Sakata la Makontena ya Mchanga: Wamiliki wa Makotena waongea na Wanahabari, wadai wanapata hasara

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,719
55,830
Heshima kwenu Wakuu,

Leo kuna mkutano wa Wandishi wa habari unafanyika magomeni. Kubwa katika yote ni kuelezea Sakata la Mchanga. Nimepata habari ikisema, "baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini ambao ni wamiliki wa makonteina yanayodaiwa kukamatwa bandarini, watakuwa na Press Conference leo Saa 5:30 asubuhi hii Hoteli ya Travatine Magomeni.

Wanaomba waandishi wa Habari na Wapigapicha. Good morning once again"


Ntawaletea kinachojiri kutoka hapa Magomeni. Nshafika sehemu ya Tukio.

Karibuni.

=========

UPDATES:

=========

1130HRS: Wanahabari wameshafika Sehemu ya tukio, ila wahusika bado hawajaonekana

1200HRS: Wahusika wameshawasili eneo la tukio

WhatsApp Image 2017-03-28 at 12.03.11 PM.jpeg


Wanaanza kujitambulisha kuna Rweyemamu Kente ni msafirishaji na mchimbaji
pia kuna Laurent Matemu mdau katika madini, Salum Nassoro, Mohamed Mkwayu ni mchimbaji paul ndo wameongezana naye

Rweyemamu Kante anaongea:
Sisi ni wachimbaji wadogo, makontena yetu yamezuiwa Mkuba, tumekuja kupaza sauti rais aelewe, ingawa wakubwa wamezuiwa, tunataka ieleweke kwamba na sisi wachimbaji wadogo tumeathirika

Mimi nimeathirika kutokana na zuio sababu Kontena 13 zimezuiliwa Mkuba ICD
Madini yapo sehemu nyingi, mimi ni mchimbaji na msafirishaji, migodi ambayo tupo nayo na vibali tunavyo vya wachimbaji wadogowadogo, migodi yetu sisi ni ya copper sio dhahabu

Tatizo la Tanzania ni kwamba deposit ya copper ni ndogo, migodi yetu sisi ni ya shaba, ukiseme uweke mitambo ya kuyeyusha, hauwezi kwani hatuna madini ya kutosha

Hili zuio lilikuwa linalenga wachimbaji wakubwa lakini watu wa Serikali wametuunganisha na sisi.

Sisi kwa mwezi tunapata Contena tano au sita, sisi ni wamachinga katika sekta ya Madini kama walivyo wa kariakoo, hivyo tunamuomba rais atuwekee mazingira rafiki.

Mohamed Mkwayu mchimbaji wa shaba Mpwapwa. Anasema:
Tunampongeza rais kwa hatua anazozichukua, tatizo la kutokusafirisha mchanga wameunganisha na sisi, sisi tuna kiwanda nchini cha kuongeza thamani. Baada ya hapo ndo tunasafirisha. Hata sisi tumezuiwa

Sisi tulikuwa tunachimba copper, hatupo kwenye dhahabu, hili swala tunaomba watu wa Wizara washughulikie, tulikuwa tunalipia baada ya mchanga wetu kupimwa ndo tunasafirisha

Rais aangalie kwa kina hili swala. Wenzetu wa dhahabu wanaendelea na kuandaa dhahabu yao, lakini sisi tumeshindwa sababu ni wachimbaji wadogo, kikubwa tunampongeza rais, sisi ni wachimbaji wa hapahapa nchini.

Paul kalyembe mchimbaji wa Zinc na Copper anasema:
Sisi tumekata leseni ya kuchimba na kuuza. Sisi hatuhusiki na dhahabu
Hatuna uwezo wa kuchimba na kuweka kiwanda cha kuyeyusha madini, sisi ni machinga.

Kwa kutumia waandishi wa habari, tunaomba mtusaidie kufikishia rais hili swala kwamba atuonee huruma sisi wachimbaji wadogo wadogo ili tuendelee na kazi zetu

Tunachohitaji kutoka kwa rais ni
1. Atuondolee zuio la kusafirisha madini yetu, bado tuna madini ambayo bado yapo kwenye utafiti kama Nickel, mlezi wetu ni stamico, tunafanya kwa uangalizi wake.

2. Sisi tunatozwa storage bandarini japo serikali ndo imezuia Makontena. Kila siku tunatozwa dollar 20 kwa siku pale Mkuba

*Kotena ambazo zimeshikiliwa ni 60 nickel na 7 copper, nikisimamisha mgodi siku moja napata hasara ya millioni nne, toka wametangaza mwezi umeisha. Hivyo unaweza kujua kiasi gani cha hasara tumepata.

