea.

“Bosi kuna watu wamekuja na gari za Ikulu nje hapo, sasa sijui kama niwaruhusu waingie?” swali la huyo mlinzi wake lilimshtua sana, alishangaa gari za ikulu zinatafuta nini kwake wakati hakuwa hata na miadi nao? Hakupata jibu hivyo ikamlazimu yeye mwenyewe kuweza kutoka ili kujua kwamba watu hao walikuwa wanahitaji kitu gani hasa mpaka wamfuate nyumbani kwake.

Alitoka akiwa na wasiwasi sana kwenye nafsi yake hata geti hilo alienda kulifungua yeye mwenyewe ndipo alipo kutana kweli na gari hizo za Ikulu tatu zikiwa zimesimamishwa nje ya nyumba yake huku wanaume waliokuwa waamevaa suti nyeusi wakiwa wamezizunguka gari hizo.

“Mheshimiwa tunaomba utusamehe sana kwa kuja kwako bila taarifa ila ni maagizo kutoka juu hivyo hatukuwa na namna zaidi ya kuyatekeleza” aliongea mwanaume mmoja ambaye alionekana kuwa kiongozi wa wengine huku akiwa anaguna kidogo kumpa nafasi mheshimiwa kuweza kuwajibu kwa maana walimuona kama bado alikuwa kwenye mshangao sana.

“Hii yote inamaanisha nini?”

“Ni maagizo ya mheshimiwa raisi anakuhitaji Ikulu kwa sasa, amesema kwamba ana mazungumzo marefu na nyeti sana na wewe” alijibu mwanaume huyo

“Mhhhhhh kwahiyo raisi anahisi kwamba nafasi yake inamfanya kumpata kila ambaye anamhitaji na kwa muda ambao anautaka yeye?”

“Sidhani kama ni hivyo mheshimiwa ila ni bora kubali wito ukatae maneno, itakuwa kama dharau sana kumkatalia mkubwa wa nchi kwa kukualika Ikulu”

“Sawa nakuja” aliongea kwa hasira sana huku akielekea ndani, bila shaka alienda kumuaga mkewe ambaye alimsindikiza kwa wasiwasi sana wakati wa kutoka na Mr Apson Limo akapanda kwenye gari ili kuweza kufika huko Ikulu”

Ndani ya nusu saa gari hizo zilikuwa zinaingia Ikulu bila wasiwasi huku mr Limo akiwa ana hasira sana na alipanga kumpa makavu raisi wake lakini ni kama hata aliyekuwa amepanga kumpa makavu yake alikuwa amejipanga juu ya hilo.

“Akili ni kitu bora zaidi kwa mwanadamu na siku zote watu wenye akili huwa hawakurupuki wala kutanguliza hasira mbele kwa kuamini kwamba kila lililopo mbele yao linaweza kuwa na umuhimu mkubwa sana kwao. Ni jambo jema sana kama umekubali kuja kuongea na mimi, karibu sana mr Apson Limo” mheshimiwa huyo aliongea huku akiwa anampa mkono mwanaume ambaye macho yake yaliingia kwenye ofisi hiyo kwa hasira sana lakini kwa maneno ambayo alipewa aliamua kuwa mpole mwenyewe naye akaishia kumsalimia kiongozi wake kisha akaketi ili kumsikiliza kuhusu kile ambacho alikuwa amemuitia usiku huo.

