samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema aliingia matatani baada ya kuomba muongozo kwa spika akitaka aelezwa ni hatua zipi zinaweza kuchukuliwa endapo itabainika waziri mkuu analidaganya bunge na taifa? Baada ya kauli hiyo spika wa bunge anna makinda kutokana na ama ubabe wake au uelewa wake mdogo wa hoja akamtaka mh. Lema athibitishe bungeni kauli yake kwamba pinda kadanganya au vinginevo afute kauli yake. Baadaye baada ya kushauriwa na watu makini akaona waziri mkuu atadhalilika endapo lema atawasilisha ushahidi wake bungeni hivyo akamwambia lema apeleke ushahidi wake kwa maandishi. Wengi tulitegemea makinda angetoa hukumu kwa lema kwa kumdhalilisha waziri mkuu au angeuambia umma kwamba ushahidi unaonesha kweli pinda alidanganya.bunge na taifa. Nilisoma baadhi ya ushahidi wa lema kwenye gazeti la raia mwema ambao kwa kiasi kikubwa pinda alidanganya. Kwanza pinda alisema watanzania watatu walipoteza maisha wakati ukweli ni watanzania 2 na mkenya mmoja. Pili pinda anasema mauaji yalitokea takribani mita 500 kutoka kituo cha polisi wakati ushahidi unaonesha wengine waliuawa umbali wa kilomita tatu kutoka kituo cha polisi. Pinda pia alisema chadema wasiweza kushinda uchaguzi wa umeya kwa kua walikua na madiwani 14 na ccm wana madiwani 16. Kwanza kura zinapigwa kwa siri ukizingatia mgawanyiko uliokuwepo ndani ya ccm mkoa wa arusha ni wazi madiwani wengine wangeasi, pili chadema walishinda hai wakati walikua na madiwani wachache kuliko ccm. Hayo ni machache tu mengi anayo lema mwenyewe..