Baadhi ya Wachimbaji walioongea na Waandishi ni;

Mohamed Mkwayu - Mcimbaji wa Madini ya aina ya Shaba Mpwapwa, Mmiliki wa Migodi na Msafirishaji wa Mchanga.

King Selemani - Mnunuzi wa Madini ya Metal

Paul Obed Kalyembe - Mchimbaji wa madini ya Shaba.

Thobias weyemamu - Mwenyekiti wa Wachimbaji wadogo wa Madini ya Metalic
 
Hans Zakaria Pope alikuwa ni Mmoja wa Wafadhili wa Timu ya Kampeni ya Mgombea mmoja wa Rais ajitafakari sana hata Kama kasimamia kwny haki maana pia waliwahi kuzozana na aliekuwa na Waziri wa Ujenzi wakat wa Jk kwny Mzozo wa wenye Malori!

Waziri huyo Sasa hivi ndie Mwenye Mbwa kwa sasa
 
Wewe utakuwa upande upi ? wa Watanzania wazawa au hao ma-Vampire ..
"Unnu old vampire only like to see blood running"
with Tosh voice
 
Mmm sitashanga kitakachozungumziwa sicho kinachotegemewa kusikika leo kwenye masikio ya watz wengi.
 
Hans Zakaria Pope alikuwa ni Mmoja wa Wafadhili wa Timu ya Kampeni ya Mgombea mmoja wa Rais ajitafakari sana hata Kama kasimamia kwny haki maana pia waliwahi kuzozana na aliekuwa na Waziri wa Ujenzi wakat wa Jk kwny Mzozo wa wenye Malori!

Waziri huyo Sasa hivi ndie Mwenye Mbwa kwa sasa
Luteni mstaafu ni mbambanaji sana ila kuna kitu kinafichwa nyuma ya pazia
 
transporters wanapata hasara...kumbe usafirishaji wa huu mchanga ulikuwa ajira kwa wengi
 
transporters wanapata hasara...kumbe usafirishaji wa huu mchanga ulikuwa ajira kwa wengi
 
Naiona hasara kubwa sana ambayo hatutakuja kuisahau kiurahisi kama samaki wa kipindi cha JK waliosababishwa na huyu huyu jamaa, hasara atayotuletea safari hii kila mtu atalia kilio cha kusaga meno
 
Heshima kwenu Wakuu,

Leo kuna mkutano wa Wandishi wa habari unafanyika magomeni. Kubwa katika yote ni kuelezea Sakata la Mchanga. Nimepata habari ikisema, "baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini ambao ni wamiliki wa makonteina yanayodaiwa kukamatwa bandarini, watakuwa na Press Conference leo Saa 5:30 asubuhi hii Hoteli ya Travatine Magomeni.

Wanaomba waandishi wa Habari na Wapigapicha. Good morning once again"


Ntawaletea kinachojiri kutoka hapa Magomeni. Nshafika sehemu ya Tukio.

Karibuni.

=========

UPDATES:

=========

1130HRS: Wanahabari wameshafika Sehemu ya tukio, ila wahusika bado hawajaonekana

1200HRS: Wahusika wameshawasili eneo la tukio

View attachment 487865

Wanaanza kujitambulisha kuna Rweyemamu Kente ni msafirishaji na mchimbaji
pia kuna Laurent Matemu mdau katika madini, Salum Nassoro, Mohamed Mkwayu ni mchimbaji paul ndo wameongezana naye

Muwakilishi wao anaongea:
Sisi ni wachimbaji wadogo, makontena yetu yamezuiwa Mkuba, tumekuja kupaza sauti rais aelewe, ingawa wakubwa wamezuiwa, tunataka ieleweke kwamba na sisi wachimbaji wadogo tumeathirika
Mimi nimeathirika kutokana na zuio sababu Kontena 13 zimezuiliwa Mkuba ICD

Madini yapo sehemu nyingi, mimi ni mchimbaji na msafirishaji, migodi ambayo tupo nayo na vibali tunavyo vya wachimbaji wadogowadogo, migodi yetu sisi ni ya copper sio dhahabu
Tatizo la Tanzania ni kwamba deposit ya copper ni ndogo
hawa ndio wanaingiza billioni 40 kwa wiki? acheni utani.
 