“Nimeukubali wito wako kwa sababu wewe ni mheshimiwa raisi na napaswa kukusikiliza kama kiongozi wangu japo hili ni baya sana kwa sehemu mbili. Sehemu ya kwanza kistaarabu ulitakiwa kunipigia simu na kunitaarifu mapema maana hata mimi nina ratiba zangu za kifamilia na kikazi, sio ustaarabu kwa sababu ni raisi basi unajiamulia kila linalo kuja mbele yako. Lakini jambo la pili usiyatumie madaraka vibaya mheshimiwa, kumbuka hata kabla ya kuingia hapa wewe pia ulikuwa raia wa kawaida tu mtaani, sasa unapo anza kutumia nguvu kama hivi sio sawa. Walicho kifanya vijana wako ni kama uvamizi tu nyumbani kwangu huku wakiamini kwamba kwa sababu wewe ni raisi basi wapo sahihi kwa kila jambo ila sio kweli” alimpa vidonge vyake mheshimiwa kama alivyokuwa amekusudia tangu mwanzo. Boniphace Walawalaa alitabasamu ila kwa uchungu, kuwa raisi alihisi kwamba yeye yupo juu ya kila kitu sasa inapotokea mtu ndani ya nchi yake anataka kumchukulia kawaida alikuwa anajihisi kutokamilika kama raisi ila aliamua kumezea kwanza maana huyo mtu ilikuwa ni karata mhimu sana kwake kuweza kuichanga vyema.

“Mr Apson Limo najua nimekukosea wewe na familia yako ila kuna muda ukiwa kiongozi hauna budi kufanya maamuzi magumu hata kama hayata wafurahisha wale ambao wanayapokea. Kuwa kiongozi ni moja ya jukumu kubwa sana japo wanasema kwamba kiongozi anapaswa kuwasikiliza wale ambao anawaongoza lakini sio kila muda kwani ukisema umsikilize kila mtu basi mtachelewa sana kufikia maamuzi ya mwisho kitu ambacho kitapelekea kuchelewa sana kuweza kufanikiwa au kuendelea” mheshimiwa raisi aligeuka kuwa kama mwanafalsafa kuanzia mbali kumrubuni mtu huyo.

“Mheshimiwa mke wangu atakuwa na wasiwasi sana kwa jinsi nilivyo ondoka nyumbani, nitafurahi sana kama utaenda moja kwa moja kwenye pointi yako ya msingi kwani kwa kipindi tulichopo hata wananchi wakijua mimi na wewe tunakutana italeta picha mbaya sana kwetu sote wawili wakihisi kwamba labda kuna mambo ambayo tunakubaliana au tunayapanga pamoja kitu ambacho sitaki kukifanya kwani wananchi wangu wananiamini sana” hakuhitaji ngonjera za bwana huyo hivyo alimwambia aende kwenye pointi ya msingi moja kwa moja.

“Ok nahitaji uiachie hiyo nafasi ambayo wewe upo na tutamuweka mtu mwingine hapo” raisi alizungumza huku akiwa amemkazia macho asiwe hata na tone la wasiwasi kwa upande wake.

“Unaweza ukanipa sababu ya msingi ya wewe kuniambia maneno kama hayo?” Mr Apson Limo hakushangazwa sana na kauli hiyo kwa sababu hata mr Mafupa alikutana naye na kumuomba kitu kama hicho, ilikuwa ni kawaida sana hayo mambo kutokea kwenye siasa.

“Nahitaji kuendelea kubaki Ikulu bado ndiyo maana sitaki upinzani wowote kutoka kwako kwa sababu mr Mafupa hana shida yule ni wa chama changu hivyo tutamalizana ndani ya chama ila wewe ndiye wa mhimu maana upo kwenye chama kingine tofauti kabisa na wananchi wanakuamini sana. Nina imani kama ukiwa upande wangu basi kauli yako moja tu inatosha kuwafanya wananchi wote wanao kuamini wakaweza kunipigia kura mimi kisha nitakupa nafasi yoyote ambayo wewe utaitaka” aliendelea kushusha sera zake mheshimiwa raisi.

“Umesema utanipa nafasi yoyote ile?”

“Ndiyo”

“Unaweza kuniachia Ikulu?”

“Whaaaaat?”

