Sakata la mahindi litaondoka na serikali?

Hili tatizo limesababishwa na serikali wenyewe kila siku wanakuja na sheria mpya wanawanyima wafanya biashara kuuza soko wanalotaka wao kwa manufaa ya wakulima. Kuna wakati hakuna kuuza mahindi nje mara uzeni mara tutanunua hata hujui kesho watakuja na sheria zipi bila kujali watu wame invest wewe huchangii katika gharama zao ikifika siku wanataka kufanya biashara wanaingiza pua zao utasema walitoa ruzuku kusaidia kilimo. acha soko huru wauze wanakotaka ili uhitaji uwe mkubwa na bei itapanda wateja wakiwa ni wengi bei itajihukumu yenyewe kama soko huru tuache kuingilia biashara za watu. Ni kama ndege wakiona booking watu wengi bei zinapanda mnaweza kuwa mko wote ndani ya ndege lakini kila mtu kalipa bei tofauti. Usifanye regulation katika bei acha soko lihukumu iwe usafirishaji, wakulima hata real estate. Mwezi wa 6 nilikuwa Dar hotel zote bei juu sababu high season ni sawa lakini sasa ije mfano mwaka mpya wenye magari hakuna kupandisha bei askari wameshajaa mbona hawafanyi kwa biashara zingine. Kama Mahindi waacheni wauze wanakotaka kwenye maslahi kwao serikali kusanya kodo stahiki tu biashara sio jukumu lako.
 
Kilimo chetu cha kijamaa hakitatufikisha popote. Kitatutia umaskini na nchi ipo siku itaanguka kwenye njaa. Wanaolisha nchi ni wazee vijijini. Matajiri wakubwa na vijana hawataki kulima, kwanini? Sababu kilimo hakilipi. Kwanini hakilipi? Sababu serikali inafunga mipaka inapojisikia, inawapangia watu kwa kuuza mazao yao! Matokeo yake bei inakuwa si rafiki, hairudishi hata gharama. Hakuna atakayelima kwa mazingira hayo.

Tunakoenda kwa bei hizo hakuna atakayelima ili kuuza. Watu watalima kiduchu tu ya kula. Nchi itaingia kwenye njaa.

Cha kufanya, serikali iruhusu mtu auze mahindi yake popote anapotaka. Itungwe sheria kuwa serikali hairuhusiwi kumzuia mtu kuuza mazao yake atakako. Mtu alime akiwa na uhakika wa soko zuri South Sudan, Congo nk. Hapo ndipo mkulima atachomoka na uwekezaji mkubwa utafanyika kwenye kilimo.
Mkuu Nawatania, huwatani unasema kweli tu. Matatizo ya kilimo chetu hayapewi ufumbuzi sahihi wa kuyatatua, ndio maana leo vijana wengi wapo mjini na kufanyabiashara ya umachinga baada ya kuona kwamba kilimo hakilipi inavyotakiwa kwa sababu ya gharama za kilimo. Wakulima wengi sasa ni wazee ambao hawana uwezo na pilikapilika za kutafuta masoko mbali. Aidha kwenye kilimo kuna matatizo mengi sana, ila kwa sababu kilimo ni nature basi twende hivyo hivyo.
 
Kumekuwa na kelele sana juu ya anguko la bei ya mahindi kote nchini. Kiasi ambacho imebidi CCM iingilie kati. Nimewaona wabunge wote hasa wa CCM wakionyesha kutorodhishwa kwao jinsi NFRA inavyonunua mahindi toka kwa wakulima.

Ongezekeo hili la wingi wa mahindi ni mwitikio wa wakulima kwani wakati wa CORONA wakulima waliambiwa walime kwa wingi kwani baadhi ya mataifa yanaweza kukumbwa na baa la njaa kwani kujifungia kwao ndani wengi wao walishindwa kulima kwa wakati na kwa ufasaha.

Kwa kuwa CCM ni chama na Wakulima na wafanyakazi hakiwezi kujisikia furaha kwa kuwaona wakulima wakipata taabu.

Je, ni kutokana na ukaribu huo wa CCM na wakulima serikali inaweza undwa upya?

Ni jambo la kusubiri kuona mambo yataendaje ikizingatiwa kuwa mikoa inayolima mahindi kwa wingi kama Ruvuma, Iringa, Njombe na Katavi ndiko waliko wana CCM wasiobadilika hivyo wana mchango sana kwa CCM kuendelea kuwa madarakani
Watu Hawali milo mitatu siku hizi..umasikini umezidi...ndio maana mahindi hayatoki. Walishaharibu masoko...it is hard to get masoko tuliyokuwa nayo wakati wa kikwete...
 
Kumekuwa na kelele sana juu ya anguko la bei ya mahindi kote nchini. Kiasi ambacho imebidi CCM iingilie kati. Nimewaona wabunge wote hasa wa CCM wakionyesha kutorodhishwa kwao jinsi NFRA inavyonunua mahindi toka kwa wakulima.

Ongezekeo hili la wingi wa mahindi ni mwitikio wa wakulima kwani wakati wa CORONA wakulima waliambiwa walime kwa wingi kwani baadhi ya mataifa yanaweza kukumbwa na baa la njaa kwani kujifungia kwao ndani wengi wao walishindwa kulima kwa wakati na kwa ufasaha.

Kwa kuwa CCM ni chama na Wakulima na wafanyakazi hakiwezi kujisikia furaha kwa kuwaona wakulima wakipata taabu.

Je, ni kutokana na ukaribu huo wa CCM na wakulima serikali inaweza undwa upya?

Ni jambo la kusubiri kuona mambo yataendaje ikizingatiwa kuwa mikoa inayolima mahindi kwa wingi kama Ruvuma, Iringa, Njombe na Katavi ndiko waliko wana CCM wasiobadilika hivyo wana mchango sana kwa CCM kuendelea kuwa madarakani.
Serikali ya wajinga labda, serikali ndio inapanga bei ya mahindi sokoni? Kuna mtu aliambiwa alime? Alafu hizi bei ziko hivi mwaka wa 3 huu sasa sijui kiwewe kinatoka wapi kwa sasa.
 
Back
Top Bottom