Heshima kwenu Wakuu,

Leo kuna mkutano wa Wandishi wa habari unafanyika magomeni. Kubwa katika yote ni kuelezea Sakata la Mchanga. Nimepata habari ikisema, "baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini ambao ni wamiliki wa makonteina yanayodaiwa kukamatwa bandarini, watakuwa na Press Conference leo Saa 5:30 asubuhi hii Hoteli ya Travatine Magomeni.

Wanaomba waandishi wa Habari na Wapigapicha. Good morning once again"


Ntawaletea kinachojiri kutoka hapa Magomeni. Nshafika sehemu ya Tukio.

Karibuni.

=========

UPDATES:

=========

1130HRS: Wanahabari wameshafika Sehemu ya tukio, ila wahusika bado hawajaonekana

1200HRS: Wahusika wameshawasili eneo la tukio

View attachment 487865

Wanaanza kujitambulisha kuna Rweyemamu Kente ni msafirishaji na mchimbaji
pia kuna Laurent Matemu mdau katika madini, Salum Nassoro, Mohamed Mkwayu ni mchimbaji paul ndo wameongezana naye

Muwakilishi wao anaongea:
Sisi ni wachimbaji wadogo, makontena yetu yamezuiwa Mkuba, tumekuja kupaza sauti rais aelewe, ingawa wakubwa wamezuiwa, tunataka ieleweke kwamba na sisi wachimbaji wadogo tumeathirika
Mimi nimeathirika kutokana na zuio sababu Kontena 13 zimezuiliwa Mkuba ICD

Madini yapo sehemu nyingi, mimi ni mchimbaji na msafirishaji, migodi ambayo tupo nayo na vibali tunavyo vya wachimbaji wadogowadogo, migodi yetu sisi ni ya copper sio dhahabu
Tatizo la Tanzania ni kwamba deposit ya copper ni ndogo, migodi yetu sisi ni ya shaba, ukiseme uweke mitambo ya kuyeyusha, hauwezi kwani hatuna madini ya kutosha
Hili zuio lilikuwa linalenga wachimbaji wakubwa lakini watu wa Serikali wametuunganisha na sisi.
Sisi kwa mwezi tunapata Contena tano au sita, sisi ni wamachinga katika sekta ya Madini kama walivyo wa kariakoo, hivyo tunamuomba rais atuwekee mazingira rafiki.

Mohamed mkwayu mchimbaji wa shaba Mpwapwa. Anasema:
Tunampongeza rais kwa hatua anazozichukua, tatizo la kutokusafirisha mchanga wameunganisha na sisi, sisi tuna kiwanda nchini cha kuongeza thamani. Baada ya hapo ndo tunasafirisha. Hata sisi tumezuiwa

Sisi tulikuwa tunachimba copper, hatupo kwenye dhahabu, hili swala tunaomba watu wa Wizara washughulikie, tulikuwa tunalipia baada ya mchanga wetu kupimwa ndo tunasafirisha
Rais aangalie kwa kina hili swala. Wenzetu wa dhahabu wanaendelea na kuandaa dhahabu yao, lakini sisi tumeshindwa sababu ni wachimbaji wadogo, kikubwa tunampongeza rais, sisi ni wachimbaji wa hapahapa nchini.

Paul kalyembe mchimbaji wa Zinc na Copper anasema


Ukisikia Usanii ndo huu, Acasia Gold wakakutane Magomeni?
 
Hans Zakaria Pope alikuwa ni Mmoja wa Wafadhili wa Timu ya Kampeni ya Mgombea mmoja wa Rais ajitafakari sana hata Kama kasimamia kwny haki maana pia waliwahi kuzozana na aliekuwa na Waziri wa Ujenzi wakat wa Jk kwny Mzozo wa wenye Malori!

Waziri huyo Sasa hivi ndie Mwenye Mbwa kwa sasa
Acha mambo za timu na ubaguzi.
Viongozi wanatakiwa kutenda haki na kufuata na sheria na katiba.
 
Hahahaha, maigizo ya enzi za jk yanajirudia tena....eti hao ni wachimbaji wadogo wadogo ambao wanasafirisha mchanga wa madini kwenda Tokyo.
 
Hans Zakaria Pope alikuwa ni Mmoja wa Wafadhili wa Timu ya Kampeni ya Mgombea mmoja wa Rais ajitafakari sana hata Kama kasimamia kwny haki maana pia waliwahi kuzozana na aliekuwa na Waziri wa Ujenzi wakat wa Jk kwny Mzozo wa wenye Malori!

Waziri huyo Sasa hivi ndie Mwenye Mbwa kwa sasa

Uyu uliemtaja yuko hapo?
 
Back
Top Bottom