“Nisikilize mheshimiwa, mimi sio wale watu ambao wanarubunika kwa maneno au kwa pesa, nimebahatika kuwa na kila kitu kwenye maisha yangu ila kitu pekee ambacho ninatamani kwa sasa ni kuwalipa mema wananchi wangu ambao wana imani kubwa sana na mimi. Nchi haina miundombinu ya kuridhisha kila mwaka mnawapiga porojo tu huku mkizinufaisha familia zenu na matumbo yenu kwa kuiba mali nyingi za serikali na kuzihifadhi kwenye mabenki ya nje. Kuna watoto mpaka leo hawana hata madarasa ya kusomea, kuna watoto hawana hata walimu wa kuwafundisha na walimu kibao wapo mtaani hawana ajira mkisingizia kwamba uchumi wa nchi sio mzuri, watoto wanakosa elimu bora, vijijini wananchi hawapati huduma za kijamii zaidi ya kujisaidia wenyewe, kuna vijiji vingi havina hata umeme, vijiji vingi havina huduma za afya tunaishia kupoteza wamama wanao jifungua na watoto kila mwaka huku nyie mkiishia tu kupiga picha kwenye maeneo yenye hali nzuri mkiyatumia kwenye kampeni. Unahitaji niwe chini yako tukaendelee kufanya ufisadi kwa pamoja niwaache wananchi wangu wakiwa wanataabika namna hiyo bado? Mheshimiwa kuna maisha ambayo baadhi ya watu wanayaishi ndani ya nchi hii hata watu wa nje huko wakijua watatucheka sana na kutushangaa kwamba raisi huwa unafanya kazi gani labda. Hivyo kiufupi ni kwamba siwezi kufanya hicho unacho kitaka, siwezi kuwasaliti wananchi wangu na sidhani kama nitakuja kukubali wito wako tena kama ndio huu ujinga ambao umeniitia hapa” aliongea kwa ukali sana na kumwambia ukweli raisi huyo. Alikuwa ni mzuri tu wa ahadi na visingizio vingi sana ila kiuhalisia kwenye nchi yake wananchi wengi sana walikuwa na maisha magumu mno.

Alimchana ukweli kwamba zama hizi hazikuwa za watoto kukosa madarasa wala sehemu za kusomea, hazikuwa zama za nchi kushindwa kutekeleza huduma za kijamii wakati viongozi wanatanua kwa kuishi maisha mazuri isivyokuwa kawaida kwenye nchi yao. Mheshimiwa raisi mpaka wakati huo ndita zilikuwa zimejichora vibaya sana kwenye paji lake la uso, ukweli ambao unaumiza huwa ni kisu kikali sana kwa mtu mwenye jeraha la namna hiyo.

Wakati huo mr Apson Limo alikuwa amenyanyuka na kuanza kutoka hapo bila hata kuaga lakini alisimama baada ya meza kugongwa kwa nguvu sana na mheshimiwa raisi ikamfanya asimame;

“Naona umeanza kunikosea heshima, unasahau kwamba unaongea na nani na uko wapi wakati huu! Unajua nina uwezo wa kukufanya usifike kwako mpuuzi wewe? Unawaongelea wananchi gani wa kuwapigania? Wananchi ambao hata hawajielewi hawa, wananchi ambao kila wakati wanawaza ujinga tu na hakuna jambo la maana lolote lile ambalo wanaliwaza? Nilikuwa nakuona mtu wa maana sana ila kumbe naongea na moja kati ya watu wajinga sana kuwahi kutokea duniani mpuuzi mkubwa wewe” mheshimiwa maneno yale yalimuuma sana kiasi kwamba hakuweza kabisa kuyavumilia ndiyo maana aliongea kwa ukali sana na kumtisha mr Apson Limo. Mr Apson Limo alitabasamu na kurudi kisha akainamia kwenye hiyo meza ya mheshimiwa akiwa anamwangalia usoni.

Unatamani kujua kwamba mr Apson Limo alimwambia nini mheshimiwa raisi baada ya hapo? Ukurasa wa saba naweka nukta hapa, panapo majaaliwa tukutane wakati ujao.

Febiani Babuya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom