Lu-ma-ga
JF-Expert Member
- Sep 21, 2010
- 4,780
- 3,227
Nawaomba taarifa hii muifikishe kwa wote wapenda mabadiliko kwa haraka
Jana nilipata taarifa kuwa baada ya mpango wa kumpatia Askofu Mokiwa Tshs.11milioni ili asaidie chama Fulani kuwashawishi waumini wake kushindikana, Chama hicho hakijakata tama kuitumia karata hiyo.
Kuna taarifa kuwa kuna mpango unaendelea kuandaliwa wa kujaribu kuwapatia baadhi ya MAASKOFU wa madhehebu ya kikristu makubwa, mfano RC, KKKT, FGC n.k kiasi kikubwa cha fedha ili katika muda wa wiki mbili kuanzia leo wajaribu kuwashawishi waumini wake ili wakipigie kura chama hicho.
Taarifa hizi ni za uhakika na tusipoteze muda kuuliza source of information, kwani jaribio la kumhonga askofu tayari lilishafanyika japo halikufanikiwa.Ili kutekeleza mpango huu chama hicho kinatumia kikosi chake cha kampeni kwa kuwatumia wazee wa makanisa hayo ili wapate urahisi wa kuwaingia maaskofu hao.Maeneo ambayo yamewekewa umuhimu ni kanda ya Ziwa, Kanda nyanda za juu kusini ambako kuna madhehebu mengi ya kikristu ambako pia kuna idadi kubwa ya wapiga kura na upepo wa mabadiliko unavuma kwa kasi.
Mtoa habari alinidokeza kuwa kuna ubishani katika hiyo kamati ya kampeni ni kwamba uwezekano wa kutofanikiwa mbinu hiyo chafu kwani misimamo ya maaskofu imekuwa kinyume sana na rushwa ila wanataka wajaribu Zari kwani mbinu zao nyingi inaonekana zinagonga mwamba.Inaonekana swala la kuiba kura limedhibitiwa sana mwaka huu, na hivyo kwao wanaona linaweza lisisaidie , wanataka kujaribu mbinu nyingi kadri iwezekanavyo.
Lakini pia alidokeza kuwa inawezekana wajanja ndani ya chama hicho wanaanza kubuni namna ya kuzichukua pesa kwani mwaka huu imekuwa vigumu kuchukua kwa kuwa fungu linadhibitiwa na watu wa karibu wa mgombea.
Nawaomba mfikishe taarifa hizi kwa chadema na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania na pia maaskofu wapewe taarifa hizi ili wajue nini kinawanyemelea.
Jana nilipata taarifa kuwa baada ya mpango wa kumpatia Askofu Mokiwa Tshs.11milioni ili asaidie chama Fulani kuwashawishi waumini wake kushindikana, Chama hicho hakijakata tama kuitumia karata hiyo.
Kuna taarifa kuwa kuna mpango unaendelea kuandaliwa wa kujaribu kuwapatia baadhi ya MAASKOFU wa madhehebu ya kikristu makubwa, mfano RC, KKKT, FGC n.k kiasi kikubwa cha fedha ili katika muda wa wiki mbili kuanzia leo wajaribu kuwashawishi waumini wake ili wakipigie kura chama hicho.
Taarifa hizi ni za uhakika na tusipoteze muda kuuliza source of information, kwani jaribio la kumhonga askofu tayari lilishafanyika japo halikufanikiwa.Ili kutekeleza mpango huu chama hicho kinatumia kikosi chake cha kampeni kwa kuwatumia wazee wa makanisa hayo ili wapate urahisi wa kuwaingia maaskofu hao.Maeneo ambayo yamewekewa umuhimu ni kanda ya Ziwa, Kanda nyanda za juu kusini ambako kuna madhehebu mengi ya kikristu ambako pia kuna idadi kubwa ya wapiga kura na upepo wa mabadiliko unavuma kwa kasi.
Mtoa habari alinidokeza kuwa kuna ubishani katika hiyo kamati ya kampeni ni kwamba uwezekano wa kutofanikiwa mbinu hiyo chafu kwani misimamo ya maaskofu imekuwa kinyume sana na rushwa ila wanataka wajaribu Zari kwani mbinu zao nyingi inaonekana zinagonga mwamba.Inaonekana swala la kuiba kura limedhibitiwa sana mwaka huu, na hivyo kwao wanaona linaweza lisisaidie , wanataka kujaribu mbinu nyingi kadri iwezekanavyo.
Lakini pia alidokeza kuwa inawezekana wajanja ndani ya chama hicho wanaanza kubuni namna ya kuzichukua pesa kwani mwaka huu imekuwa vigumu kuchukua kwa kuwa fungu linadhibitiwa na watu wa karibu wa mgombea.
Nawaomba mfikishe taarifa hizi kwa chadema na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania na pia maaskofu wapewe taarifa hizi ili wajue nini kinawanyemelea.