Nteko Vano
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 434
- 113
Ndugu yangu Tuko wewe unadhani Ile kauli ya Mwigulu Nchemba ni Kauli ya nani? na Kauli ya CCM ni ipi mpaka sasa?
*Jaribu kuunganisha haya ndio utajua kauli ya Mwigulu ndio kauli ya CCM:
1/Mwigulu Nchemba ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM(Mahali popote anakuwepo pasipo Katibu mkuu basi Atakuwa anakaimu nafasi ya katibu mkuu wa CCM ambaye ndiye mtendaji/mratibu mkuu wa CCM)
2/Mwigulu Nchemba alitumwa rasmi na Secretariety ya CCM kama mjumbe mkuu rasmi kwenda kutatua mgogoro wa Loliondo Kisiasa!!(Alienda kujadiliana, kushawishi au kuhitimisha kiini cha mgogoro ule kwa niaba ya CCM, kwa hivyo ni lazima alitakiwa kutoa kauli)
3/Kauli ile aliitoa kwenye mkutano rasmi wa Kichama mbele ya Wananchi(WanaCCM!!), watendaji wote muhimu wa CCM na Serikali.
4/Kabla na hata baada ya Kauli ya Mwigulu Nchemba kutoka hakuna kauli nyingine yoyote uliyowahi kutolewa na CCM taifa kuhusiana na mgogoro wa Loliondo.
5/Toka Secretariety mpya ya CCM kuundwa mwishoni mwa mwaka jana, walikuja na mtindo wa kuwaadabisha viongozi wa serikali hadharani ili kukinusuru Chama mbele ya wananchi(Kauli mbiu ya Chama kuidabisha serikali!!)
umedadafua viizuri sana. lakini sekretariat iliktana na kutoka na maamuzi pamoja na njia ya kukabili mgogoro huu ndio maana nchemba akatumwa. nchemba ni mropokaji na ana uwezo mdogo wa kujenga hoja na upatanishi hivyo kuna uwezekano ile kauli ilimtoka tu baada ya kuona mazingira yalivyo. sasa je, ndicho walichokubaliana ktk secretariet? au uwezo wa ushawishi ulifikia kikomo?
Last edited by a moderator: